Uchaguzi 2020 CCM imeonesha demokrasia kuhesabu kura kwa uwazi, tume ya uchaguzi ifanye hivyo

Uchaguzi 2020 CCM imeonesha demokrasia kuhesabu kura kwa uwazi, tume ya uchaguzi ifanye hivyo

TUME YA UCHAGUZI IFANYE HIVYO KWENYE CHAGUZI ZA URAIS, WABUGE NA MADIWANI. Ili kuepuka usumbufu na malalamiko ya kuibwa kwa kura.

Ingekuwa vizuri kuwepo na sheria kuwa kura zote zihesabiwe kwa uwazi kwenye vituo vya kupigia kura na matokeo ya kila kituo yatangazwe pale pale kwenye kituo husika.

Kama kweli serikali ya CCM pamoja na CCM yenyewe wakikubali hili, basi watu watazidi kuiamini serikali pamoja na CCM yenyewe. Vinginevyo itakuwa CCM wametupiga change la macho tu.
Kwani ni lini kura hazikuhesabiwa kituoni? Tume yetu ni huru Sana, ndio maana kura huwa zinahesabiwa na kubandikwa vituoni mara tu baada yakumaliza zoezi lakupiga kura Tena kwauwazi kwaushiriki wa vyama vyote na waangalizi wengine.
Hizo zingine ni hofu yakushindwa
 
Kuhesabu sio issue. Hivi Walionyesha live pia kura zilivyopigwa? Term ya pili ya JK kura zilipiwa kimikoa na kila Mkoa uliambiwa kama itatokea kura ya Hapana, watapaswa kuwajua na kuwataja hao “wakorofi”. Huu ni uburuzwaji
 
Ukitulia na kutafakari vizuri,unagundua kuwa CCM wanafanya siasa kweli kweli na CHADEMA wanafanya harakati,harakati zinaweza kuwa sehemu ya siasa ila si wakati wote. Ccm wamehesabu kura hadharani ilawakiwa wamejipanga na wako oncontrol. Uchaguzi wa 2015 wasingeweza kufanya vile.
Mimi binafsi nawasifu ccm wanavyofanya siasa
 
Kwa namna mchakato mzima wa kuwapata wagombea ulivyoendeshwa ndani ya CCM, hapakuwa na haja hata ya kwenda kupoteza muda wa kupiga kura! Hii ni sababu wagombea urais wa pande zote mbili tayari walishatengenezewa mazingira na walishajulikana hata kabla ya kupiga kura! Kwa upande wa Zenji ilishajulikana DK Mwinyi ndiye alikuwa chaguo la wenye nguvu na mamlaka, hivyo tayari mchezo ulishamalizwa mapema kabisa! Kwa upande wa bara kwanza wale wote waliokuwa na nia ya kutaka kuja kushindana na Magu, walishafukuzwa toka ndani ya chama na zaidi yote hata formu ya mgombea iliandaliwa moja tu, hivyo kilichokwenda kufanyika kuthibitishwa na wala si kuchagua tena maana kila kitu kilishachongwa tangu mwanzo! Alafu utasikia vyombo vya habari vikisema kashinda kwa kishindo! Najiuliza alishindana na nani????...
 
kuhesabu kura mia sio sawa kuhesabu kura milioni. Wacha wahesabu kikawaida wamalize haraka watoe jibu tu.
Nigeria walihesabu kuea hadharani, zikahkikiwa hadgarani. Wapiga kura ni wengi, zaudi ya mara 6 ya Watanzania. Na bafo majibu yalitoka haraka.

Majibu ya kura huwa yanacheleweshwa na uchakachuaji.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wafanye hivyo yaani unaandika jina lako halafu karatasi haikunjwi kila mmoja anaweza kusoma ulichoandika hiyo ndiyo demokrasia unayo itaka?
 
TUME YA UCHAGUZI IFANYE HIVYO KWENYE CHAGUZI ZA URAIS, WABUGE NA MADIWANI. Ili kuepuka usumbufu na malalamiko ya kuibwa kwa kura.

Ingekuwa vizuri kuwepo na sheria kuwa kura zote zihesabiwe kwa uwazi kwenye vituo vya kupigia kura na matokeo ya kila kituo yatangazwe pale pale kwenye kituo husika.

