Uchaguzi 2020 CCM, michanganyo hii mwisho mtachanganyikiwa kabisa na kupoteana

Uchaguzi 2020 CCM, michanganyo hii mwisho mtachanganyikiwa kabisa na kupoteana

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Mungu si mwanasiasa bali wanasiasa wana miungu. Shetani si mwanasiasa bali wanasiasa wana vishetani vyao.

Siasa ni imani lakini siasa sio dini. Siasa ina wafuasi na dini pia ina wafuasi, lakini si lazima mfuasi wa dini awe mfuasi wa siasa na kinyume chake.

Ni muhimu think tank ya CCM ielimishwe sasa kwakuwa ikizidisha hii michanganyo mwisho itachanganyikiwa, na ikichanganyikiwa inaweza kufanya mambo bila ufahamu kamili. Sijui ni hofu ama ni nini, lakini dalili zinaonesha wazi CCM imejawa hofu.

Hofu huleta woga
Hofu huondoa ujasiri
Hofu huleta taharuki
Hofu huondoa ufahamu

Kila jambo ni mchakato na kila mchakato una formula zake, wabobezi wa kemia wanalijua hili vema. Ukikosea formula huwezi kupata matokeo tarajiwa.

Usijaribu kumchanganya Mungu na shetani ..hizi ni falme mbili kinzani..japo ufalme wa Mungu ni mkubwa kuliko ufalme wa shetani. Kuna namna ya kuenenda na shetani na kuna namna ya kuenenda na Mungu; hupaswi kuzichanganya hizi falme mbili kwenye jambo moja.

Ndani ya wiki moja CCM imezichanganya falme mbili, matokeo yamekuwa hasi. Lilianza kitu kinachoitwa 'tamasha la wasanii' wasiopungua 200, wote tulishuhudia ufalme wa giza ulivyosujudiwa pale. Shetani alipewa airtime ya kutosha kabisa.

Siku chache baadae likaja kitu kinaitwa 'kongamano la amani' wahusika walikuwa ni viongozi wa dini mbalimbali walionona kweli kweli, wakajaribu kuusimika ufalme wa Mungu pale.

Mwaka uliopita lilijitokeza kundi la watu mia moja taslimu waliojiita waganga wa kienyeji mashuhuri Tanzania, wakatoa onyo na kupiga mikwara yao.

Think tank ama kitengo cha propaganda, kilitakiwa kufanya nini ili kisiharibu taswira ya chama mbele ya wananchi?

Wale watu mia moja taslimu hawakupaswa kupewa jina la WAGANGA WA KIENYEJI, walau basi wangeitwa wazee wa mila. Lakini je, ni kweli kabisa uganga wa kienyeji unafanya kazi kwa jinsi ile? Jibu ni HAPANA. Kwahiyo basi kule kulikuwa ndiyo mwanzo wa kuchanganyikiwa.

Hiki kilichokuja kuitwa TAMASHA LA WASANII kingetakiwa kufanya nini?

Ili kuonesha UTU na kujali pamoja na nyimbo zao zile wangetawanywa na kwenda kutoa huduma za kijamii kwa wahitaji na wasiojiweza, wangetawanywa kwenye mahospitali, nyumba za watoto yatima na zile za kulelea wazee wasiojiweza. Ssehemu ya pesa iliyotumika kuwalipa wasanii ingetumika kuwahudumia hawa wahitaji.

Hiki kilichoitwa jana KONGAMANO LA AMANI, badala ya kujikusanya pale kwenye ukumbi wa gharama na kula vinono kwenye AC, walitakiwa wakusanyike sehemu kama uwanja wa taifa na kufanya ibada ya kuliombea Taifa na watu wake wote. Kuombea:
  • Amani ya Taifa
  • Mshikamano
  • Upendo
  • Umoja
  • Msamaha na kusameheana
  • Ustawi wa Taifa na watu wake n.k, n.k
Hivi inaleta picha gani kwa wagonjwa wenye uhitaji mkubwa wa vifaa tiba na madawa pale Hospital ya Temeke wakiwa hawajapewa kwa serikali kukosa pesa lakini wakati huohuo chama chenye serikali kikifanya ufujaji mkubwa wa pesa kwa vijana wahuni, barobaro na 'wavuta bhangi' wasiojitambua waliolipwa malipo wasiyostahili?

Hivi inaleta picha gani kwa wagonjwa waliolala pale Ocean rd na Muhimbili wakidaiwa pesa za matibabu ambazo hawana uwezo nazo wanakufa wanajiona huku viongozi wao wa kidini kwa sura zilizong'aa na nyuso zilizonona wakikaribishwa kwenye hafla ya kusifu na kuabudu? Badala ya kupendwa ndio kwanza wataanza kutengeneza chuki.

