Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 2,203
- 5,610
Wagombea wa Udiwani wa Kata za Mukendo na Kwangwa, Manispaa ya Musoma Mjini, wameshindwa kuchukua fomu zao za kugombea udiwani katika kata hizo, baada ya watu waliojitambulisha kuwa wagombea wa CCM kuchukua fomu hizo na kutokomea nazo!
Chanzo cha habari hizi kinaeleza kwamba hadi sasa Mgombea wa Kata ya Mukendo kupitia Chama cha CCM hajapewa fomu na Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi wa Kata ya Mukendo!
Ni wazi sasa kwa hicho kilichotokea Musoma, katika kata za Mukendo na Kwangwa, kinawaweka CCM na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwenye mtanziko mkubwa sana.
Kwa takriban wiki nzima sasa na usheee hivi, kumekuwepo na taarifa za Wasimamizi wa Uchaguzi katika majimbo fulani fulani kuwapatia fomu za Chadema wagombea ambao hawajapitishwa na Chadema na wala chama hicho hakiwatambui lakini Wasimamizi wa Uchaguzi wamewapatia fomu na kuwanyima fomu hizo wagombea sahihi walioteuliwa na Chadema.
Mifano ya haraka na mizuri ni katika majimbo ya Kilombero na Kibamba. Huko Kilombero Msimamizi aliamua kumpatia fomu kijana mmoja ambaye Wanachadema wenyewe wanajiuliza ametokea wapi, lakini Msimamizi akampatia fomu huku akiwa hana utambulisho wa kutoka mamlaka rasmi zinazohusika na itifaki ya mawasiliano kati ya Chadema na Msimamizi wa Uchaguzi kwa mujibu wa taratibu za uchaguzi, ambapo Katibu wa Jimbo huwasiliana na Msimamizi wa Uchaguzi na si vinginevyo.
Huko Kibamba ndiko ambako bila shaka itakuwa patashika na nguo zitachanikia uwanjani. Watu wanaodaiwa kuwa ni CCM au washirika wa mfumo na CCM au wote kwa pamoja, ukiwa ni ushirika wa kihalifu, kwa mara nyingine wameionesha Ofisi ya Mkurugenzi wa Ubungo inapaswa kupigwa MITAMA mikali sana kama Mbasha. Watu ambao Msimamizi wa Uchaguzi amegoma kuwataja, wameandika barua na kumtambulisha mtu mwingine, ambaye pia Msimamizi amegoma kumtaja, amechukua fomu za kugombea nafasi hiyo ya ubunge kupitia Chadema.
Ni kwamba Ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Kibamba, imeandikiwa barua feki, nayo ikawasiliana na mtu feki, kisha ikatekeleza kwa kuzingatia barua feki na kumpatia mgombea feki fomu. Maana yake hata fomu hiyo ni feki kwa sababu mchakato mzima huo umekuwa feki na hila. Wamempatia fomu mtu ambaye hajulikani (wao wanamjua), hajawahi kushiriki hata mchakato wa ndani wa Chadema, wala si mwanachama wa Chadema na hakuna mtu anamjua, lakini wanalazimisha kuwa fomu za Chadema zimechukuliwa.
Tangu matukio ya kihalifu ya Kilombero na Kibamba yatokee wiki iliyopita, NEC wamepatwa kigugumizi sana kuchukua hatua na maamuzi kwa masuala ambayo yako wazi kabisa kuwa ni njama na hila za CCM. Kuendelea kuyakalia kimya inamaanisha kuwa NEC inajua mkakati huo mpya wa kupora fomu kupitia kuwapatia watu wengine. Kisha inawaambia Chadema wakawatafute watu hao kupata fomu zao.
Kwa hicho kilichofanyika Musoma kwenye hizo kata mbili, itabidi CCM na NEC yao watokea tu tunduni walikojificha wakishirikiana kwa siri. Je nako huko pia watawaambia CCM wakawatafute hao waliochukua fomu?
Tunasubiri kuona na kusikia. Je, Msimamizi ataendelea kusimamia anachokiamini (wanachofanya kwa Chadema wakiamini ndiyo sahihi) au atabadili msimamo kwa kuwa tu wagombea hao ni wa CCM!?
