Continental Ground
JF-Expert Member
- Jun 16, 2016
- 1,907
- 3,895
Bado tupo zama za mawe
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Naona mafuriko ya Mama yamewavuruga kabisa akili wapinzani na kubakia kutapatapa tu.
Endelea na ushabiki, mimi sipo huko.Naona mafuriko ya Mama yamewavuruga kabisa akili wapinzani na kubakia kutapatapa tu.
Nimeona hii inafanyika maeneo mengi anapopita Rais, sasa hapa sasa lengo huwa ni kumdanganya nanii? Je? Rais, wananchi, vyombo vya habari au nani?
Watoto darasa la 5,6,7 na wanafunzi wa sekondari na vyuo wanabebwa na malori,wengine na mabasi kutoka maeneo mbali mbali hata kama ni siku za masomo.
Watoto wanaahirishiwa masomo kwa ajili ya kubebwa kwenda kwenye mkutano wa Rais ,hii maana yake ni nini hasa? Huu ni ujinga ulio pitwa na wakati kabisa na unakiuka misingi ya haki.
Kabla ya mimi kumaliza shule hiyo ilikuwa taratibu tunarudishwa shule nakuambiwa twende kwenye mikutano ya ccm. Hata usiwe na picha hiyo ndio hali halisi labda ukatae tu kwa ubishi.Tuma picha ili kuthibitisha hoja yako