Elections 2010 CCM demokrasia zaidi 2010 kumekucha!!!

Elections 2010 CCM demokrasia zaidi 2010 kumekucha!!!

Kura zitaendelea kununuliwa na wagombea kwa kutumia mawakala wao. Hapa wamewaongezea gharama wagombea wao. Njia nzuri ya kuwapata wagombea safi pamoja na kura hizi za wanachama ni kwafahamu kwa undani wagombea wetu na mema na mabaya yao yakawekwa hadharani. Vinginevyo tuendelee kutumia umasikini wa wapiga kura wetu kushinda kwa kishindo.

Mkuu WildCard, unapofanya uamuzi wa kuleta demokrasia, sio kwamba suala la rushwa litaondoka kabisa, lakini ni mojawapo ya mbinu ya kulipunguza. Kuongeza wigo wa wapiga kura ni jambo zuri, kuliko watu wachache waliokuwa wanatoa maamuzi ya wanachama kibao. Kununua kundi dogo ni rahisi kuliko watu kibao.

Unapozungumzia njia nzuri ya kuwapata wagombea kwa kujua mema na mabaya yao, ni wazo zuri. Lakini hata chaguzi zilizopita kuna watu walijulikana mabaya yao na wakapitishwa kugombea, huenda sababu ya rushwa. Hivyo kuongeza wapiga kura kwa hizi hatua za mwanzo ni wazo jema kabisa.

Kwa hili nawapa CCM hongera kubwa sana. Ila jitahidini basi mkiwekana sawa ndani ya CCM mtupe na tume ya uchaguzi huru, ndio uchaguzi utanoga.
 
Nimefurahi kuliko!

Nilishanena humu ndani kuhusu demokrasia ndani ya chama chetu mtanzania😀
CCM!
Kweli huu ni mpito mzuri kabla ya 2010 na 2015 kwani wameona itakuwa vigumu kupata wanachama wanaochagulika kiufiadi-fisadi🙄

Nafikiri hili linabidi lifurahiwe na Watanzania wote.😎

Kidumu!

Sura-ya-Kwanza,

Wacha nikakate kadi yangu ya ganda la kijani, tayari kwa mapambano 2010. Kwa mtindo huu mpya nina chance ya kuuza sera zangu na wananchi wakanielewa.

Rushwa bado itaendelea kutumika ingawaje nafikiri kwa utaratibu huu effect yake inaweza isiwe kubwa. Pia kuzungukia jimbo zima kutatoa nafasi kwa usanii kuibuliwa nje ili wananchi wajue.

Kwenye uchaguzi wa rais, kwani ni lazima mgombea urais naye atembelee kila kijiji? Ingetosha kutembelea kila wilaya na wajumbe wangepiga kura pamoja.

Labda kama alivyosema Yebo Yebo, hii ingelikuwa mabadiliko makubwa mno kufanywa kwa pamoja. Labda wakiona utaratibu huu unafaa, basi 2015 hata urais unaweza kuingizwa.

Wacha nianze kuandaa sera za kushinda Kajunjumele kwa wakwe zake Ogah! kwi kwi kwi!!!
 
Haya mabadiliko hata kuwa na maana iwapo wale wote wenye kutuka kuleta hayo mabadiliko (wapiga kura katika matawi) kuwa wanachama HAI wa CCM. Tutapiga kelele lakini kama hatutafanya mambo ya msingi (kuwa wanachama hai) mabadiliko hayatatokea. Muda ni sasa kwa sababu nadhani moja ya msharti itakuwa lazima uwe mwanachama labda kati ya meizi sita mpaka mwaka (kukwepa mamluki).
 
Sura-ya-Kwanza,

Wacha nikakate kadi yangu ya ganda la kijani, tayari kwa mapambano 2010. Kwa mtindo huu mpya nina chance ya kuuza sera zangu na wananchi wakanielewa.

Rushwa bado itaendelea kutumika ingawaje nafikiri kwa utaratibu huu effect yake inaweza isiwe kubwa. Pia kuzungukia jimbo zima kutatoa nafasi kwa usanii kuibuliwa nje ili wananchi wajue.

Kwenye uchaguzi wa rais, kwani ni lazima mgombea urais naye atembelee kila kijiji? Ingetosha kutembelea kila wilaya na wajumbe wangepiga kura pamoja.

Labda kama alivyosema Yebo Yebo, hii ingelikuwa mabadiliko makubwa mno kufanywa kwa pamoja. Labda wakiona utaratibu huu unafaa, basi 2015 hata urais unaweza kuingizwa.

Wacha nianze kuandaa sera za kushinda Kajunjumele kwa wakwe zake Ogah! kwi kwi kwi!!!


