CAG na waliojikopesha Sh41 bilioni NHIF

Kwahiyo anachosema mama Mziray ni kwamba CAG ni muongo, maana naona kakanusha kila taarifa iliyotolewa na CAG. Na kama hayo maswali yote yalikua na majibu hayo aliyotaja, kwanini hakuyampa CAG ili hizo hoja ziondolewe kwenye ripoti?
 
waandishi wetu wa habari hawana huo uwezo wa kuhoji hiki ulichokiandika hapa
 
NHIF halafu unakuta dawa zingine hazipo kwenye bima!!!! unatakiwa uingie mfukoni!!!!

Kumbe wao wapo tu wanajikopesha fedha zetu!!!!

Kwakweli Serikali/viongozi wetu walio pewa dhamana wanapaswa wawe wakali ili kuepusha baadhi ya mambo ya ovyo kama haya.

Kinacho shangaza zaidi, viongozi wapo, watendaji wapo!!!!! Wee Mungu wangu duh!!!

Nimechoka Moyo unaenda mbio.

Sent from my V2118 using JamiiForums mobile app
 
Unapoenda kupata huduma hospitali unaambiwa hii hailipiwi na bima, kumbe pesa wameshajikopesha........

Huu mfuko una madudu mengi, wabadili namna ya kuuendesha kwa kutumia watu wachache tu wa utawala, wataalamu wa IT na wahasibu.

Waweke na kikomo cha asilimia ya makusanyo ambacho kinatakiwa kutumika kwenye shughuli za uendeshaji maana hawachelewi kujikopesha za kununua ma viieite huku wagonjwa wakisoteshwa kwenye mahospitali kwa kunyimwa huduma au kupewa huduma duni.​
 
waandishi wetu wa habari hawana huo uwezo wa kuhoji hiki ulichokiandika hapa
Kipindi cha Magufuli alitaka waandishi wote wa habari wawe na degree na bodi ya kuwasajili ya taaluma yao na kuwasimamia utendaji wao Kama mainijinia,madaktari,manesi mswada ukaandaliwa wakapinga kafa haujapita

Matokeo ndio haya sasa

Tanzania hatuna waandishi wa habari tuna Reporters wa habari wa ku ripoti tu Raisi kasema nini,NHIF wamesema nini nk.,

Ni Reporters tu

Kazi ambavyo bwege yetote aweza fanya hata bila kwenda chuo cha uandishi wa habari hata mkulima aweza kuwa Reporter wa habari hata panya Road aweza

Hawezi shindwa ripoti kilichotokea au ambacho raisi,au mbunge au mbowe au Lisu au Lema kasema
 
Waondikane na nfuno huo, wawape madhirika binafsi ya bims ya uendeshe uone kama yatatokea huko yanayotojea hili shirika la serikali.

Serikqli haiwezi kuendesha biashara yoyote ile.
 
Taasis za kifedha zilivyo nyingi hivi bado taasis na mashirika ya umma yanakopesha wafanyakazi wake?
 
Lau kama ningekuwa na dawa ya kuwaloga mafisadi, wabadhiriifu,wezi na wazembe wa fedha za umma basi ningefanya hivyo haraka kabla ya kusubiria Kamati za Bunge zikae na kujadili ripoti ya CAG na Kisha kutoa mapendekezo mwakani 2024!!!!!

naumia sana moyo
 
Kwahiyo anachosema mama Mziray ni kwamba CAG ni muongo, maana naona kakanusha kila taarifa iliyotolewa na CAG. Na kama hayo maswali yote yalikua na majibu hayo aliyotaja, kwanini hakuyampa CAG ili hizo hoja ziondolewe kwenye ripoti?
Hoja ndio zinajibiwa sasaivi, isiyopata majibu sahihi haifutwi inafikushwa bungeni na mahakamani kama ikibidi. Kila kitu kinajibiwa kwa time frame, auditing haiingiliwi kwamajibu ya papo kwa papo.
 
Inasikitisha mnoo,sijui ni kiongozi gani atakuja kulikomboa hili taifa letu la Tanzania
 
Naomba kufahamishwa vizuri. CAG anasema: wafanyakazi wa mfuko wamejikopesha hizo fedha mabilioni ya shilingi, gharama zinazolipwa, hasa kwa hospitali binafsi ni kubwa kuliko uhalisia, mfuko umelipa madawa yaliyoisha muda etc... Sasa wao solution wanasema watanzania wote waingizwe kwenye huu mfuko (NHIF), how? Yaani una wanachama milioni 2 kwa mfano kwenye huo mfuko but umeshindwa kuzikabili changamoto za watu milioni mbili, sasa itawezekanaje kuwamudu watu milioni 60??
 
Hawa VIONGOZI wanyonyaji wanataka kuleta bima ya afya kwa wote.!! ??

Bima ya Afya kwa wote lengo lake ni kuukoa mfuko kama ilivyo kwa KIKOKOTOO.
Mimi ndiyo ninaposhangaa kwamba CAG anasema huu mfuko kwa hawa wanachama wachache na michango yao michache tuu ubadhirifu ni mkubwa, je bima ya afya kwa wote hayo mabilioni au Trilioni si ndiyo watajipigia Mpaka wavimbiwe??
 
Chief acha ujinga😂😂😂😂, mimi sihusiki na NHIF, maisha yangu na ajira wapi na wapi!
Umeamua kuwaruka siyo. Zingatia hoja zetu hawa jamaa ni bomba la kutuibia wala si vinginevyo:

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…