Ondoa hii zana.
Itakurudisha nyuma.
----------
C & P
Imeandikwa na: Makirita Amani
Macho Ya Wengine Ndiyo Yanayokutesa...
Kama ungekuwa unaishi porini, wewe peke yako na hakuna mtu mwingine yeyote unayekutana naye, unafikiri ungesumbuka kama unavyosumbuka sasa.
Unafikiri ungejali sana kwamba unavaa nini, unaendesha nini, unakaa wapi na hata unafanya nini?
Kwa hakika usingesumbuka, ungeweka mkazo wako kwenye nini ufanye ili uendelee kuwa hai.
Macho ya wengine ndiyo yanayokutesa, kutaka kuwaridhisha wengine ndiyo kunakufanya uwe na maisha magumu.
Kujilinganisha na wengine, kutaka na wewe uonekane upo au unaweza kufanya vitu fulani ndiyo kunakufanya uwe mtumwa kwenye maisha yako.
Watu wengi wanaoingia kwenye mikopo isiyozalisha, huwa siyo kwa ajili yao, bali kwa ajili ya wengine, kutaka nao waonekane wapo.
Tafakari hili kwenye kila unachojisukuma kufanya, jiulize je unafanya kwa ajili yako au ili uonekane na wengine. Kama msukumo pekee ni uonekane na wengine, basi jua unajitesa, unaacha kuishi maisha yako na mbaya zaidi, hao unaofanya vitu kwa ajili yao, wala hawajali sana kuhusu wewe.
Chagua kuishi kwa ajili yako, chagua kufanya yale ambayo ni muhimu zaidi kwako na fanya kwa umakini na usahihi. Usijitese kwa ajili ya wengine.