CCM kumbukeni Watanzania hata muwajengee madarasa na zahanati za dhahabu, kama hawana hela mifukoni ni kazi bure!

CCM kumbukeni Watanzania hata muwajengee madarasa na zahanati za dhahabu, kama hawana hela mifukoni ni kazi bure!

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Hayati Magufuli aliweza kujenga barabara na miundombinu yake tangu akiwa waziri wa Mkapa hadi anakuwa Rais lakini watanzania hawakuliona hilo

Wajazeni wananchi fedha mifukoni ndipo mtaiona furaha yao na CCM itang'ara vinginevyo inaonekana kana kwamba maji yanotolewa mtoni na kuingizwa baharini kama Masoud kipanya alivyotuchorea jana

Mitaani kwa akina mzee Mgaya mambo siyo poa kabisa!
 
Na tozo hizi zinazoendelea kutoa pesa mifukoni mwa watanzania?
Sidhani!
 
Hawaelewi magonjwa yanaongezeka watu wakikosa ela.
 
Ukishinda vijiweni na kusubiri pesa kutoka serikali utasubiri mpaka uzeeni. Jielimishe na fanya miradi hata kama midogo ya kilimo. Jiunge na vikundi kwa uwekezaji kusubiri na kulalamika haisaidii
 
CCM inatugeuza inavyo jisikia. Sawa lakini wakati wao huu.
Nikiangalia hii nchi inavyoenda kiundani-naona giza totoro kabisa. CCM & upinzani hawamtaki huyu mama kwa mambo yake ya hovyo,kundi ambalo linam-support huyu mama limejificha chini ya kivuli cha udini na ukanda (Wanamtetea kwa sababu ni mwana dini mwenzao au mzanzibari mwenzao).Mbeleni kunaweza kuzuka mambo ya udini au ueneo sana na yatakuwa hatari kwa usalama wa taifa hili.
 
Hayati Magufuli aliweza kujenga barabara na miundombinu yake tangu akiwa waziri wa Mkapa hadi anakuwa Rais lakini watanzania hawakuliona hilo

Wajazeni wananchi fedha mifukoni ndipo mtaiona furaha yao na CCM itang'ara vinginevyo inaonekana kana kwamba maji yanotolewa mtoni na kuingizwa baharini kama Masoud kipanya alivyotuchorea jana

Mitaani kwa akina mzee Mgaya mambo siyo poa kabisa!
Wajazwe bila kufanya kazi,kila mtu awajibike kivyake.
 
Serikali inatumia kuliko inqvyokusanya....Waziri katika nchi maskini kama Tanzania eti anatembelea V8 ya mil 400 kweli.

Yaani Tanzania nzima kuna V8 zaidi ya 300 za watumishi wa umma piga hesabu mwenyewe wese tu kwa siku ni zaidi ya 80,000 kwa gari moja... kwa siku 2.4 mil
Bado kuyanunua ...

Afu wanahangaika na sisi tozo za kumtumia bi mkubwa kijijini elfu 20.
 
Back
Top Bottom