VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,137
- 17,908
CCM imeitisha Kikao cha Dharura cha Kamati Kuu kitakachofanyika mjini Dodoma. Lengo hasa la kikao hicho ni kuipitia na kuichambua Rasimu ya Katiba mpya iliyowasilishwa kwa watanzania na Tume ya Jaji Joseph Sinde Warioba.
Katibu Mkuu Abdulrahman Kinana amenukuliwa na vyombo vya habari leo akisema kuwa CCM haikubaliani na mambo yote yaliyomo kwenye Rasimu.Baadaye leo,Katibu wa Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye akasema kuwa maneno ya Kinana ni 'ya mtaani' na msimamo wa chama utatolewa baada ya kikao husika.
Nape,akihojiwa na BBC, akadai kuwa CCM wanajiandaa pia kuunda Mabaraza ya Katiba kama Taasisi. Amini nawaambia,CCM haitaipinga Rasimu hii.Kiukweli,Tume ya Warioba imedhibitiwa na CCM. Imeandaliwa na kuwasilishwa na watiifu wengi wa CCM wakiongozwa na Jaji Warioba. Itajadiliwa na kupitishwa chini ya CCM. Kwasasa na ilikofikia ,CCM haitaipinga.
Chama changu kimezoea mchezo wa kuvuta hisia za watanzania. Hufanya hivi hasa kwenye Uteuzi wa Mgombea wa Urais na wale wa Ubunge.Wanapenda kuteka bongo za wananchi ili wafuatiliwe na kusikilizwa watakachojadili huko Dodoma. Wanapenda 'kuwa hewani sana'.Hakuna zaidi. Hakuna jipya. CCM haitathubutu kuipinga Rasimu ya Warioba. Wanataka 'attention' tu!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Katibu Mkuu Abdulrahman Kinana amenukuliwa na vyombo vya habari leo akisema kuwa CCM haikubaliani na mambo yote yaliyomo kwenye Rasimu.Baadaye leo,Katibu wa Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye akasema kuwa maneno ya Kinana ni 'ya mtaani' na msimamo wa chama utatolewa baada ya kikao husika.
Nape,akihojiwa na BBC, akadai kuwa CCM wanajiandaa pia kuunda Mabaraza ya Katiba kama Taasisi. Amini nawaambia,CCM haitaipinga Rasimu hii.Kiukweli,Tume ya Warioba imedhibitiwa na CCM. Imeandaliwa na kuwasilishwa na watiifu wengi wa CCM wakiongozwa na Jaji Warioba. Itajadiliwa na kupitishwa chini ya CCM. Kwasasa na ilikofikia ,CCM haitaipinga.
Chama changu kimezoea mchezo wa kuvuta hisia za watanzania. Hufanya hivi hasa kwenye Uteuzi wa Mgombea wa Urais na wale wa Ubunge.Wanapenda kuteka bongo za wananchi ili wafuatiliwe na kusikilizwa watakachojadili huko Dodoma. Wanapenda 'kuwa hewani sana'.Hakuna zaidi. Hakuna jipya. CCM haitathubutu kuipinga Rasimu ya Warioba. Wanataka 'attention' tu!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam