Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 12,699
- 22,598
Nimeshangaa kuona kwamba wengi wa wanachama wa CCM pamoja na viongizi wao wamekuwa wakiwashambulia watu wa upinzani kila wanapotoa maoni juu ya miradi kama SGR, ndege za ATC, mradi wa umeme wa SGR, flyover nk
Utakuta mtu anasema kwa nini unapanda ndege za ATC alizonunua Magufuli wakati mlipinga?
Huu ni upotoshaji wa makusudi au watu kuwa wavivu kutumia akili na busara zao SGR kwa mfano, mtu akiuliza mbona mradi huu unachelwa anajibiwa wewe ni mpinzani kwa nini unauulizia? Kuna watu hata walionyesha picha ya Zitto akishuka ndege ya ATC wakidai kwa nini anapanda ndege na yeye alikosoa ununuaji wa hizo ndege?
NI wazi kwamba wale wote, mashabiki na viongozi wa CCM, wenye mtazamo huu wana tatizo katika kufikiri. Ni sawa na mtu anapiga kelele kwamba usije kwenye harusi yangu kwa kuwa uliniambia nisiendekeze ngono kuna ukimwi!
NIngeshauri mashabiki wa CCM na viongozi wao wajaribu kutumia akili na busara katika kuelewa maoni yanayotolewa na viongozi wa upinzani juu ya maendeleo ya Tanzania. Viongozi wa upinzani wanaposhauri kwamba CCM msiendekeze ngono mnaweza kuambuizwa ukimwi, hawawakatazi CCM kuoa au kuolewa.
Na pale viongozi wa upinzani wanaposema taratibu zilikiukwa katika kutekeleza miradi kama ya kununua ndege au SGR, hawana maana hawapendi vitu hivi vijajengwa nchini au kwamba hawatavitumia. Wanachomaanisha ni kwamba vifanyike kwa utaratibu wa kisheria na ulioainishwa katika taratibu za manunuzi au miradi ya Serikali, kutia ndani Bunge kuhusishwa pale inapostahili.
Mtu mmoja kuwa anaamua juu ya miradi mikubwa peke yake kwa msisimko tu wa kisiasa bila kufuata utaratibu wa matumizi ya fedha za serikali kama kupeleka Bunge likaiizinishe matumizi ya fedha za miradi hiyo, huko ni sawa na kufanya ngono za uzembe - ni wazi watu wenye busara watakuonya kwamba usiendekeze ngono za namna hiyo kuna hatari ya UKIMWI.
Na wakikuambia hivyo utakuwa na akili ya mwendawazimu sana kuanza kupiga kelele kwamba umekatazwa kuoa au kuolewa kwa kuwa umeambiwa usiendekeze ngono, au kuwakataza waliokuonya wasije kwenye harusi yako kwa kuwa walisema usiendekeze ngono.
NIna uhakika Watanzania tuna akili na busara, basi tujitahidi kuzionyesha katika kauli zetu.
Utakuta mtu anasema kwa nini unapanda ndege za ATC alizonunua Magufuli wakati mlipinga?
Huu ni upotoshaji wa makusudi au watu kuwa wavivu kutumia akili na busara zao SGR kwa mfano, mtu akiuliza mbona mradi huu unachelwa anajibiwa wewe ni mpinzani kwa nini unauulizia? Kuna watu hata walionyesha picha ya Zitto akishuka ndege ya ATC wakidai kwa nini anapanda ndege na yeye alikosoa ununuaji wa hizo ndege?
NI wazi kwamba wale wote, mashabiki na viongozi wa CCM, wenye mtazamo huu wana tatizo katika kufikiri. Ni sawa na mtu anapiga kelele kwamba usije kwenye harusi yangu kwa kuwa uliniambia nisiendekeze ngono kuna ukimwi!
NIngeshauri mashabiki wa CCM na viongozi wao wajaribu kutumia akili na busara katika kuelewa maoni yanayotolewa na viongozi wa upinzani juu ya maendeleo ya Tanzania. Viongozi wa upinzani wanaposhauri kwamba CCM msiendekeze ngono mnaweza kuambuizwa ukimwi, hawawakatazi CCM kuoa au kuolewa.
Na pale viongozi wa upinzani wanaposema taratibu zilikiukwa katika kutekeleza miradi kama ya kununua ndege au SGR, hawana maana hawapendi vitu hivi vijajengwa nchini au kwamba hawatavitumia. Wanachomaanisha ni kwamba vifanyike kwa utaratibu wa kisheria na ulioainishwa katika taratibu za manunuzi au miradi ya Serikali, kutia ndani Bunge kuhusishwa pale inapostahili.
Mtu mmoja kuwa anaamua juu ya miradi mikubwa peke yake kwa msisimko tu wa kisiasa bila kufuata utaratibu wa matumizi ya fedha za serikali kama kupeleka Bunge likaiizinishe matumizi ya fedha za miradi hiyo, huko ni sawa na kufanya ngono za uzembe - ni wazi watu wenye busara watakuonya kwamba usiendekeze ngono za namna hiyo kuna hatari ya UKIMWI.
Na wakikuambia hivyo utakuwa na akili ya mwendawazimu sana kuanza kupiga kelele kwamba umekatazwa kuoa au kuolewa kwa kuwa umeambiwa usiendekeze ngono, au kuwakataza waliokuonya wasije kwenye harusi yako kwa kuwa walisema usiendekeze ngono.
NIna uhakika Watanzania tuna akili na busara, basi tujitahidi kuzionyesha katika kauli zetu.