Kama kweli serikali ya CCM pamoja na CCM yenyewe wakikubali hili, basi watu watazidi kuiamini serikali pamoja na CCM yenyewe. Vinginevyo itakuwa CCM wametupiga change la macho tu
Bonge ka point!
Na wala kilio cha tume huru kisingelikuwa na maana yoyote.

Baada ya kura kupigwa, wagombea na wawakilishi wao wanajitoma ndani kushiriki kuhesabu kwa kupokea matokeo yao moja kwa moja, pasingekuwa na majungu wala lawama.
 
demokrasia ni kura ya siri, siyo wazi kama ilivyofanyika!
Kura ya siri! Kwani kura haikupigwa kwa siri?
Kura ilipigwa kwa siri, ila namna ya kuhesabu ndiyo inayoongelewa hapa ili kuondoa utata na majungu yasiyokuwa na ulazima wowote.
 
Zile za kikaoni kwao hazikuzidi 200 kama sikosei....si tunazungumzia hizi za juzi apa kumchagua rais wa Zanzibar?

Hapo kituoni si kunakuwa na mawakala kutoka kila chama wakihesabu kura? wakimaliza wanatia saini halafu zinapelekwa makao makuu ama utaratibu kwenu ukoje? Mana huku kisiwani uliopita ulikuwa umewekwa wazi, ila baada ya kuona kuwa ngoma imewaelemea na mambo kuwa wazi wakaamua kujecharize matokeo.
Kujecharize matokeo[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]!
 
Kura ya siri! Kwani kura haikupigwa kwa siri?
Kura ilipigwa kwa siri, ila namna ya kuhesabu ndiyo inayoongelewa hapa ili kuondoa utata na majungu yasiyokuwa na ulazima wowote.
karatasi hazikukunjwa.
kila aliyepiga NDIYO/SIYO kamera zilikuwa zinamdeku tu kwa ajili ya figisu baadaye!
 
Ndo maana kila chama kinakuwa na wakala wake wa kuhesabu kura na matokeo yanatangazwa na kubandikwa na mawakala wanasaini.huo ni uwazi wa hali ya juu.
 
Demokrasia ni kkumchagua mgombea wao wa Urais pale Kisiwandui
 
TUME YA UCHAGUZI IFANYE HIVYO KWENYE CHAGUZI ZA URAIS, WABUGE NA MADIWANI. Ili kuepuka usumbufu na malalamiko ya kuibwa kwa kura.

Ingekuwa vizuri kuwepo na sheria kuwa kura zote zihesabiwe kwa uwazi kwenye vituo vya kupigia kura na matokeo ya kila kituo yatangazwe pale pale kwenye kituo husika.

Kama kweli serikali ya CCM pamoja na CCM yenyewe wakikubali hili, basi watu watazidi kuiamini serikali pamoja na CCM yenyewe. Vinginevyo itakuwa CCM wametupiga change la macho tu
Thubutu! Umeona taratibu za maadili zilizotungwa na msajiri wa vyama? Zinasisitiza usiri wa hali ya juu.
 
TUME YA UCHAGUZI IFANYE HIVYO KWENYE CHAGUZI ZA URAIS, WABUGE NA MADIWANI. Ili kuepuka usumbufu na malalamiko ya kuibwa kwa kura.

Ingekuwa vizuri kuwepo na sheria kuwa kura zote zihesabiwe kwa uwazi kwenye vituo vya kupigia kura na matokeo ya kila kituo yatangazwe pale pale kwenye kituo husika.

Kama kweli serikali ya CCM pamoja na CCM yenyewe wakikubali hili, basi watu watazidi kuiamini serikali pamoja na CCM yenyewe. Vinginevyo itakuwa CCM wametupiga change la macho tu
Tena uwazi wa aina hiyo ni wa kuigwa , maana upigaji kura kila mtu anakuona , kutumbukiza kura sandukuni bila kukunjwa na sanduku unaloweka kura linajulikana wapigaji kura wake wote
 
Hata kura huwa zinahesabiwa kwa uwazi mbele ya wasimamizi na mawakala. Wasimamizi huwa hawafaamiani na mawakala wanatoka vyama mbalimbali swala la uwazi huwa ni kubwa mno
 
Back
Top Bottom