Case File 1: Mwanaume aliyekodi watu ili kumuua mkewe wakiwa Honeymoon (True Story) Part 1

Case File 1: Mwanaume aliyekodi watu ili kumuua mkewe wakiwa Honeymoon (True Story) Part 1

Sehemu ya Tatu

Baada ya kesi kuendeshwa kwa muda nchi Afrika kusini mwendesha Mashtaka akawaahidi Umzi Wamamdodo na dereva taxi Zola Tongo kuwa iwapo watakiri kosa na kutoa ushahidi dhidi ya Shren Dewani basi watapunguziwa adhabu.
Kwa upande mwingine Monde Mbombo yeye akahaidiwa msamaha kamili iwapo pia atatoa ushahidi wa kutia hatiani Shren Diwani. Kiufupi ni kwamba mwendesha mashtaka alitaka kutumia kila mbinu kumtia hatiani Shren Diwani.

Tarehe 7 Desemba 2010, dereva tax Zola Tongo akafikifishwa katika mahakama kuu ya Western Cape, akakiri makosa ya kuiba kwa kutumia silaha, kuteka na kuhusika katika mauaji ya Ani Hindocha lakini akaongeza kwa kusema alifanya yote haya akishirikiana na mume wa Ani anayeitwa Shren Diwani. Mahakama ikampa Zola Tongo adhabu ya kifungo cha miaka 18 jela na akapelekwa katika gereza la Malmesbury.

Tarehe 18 February 2011 Umzi Wamadodo akahukumiwa kifungo cha miaka 25 kwenda jela kwa kosa la kuteka, kupora na kuua.

Tarehe 19 February 2012 baada ya kesi kuendeshwa kwa muda mrefu mtuhumiwa mwingie Kolile Mngeni naye akatiwa hatiani na kuhukumiwa kifungo cha maisha jela.

Tarehe 14 Julai mwaka 2014 Kolile Mungeni akiwa anatumikia kifungo cha maisha jela ikagundulika kuwa anaugua kansa ya ubongo, wamasheria kadhaa wakaomba apatiwe msamaha lakini mahakama ikakataa ombi la hilo.
Tarehe 18 Oktoba mwaka 2014 Kolile Mungeni akafariki katika gereza la Goodwood.

Turudi kwa Shren akiwa London, Uingereza

Tarehe 12 Agosti 2013 kijana mmoja wa kiume amwenye umri wa miaka 25 akajitokeza na kudai kuwa ana mahusiano ya kimapenzi na Shren Diwani, baada ya taarifa hizi kuandikwa gazetini, Shren na familia yake walikana lakini baadaye yule kijana akaachia meseji na picha zilizothibitisha kuwa walikuwa na mahusiano ya kimapenzi ya jinsia moja.
Baada ya taarifa hizi ikawa wazi kwamba Shren alioa kwa sababu ya shinikizo la wazazi na ndugu zake lakini alikuwa ni tu wa mapenzi ya jinsia moja yaani jamaa alikuwa Gay (shoga).
Hii ikawa taarifa mbaya zaidi kwa familia ya Diwani na familia ya mzee Vinod Hindocha, maana sasa ilikuwa wazi kuwa mauaji yalipangwa ili kuficha ukweli huu wa Shren kuwa shoga na hakuwa mwanamume kamili.

Hili halikuwa tatizo kwa Shren kwa sababu nchini Uingereza kuwa shoga au kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja sio kosa kisheria.

Tarehe 1 Mei mwaka 2014 Mahakama ya Afrika kusini ikatuma ombi kwa idara ya usalama ya Uingereza kuomba Shren Diwani, apelekwe Afrika kusini kujibu tuhuma za kupanga mauaji ya mke wake Ani Hindocha.
Baada ya majadiliano na maombi kadhaa ya Shren kuomba asipelekwe Afrika Kusini hatimaye tarehe 7 April 2014 Shren Diwani akapandishwa ndege na maafisa wa Uingereza kupelekwa Afrika kusini kujibu tuhuma zake.
Alipofika tu uwanja wa ndege wa Cape Town, alikamatwa na maafisa wa Afrika kusini na kuweka rumande kwa tuhuma za makosa ya kupanga njama za kumuua mkewe, unyanganyi na kuzuia ushahidi muhimu katika kesi.

Shren Diwan kwa ujasiri kabisa akakataa makosa yote licha ya kuonyeshwa ushahid kutoka kwa dereva tax na Umzi Wamadodo.

