Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Na hawa ndiyo magreat thinkers wetu wa siku hizi ambao chuki za udini zimewatawala kwa kila jambo hata pasipohusika!!Kuna mtu ameambiwa avae hijab kweli hapo?hivi unapajua CBE kweli wewe?umeshawahi kuwaona wanafunzi wa kike wanavyovaa?Nauhakika kama wewe ni mzazi usingethubutu kumruhusu mwanao wa kike avae vile,hebu vitu vingine jamani tuache ushabiki usio na kichwa wala miguu!!
Utandawazi upo sana tu lakini tunacopy vibaya,hata hao tunaowacopy hawavai nguo za namna hiyo wanapokuwa shuleni/vyuoni.Hivi dada zetu huwa mnakuwa comfortable kabisa na vile vinguo vyenu kweli?Naunga mkono kwa 100% uamuzi uliofikiwa na uongozi wa CBE juu ya mavazi,wasiishie Campus ya Dar peke yake waende mpaka Dodoma pia maana na ile imekuwa kama danguro la waheshimiwa kipindi cha vikao vya bunge!!
Mkuu umeshindwa kujibu hoja matokeo yake unaingia kwenye "character assassination" Sidhani kama hapa JF kuna vigezo ambavyo eti ndo standard ya great thinker, imekuwa desturi kwa baadhi ya members kama hawakubaliani na mawazo ya wenzao basi jibu lahisi ni kuhoji u great thinker wa wenzao, aibu!!!!
Tukirudi kwenye mada husika
1. CBE kama chuo kinaweza kuwa na mamlaka ya ku enforce a dressing code ndani ya mipaka ya chuo ila nina wasiwasi kama high learning institutions hapa bongo zina dressing code policy, hivyo uamuzi wa namna ya kuvaa umeachwa mikononi mwa wanavyuo wenyewe wa kike na wakiume, na hili ni jambo la kujivunia kwa sababu linawapa watu uhuru wa kuamua juu ya wanavyotaka kuishi maisha yao bila kuingiliwa na mamlaka au wahuni.
2. Kama CBE wamegundua kuwa uvaazi wa wanafunzi wa kike unachangia kutofaulu kwa wanafunzi (wakike? wakiume? wote?) basi jukumu lao ni kuripoti kwa vyombo husika na siyo kujiamlia wenyewe. Kuna mamia ya vyuo nchini vyenye wanafunzi wa kike na kiume je iweje CBE tu ndo wasifaulu kwa ajili ya mavazi na vyuo vingine visiathirike? hapa panahitaji utafiti wa kina sababu inaweza kuwa ni tofauti kabisa na mavazi, je kuna walimu wakutosha wenye qualification zinazostahili kufundisha hayo masomo au ni wale wa kuchakachua vyeti na udungunization? je kuna nyezo za kufundishia za kutosha? je wanafunzi wanapata mahitaji muhimu ya malazi, chakula, umeme, maji nk bila usumbufu au kuingilia utaratibu wa masomo yao? haya yote na mengineo ni lazima yaangaliwe kabla ya mjinga mmoja ku conclude na kutoa maamuzi ya kijinga
3. Enforcement of dressing code, kwanza kwa nini wasichana tu ndo wawe affected?? je hao walinzi wana uzoefu gani na mavazi ya kike ili waamue linalostahili na lisilostahili? Hapa unawapa walinzi nafasi ya kuchukua rushwa ya ngono au pesa kutoka kwa wanafunzi ili kuwaruhusu kutoka na mavazi wanayoyataka na suala zima ni unyanyasaji tu wa kijinsia!!!!
4. Mob justice - kuwahukumu wanafunzi wa kike kwa mavazi yao siyo sahihi hakuna tofauti ya kumkoromea msela mitaani mwizi! mwizi! mwizi! na kumsababishia mauti
5. Mahakama ya kadhi - nimelileta hili jambo kwa sababu ukiangalia mtitiriko mzima wa suala hili unashangaa, Tanzania ni secular country, haina sheria za mavazi au marality. Sasa inakuwaje uongozi wa chuo unajichukulia maamuzi kama haya?? kwa nini suala kama hili ambalo linagusa maisha ya maelfu ya watu liamriwe kiholela holela tu bila kutumia vyombo husika?? Nchi zenye sharia (kadhi) ndo mambo kama haya yanafanyika na kwa vile kuna wale wanaopenda tanzania pia ifuate taratibu hizo wanaweza kuwa wanaanza kujipenyeza kidogo kidogo na kupanda hizo mbegu za kadhi
6. Wale tunaoipenda nchi yetu na tunafurahia uhuru tulionao hivi sasa bila kujali itikadi za kiimani, tusikubali kuingiziwa taratibu tatanishi kama hizi kwenye sekta zetu za umma iwe kwenye mabenki, mashule, vyuoni, maofisini nk . Kuna usemi wa haba na haba ujaza kibaba, tusipokuwa makini sasa hivi tutakuja shtuka when is too late!!!
