CAG na waliojikopesha Sh41 bilioni NHIF

CAG na waliojikopesha Sh41 bilioni NHIF

changamoto za mfumo wa bima ya afya nchini hasa wa umma haziwezi kupata suluhu kwa kubadilisha bodi au menejiment Au wafanyakazi bila kujua kiini cha tatizo.

Mfumo wa bima ya afya lazima uboreshwe kwa kuweka sera au sheria ambayo itaweka mazingira kwa kila mtanzania kushiriki kuchangia bima ya afya.

Duniani kote hakuna mfumo wa bima ya afya unaoweza ku survive kwa kutegemea wanachama wanaojiunga kwa hiari wakiwa tayari ni wagonjwa.

Suluhu ni kuwa na sheria ya bima ya afya kwa wote au kuondoa makundi yote ya hiari na mfuko kubaki na watumishi wa Umma tu. Kuhusu mikopo, NHIF ni taasisi ya umma inayoendeshwa bila kutegemea ruzuku kutoja Serikalini , mikopo inayotolewa kwa wafanyakzi wake ni sehemu ya motisha kwa wafanyakazi kama ilivyo kwa watumishi wengine wa taasisi za umma na binafsi. Mapato yatokanayo na riba ya mikopo hiyo ya wafanyakazi huwezesha mfuko kupata mapato ya ziada na kujiendesha na kuboresha huduma kwa wanufaika wake.
Kwani utaratibu wa sasa ukoje? Mtoto akiwa mdogo au shule anasajiriwa akiwa akiwa mzima wala si mgonjwa, same kwa mfanyakazi na wategemezi wake wote wanakuwa sio wagonjwa. Hata hivyo ukijiunga kama mwanacha binafsi kuna kusubiri miezi kadhaa kabla hujaanza kutumia baadhi ya huduma.

Mkuu hapa tatizo ni kwenye matumizi ya mfuko ndio hakuna udhibiti sababu ya upigaji na 10%. Kama watu wanalipa huduma hewa unatarajia nini? Watu wanajikopesha hela za wanachama unategemea nini?

Tena unashauri watu wajiunge wote ili michango iwe mingi mtupige vizuri?
 
MPAKA SASA HAKUNA ENEO AMBALO SISI WEUSI TUNALIFANYA KWA UKAMILIFU NA USAHIHI.
SIASA
UCHUMI
JAMII
UTAWALA/USIMAMIZI
TECKNOLOJIA
ELIMU
IMANI

VYOTE HIVI NI MPAKA KWA USIMAMIZI WA MTU MWEUPE NDIO UFANISI UONEKANE
 
Kwani ni NHIF pekee yake ndio inajikopesha? Au mna agenda binafsi, nendeni Kwingine pia muone mikopo inavyotolewa na mikopo hiyo mbona ina riba? Au hilo hamlioni?
Hata kama taasisi zingine zinajikopesaha but kwa NHIF hawawezi kujukopesha kwa michango ya watumishi ya matibabu aiseeee. It doesn't make any sense..
 
Mbna NHIF walishatolea ufafanuzi hilo suala, acheni Serikali ifanye kazi yake. Mwananchi nao ni changamoto
Yaani unategemea aliyejikopesha 41 billion za members atoe ufafanuzi wa maana kumzidi CAG??
 
changamoto za mfumo wa bima ya afya nchini hasa wa umma haziwezi kupata suluhu kwa kubadilisha bodi au menejiment Au wafanyakazi bila kujua kiini cha tatizo.

Mfumo wa bima ya afya lazima uboreshwe kwa kuweka sera au sheria ambayo itaweka mazingira kwa kila mtanzania kushiriki kuchangia bima ya afya.

Duniani kote hakuna mfumo wa bima ya afya unaoweza ku survive kwa kutegemea wanachama wanaojiunga kwa hiari wakiwa tayari ni wagonjwa.

