Mambo ya mahakama ya kadhi ndo yanaanza hivyo muda si mrefu utasikia wanawake wajistili na hijab, unaambiwa hata huko misri au Chechnya waliaanza hivi hivi kwa kutoa visingizio ambavyo huonekana kukubalika na jamii but the real devil is underneath. Hao walinzi sheria ipi ya chuo au ya JMT inawapa mamlaka ya kuwazuia wanafunzi wa kike kuingia na kutoka chuoni kwa vigezo vya mavazi yao? je hao walinzi wamesomea wapi utaalam wa mavazi ya kike kuamua ipi inafaa na ipi haifai. First victims wa kadhi always ni wanawake, lakini hao wanawake ni dada zetu, mama zetu, shangazi, binti zetu, wake zetu na wachumba zetu kwa nini wanaume tujipe mamlaka juu yao??? Kuna vyombo mbali mbali hapa nchini vinavyoshughurika na masuala ya wanawake mfano wizara ya wanawake na watoto, UWT, NGOs nk badala ya kujichukulia sheria mkononi chuo kinabidi kiwasiliane na vyombo husika, wajibu wa chuo ni kufundisha wanafunzi na kama wanafail wajibu wao ni kufanya utafiti wa kina na kupeleka mapendekezo wizarani au kunakohusika, hii tabia ya mjinga mmoja mwenye madaraka kuamua jambo ambalo linahusu maisha ya maelfu ya watu litakuja kutu cost