CCM: Kamati Kuu Kukaa Chini Dar

Haya . . . Kanyaga twende . . . .

Source: UPL-Homepage


 
1. Mukasa, ambaye hivi karibuni anatarajia kuhitimu shahada ya uzamivu (PhD) nchini Uswisi,

2. ALIKOTOKA


3. Mukasa aliyezaliwa Julai 1970, ni mtoto wa tano kati ya 10 katika familia ya Mzee William Mukasa na Mama Apolonia Mukasa. Alizaliwa katika kijiji cha Rukaragata kilichopo takriban kilometa tatu kutoka mji Biharamulo, barabara ya kwenda wilayani Ngara.

4. Baba yake ni mtumishi wa umma mstaafu ambaye amewahi kuwa Ofisa Afya wa wilaya ya Biharamulo kati ya mwaka 1977 na mwaka 1987 kabla ya kuwa Ofisa Afya wa mkoa wa Kagera kati ya mwaka 1987 na 1992 alipostaafu kwa mujibu wa sheria. Kabla ya hapo, aliwahi kuwa mtumishi wa umma sehemu mbalimbali nchini.

5. Alipata elimu ya msingi katika shule ya msingi Biharamulo kuanzia mwaka 1978 mpaka 1984

6. na baada ya hapo alichaguliwa kujiunga na elimu ya sekondari katika shule ya Nyakato iliyopo nje kidogo ya mji wa Bukoba.


7. Mwaka 1989 alichaguliwa kuendelea na masomo ya kidato cha tano na cha sita katika shule ya sekondari ya Pugu, Dar es Salaam katika masomo ya Fizikia, Kemia na Hisabati.

8. Mwaka 1991/1992, alitumikia Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa mujibu wa sheria katika kambi za Ruvu mkoani Pwani na Maramba, Tanga.

9. Baada ya hapo, mwaka 1993 alijiunga na Chuo kikuu cha Dar es Salaam kwa masomo ya shahada ya kwanza ya sayansi katika hisabati na takwimu.

10. Hakuishia hapo kwani baada ya kufanya kazi kwa muda katika Kituo cha Utafiti na Maendeleo ya Afya cha Ifakara, alikwenda Uholanzi kwa masomo ya shahada ya uzamili ya sayansi katika Teknolojia ya Mawasiliano na Habari katika tiba (MSc in Medical Informatics) kwenye Taasisi ya Sayansi za Afya. Alihitimu shahada hiyo mwaka 2001.

11. Hivi sasa ni mwanafunzi wa masomo ya shahada ya uzamivu katika teknolojia ya habari na mawasiliani kwenye fani ya afya katika chuo kikuu cha Basel, Uswisi.

12. Mfumo wa masomo anayosomea ni ya mazoezi ya vitendo na ukusanyaji wa takwimu kwa ajili ya masomo. Alisema mfumo huo unamwezesha mwanafunzi kuendelea na kazi pia na unatoa nafasi ya kuoanisha masomo ya nadharia na vitendo.

13. Baadhi ya nchi alizotembelea kutokana na masomo, warsha na ziara za kikazi ni ndani na nje ya bara la Afrika, Kenya, Uganda, Ghana, Afrika ya Kusini, Uholanzi, Scotland, Uingereza, Ethiopia, Canada, Italia, Uswisi na Vietnam.

14. Vile vile amekwishafanya machapisho ya kisayansi 10 na kuongoza, kusimamaia, au kuandika miradi takriban 13 ya kitaalamu iliyostahili na kupata ufadhili mkubwa wa fedha.

15. Mukasa hayuko mbali sana kijamii kwani ni mjumbe wa kamati ya usimamizi na tathmini ya masuala ya kitaalamu ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.

16. Vile vile ni mwakilishi wa umoja wa kimataifa wa wanataaluma wa sayansi na teknolojia ya habari na mawasilino katika afya kanda ya Tanzania.

 
Source: Oscar Mukasa



 


Mukasa/Rwegasira - One and the same ?
 
Mukasa/Rwegasira - One and the same ?


Anaitwa Oscar Rwegasira Mukasa ni mtu mmoja! CHADEMA lazima waweke mgombea makini, vinginevyo jimbo walisahau! Hawa CCM wako makini, siipendi lakini ndo hivyo! Maana naona hata hapa JF kampeni ni kali zimeisha aanza naona watu wapo kiitikadi zaidi...

Mas
 
Mukasa/Rwegasira - One and the same ?

