CCM haina Mwenyekiti wala Katibu Mkuu, hivi sasa inaendeshwa na Dola

CCM haina Mwenyekiti wala Katibu Mkuu, hivi sasa inaendeshwa na Dola

Ileje

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2011
Posts
9,524
Reaction score
13,682
Baada ya kifo cha Magufuli aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM na Bashiru kuwa Katibu Mkuu Kiongozi na baadaye kutenguliwa na kuteuliwa kuwa Mbunge, CCM haina uongozi wa juu na hivi sasa inategemea Dola kuendeshwa katika shughuli zake za kila siku.

Jambo hili si la afya kwa mustakabali wa siasa za nchi na rasilimali za umma.

Kwa vyovyote vile rasilimali nyingi za umma zinatumiwa na CCM kinyume na sheria za nchi na hivyo kukosa sifa za kuwa chama cha siasa.

Wito kwa msajili wa vyama vya siasa kuwakumbusha CCM kujaza haraka iwezekanavyo nafasi za uongozi zilizo wazi ili kuepusha muingiliano wa kimaslahi baina ya Serikali na CCM.
 
Mzee Mangula yupo na Mpogolo kama makamu wote.
 
Kweli mkuu?

Nani aliyehitisha na kusimamia kikao cha kumchagua VICE president(mheshimiwa Mpango)?
Hata kama kuna kikao kilikaa lakini Mama alisema aliwachambua wote akamuona Mpango anaweza kuendana naye kwani kwa mtazamo wake ni mcha Mungu.
 
Hata kama kuna kikao kilikaa lakini Mama alisema aliwachambua wote akamuona Mpango anaweza kuendana naye kwani kwa mtazamo wake ni mcha Mungu.
Mbona mkuu ujajibu, kwenye kikao si kuna mwenyekiti mwenye kusimamia,je alikuwa nani?
 
Mbona mkuu ujajibu, kwenye kikao si kuna mwenyekiti mwenye kusimamia,je alikuwa nani?
Ndiyo lazima awepo mwenyekiti wa muda kupitisha ajenda ya dharula lakini hana mamlaka kamili!
 
Baada ya kifo cha Magufuli aliyekuwa mwenyekiti wa CCM na Bashiru kuwa Katibu Mkuu Kiongozi na baadaye kutenguliwa na kuteuliwa kuwa mbunge, CCM haina uongozi wa juu na hivi sasa inategemea dola kuendeshwa katika shughuli zake za kila siku...
CCM kuwaondoa bashiru, nape, pole pole, kaeni mjitadhimini. Itawagharimu muda sio mfupi. Waliopo sio wanasiasa.
 
Kamati kuu ndo ina mamlaka kupita hata Mwenyekiti na katibu..
Huwa wanakuwaga waoga Tu Kwa Mwenyekiti sababu Mwenyekiti ndo most of time anakuwaga Rais..

Lakini ki structure
Kamati kuu inaweza fukuza hata Mwenyekiti na katibu..
 
Baada ya kifo cha Magufuli aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM na Bashiru kuwa Katibu Mkuu Kiongozi na baadaye kutenguliwa na kuteuliwa kuwa Mbunge, CCM haina uongozi wa juu na hivi sasa inategemea Dola kuendeshwa katika shughuli zake za kila siku....
Msajili mwenyewe anaishi kwa hisani ya CCM
 
Kamati kuu ndo ina mamlaka kupita hata Mwenyekiti na katibu..
Huwa wanakuwaga waoga Tu Kwa Mwenyekiti sababu Mwenyekiti ndo most of time anakuwaga Rais..

Lakini ki structure
Kamati kuu inaweza fukuza hata Mwenyekiti na katibu..
Siyo kwa CCM mkuu
 
Kamati kuu ndo ina mamlaka kupita hata Mwenyekiti na katibu..
Huwa wanakuwaga waoga Tu Kwa Mwenyekiti sababu Mwenyekiti ndo most of time anakuwaga Rais..

Lakini ki structure
Kamati kuu inaweza fukuza hata Mwenyekiti na katibu..
Magufuli aliwahi kumwambia JK kuwa kama angekuwa mwenyekiti wakati wajumbe wa mkutano mkuu walipoimba tunaimani na Lowassa angefyeka wote!

Nani zaidi hapo?
 
Back
Top Bottom