Tetesi: CCM inawaka moto kwa ndani, siku si nyingi yataibuka makubwa

Tetesi: CCM inawaka moto kwa ndani, siku si nyingi yataibuka makubwa

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2015
Posts
14,242
Reaction score
34,903
Muda sio mrefu madai ya wanaCCM yataibuka na kuwekwa wazi, ikiwa ni kilio na malalamiko juu ya uwezo wa Mwenyekiti wa Chama hicho ngazi ya Taifa, kwamba anashindwa kukiongoza chama, sababu za msingi hazikuwekwa wazi ni nini hasa kinachomfanya mwenyekiti huyo mpya ambaye hajamaliza hata mwaka mmoja kuonekana hatoshi, lakini wachambuzi wachache wa masuala hayo walidai ni ukiukwaji wa demokrasia, ukiukwaji wa utawala bora na kukiuka sheria na taratibu, kutokusikiliza ushauri na kuendesha nchi kwa hisia, mapenzi, chuki na matakwa binafsi bila kufuata utaratibu.

Kubwa zaidi; ndani ya chama hicho kuna ubadhilifu mkubwa wa fedha ambao mwenyekiti huyo ameshindwa kuushughulikia na kuudhibiti, kuna matumizi mabaya ya fedha ambayo yanazidi kukiondolea chama hicho sifa, kuna vyanzo vya mapato vya chama hicho ambavyo havijulikano, yaani hewa, lakini wadadisi wanavyosema kuwa inawezekana fedha hizo zinatoka serikalini na zinaingizwa kwenye chama hicho tayari kwa kuanza rasmi kazi za chama.. ambapo wachache hao wazalendo walidai kuwa chama hakipaswi kuihujumu mali ya umma kwani hata kama wananchi hawatakichagua tena, ni halali kwani ni kweli kimepoteza sifa, mvuto na nguvu kiliyokuwa nayo awali.

Baadhi ya viongozi waandamizi wa chama hicho ambao nilipata kuwadadisi kwa kufanya mazungumzo nao kwa njia ya VoiP, walinihakikishia kuwa chama hicho mpaka sasa hakina Dira, na waliyakumbuka maneno ya marehemu Horace Kolimba.

Malalamiko na manung'uniko hayo ni ya chini kwa chini yaliyodumu kwa muda mrefu sasa, yaliyopelekea maafisa kadhaa kwenye chama hicho kuondolewa nyadhifa zao na kuonywa vikali kutokuzungumza chochote, pia wengine kuamua kuachia nafasi zao bila taarifa rasmi..Lakini mwengi wamedai uwezo wake ni mdogo kushika madaraka makubwa mawili, yaani zile kofia mbili.

Taarifa kamili nitazileta kadiri nitakavyozipata kutoka vyanzo vya kuaminika ndani ya Chama hicho, chama cha mapinduzi CCM.
 
Muda sio mrefu madai ya wanaCCM yataibuka na kuwekwa wazi, ikiwa ni kilio na malalamiko juu ya uwezo wa Mwenyekiti wa Chama hicho ngazi ya Taifa, kwamba anashindwa kukiongoza chama, sababu za msingi hazikuwekwa wazi ni nini hasa kinachomfanya mwenyekiti huyo mpya ambaye hajamaliza hata mwaka mmoja kuonekana hatoshi, lakini wachambuzi wachache wa masuala hayo walidai ni ukiukwaji wa demokrasia, ukiukwaji wa utawala bora na kukiuka sheria na taratibu, kutokusikiliza ushauri na kuendesha nchi kwa hisia, mapenzi, chuki na matakwa binafsi bila kufuata utaratibu.

Kubwa zaidi; ndani ya chama hicho kuna ubadhilifu mkubwa wa fedha ambao mwenyekiti huyo ameshindwa kuushughulikia na kuudhibiti, kuna matumizi mabaya ya fedha ambayo yanazidi kukiondolea chama hicho sifa, kuna vyanzo vya mapato vya chama hicho ambavyo havijulikano, yaani hewa, lakini wadadisi wanavyosema kuwa inawezekana fedha hizo zinatoka serikalini na zinaingizwa kwenye chama hicho tayari kwa kuanza rasmi kazi za chama.. ambapo wachache hao wazalendo walidai kuwa chama hakipaswi kuihujumu mali ya umma kwani hata kama wananchi hawatakichagua tena, ni halali kwani ni kweli kimepoteza sifa, mvuto na nguvu kiliyokuwa nayo awali.

Baadhi ya viongozi waandamizi wa chama hicho ambao nilipata kuwadadisi kwa kufanya mazungumzo nao kwa njia ya VoiP, walinihakikishia kuwa chama hicho mpaka sasa hakina Dira, na waliyakumbuka maneno ya marehemu Horace Kolimba.

Malalamiko na manung'uniko hayo ni ya chini kwa chini yaliyodumu kwa muda mrefu sasa, yaliyopelekea maafisa kadhaa kwenye chama hicho kuondolewa nyadhifa zao na kuonywa vikali kutokuzungumza chochote, pia wengine kuamua kuachia nafasi zao bila taarifa rasmi..Lakini mwengi wamedai uwezo wake ni mdogo kushika madaraka makubwa mawili, yaani zile kofia mbili.

Taarifa kamili nitazileta kadiri nitakavyozipata kutoka vyanzo vya kuaminika ndani ya Chama hicho, chama cha mapinduzi CCM.
Kwa CCM tutasubiri sana.Hata kama kuna mpasuko lakini hauwezi kuzidi utamu wa kukamata dola na kwa mantiki hiyo utatulizwa tu.
 
tatizo ni wanachama kutaka magufuli akiongoze hicho chama chao kifisadi lazma wachefukwe!!!!!!!!!!!!!!!!!!!


kidumu hakunaga tena wanazoma namba za gwanzugwa
 
asilimia 75 ya makatibu wa ccm wa mikoa na wenyevuti,asilimia 75 ya makatibu wa wilaya na wenyeviti na wajumbe wa NEC pamoja na watumishi wa makao makuu na sekretariet wanatakiwa watupwe nje.

wale walioimba wana imani na lowasa mpaka sasa wako stendi wanajiandaa kuondoka,

listi inaandaliwa na imekamilika na muda wowote watatangazwa kuondolewa kama hatua ya awali ya maandalizi ya uchaguzi wa ndani ya ccm mapema 2017
 
Ndo hasara za kumpa mtu uenyekiti wa Taifa wakati hajawahi kuwa kiongozi yoyote wa ngazi ya chini ya chama.
Dereva wa Chama cha mwendo kasi
 
Mkuu ni ngumu huo mpasuko kuonekana,madaraka ni matamu ata iweje hawawezi kutofautiana na mwenyekiti wao.
 
Blah blah blah!
Tangu mkutano mkuu wa uchaguzi Dodoma 2015 mlikuwa mnatabiri mgogoro ndani ya CCM! Lakini wote tunajua CCM inazidi kuwa imara huku migogoro hiyo ikihamia vyama vya upinzani
 
Kama aliondoka ma Mvi basi chama kitaendea kustawi kwakua Mkuu wa piga dili alisha amia Chama kingine.
 
Back
Top Bottom