LGE2024 CCM Mkoa wa Simiyu: Uzinduzi wa Kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

LGE2024 CCM Mkoa wa Simiyu: Uzinduzi wa Kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Simiyu kimezindua rasmi kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji, ikiwa ni hatua muhimu katika kuhakikisha wananchi wanashiriki kikamilifu katika uchaguzi huu muhimu. Uzinduzi wa kampeni hizi umefanyika katika kijiji cha Dutwa, Wilaya ya Bariadi.
WhatsApp Image 2024-11-21 at 09.34.58.jpeg
Akizungumza katika uzinduzi huo, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Ndg. Shamsa Mohammed, alisema kuwa kampeni za uchaguzi zitafanyika kwa njia ya kistarabu, ambapo chama kitawaeleza wananchi kazi ambazo kimefanya na mafanikio yaliopatikana chini ya uongozi wa CCM. Alisisitiza kuwa: "Tunaamini katika uwazi na ufanisi, na kama hatutosema, Miti itasema. Tumetekeleza Ilani ya Chama kwa vitendo, na wananchi wanapaswa kuona na kuthamini kazi tunayofanya."
WhatsApp Image 2024-11-21 at 09.35.09 (1).jpeg
Aidha, Ndg. Shamsa Mohammed alieleza kuwa Chama Cha Mapinduzi kimejizatiti kuhakikisha kuwa uchaguzi huu unakuwa wa amani, haki na umoja, huku lengo kuu likiwa ni kuendeleza maendeleo ya wananchi na kuhakikisha huduma bora kwa kila mkoa, wilaya na kijiji.
WhatsApp Image 2024-11-21 at 09.35.08.jpeg
WhatsApp Image 2024-11-21 at 10.28.18.jpeg
WhatsApp Image 2024-11-21 at 09.37.46.jpeg
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2024-11-21 at 09.35.08 (1).jpeg
    WhatsApp Image 2024-11-21 at 09.35.08 (1).jpeg
    167.2 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2024-11-21 at 09.35.09.jpeg
    WhatsApp Image 2024-11-21 at 09.35.09.jpeg
    164.1 KB · Views: 3
  • WhatsApp Image 2024-11-21 at 09.35.12.jpeg
    WhatsApp Image 2024-11-21 at 09.35.12.jpeg
    277.4 KB · Views: 3
  • WhatsApp Image 2024-11-21 at 09.37.39.jpeg
    WhatsApp Image 2024-11-21 at 09.37.39.jpeg
    238.4 KB · Views: 2
Back
Top Bottom