Zoezi likifanywa vizuri maana yake ni kwamba mgombea uraisi wa 2015 na kuendelea akiwa mmoja wa Wabunge ni lazima atakuwa amepitia kwenye mchujo huu kutoka kwenye matawi.

CCM ilivyo sio raisi mgombea Uraisi asiwe Mbunge. Ikiwa hivyo, huenda hakuna haja ya Raisi kupitia kwenye mchujo kama huu tena.
 
Lazima kuwe na njia ya kuokoa jahazi, 2010 ujanjaujanja na wizi wa kura hautafanya kazi sana kama before. Kwa Zanzibar huenda itakuwa usual, nguvu.
 
waheshimiwa naona demokalasia inakua kwenye chama cha mapinduzi ccm.hongela mwenyekiti na wajumbe.sasa kambi ya upinzani ina mkakati gani?kwa sababu wana ccm wameanza kukomalia majambazi yanayojitokeza kugombea labuda mambo yatakuwa bomba.
 
Ha ha ha ,wameiba utamaduni wa CUF , ila sikio la kufa halisikii dawa ,utamaduni huo utawamaliza wafuasi wa Sultani CCM kiulaini kabisa ,tupo hapa hapa ,msije mkasahau tu.

CCM kwishaa , yaani mkiziba huku kunatoboka kwengine ,huko kwenye mashina na matawi ndio msikuchezee kabisa maana wafuasi wa CCM sio watagawika mafungu bali watajua wapi pa kupeleka kura zao.

Hilo litammaliza SUltani CCM na kujikuta hoi bin taaban ,ila kitu kimoja ambacho kitamsaidia Sultani CCM ni kutumia vyombo vya dola kupora kura na pia kuitumia tume kubadilisha matokeo kwa hayo ndio yaliyobaki kwa Sultani CCM.

Sasa kwa mfumo huo naona nguvu za wananchi zinaweza kutumika kama kule Pemba na kuzishinda mbinu za Sultani CCM kutumia vyombo vya dola.
 
sasa ni kujipanga tu na kwenda kuuza sera.wale miungu watu wa wilayani waliokuwa na mchezo wa kuweka zengwe na kukata majina ya watu bila sababu za msingi sasa wamekwisha.
tujitokeze kwa wingi vijana 2010!
 
CCM mwendo mdundo!

Kwa mikakati hii itawachukua Upinzani muda mrefu kushinda uchaguzi!

Uchaguzi mwakani vipi mbona hadi sasa cheche na mikakati ya Upinzani hatujaona?
 
CCM mwendo mdundo!

Kwa mikakati hii itawachukua Upinzani muda mrefu kushinda uchaguzi!

Uchaguzi mwakani vipi mbona hadi sasa cheche na mikakati ya Upinzani hatujaona?

Hujasikia au hutaki kusikia ,Sultani CCM ameshaamrisha wafuasi au mamluki ambao huwavutisha bangi na kuwapikia sufuria la ugali na maharage kisha kuwavisha fulana nyekundu na kuenda kuwashambulia wanajiandikisha kumpinga , si umesikia ya Magogoni kushinda Kiteto.Lakini wananchi waliochoka na utawala wa Sultani CCM na mafisadi wake wanasema Sultani CCM hawampi kura zao hata akitembeza risasi za moto.
 
Hujasikia au hutaki kusikia ,Sultani CCM ameshaamrisha wafuasi au mamluki ambao huwavutisha bangi na kuwapikia sufuria la ugali na maharage kisha kuwavisha fulana nyekundu na kuenda kuwashambulia wanajiandikisha kumpinga , si umesikia ya Magogoni kushinda Kiteto.Lakini wananchi waliochoka na utawala wa Sultani CCM na mafisadi wake wanasema Sultani CCM hawampi kura zao hata akitembeza risasi za moto.

Kama kawaida yako,kila siku kubwabwaja tu sultani CCM,sultani CCM.Mwageni sera watu wawachague badala ya shutuma za kila siku zisizo kuwa na maana.Wenzenu CCM tayari washaanza mikakati ya ushindi mwakani(ikiwa ni pamoja na huu unaolenga 'kukisafisha' chama).Utakalia hayohayo ya Sultani CCM,Sulatni CCM na 2010 ndo hiyoooo inakaribia...Otherwise CCM itaendelea kuwa 'pamwanya'
 
Mzalendohalisi,

Hii ni habari nzuri sana. Waliokuwa wamezoea kuwahonga wajumbe, sasa kama wana pesa wahonge wilaya nzima.