Kesi ya Shren Diwani ikaanza kusikilizwa tarehe 6 Oktoba 2014 katika mahakama kuu ya Cape Town chini ya Jaji maarufu Traverso, Shren alikuwa anatetewa na wanasheria wa kimataifa katika kesi hiyo.
Wakati kwa maswali kwa mashahidi ambao ni Umzi Wamadodo, dereva Tax Zola Tongo, wakajichanganya katika mpangilio wa tukio. Wakati Zola Tongo akidai kuwa aliambiwa na Shren kutafuta mtu wa kumuua mkewe, Umzi Wamadodo alisema yeye alipewa taarifa za kumteka tu Ani na sio kuua. Hilo likawa kosa kubwa sana lilioathiri mwenendo mzima wa kesi. Mawakili wa kimataifa kutoka Uingereza wakapeleka ombi kwa Hakimu Traverso.
Tarehe 24 Novemba mwaka 2014 Jaji Traverso akaiambia mahakama kuwa hakuna ushahidi wa kutosha unaomhusisha moja kwa moja Shren Diwani katika utekwaji wa gari na kifo cha mkewe Ani Hindocha. Kufikia hapo Mahakama kuu ya Cape Town ilikuwa imeamua kuwa Shren Diwani hana kesi ya kujibu, hivyo yupo huru.

Baada ya maamuzi haya watu wengi na mashirika kadhaa yalilaumu uamuzi wa Jaji Traverso wakidai kuwa Jaji ameamua kwa makusudi kumuachia mtu aliyepanga mauaji ya mke wake katika ardhi ya Afrika Kusini.

Familia ya Ani Hindocha, ilijaribu mara kadhaa kufungua shauri na mashtaka kwa Shren Diwani lakini polisi na mwendesha mashtaka walikataa kwa kuwa hakukuwa na ushahidi wa kutosha kumtia hatiani Shren Diwani.

Shren alirudi London Uingereza kuendelea na maisha yake akiwa mtu huru kabisa, japo kwa sasa sio mtu anayeonekana kila mahali na inadhaniwa kuwa amehama kabisa nchi Uingereza.

Kauli ya mwisho kutoka kwa familia ya Ani Hindocha

Tarehe 4 Agosti 2018 familia ya Ani Hindocha kupitia kwa msemaji wa familia ikasema ‘’ tunakubali kuwa binti yetu ameshafariki, hakuna tunachoweza kufanya kwa sasa, tunajua kuwa Shren alihusika kwa namna moja ama nyingine, hii inatuumiza sana. Inasikitisha kwamba tulikubali binti yetu kuolewa na mtu ambaye alikuwa na maisha ya siri katika ushoga, ni maisha yake lakini hakupaswa hata kuja kuomba kumuoa binti yetu, tumeumia sana na tunastahili kuombwa japo samahani kutoka kwa Shren.’’

Mwisho.
 
Sehemu ya Tatu

Baada ya kesi kuendeshwa kwa muda nchi Afrika kusini mwendesha Mashtaka akawaahidi Umzi Wamamdodo na dereva taxi Zola Tongo kuwa iwapo watakiri kosa na kutoa ushahidi dhidi ya Shren Dewani basi watapunguziwa adhabu.
Kwa upande mwingine Monde Mbombo yeye akahaidiwa msamaha kamili iwapo pia atatoa ushahidi wa kutia hatiani Shren Diwani. Kiufupi ni kwamba mwendesha mashtaka alitaka kutumia kila mbinu kumtia hatiani Shren Diwani.

Tarehe 7 Desemba 2010, dereva tax Zola Tongo akafikifishwa katika mahakama kuu ya Western Cape, akakiri makosa ya kuiba kwa kutumia silaha, kuteka na kuhusika katika mauaji ya Ani Hindocha lakini akaongeza kwa kusema alifanya yote haya akishirikiana na mume wa Ani anayeitwa Shren Diwani. Mahakama ikampa Zola Tongo adhabu ya kifungo cha miaka 18 jela na akapelekwa katika gereza la Malmesbury.

Tarehe 18 February 2011 Umzi Wamadodo akahukumiwa kifungo cha miaka 25 kwenda jela kwa kosa la kuteka, kupora na kuua.

Tarehe 19 February 2012 baada ya kesi kuendeshwa kwa muda mrefu mtuhumiwa mwingie Kolile Mngeni naye akatiwa hatiani na kuhukumiwa kifungo cha maisha jela.

Tarehe 14 Julai mwaka 2014 Kolile Mungeni akiwa anatumikia kifungo cha maisha jela ikagundulika kuwa anaugua kansa ya ubongo, wamasheria kadhaa wakaomba apatiwe msamaha lakini mahakama ikakataa ombi la hilo.
Tarehe 18 Oktoba mwaka 2014 Kolile Mungeni akafariki katika gereza la Goodwood.

Turudi kwa Shren akiwa London, Uingereza

Tarehe 12 Agosti 2013 kijana mmoja wa kiume amwenye umri wa miaka 25 akajitokeza na kudai kuwa ana mahusiano ya kimapenzi na Shren Diwani, baada ya taarifa hizi kuandikwa gazetini, Shren na familia yake walikana lakini baadaye yule kijana akaachia meseji na picha zilizothibitisha kuwa walikuwa na mahusiano ya kimapenzi ya jinsia moja.
Baada ya taarifa hizi ikawa wazi kwamba Shren alioa kwa sababu ya shinikizo la wazazi na ndugu zake lakini alikuwa ni tu wa mapenzi ya jinsia moja yaani jamaa alikuwa Gay (shoga).
Hii ikawa taarifa mbaya zaidi kwa familia ya Diwani na familia ya mzee Vinod Hindocha, maana sasa ilikuwa wazi kuwa mauaji yalipangwa ili kuficha ukweli huu wa Shren kuwa shoga na hakuwa mwanamume kamili.

