THE BIG SHOW,
SHERRIF ARPAIO,
..mimi nadhani mngepigania umeme usambazwe wilaya zote ktk mikoa ya kusini.
..pia suala la ELIMU litafutiwe ufumbuzi ktk mikoa ya kusini.
..elimu ina matatizo sana maeneo ya kusini. kuna maeneo waalimu wanabakwa, kwingine kuna migogoro ya udini, halafu uchanganye na suala la utoro na wazazi kuozesha watoto wa kike.
..bila kutatua matatizo ktk sekta ya elimu wananchi wa kusini hawawezi kufaidika na uchimbaji wa gesi ktk maeneo yao.
..pia kuwe na mfumo mzuri zaidi wa manunuzi ya mazao kama Korosho na mengine yanayopatikana huko.
..Shiyanga, Geita, Tabora, wana migodi ya dhahabu lakini hali zao hazina tofauti na wakati hawana migodi hiyo. kwa msingi huo hoja ya wananchi wa kusini inapaswa kujumuisha mambo mengi sana na siyo kulazimisha tu "gesi haitatoka Mtwara."