CCM Momba Tunduma waandamana kuadhimisha kuzaliwa kwake

CCM Momba Tunduma waandamana kuadhimisha kuzaliwa kwake

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869
02 February 2023
Tunduma, Tanzania

CCM WAWASHA MITAMBO, WARUSHA "MAKOMBORA' KWA WALICHOKIITA CHAMA CHA UPANDE WA PILI



Wanachama wa CCM jimbo la Momba wamejitokeza kwa wingi barabarani kufanya shughuli za kisiasa kujibu walichoita mapigo upande wa pili walioanza mikutano ya hadhara.

Baada ya Kikao cha ndani wameenda kufanya kikao cha nje kuadhimisha miaka 46 toka kuzaliwa CCM tarehe 5 February 1977 na kujadili mafanikio waliyoita makubwa ingawa upande wa pili ambao hawajautaja hawaamini kuwa yapo.

Walipopanda jukwaani Viongozi wa CCM wazungumzia hotuba za chama kimoja ambacho hawajakitaja jina kilichofanya mikutano yao kanda za ziwa mikoa ya Mwanza, Simiyu na Mara wakiongozwa na kiongozi mmoja mkuu na mwingine aliyerudi kutoa nje ya nchi.

Viongozi wa CCM wakihutubia wanachama na wapenzi wa CCM Tunduma kwamba upande pili wanaona mazuri na makubwa lakini wanabeza tu na hawakubaliani na mengi lukuki mazuri yanayoonekana.

Viongozi hao wa CCM wasema nchi ni ya raha mustarehe na kushangaa watu kukimbilia kukipenda na kukishabikia chama cha upande wa pili kisicho kuwa na serikali.

Source : Jay TV Tanzania
 
27 January 2023
Tunduma

JUMUIYA YA WAZAZI NAO WAJITOKEZA

Akizungumza na jumuiya hiyo ya Chama cha Mapinduzi, mjumbe MNEC asema sasa CCM inaonekana Tunduma ...

Source : Jay TV Tanzania
 
Tabora , Tanzania

Miaka 46 ya CCM tangu kuzaliwa

 
05 February 2023
Viwanja vya Furahisha, Mwanza
Tanzania

CCM Mwanza walia na mfumuko wa bei

 
05 February 2023
Morogoro, Tanzania

Hussein Bashe awa mbogo mbele ya katibu mkuu wa CCM Taifa ndugu Chongolo, serikali haiwezi kuwapangia bei wakulima mazao yao



Wana CCM walipishana kauli huku waziri Hussein Bashe akishangiliwa na jamii ya wakulima waliohudhuria mkutano huo baada ya katibu mkuu wa CCM kujaribu kumbana waziri Bashe juu ya alichoita mfumuko wa bei ...
 
5 February 2023
Mwanza, Tanzania

MIAKA 46 YA KUZALIWA CCM

VILIO SEKTA YA ELIMU VYATIKISA MWANZA WAZAZI WAKIDAI MATOKEO YA WATOTO 140



WAZAZI wenye Watoto waliokuwa wanasoma katika shule ya sekondari Thaqaafa iliyopo wilayani Nyamagana jijini Mwanza wamemwangukia Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan na kumuomba atatue sintofahamyu iliyopo kuhusu matokeo ya watoto wao waliomaliza kidato cha nne mwaka jana katika shule hiyo.

Wakizungumza kwa masikitiko na simanzi wazazi hao wamesema wanafunzi waliomaliza kidato cha nne mwaka jana katika shule hiyo walikuwa 164 wawili hawakufanya mitihani katika matokeo ya mtihani ya mwaka jana yametoka ya wanafunzi 22 pekee wengine matokeo yao hayajulikani kama yamefutwa au la ndipo wakaamua kumuomba Rais Samia awasaidie
 
Viongozi hao wa CCM wasema nchi ni ya raha mustarehe na kushangaa watu kukimbilia kukipenda na kukishabikia chama cha upande wa pili kisicho kuwa na serikali.
Sisi mbona cha cha ccm tunakitaja wao chama cha upande wa pili ambacho wanaona kinapendwa sana wanashindwa hata kukitaja jina?😅😅
 
Sisi mbona cha cha ccm tunakitaja wao chama cha upande wa pili ambacho wanaona kinapendwa sana wanashindwa hata kukitaja jina?😅😅

Wanajua moto wa hoja za makamanda, hivyo wanaongea kwa tahadhari kubwa sije chama chao cha CCM wakaelemewa na hoja nzito toka CHADEMA
 
05 February 2023
Morogoro, Tanzania

Hussein Bashe awa mbogo mbele ya katibu mkuu wa CCM Taifa ndugu Chongolo, serikali haiwezi kuwapangia bei wakulima mazao yao



Wana CCM walipishana kauli huku waziri Hussein Bashe akishangiliwa na jamii ya wakulima waliohudhuria mkutano huo baada ya katibu mkuu wa CCM kujaribu kumbana waziri Bashe juu ya alichoita mfumuko wa bei ...

Bashe hapa hakutaka unafiki. Chongoro ameangukia pua.
 
Back
Top Bottom