CAG: ATCL imeendeshwa kwa hasara kwa miaka 5 mfululizo

CAG: ATCL imeendeshwa kwa hasara kwa miaka 5 mfululizo

Kuna kitu unatakiwa kujua kihasibu. Uwekezaji mkubwa mara nyingi unachukua miaka kadhaa kuanza kuleta faida. Faida maana yake hela inayoingia ni kubwa kuliko inayotoka. Hasara ni kinyume chake. Kuna ndege zimenunuliwa tu juzi unatakaje zipate faida ndani ya siku mbili? Haiwezekani kabisaa duniani kote. Baada ya muda shirika litatulia. Ukianza biashara ya kupanda mitiki leo, mwakani si rahisi ukapata faida.
ill prove you wrong. at one time atcl ilitangaza imepata faida.. almost katibia 20b na ushee.
walipataje hii faida?
au walikuwa wanamuongopea hayati?
 
Biashara ya ndege si mchezo, hata kwa nchi zenye uzoefu na mashirika makubwa , bado wanaendelea kuyaendesha kwa hasara. Tena baada ya corona kuingia basi ni taabu sana. Umeona mashirika kama Ethiopian Airlines na mengine ikabidi kuchangamkia haraka cargo ili kuweza kusurvive... mashirika mengine huku southern Afrika mpaka serikali zao zinanawa sasa mikono kuacha tu yafilisiwe i.e. kama SAA ambayo serikali imekuwa kuwa inabail out pesa mfululizo kila mwaka since 2010...Na vilevile Namibia Airways nayo imekuwa liquidated hivi karibuni for similar reasons.. Kwa hiyo biashara ya ndege si rahisi kama wengi wetu tunavyofikiri inahitaji bussines plan iliyosheni na mambo mengi, na bila kuingiza sana ' politics' ktk uendeshaji wake. Hata wenzetu Kenya Airways currently, wamekuwa wanaoperate kwa losses .. Mie ningeshauri Mh. Samia Suluhu na serikali yake, kwa issue ya ATC na kwa vile hayati Mzee wetu aliiweka chini ya ikulu moja kwa moja, na ikimaanisha kwamba kwa yeye Rais kwa sasa ndo itabidi awajibike vilevile kwa masaibu ya ATC, hivyo kwake labda akiwa na washauri wake na ikimpendeza kulingana na all options, vilevile kufikiria kuipatia ATC, deadline period ya ku break-even ambapo wakishindwa, itabidi market forces ziongeee ili kuepusha further losses. Serikali ijitahidi kutojiingiza kuimiliki 100 percent kwenye biashara na labda mostly, wanakuwa na shares tu na other entities kuepuka hasara kubwa kwa taxpayers money.
Nawatakia heri Rais Mama Samia Suluhu na serikali ya Tz mafanikio mema.
Japokuwa si muandishi mzuri, lakini mkuu umeongea facts. Hichi ndicho wenye akili walikuwa wakishauri siku zote, wamesema sana wakaitwa majina sijui wasaliti sijui wakwamishaji sijui wamekosa uzalendo.

Hii mada imewazidi uwezo watu wengi sana hasa mataga, narudia tena mataga. Hawaelewi wanatetea nini na hawaelewi hawatetei nini na wengine wameanza kuhamisha magoli eti ni mbinu za kulifilisi na kutaka kulibinafsisha shirika.

Ni lini serikali itaelewa umuhimu wa kutokuweka mtaji 100% ambao ni pesa ya walipa kodi katika biashara na badala yake imiliki shares kadhaa na ijiondoke katika uendeshaji ila ilinde maslahi yake.
 
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu Serikali, Charles E. Kichere amesema Shirika la ndege la Tanzania (ATCL) limetengeneza hasara ya shilingi bilioni 60 (60B) kwa mwaka na kwa kipindi Chote cha miaka ya nyuma shirika hilo limekuwa likitengeneza Hasara.

Screenshot_20210328-115528.jpg


“Katika ukaguzi wetu wa mwaka 2019/2020 tumegundua Shirika letu la Ndege limetengeneza hasara mwaka huu ya Tsh.Bilioni 60 ila kwa miaka mitano pia limekuwa likitengeneza hasara, kuna changamoto ambazo Serikali inabidi iziangalie ili Shirika letu litekeleze majukumu yake vizuri”
 
Ningewaonaga wathamani sana endapo wangelinunuaga mabasi ya mikoani alafu nauli zishushe ili sisi makapuku tufaidi hela zetu. Unanunua mandege alafu et unatetea wanyonge, kuna mnyonge anaweza kupanda ndege kweli???🤔
 
Wapunguze mishahara ya marubani
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu Serikali, Charles E. Kichere amesema Shirika la ndege la Tanzania (ATCL) limetengeneza hasara ya shilingi bilioni 60 (60B) kwa mwaka na kwa kipindi Chote cha miaka ya nyuma shirika hilo limekuwa likitengeneza Hasara.