7. Ushauri wangu wa CBE na watanzania wote ambao tunakerwa na uvaaji wa vijana wetu ni kwamba tutumie sheria na vyombo vilivyopo, mawizara, NGOs, bunge nk ili tupate mwafaka wa suluhisho la hili tatizo badala ya kuwachia wale wenye ajenda za siri kutumia mwanya huo kwa lengo la kutimiza yale waliyokusudia. MUNGU IBARIKI TANZANIA
Mkuu , CBE si wa kwanza kufanya hichi kitu , St Joseph na wenyewe wanafanya hii mambo even though kwao dressing ipo kwa wote ie wavulana na wasichana , na ki ukweli ni utaratibu mzuri sababu unaleta unadhifu na umaridadi hata kama ni wakulazimishwa .
Pili , unaongea kama vile Tz hatuna moral standard katika mavazi yetu , kwa taarifa yako hata sheria za nchi zina discourage mavazi yasiyo endana na utamaduni wetu , na nani aliyekwambia sheria za KIKRISTO zinafurahia mavazi ya
ajabu hadi uanze kuhiusishanisha hiyo ban na mahakama ya kadhi.
Pole kwa kukasirika. uanzishwaji wa taasisi nyingi za serikali vyuo vya elimu vikiwemo vinaongozwa na kanuni, na nyingine zinakuwa zimeridhiwa na sheria za bunge. Chuo cha CBE kipo chini ya Wizara ya Biashara na Masoko. Pia kipo chini ya NACTE. Hivyo kanuni za mavazi yanayositiri maungo( ndiyo maneno swadakta ya kutumia) yapo wazi kwa taasisi zote za Tanzania. Makao makuu ya Jeshi pale Upanga huruhusiwi kuingia umevaa dengreez(jeans) au kitop, MP hakuruhusu kuingia. Maofisini huruhusiwi kwenda umevaa kandambili unless una cheti cha daktari ama una majeraha au una fungus. Ofisini huruhusiwi kwenda umejitanda khanga labda kama unaenda msibani unataka ruhusa kwa afisa utawala wako. Kujua nguo ipi si sahihi kuvaliwa mahala fulani haihitaji elimu ya shule ni ubingo tambuzi unaokuambia kuwa sasa umevaa nguo zisizistahili mahala hapo. Huwezi kuvaa OVER ROLL ukaenda kucheza mpira au huwezi kuvaa buktan ukaenda gereji.Mambo ya mahakama ya kadhi ndo yanaanza hivyo muda si mrefu utasikia wanawake wajistili na hijab, unaambiwa hata huko misri au Chechnya waliaanza hivi hivi kwa kutoa visingizio ambavyo huonekana kukubalika na jamii but the real devil is underneath. Hao walinzi sheria ipi ya chuo au ya JMT inawapa mamlaka ya kuwazuia wanafunzi wa kike kuingia na kutoka chuoni kwa vigezo vya mavazi yao? je hao walinzi wamesomea wapi utaalam wa mavazi ya kike kuamua ipi inafaa na ipi haifai. First victims wa kadhi always ni wanawake, lakini hao wanawake ni dada zetu, mama zetu, shangazi, binti zetu, wake zetu na wachumba zetu kwa nini wanaume tujipe mamlaka juu yao??? Kuna vyombo mbali mbali hapa nchini vinavyoshughurika na masuala ya wanawake mfano wizara ya wanawake na watoto, UWT, NGOs nk badala ya kujichukulia sheria mkononi chuo kinabidi kiwasiliane na vyombo husika, wajibu wa chuo ni kufundisha wanafunzi na kama wanafail wajibu wao ni kufanya utafiti wa kina na kupeleka mapendekezo wizarani au kunakohusika, hii tabia ya mjinga mmoja mwenye madaraka kuamua jambo ambalo linahusu maisha ya maelfu ya watu litakuja kutu cost
Kutoka na vitendo vya ngono kushamili chuo ya biashara CBE Dsm. Namatokeo mabaya wa wanafunzi wa kike . NImarufuku kuvaa suluari za mchina zinazobana na kuonyesha maumbile yake.NImarufuku kuvaa siketi fupi .Nimarufuku kuvaa nguo inayobana mwili . Kazi hiyo wamepewa walinzi wagetini hakuna kupita kama umevaa tofauti na Tangazo hilo