Hii naona itakuwa kama ilivyo kura ya maoni USA. Itafanya wanaowania nafasi sera zao zilijulikane vizuri kwa wananchi na sio udanganyifu na usanii wa siku moja kwenye mkutano wa uchaguzi.

Mimi ningetaka utaratibu huu utumike hata kwenye kumpata mgombea urais wa chama. Na yeye apigiwe kura za maoni na wanachama wote wa CCM.

Mnaowania 2010 jiandaeni vizuri maana ngoma itakuwa nzito hasa! Unaweza kufanya usanii siku moja lakini kufanya usanii kwenye viijiji au kata 50 sio rahisi sana.

Mtanzania,

Inasemekana umeshaanza "kampeni" hata kabla ya filimbi kupigwa 🙂 ..... Nakubaliana nawe kwamba uamuzi huu, kama utatekelezwa vizuri utaimarisha demokrasia kwa kutupatia viongozi wanaostahili.
 
Ha ha ha ,wameiba utamaduni wa CUF , ila sikio la kufa halisikii dawa ,utamaduni huo utawamaliza wafuasi wa Sultani CCM kiulaini kabisa ,tupo hapa hapa ,msije mkasahau tu.

CCM kwishaa , yaani mkiziba huku kunatoboka kwengine ,huko kwenye mashina na matawi ndio msikuchezee kabisa maana wafuasi wa CCM sio watagawika mafungu bali watajua wapi pa kupeleka kura zao.

Hilo litammaliza SUltani CCM na kujikuta hoi bin taaban ,ila kitu kimoja ambacho kitamsaidia Sultani CCM ni kutumia vyombo vya dola kupora kura na pia kuitumia tume kubadilisha matokeo kwa hayo ndio yaliyobaki kwa Sultani CCM.

Sasa kwa mfumo huo naona nguvu za wananchi zinaweza kutumika kama kule Pemba na kuzishinda mbinu za Sultani CCM kutumia vyombo vya dola.
Utakalia hayohayo ooh mara wameiba utamaduni wa CUF mara sijui nini,cha msingi sasa hivi ni nyie kujipanga upya na kujiandaa kwa mechi ya mwakani,maana katika hali halisi CUF ndo wako hoi bin taaban now,msipongalia hata NCCR,TLP,UDP na vyama vingine vidogo vitawa'overtake'.Kaeni chini mjipange upya..Kwa hali ilivyo sasa msipoangalia hata Mtaji wenu wa PEMBA utapigwa ile inaitwa Sandakalwe Amina,mwenye kupata apate
 
Who's brilliant idea is this?

CCM iko juu sana!

Utaratibu huu ninaupokea kwa mikono miwili kabisa kwani unatoa fursa kwa wanachama kufanya maamuzi makubwa katika jimbo lao. Wanachama wanafahamu ni nani anayeweza kuwaongoza kikweli-kweli na wala si vinginevyo. Utaratibu huu pia utatoa fursa sawa kwa kila mtu mwenye sifa ya kugombea kufanya hivo bila ya kuwa na wasiwasi wa kutafuta resources za ziada ambazo mara nyingi huwaacha watu wakiwa na madeni au kuwa vyanzo vya rushwa.

Wazo jingine ambalo ninalo akilini mwangu, ni kuangalia upya kwa kufanya utafiti labda kwa matumizi ya 2015 (endapo kama tumechelewa kwa 2010), ni suala la ukazi wa kudumu. Majimbo mengi yamekuwa na wabunge 'wageni' kwa maana si wakazi wa kudumu wa majimbo hayo. Ukiangalia residence addresses zao utakuta ni nje na jimbo lake na pengine ni mamia ya miles. Hakika namna hii ya wabunge haiwasaidii sana wanachi wanaowakilishwa kwani mbunge kwa njia moja au nyingine 'si mwenzao' wala hajui hali halisi ya kila siku ya jimbo lake kwa maana ya maisha ya kila siku.

Hata hivyo sasa watendaji katika chama waandae utaratibu ambao utakuwa effective including taratibu zitakazofuata baada ya kura za maoni. Ni vyema wakati taratibu hizo zinatarishwa basi na elimu kwa wapiga kura yaani wanachama itayarishwe pia. Wanachama pamoja na mambo mengine waelewe kuwa matokeo ya uchaguzi kwenye matawi ni matokeo ya wanachama na siyo ya mtu mmoja mmoja, kwa maana kuwa kila mwanachama anawajibika kuyapokea na kuyakubali. Baada ya uchaguzi kwisha aliyeshinda anakuwa ni mshindi wa CHAMA CHA MAPINDUZI na atatakiwa kuungwa mkono na wanachama wote bila ya kujali tofauti zao kabla ya uchaguzi.