Ngoma inogile sasa wakunyumba mbombo ngafu
Chanzo cha habari hizi kinaeleza kwamba hadi sasa Mgombea wa Kata ya Mukendo kupitia Chama cha CCM hajapewa fomu na Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi wa Kata ya Mukendo!
Ni wazi sasa kwa hicho kilichotokea Musoma, katika kata za Mukendo na Kwangwa, kinawaweka CCM na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwenye mtanziko mkubwa sana.
Kwa takriban wiki nzima sasa na usheee hivi, kumekuwepo na taarifa za Wasimamizi wa Uchaguzi katika majimbo fulani fulani kuwapatia fomu za Chadema wagombea ambao hawajapitishwa na Chadema na wala chama hicho hakiwatambui lakini Wasimamizi wa Uchaguzi wamewapatia fomu na kuwanyima fomu hizo wagombea sahihi walioteuliwa na Chadema.
Mifano ya haraka na mizuri ni katika majimbo ya Kilombero na Kibamba. Huko Kilombero Msimamizi aliamua kumpatia fomu kijana mmoja ambaye Wanachadema wenyewe wanajiuliza ametokea wapi, lakini Msimamizi akampatia fomu huku akiwa hana utambulisho wa kutoka mamlaka rasmi zinazohusika na itifaki ya mawasiliano kati ya Chadema na Msimamizi wa Uchaguzi kwa mujibu wa taratibu za uchaguzi, ambapo Katibu wa Jimbo huwasiliana na Msimamizi wa Uchaguzi na si vinginevyo.
Huko Kibamba ndiko ambako bila shaka itakuwa patashika na nguo zitachanikia uwanjani. Watu wanaodaiwa kuwa ni CCM au washirika wa mfumo na CCM au wote kwa pamoja, ukiwa ni ushirika wa kihalifu, kwa mara nyingine wameionesha Ofisi ya Mkurugenzi wa Ubungo inapaswa kupigwa MITAMA mikali sana kama Mbasha. Watu ambao Msimamizi wa Uchaguzi amegoma kuwataja, wameandika barua na kumtambulisha mtu mwingine, ambaye pia Msimamizi amegoma kumtaja, amechukua fomu za kugombea nafasi hiyo ya ubunge kupitia Chadema.
Ni kwamba Ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Kibamba, imeandikiwa barua feki, nayo ikawasiliana na mtu feki, kisha ikatekeleza kwa kuzingatia barua feki na kumpatia mgombea feki fomu. Maana yake hata fomu hiyo ni feki kwa sababu mchakato mzima huo umekuwa feki na hila. Wamempatia fomu mtu ambaye hajulikani (wao wanamjua), hajawahi kushiriki hata mchakato wa ndani wa Chadema, wala si mwanachama wa Chadema na hakuna mtu anamjua, lakini wanalazimisha kuwa fomu za Chadema zimechukuliwa.
Tangu matukio ya kihalifu ya Kilombero na Kibamba yatokee wiki iliyopita, NEC wamepatwa kigugumizi sana kuchukua hatua na maamuzi kwa masuala ambayo yako wazi kabisa kuwa ni njama na hila za CCM. Kuendelea kuyakalia kimya inamaanisha kuwa NEC inajua mkakati huo mpya wa kupora fomu kupitia kuwapatia watu wengine. Kisha inawaambia Chadema wakawatafute watu hao kupata fomu zao.
Kwa hicho kilichofanyika Musoma kwenye hizo kata mbili, itabidi CCM na NEC yao watokea tu tunduni walikojificha wakishirikiana kwa siri. Je nako huko pia watawaambia CCM wakawatafute hao waliochukua fomu?
Tunasubiri kuona na kusikia. Je, Msimamizi ataendelea kusimamia anachokiamini (wanachofanya kwa Chadema wakiamini ndiyo sahihi) au atabadili msimamo kwa kuwa tu wagombea hao ni wa CCM!?
Ngoma inogile sasa wakunyumba mbombo ngafu