Kuchitimbo
JF-Expert Member
- Oct 20, 2019
- 439
- 366
Ni wazee wa maslahi,Ina maana mi macho alienda kuwabebembeleza awape na kuwaongezea migodi ya uranium kule Namtumbo ili wasishinikize jamaa kutoka madarakani kutokana na kuonesha kubariki uchafu wote unaotendeka nchini kwa kukaa kimya bila hata kuwakemea wanaofanya hivo?.Naona upinzani safari hii watashinda uchaguzi kwa kupigiwa kura na wamarekani. Mimi nashangaa hivi wamarekani nyinyi mnawaona watu sana eeh? Pole sana wale hawanaga marafiki huwaga wazee wa masilahi basi. Mjitathimini
Tuliza mshono hujapona vizuriNdoto unazoota baada ya kunywa kvant ipo siku utaenda kumshika makalio mamako mkwe, ndugu hizo pombe zimekushinda ziache, ni hivyo tyu. La maaskofu wenu limekuchachia umerukia jengine.
Mkuu Rubawa, Kamandoo hata mimi nilizungumza nae, ni kweli alipanga kujiongezea au kumuweka mtu wake naomba nimuhifadhi, CCM bara ikafanya mambo, Karume akasimamishwa na kwenye matokeo, kiukweli naomba nisiseme ila wote wanajua kilichotokea.Sio yy tu wanasiasa wetu wote ngoja nikupe mfano mwaka fulani nilikuwa Ikulu ya Zanzibar kwenye maongezi na Komandoo akaniuliza hv una fikiria Ukarume unaweza kurudi tna znz siku jibu kitu mwenyewe akasema ilo aliwezekani ila baada muda nasikia alitaka kujiongezea muda madarakani isiwe miaka 10 tna...
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Rubawa, hayo unayoyasema mimi pia nayapitia, baada ya lile swali la Ikulu, kuna watu wanafanya mambo ya kiajabu ajubu as if wametumwa na yeye, kwasababu wanajua huwezi kupata access kuuliza, lakini through circumnavigating, nimeweza kubaini hao watu hawajatumwa na Magufuli, tena usikute hata Magufuli mwenyewe hajui nini watu wake wanawafanyia dhulma kubwa watu in his name!.Ukiacha watu wachache ambao kwa sababu zake mwenyewe Mh Magufuli amekubari kuwapa madaraka makubwa kudhurumu kunyanyasa sie wote tunao jaribu kuonyesha mapungufu machache ili km Taifa twende Pamoja. Ila yupo Sawa kwenye mengi Nasimama Nae Mh Magufuli Pamoja Dhuruma zote juu yngu na baadhi unazijua vzuri...
Sent using Jamii Forums mobile app
Ndoto unazoota baada ya kunywa kvant ipo siku utaenda kumshika makalio mamako mkwe, ndugu hizo pombe zimekushinda ziache, ni hivyo tyu. La maaskofu wenu limekuchachia umerukia jengine.
Ni ajabu sana kuwa washabiki was CCM hamtaki kuamini hivyo lakini walio madarakani wameshaujua ukweli huo ndio maana wanataka kutumia ujio wa ugonjwa wa Corona kama excuse ya kuahirisha uchaguzi wa Octoba.
CCM wanajua wazi kuwa kiburi cha Magufuli kimewaponza sana na kuwaondolea trust ndani na nje ya nchi na akakosekana wa kumshauri.
Suala la Tumehuru wamegundua wapinzani hawatanii tena, na nchi wahisani wameshika bango. Jee wataponea wapi?View attachment 1395442
Sent using Jamii Forums mobile app
Na US hajawahi kuwanunulia China vyandalua vya malaria au msaada wa ARV.Sijawah kusikia taarifa ya USA kuhusu democrasia ya China... Tumejirahisisha sana
Maneno haya ya Mwalimu Nyerere ni ushahidi wa CCM kutawala milele" Rais bora atatoka CCM". ni ukweli mchungu lakini lazima mkubali Hilo.
Kila nikifikiri ni kwa namna gani CCM itaondoka nakosa majibu ya kuniridhisha hivyo Imani na matumaini yangu ya CCM kutawala milele yakishika kasi.
Ukweli ,CCM haina mpinzani hata tukibeza ukweli huu utatuweka huru tukiweka matumaini ya CCM kutawala milele kuliko kutoka miaka ya karibuni
Unajua kwamba katika kipindi cha miaka minne iliyopita hakuna siasa za upinzani zilizo fanyika nchini kote zaidi ya kesi za polisi na mahakama kwa wapinzani? Unajua kwamba viongozi wengi wa upinzani walidhoofishwa kisha kulazimika kuikubali CCM hadharani ikiwa ni mbinu ya kuipaisha CCM?Mawazo uliyo nayo wewe leo ndio mimi pia nilikuwa nayo kabla ya July,2017, Baada ya kupata kibarua cha kuwa National Sales Manager wa kampuni kubwa binafsi ya usambazaji bidha za matumizi mbali mbali ya nyumbani, ilinipa fursa ya kutembelea karibu Wilaya zote na hasa miji mikubwa na midogo karibu maeneo yote ya Tanzania.
Nimejifunza mengi katika mzunguuko huo ambao nakaribia miaka 3, hali hiyo imenibadilisha sana na nilivyokuwa nafikiri kabla kuhusu kukubalika kwa vyama hasa vyama vya upinzani kulinganisha na CCM, kwa ushuhuda wa matembezi ya kikazi nilibadilisha muono wangu. Hatuna mgombea wa kuitikisha CCM kwa nafasi ya Urais labda kwa ushabiki. Tuna kazi ngumu sana ya kufanya na tunahitaji kufanya kazi ya kutosha.