Suluhu ni kuwa na sheria ya bima ya afya kwa wote au kuondoa makundi yote ya hiari na mfuko kubaki na watumishi wa Umma tu. Kuhusu mikopo, NHIF ni taasisi ya umma inayoendeshwa bila kutegemea ruzuku kutoja Serikalini , mikopo inayotolewa kwa wafanyakzi wake ni sehemu ya motisha kwa wafanyakazi kama ilivyo kwa watumishi wengine wa taasisi za umma na binafsi. Mapato yatokanayo na riba ya mikopo hiyo ya wafanyakazi huwezesha mfuko kupata mapato ya ziada na kujiendesha na kuboresha huduma kwa wanufaika wake.
1. Hii hoja ya kutaka kila Mtanzania awe member wa NHIF mnaipenda sana kuizungumzia, lakini mimi najiuliza hizi fedha kidogo tuu za wanachama wachache CAG ameripoti ubadhirifu mkubwa mnooo, sasa ndiyo Mtaweza kweli kusimamia fedha za watanzania wote nyie kweli?? 2. Unadai kukopeshana ni motisha kwa wafanyakazi wa NHIF really?? Mbona serikali imetoa motisha watumishi kukopa benk kwa dhamana ya mishahara yao? Kama ni kukopeshana basi ingetakiwa na wanachama wenye fedha wakopeshwe basi. Je mifuko ya jamii kama NSSF na PSSSF nao wanakopeshana? Nimeuliza hapo juu sheria iliyounda NHIF inaruhusu kukopeshana? Kama inaruhusu basi na wachangiaji wawe wanakopeshwa tuone kama huo mfuko utakuwa na pesa za kutibia wanachama.
 
Sio kila kitu ni ubadhilifu. Mikopo ya watumishi iko kila mahali na ina utaratibu wake wa kurejesha. Huu kama ni ubadhilifu mamlaka zitachukua hatua stahiki
Nendeni Benki huko mkakopeshwe bwanaaa, acheni fedha za wanachama. Hivi mfano mwalimu, nesi, bwana shamba, polisi na wengineo wao siyo wafanyakazi? Hawachangii NHIF? Mbona wao hawakopeshwi pesa zao? Kwani nyie mna kitu gani special cha kufanya mkopeshwe michango ya wanachama?
 
NHIF wanafanya biashara? Maana utasema hata muhimbili, Amana hodpitaly nazo wapewe watu binafsi
Kuna jamaa hapo juu kasema wanakopeshana ili wapate interest na waizungushe, hiyo si ni biashara?? Ukimkopesha mtu milioni moja na akarudisha milion moja na laki moja hiyo si ni biashara?
 
Yaani unategemea aliyejikopesha 41 billion za members atoe ufafanuzi wa maana kumzidi CAG??
Lilishaisha broo[emoji23][emoji23][emoji23], hii hoja mbona ilishafungwa. Mtanzania ni mtu mmoja mbishi. CAG anachunguza ubadhirifu ikiwemo na kama ukiukwaji wa process.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna jamaa hapo juu kasema wanakopeshana ili wapate interest na waizungushe, hiyo si ni biashara?? Ukimkopesha mtu milioni moja na akarudisha milion moja na laki moja hiyo si ni biashara?
[emoji23][emoji23][emoji23] ushawahi kufanya kazi katika taasisi boss wangu. Dah! [emoji23][emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
We watu wamekula harafu unawaambia wajitee ,poor tanzania
 
Majamaa yameitana humu yanatetea kujikopesha na kuua mfuko!

Same trend as NSSF yanajikopesha hela zetu alafu wanaanza kuleta vijisababu, kama mfuko unashindwa ku perform rationale ya kujikopesha inatoka wapi? Si mkakope kwenye commercial banks!

Imagine mmeshindwa management ya hela za watumishi, je ikiwa kila
Mwananchi mtaweza? Aibu hii
 
Back
Top Bottom