KIDUMU CHA MAPINDUZI
 
Who's brilliant idea is this?

CCM iko juu sana!

Utaratibu huu ninaupokea kwa mikono miwili kabisa kwani unatoa fursa kwa wanachama kufanya maamuzi makubwa katika jimbo lao. Wanachama wanafahamu ni nani anayeweza kuwaongoza kikweli-kweli na wala si vinginevyo. Utaratibu huu pia utatoa fursa sawa kwa kila mtu mwenye sifa ya kugombea kufanya hivo bila ya kuwa na wasiwasi wa kutafuta resources za ziada ambazo mara nyingi huwaacha watu wakiwa na madeni au kuwa vyanzo vya rushwa.

Wazo jingine ambalo ninalo akilini mwangu, ni kuangalia upya kwa kufanya utafiti labda kwa matumizi ya 2015 (endapo kama tumechelewa kwa 2010), ni suala la ukazi wa kudumu. Majimbo mengi yamekuwa na wabunge 'wageni' kwa maana si wakazi wa kudumu wa majimbo hayo. Ukiangalia residence addresses zao utakuta ni nje na jimbo lake na pengine ni mamia ya miles. Hakika namna hii ya wabunge haiwasaidii sana wanachi wanaowakilishwa kwani mbunge kwa njia moja au nyingine 'si mwenzao' wala hajui hali halisi ya kila siku ya jimbo lake kwa maana ya maisha ya kila siku.

Hata hivyo sasa watendaji katika chama waandae utaratibu ambao utakuwa effective including taratibu zitakazofuata baada ya kura za maoni. Ni vyema wakati taratibu hizo zinatarishwa basi na elimu kwa wapiga kura yaani wanachama itayarishwe pia. Wanachama pamoja na mambo mengine waelewe kuwa matokeo ya uchaguzi kwenye matawi ni matokeo ya wanachama na siyo ya mtu mmoja mmoja, kwa maana kuwa kila mwanachama anawajibika kuyapokea na kuyakubali. Baada ya uchaguzi kwisha aliyeshinda anakuwa ni mshindi wa CHAMA CHA MAPINDUZI na atatakiwa kuungwa mkono na wanachama wote bila ya kujali tofauti zao kabla ya uchaguzi.

KIDUMU CHA MAPINDUZI

CCM Pamwanya!!!!!!!!!
 
LABDA ITASADIA, YALE MAMBO YA KUCHUKUA WAJUMBE WANAFUNGIWA GUEST ILI WASIBADILIKE BAADA YA KUWAHONGA LABDA YATAPUNGUA!

TUNAHITAJI MABADILIKO YA KWELI, ILA TUSISHANGAE MAFISADI WAKABUNI MBINU NYINGINE KUKABILIANA NA HII, IKIWA NI PAMOJA NA KUNUNUA KADI ZA WANACCM KWA MUDA ILI WASIPIGE KURA, MFANO KWA MTAJI WA 5,000,000 MTU ANAWEZA KUNUNUA KADI1000 ZA WANACHAMA KWA 5,000 KILA MOJA, MATAWI MENNGI YANA WANANCHAMA AROUND 200, HIVYO ATAKUWA AMENUNUA MATAWI 5. MTU KAMA RA AKITUMIA 100,000,000 ATANUNUA WANGAPI?
NI VEMA MKAZO UKAWEKWA PIA KUPAMBANA NA UFISADI NDANI YA CHAMA, KWA MFANO MTU AKICHEZA FAULU YA NAMNA HIYO AFUKUZWE KWENYE CHAMA BILA KUANGALIA WADHIFA WAKE, KAMA NI HIVYO WALIKUWA WAANZE NA SOFIA SIMBA WA UWT

HATA HIVYO NAWAPONGEZA KWA MARA YA KWANZA ccm NI MWANZO MZURI
 
Demokrasia ni gharama ikiwemo ya uchaguzi na mchakato mzima wa kupata wagombea.
Kwa hili ni sehemu muhimu kwa CCM kujua inawanachama hai wangapi.
Je mshindi atapatikana kwa idadi yoyote ya kura za zaida didhi ya wengine au ni kwa zaidi ya nusu ya kura zilizopigwa.
Zoezi hili halitofanikiwa sana ingawa ni wazo zuri,kwa sababu hakuna utaratibu mzuri wa kuzuia kampeni za chini chini hivyo rushwa na kuchafuana kutaendelea kuwepo tu.Pia hii itawajaza takrima wale wa chache watakao kuwa wanasimamia chaguzi hizi.
Mwisho,Hivi kuweka idadi ya wabunge wanawake wa kuteuliwa ili idadi yao iwe nusu ya wabunge wote ni sera ya CCM au ya Taifa?kama ni ya CCM itakuaje wasipo chaguliwa na kama ni sera ya Taifa,wananchi wameshirikishwa vipi kulikubali hili au ndio ule ULEVI wa CCM kuwa wao ni Taifa na watongoza MILELE?
 