Chama kilifadhili kusanyiko la waganga wa kienyeji 100
Chama kikafadhili tamasha la wasanii 200
Chama kimefadhili kongamano la amani Tanzania la viongozi wa dini- sina idadi yao
Ni jambo jema kwakuwa chama kina miradi mbalimbali, lakini je, hayo ndio matumizi sahihi ya mapato?

Think tank
ya CCM inapaswa kujitafakari upya. Maamuzi ya kukurupuka kwa ajili ya hofu yanaweza kuliweka taifa kwenye mtanziko mkubwa.
 
Niko mbele hapa nawasubiri wajumbe waje wajitetee...kwa mchanganyo huo.
Wana hofu kwamba Lissu akiibiwa kura hatakubali, na Maalimu hivyohivyo.
JamiiForums497226166.jpg
 
Haya Mambo yanakatisha tamaa Sana na kutuumiza sisi Vijana makada huku Mtaani tuna Njaa Ajira Hatuna Toka tumemaliza vyuo yaani shida tupu.

Mungu atusaidie kwa kweli,nikiona Vijana Wenzangu walivyo na Njaa na Bado tunakitumikia chama kwa moyo mmoja huku tuna Njaa hivyo hivyo.Dah tutafika tu lakini japo kwa Kuchoka.Mungu atusaidie Vijana Wenzangu wote Nchi nzima tusiokuwa na Ajira ambao tumemaliza Vyuo na bado tunakipenda Chama Cha Mapinduzi kwa moyo mmoja.
 
Haya Mambo yanakatisha tamaa Sana na kutuumiza sisi Vijana makada huku Mtaani tuna Njaa Ajira Hatuna Toka tumemaliza vyuo yaani shida tupu.

Mungu atusaidie kwa kweli,nikiona Vijana Wenzangu walivyo na Njaa na Bado tunakitumikia chama kwa moyo mmoja huku tuna Njaa hivyo hivyo.Dah tutafika tu lakini japo kwa Kuchoka.Mungu atusaidie Vijana Wenzangu wote Nchi nzima tusiokuwa na Ajira ambao tumemaliza Vyuo na bado tunakipenda Chama Cha Mapinduzi kwa moyo mmoja.
Fitnah wewee
 
Haya Mambo yanakatisha tamaa Sana na kutuumiza sisi Vijana makada huku Mtaani tuna Njaa Ajira Hatuna Toka tumemaliza vyuo yaani shida tupu.

Mungu atusaidie kwa kweli,nikiona Vijana Wenzangu walivyo na Njaa na Bado tunakitumikia chama kwa moyo mmoja huku tuna Njaa hivyo hivyo.Dah tutafika tu lakini japo kwa Kuchoka.Mungu atusaidie Vijana Wenzangu wote Nchi nzima tusiokuwa na Ajira ambao tumemaliza Vyuo na bado tunakipenda Chama Cha Mapinduzi kwa moyo mmoja.
IMG_20200816_064749.jpg
 
Baba anapompata mtoto humuelekeza tahajia sahihi za maisha, Mtoto akishaanza kupevuka huhitaji uhuru, baba akitoa nasaha zake kwa mtoto kuhusu mienendo hasi ya mtoto, Mtoto hufikiri kuwa anaonewa, Baba mwenye busara huanza kubana uhuru wa mtoto, "Mtoto akishafika (age of reasoning) Huanza eidha kumshukuru baba au kuilaumu nafsi yake"
 
Baba anapompata mtoto humuelekeza tahajia sahihi za maisha, Mtoto akishaanza kupevuka huhitaji uhuru, baba akitoa nasaha zake kwa mtoto kuhusu mienendo hasi ya mtoto, Mtoto hufikiri kuwa anaonewa, Baba mwenye busara huanza kubana uhuru wa mtoto, "Mtoto akishafika (age of reasoning) Huanza eidha kumshukuru baba au kuilaumu nafsi yake"
🤔🤔
 
Haikua ajabu Nduguy na Jiwe kumkomalia Assad aachie u CAG, Naona 1.5 ndio wakati wake wakutafunwa vizuri,
Inatia hasira kiongozi kwakuwa kashiba pilau ya bure bila aibu anasema awamu hi imefanya mambo yaliyopaswa kufanywa ndani ya miaka 25
 
Mkuu unajua shida ninayoiona hata viongozi wa dini wanaogopa badala ya kuheshimu utawala ,hivyo wamebaki kujipendekeza ili wasifutiwe usajili was vituo vya vya kujitafutia mkate wao wa Kila siku
 
Back
Top Bottom