Nina wasi wasi kuwa hata wabunge wa majimbo wanaweza wakapungua sana. Sidhani hata kumtikisa Mkulu tutaweza labda afanye blanda kubwa ambayo itamwodolea imani wapiga kura.
KWA MFANO: Ukisema hana uwezo wa kujieleza vizuri au kuelezea masuala ya kitaifa na kimataifa vizuri, MAJIBU....walikuwepo waongeaji wazuri sisi walitusaidia nini, sisi tunataka kazi na tunataka matokeo tuu na sasa tunaona jaribu kutembea nchi nzima inajengwa leo hii.
Ukiwaeleza jamaa amebana sana upande wa siasa
MAJIBU.. sasa kazi yetu ya kulima siasa inatusaidia nini?
Walioko vijijini wanaona tufauti ndogo sana ya mapato kati ya siku za nyuma na kulinganisha na leo. Hasa ukitilia maanani mazao yao mengi ya kilimo wanayauzwa na wanapata pesa labda kwa mazao machache ya biashara.
Kuna mengi ningechangia humu, lakini kwa kifupi elimu ya demokrasia bado sana miji mingi midogo na vijijini. Ngoja wazoee umeme, maji, barabara, na hospitali mpya zilizojengwa nina hakika baada ya kuzoea, mahitaji yao yatakua na hapo ndipo wataanza kuigeukia CCM kwa kuhitaji mambo mengi Zaidi..
Na wenzetu CCM wameweka watu wao katika kila ngazi ya utawala kuanzia nyumba kumi.
UPINZANI BADO TUNA KAZI KUBWA YA KUFANYA. MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Mkuu Pascal nimefurahi sana kuona muono wangu tupo wengi hasa kwa yeyote ambae kutafiti kidogo. Kwa hali inavyo endelea tutaruhusu vyama vya upinzani kukosa nguvu kabisa kama hatuta weka nguvu ya kutosha kubalisha hii hali.Mkuu Gerald Magembe, kwanza asante kwa mchango huu, kama kuna Chadema wenye akili na wamekusoma hapa, wata copy na kuwatumia viongozi wao
Hakuna kitu kigumu na kinachotumia fedha kama research, hapa umewafanyia Chadema research ya bure, wangepaswa wakulipe. Michango kama hii yenye ukweli mchungu ndio itawasaidia wapinzani wa kweli. Numbers don't lie, CCM ina wajumbe wa shina, wale wajumbe wa nyumba kumi, huko ndio grassroots level, baada ya wajumbe wa mashina, wana mashina ya wakereketwa karibu vijiwe vyote ni CCM, wanakuja matawi, wanakua vijiji, kata, wilaya, jimbo, mkoa. Ndani ya ofisi zote za CCM kuna Jumuiya zao tatu za wanawake, vijana na wazazi, wakati kwenye vyama vya upinzani kuna maeneo hakuna hata ofisi moja ya chama chochote cha upinzani wilaya nzima.
Nikawashauri Chadema as the main opposition party, they should invest on people, kwa kutumia modern ways of mass mobilization through mass communications. Fedha zilizotumika kununua yale mandinga makubwa ya M4C zingetosha kabisa kuanzisha redio yake, tv yake, gazeti lake na interactive online forum ili to reach the masses wa grassroot level, wao wameng'ang'ania siasa za kiharakati za mikutano ya siasa na maandamano.
Utamwambia nini mtu anayesomeshewa bure watoto wake, kapatiwa maji, barabara, hospitali na huduma muhimu za jamii?.
Kila ukiwaambia ukweli huu wa 2020 Chadema wanakarika na kutukana hovyo humu mitandaoni.
Trend Reading: Wanaohamia CCM wasibezwe! Wanaona mbali, 2020 Majimbo yote kurejeshwa. Je tunarejea nchi ya Chama kimoja? - JamiiForums
Je, CHADEMA inaweza kushinda 2020? Is it serious, credible & mature enough opposition?!. - JamiiForums
Ile 2015 Chadema ilikuwa ichukue nchi, ika bugi tuu step
Kuelekea 2015: CHADEMA Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...! - JamiiForums
Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni ... - JamiiForums
P.
Utabiri kutoka MAREKANI!!!Sitaki kusema mengi kwanini kinaenda kufa ila hoja kubwa ni toka baba wa taifa afariki CCM kimekuwa kikitawala kwa ujanja ujanja na propaganda
Kikubwa zaidi hawamu ya 5 imekizika kwa kupuuza wananchi wanataka nini kiufupi ccm haifanyii kazi matakwa ya watanzania walio wengi ili swala linaenda kuwaondoa madarakani kimchezo mchezo.
Wale mliokwapua pesa za umma muanze kuzilejesha bila kusahau mliokuwa mnafanya maovu mjindae kweli kweli.
Naapa kwa jina la baba la mwana na roho mtakatifu ccm haitarudi madarakani kwa sababu ya ubishi na mtakuja kukumbuka maneno yangu mlikuwa na muda wa kujirekebisha ila kibri kibri mjiandae kisaikolojia.
Huu ni ukweli mchungu...!!Unasema mwisho 2020 wakati hata mgombea hamna mnasubiri mabaki ya ccm
Ina maana mtaji wa Ccm ni hao wajinga?Kuhusu CCM, mimi hoja yangu ni hii
Uchaguzi mkuu wa mwaka 2030, ndio mwanzo wa mwisho wa CCM! Wajinga karibu wote watakuwa wamemalizika! - JamiiForums
P