Mtanzania,

Inasemekana umeshaanza "kampeni" hata kabla ya filimbi kupigwa 🙂 ..... Nakubaliana nawe kwamba uamuzi huu, kama utatekelezwa vizuri utaimarisha demokrasia kwa kutupatia viongozi wanaostahili.

Kipunguni,

Wacha nitafute kadi kwanza, ukianza kampeni hata wakati kadi huna si utaishia kama yule jamaa wa CHADEMA kule Mbeya Vijijini?

Baada ya hapo ni kupanga sera sera vizuri, sio zile za ku create 2M jobs huku hata uwezo wa kutengeneza laki moja huna. Nitajenga viwanda vya korosho huku hata uwezo wa kuleta mashine ya kukoboa mahindi huna.

Ukishaandaa sera inabidi kutembelea Bagamoyo, kwenda kuchezwa ngoma ukiwa uchi makaburini. Jamaa anakuambia ukitimiza haya masharti utakuwa mheshimiwa, mmhhh!! hivi yeye hataki kuwa mheshimiwa? Kwanini asitimize hayao masharti kwanza na akashinda?

2010 bado ni mbali hivyo hakuna haja ya kuanza kampeni na kuwapandisha pressure bure waheshimiwa.
 
Utakalia hayohayo ooh mara wameiba utamaduni wa CUF mara sijui nini,cha msingi sasa hivi ni nyie kujipanga upya na kujiandaa kwa mechi ya mwakani,maana katika hali halisi CUF ndo wako hoi bin taaban now,msipongalia hata NCCR,TLP,UDP na vyama vingine vidogo vitawa'overtake'.Kaeni chini mjipange upya..Kwa hali ilivyo sasa msipoangalia hata Mtaji wenu wa PEMBA utapigwa ile inaitwa Sandakalwe Amina,mwenye kupata apate
Hao Bwana hicho ndicho watakachokipata. Halafu watabakia kubwata ohh wakati tunapiga kura Pemba waliletwa askari. sasa askari kazi yao kulinda - Bwana! na nyinyi mnatabia ya kuzusha fujo kwa nini msilindwe ili kuepuka fujo zenu?
 
Hao Bwana hicho ndicho watakachokipata. Halafu watabakia kubwata ohh wakati tunapiga kura Pemba waliletwa askari. sasa askari kazi yao kulinda - Bwana! na nyinyi mnatabia ya kuzusha fujo kwa nini msilindwe ili kuepuka fujo zenu?
Anzeni kampeni jipangeni ,hamna jipya ,wacha watangulie maana kutangulia kwao ni kupanga wizi ,hawana jingine .CUF ni Chama pekee ambacho ndio kinajua kufanya siasa na kinajua wapi pa kushambulia na wakati gani ni mzuri kwa mapambano na ni wakati gani wa kumtega adui.

CUF ina mbinu za kimataifa katika kufanya siasa na ina washauri na wataalamu wa hali ya juu wengine si raia wa hapa lakini wanatoa msaada katika kupambana na Chama Tawala ,ni mwanachama wa vyama vya upinzani ambavyo vingine vimefanikiwa kushinda.

Hivyo mbinu zao za kuelekea Uchaguzi bado zipo na ikifika wakati ndio watakapo vamia na kufanya ile kitu inaitwa ambush ,kisiasa Sultani CCM ameshaanguka hilo halina ubishi yupo chini amelala chali. Au uongo ?

Nimesema msifanye haraka subirini tuone hiyo sera waliyoiiba itakavyowaangusha maana kama alivyosema huyo kilango kuwa mambo ni hatari tupu ,alikwisha ona ,maana itakuwa hakuna tena ile tukae pamoja baada ya kuchaguana kwenye NECK ni mapande tu moja kwa moja.

Unajua kila kitu kina mazoea yake na kujifunza ukubwani ni kutafuta matatizo ,maana kama hukucheza mpira tokea ungali mdogo basi kuucheza ukubwani ni kutafuta kuvunjika na ndio hivyo itakavyotokea kwa Sultani CCM.

CCM imeshaanguka nyie mliopo hapa mlio kwenye ajira za Sultani CCM tafuteni pa kushika kabisa au hatutawaona tena hapa. Asie sikia la mkuu. 😀
 
Back
Top Bottom