Screenshot_20210328-115528.jpg


“Katika ukaguzi wetu wa mwaka 2019/2020 tumegundua Shirika letu la Ndege limetengeneza hasara mwaka huu ya Tsh.Bilioni 60 ila kwa miaka mitano pia limekuwa likitengeneza hasara, kuna changamoto ambazo Serikali inabidi iziangalie ili Shirika letu litekeleze majukumu yake vizuri”
 
MJG.jpg


Sio kwamba ripoti hizi zina mpya sana, bali kuna mtu mpya ambaye ameamua kuzifanyia kazi. Zamani zilikua zikisomwa zinawekwa kapuni maisha yanaendelea.
Kuna watu wanadhani hii ndio hasara ya kwanza kwa ATCL. CAG aliyepita Prof.Assad amewahi kuibua hasara kubwa zaidi ya hizi. But who cares?
Mwaka 2015/16 ATCL ilipata hasara ya 94.3Bil. Mwaka 2016/17 hasara ya 109.3Bil, na mwaka 2017/18 hasara ya 113.8Bil.

Kwahiyo hii 60Bil aliyoibua Kichere ni "cha mtoto" someni ripoti za Prof.Assad mtaona hasara ya mabilioni mengi zaidi. Tofauti ni kwamba wakati wa Assad ripoti zilizimwa. Wakubwa hawakupenda serikali "ichafuke". Lakini mama amekua tofauti. Anataka mambo yawekwe hdharani wananchi wajue. Transparency and accountability.
ZZK aliwahi kusema, sio kwamba serikali ya JPM ni safi sana, bali ilijitahidi kuficha taarifa watu wasijue. We unadhani JPM angekuwepo hii ripoti ya CAG ingesomwa kama ilivyosomwa? Thubutu.!

Watu wengi walisema serikali ya JK ilijaa ufisadi, lakini wasichoelewa ni kwamba JK mwenyewe alitaka watu wajue. We unadhani alishindwa kuzuia taarifa ya Richmond, EPA, Escrow etc? Alikua na uwezo wa kuzuia na wananchi wasijue chochote. Na angeondoka madarakani mnamsifia serikali yake ni clean. Lakini JK hakutaka "mapambio fake" aliamua kuweka kila kitu hadharani ili penye makosa paonekane na hatua zichukuliwe.

Serikali ya JPM haikutaka madhaifu yawekwe hadharani. Ndio maana CAG Assad aliibua madudu mengi lakini badala ya kupongezwa, akaonekana eti anaichafua nchi. Si unakumbuka ile kashfa ya 16Bil za jeshi la polisi kununua sare hewa? Iliishia wapi zaidi ya Kange Lugola kusema anajivua nguo na kumuita Prof.Assad muongo.

Bandarini kumejaa ufisadi mkubwa, lakini mkurugenzi wa bandari amekua akisifiwa sana na serikali ya JPM kuongeza mapato. Ndo ujue kuna watu walifanya ufisadi na kujificha kwenye kichaka cha Uzalendo. Leo mama ameagiza apelekewe ripoti ya BOT kuanzia January hadi March. Inadaiwa kuna mabilioni yalichotwa kwa "kisingizio" cha matibabu ya JPM.

Kwahiyo mama ameanza vizuri, lakini asiishie hapa. Mikataba ya miradi yote mikubwa iwekwe wazi. Wananchi wana haki ya kujua. Uwazi na uwajibikaji ni silaha muhimu kwenye utawala bora.!
 
Assad hakuziona yizo taarifa ndio maana Magufuli hakuzipat! Huyu cag wa sasa anavukunyua yote, hapokei mlungul ndio maan kayaibua yote haya!
Wewe bado hujitambui vizuri, jiulize hii ni report ya ngapi ya CAG na ni kwa nini hakueleza haya katika report zilizotangulia.

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Wewe bado hujitambui vizuri, jiulize hii ni report ya ngapi ya CAG na ni kwa nini hakueleza haya katika report zilizotangulia.

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
Ndio maana nikasema hata report yenyewe sina imani nayo,vinawezekana imeandaliwa kimagumashi kwa lengo jingine!
Ndio maana hata alipoiwakirisha mbashara hakuwahi kusema hayo! Ndio maana hata mama SSH alimuonya kuwa wazi!
Assad naye hakuwahi kuileta hiyo piw! Asante na byee 4 now!
 
Afu wanajisifia eti!, Bado zingine ndege nane zinakuja
 
Bilioni 60 hasara ambayo inatakiwa ilipwe ili turudi kwenye zero kwanza.

Bilioni 60 ingefanya mabadiliko kiasi gani kama ingewekwa kwenye kilimo au elimu?
Billion 60 zingepelekwa unaposema kwenye elimu ndipo utaikuta tamisemi ya JAFO wanakula pesa halafu hawarudishi.
 
ATCL ipewe muda , tusiwe na papara ya kutengeneza faida, tuendelee kujitanua kuongeza route za nje zenye faida, bei iwe rafiki kuvutia wateja, huduma zetu ziboreke, hili ni shirika ambalo litadumu muda mrefu hivyo faida itakuja as time goes. Mashirika yote tunayoona yana pata faida yana zaidi ya miaka 30 kwenye biashara hii , tutapata faida.
 
Back
Top Bottom