LGE2024 CCM Arusha: Mgombea Serikali za Mitaa lazima awe na kazi ya kufanya inayomuingizia kipato halali la sivyo ataufanya Uenyekiti ndio kazi

LGE2024 CCM Arusha: Mgombea Serikali za Mitaa lazima awe na kazi ya kufanya inayomuingizia kipato halali la sivyo ataufanya Uenyekiti ndio kazi

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu, mambo yanazidi kunoga, kwani hawa ambao tunaenda na wanatudai hizi hela za 'copy' si ni wenyewe hawa hawa CCM? Au anaongelea watu gani? Maana wao ndio walipita kwa 99% bila kupingwa!

===

"Mgombea ni lazima awe na kazi ya kufanya inayomuingizia kipato halali kinachomuwezesha kuishi na hapa ni muhimu sana watu wangu wa Makiba. Mkiteua Mwekiti ambaye hana kazi ya kufanya inayomuingizia kipato kuendesha Maisha yake, maana yake ataufanya Uenyekiti ndiyo kazi.

"Akifanya Uenyekiti wa Kijiji ndiyo kazi muhuri mnagongewa kwa 1500, maeneo yenu hayako salama, atakuwa dalali wa hizo ardhi kwasababu mlimteua mtu ambaye hana kipato kinachomtosheleza kuendesha Maisha yake, ndiyo maana akaufanya Uenyekiti ndiyo kazi na kupitia ile kazi lazima apate kipato kinachomuwezesha kuendesha Maisha yake."


Msije mkamteua Yahaya kama alivyosema Lady JD, hajulikani yuko wapi, anafanya nini na anaishi wapi.



Pia soma:
~ Yanayojiri kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha - Novemba 27, 2024
~ Ally Hapi: Vyama vingine ni watoto shughuli za watu wazima hawataziweza, uchaguzi serikali za mitaa Isaka Kahama chagueni CCM
 
Kwa wenyevit wa mjini hilo gumu sana muda mwingi anatakiwa na wananch mf kuwajazia fomu na kuwaandikia barua za dhamana ya mkopo, dhamana za polisi& na mahakama, kusuluisha kesi mbalimbali sasa ukishakuwa bize na biashara yako lazima mtaa au kijiji kikushinde na kwa kushindwa kutatua kero za wananchi
 
Back
Top Bottom