Hili halikuwa tatizo kwa Shren kwa sababu nchini Uingereza kuwa shoga au kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja sio kosa kisheria.

Tarehe 1 Mei mwaka 2014 Mahakama ya Afrika kusini ikatuma ombi kwa idara ya usalama ya Uingereza kuomba Shren Diwani, apelekwe Afrika kusini kujibu tuhuma za kupanga mauaji ya mke wake Ani Hindocha.
Baada ya majadiliano na maombi kadhaa ya Shren kuomba asipelekwe Afrika Kusini hatimaye tarehe 7 April 2014 Shren Diwani akapandishwa ndege na maafisa wa Uingereza kupelekwa Afrika kusini kujibu tuhuma zake.
Alipofika tu uwanja wa ndege wa Cape Town, alikamatwa na maafisa wa Afrika kusini na kuweka rumande kwa tuhuma za makosa ya kupanga njama za kumuua mkewe, unyanganyi na kuzuia ushahidi muhimu katika kesi.

Shren Diwan kwa ujasiri kabisa akakataa makosa yote licha ya kuonyeshwa ushahid kutoka kwa dereva tax na Umzi Wamadodo.

Kesi ya Shren Diwani ikaanza kusikilizwa tarehe 6 Oktoba 2014 katika mahakama kuu ya Cape Town chini ya Jaji maarufu Traverso, Shren alikuwa anatetewa na wanasheria wa kimataifa katika kesi hiyo.
Wakati kwa maswali kwa mashahidi ambao ni Umzi Wamadodo, dereva Tax Zola Tongo, wakajichanganya katika mpangilio wa tukio. Wakati Zola Tongo akidai kuwa aliambiwa na Shren kutafuta mtu wa kumuua mkewe, Umzi Wamadodo alisema yeye alipewa taarifa za kumteka tu Ani na sio kuua. Hilo likawa kosa kubwa sana lilioathiri mwenendo mzima wa kesi. Mawakili wa kimataifa kutoka Uingereza wakapeleka ombi kwa Hakimu Traverso.
Tarehe 24 Novemba mwaka 2014 Jaji Traverso akaiambia mahakama kuwa hakuna ushahidi wa kutosha unaomhusisha moja kwa moja Shren Diwani katika utekwaji wa gari na kifo cha mkewe Ani Hindocha. Kufikia hapo Mahakama kuu ya Cape Town ilikuwa imeamua kuwa Shren Diwani hana kesi ya kujibu, hivyo yupo huru.

Baada ya maamuzi haya watu wengi na mashirika kadhaa yalilaumu uamuzi wa Jaji Traverso wakidai kuwa Jaji ameamua kwa makusudi kumuachia mtu aliyepanga mauaji ya mke wake katika ardhi ya Afrika Kusini.

Familia ya Ani Hindocha, ilijaribu mara kadhaa kufungua shauri na mashtaka kwa Shren Diwani lakini polisi na mwendesha mashtaka walikataa kwa kuwa hakukuwa na ushahidi wa kutosha kumtia hatiani Shren Diwani.

Shren alirudi London Uingereza kuendelea na maisha yake akiwa mtu huru kabisa, japo kwa sasa sio mtu anayeonekana kila mahali na inadhaniwa kuwa amehama kabisa nchi Uingereza.

Kauli ya mwisho kutoka kwa familia ya Ani Hindocha

Tarehe 4 Agosti 2018 familia ya Ani Hindocha kupitia kwa msemaji wa familia ikasema ‘’ tunakubali kuwa binti yetu ameshafariki, hakuna tunachoweza kufanya kwa sasa, tunajua kuwa Shren alihusika kwa namna moja ama nyingine, hii inatuumiza sana. Inasikitisha kwamba tulikubali binti yetu kuolewa na mtu ambaye alikuwa na maisha ya siri katika ushoga, ni maisha yake lakini hakupaswa hata kuja kuomba kumuoa binti yetu, tumeumia sana na tunastahili kuombwa japo samahani kutoka kwa Shren.’’



Mwisho.
 
Kwahiyo Shren, licha ya ushahidi wote huu, amekuwa huru.

Nimeona hii kwenye best documentary za Panorama
 
e28a8d97c0cbc4395c7153ed61cc43e3.webp.jpg
7b8d12d7cace6c76c90c583bdcc411cc.webp.jpg
32aa770b83c14ae26de3b3bcf474fa40.webp.jpg


1.Shrien anaenda chumba cha internet
2.Zola Tongo mwenye Cap anamfata
3.Zola Tongo ameshavuta mpunga 1000 ZAR
 
Back
Top Bottom