- Mkuu Mag3, nimeuliza wanaohusika huko ndani ya CCM baada ya kuiona hii article, ukweli ni ina utata kidogo kwa sababu waliokutana na kuamua sio NEC, ila ni CC ambayo imekutana kwa niaba ya NEC kuepuka gharama za kuita kikao kizima cha NEC na kwamba hiyo inakubalika ndani ya chama cha CCM.

- Pili nimeambiwa kwamba aliyepitishwa ni Oscar ambaye ana jina la mwisho Mukasa, lakini jina la Mukasa ni moja ya sababu kubwa zilizoleta kizaa zaa ndani ya kikao cha kumpitisha huko CC, kwa hiyo ninajaribu again kuthibitisha kama either ni yeye huyo huyo ameamua kuondoa jina la Mukasa, na kutumia Rwegasira, au ni mwingine kabisaa na kama ni mwigine kabisa sitasita kuiomba radhi JF,

- Nitarudi baadaye na more info za uthibitisho.

Respect.

FMEs!
 
- Sawa sawa ni huyo huyo mtu mmoja, nimethibitisha sasa.

Respect.

FMEs!

Oscah nakumbuka kuwa nae Secondari, JKT na UDSM. Wakati huo alikuwa kijina mzuri na analytical. Tumepotezana kwa muda kiasi, nafurahi kuona CV yake imekaa vizuri sasa. Ningependa aendelee kijiimarisha katika sector ya ICT kwenye afya ambapo naamini tuna wataalam wachache sana na mwelekeo wake utatusaidia zaidi huko mbele kama taifa. Tatizo jamii yetu imeshatekwa na utaratibu wa kila mtu kukimbilia kwenye Ubunge kwa kisingizio cha kusaidia jamii. Anyway, namtakia kila la kheri katika juhudi zake ila inaniuma kuona anaenda kwenye siasa na kuacha pengo kwenye ICT na medical services ambapo anahitajika zaidi.
 

- Mkuu wangu O, heshima mbele mimi ninamfahamu sister mmoja PhD na mtaalamu wa juu sana kutoka huko Ifakara, sasa anabeba mabox majuu, pia ninamfahamu tena mshikaji aliyekua engineer wa ndege ya rais Mwalimu, naye sasa anabeba mabox huko majuu,

- Je inaweza kuwa kubeba mabox majuu ni bora kuwa huko ICT na u-ngineer wa ndege ya rais wa bongo, au?

Respect.

FMEs!
 
Mwacheni kijana aende tu huko na kama ana nia njema basi ni baraka kwa wilaya yake na taifa.

Tatizo tu la Watanzania wengi ni hii ya kusema jambo moja wanapoomba nafasi na kufanya tofauti wanapokuwa madarakani.

Kijana ajiepushe na publicity isiyo na maana, huenda hata hayo magazeti hayafiki huko Biharamulo. Aweke nguvu zote kwenye kutimiza yale anayoyaamini kuanzia kule chini vijijini (grassroot politics) na taratibu mafanikio yake yatafika hata kitaifa.

Ni msomi huyo na ana exposure ya kutosha kufanya mabadiliko kama yuko committed; namtakia kila la heri na mungu amsaidie.
 
Mwacheni kijana aende tu huko na kama ana nia njema basi ni baraka kwa wilaya yake na taifa.

Ni msomi huyo na ana exposure ya kutosha kufanya mabadiliko kama yuko committed; namtakia kila la heri na mungu amsaidie.

- Very strong point, tupo pamoja hapo mkuu.

Respect.

FMEs!
 

Wakuu; Nimeongea kwa simu na Oscar, alikuwa njiani kuelekea Bihalamulo na nimemuuliza juu ya tuhuma hizo hapo juu zilizotolewa na Masanilo. Kwa kweli amesikitika sana na amekanusha vikali kuwa hausiki na tuhuma hizo.

Sasa kama Masanilo ana data basi azilete hapa kuliko kutoa tuhuma ambazo hazina ukweli wowote.
 

Mkuu Allien,

Tuwe wakweli, sasa ulitegemea jamaa aseme kweli alihusika? Umefanya vizuri kuweka upande wa pili wa shilingi ila sasa tumwachie Masanilo kumwaga data zote.

Mimi sitashangaa kama kuna ukweli maana jamii yetu karibu yote imeoza tu. Kwasasa tunashindana kwenye nani fisadi zaidi ya mwingine lakini watu clean wako wachache sana.
 


Nakubaliana na wewe si rahisi mtuhumiwa kukubali kirahisi.

Sasa tusubiri hizo dataz za Masanilo. lakini siyo tuambiwe tukawaulize staff wenzake ofisini kama alivyodai.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…