CCM oneni aibu kung'ang'ania viwanja nchini visivyotunzwa

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
CCM ni chama kikubwa na kikongwe kinachoongozwa na watu wenye weledi mkubwa.

Hivyo CCM hakiwezi kufa au kushindwa kujiendesha kama kitarudisha serikalini viwanja vya mpira inavyovimiliki ili vijana wavitumie.

Viwanja vinapoteza hadhi na mpira hauchezeki kwenye viwanja hivyo wakati CCM inayo Sera ya kukuza michezo.
 
"Maendeleo Hayana Vyama"
Ama kweli ukiwa mwongo usiwe msahaulifu[emoji2211]
 
Una umri gani kijana? Hivyo viwanja ni mali ya watanzania wote. Ccm wamevitaifisha tu kwa kutumia mabavu.
Mimi ni CCM kindakindaki
Kusema ukweli sisi wapenda michezo
CCM inatufanyia vibaya kwenye viwanja hivyo hatuoni radha ya mpira pichi mbovu japo tulichangushwa sana wakati wa ujenzi
 
Hivi viwanja vingi vipo half way kumalizika, ukiondoa pitch kuwa mbaya ata majukwaa unakuta hayajaisha vizuri. Havina taa, ukiona wachezaji wanaingia dressing room kama wana ingia kwenye shimo la nyoka! Giza limetawala, no running water, vyoo vichafu, pembeni ya pitch ni vichaka. Ata ikipita miaka 10 bado hali itakua hivi hivi au mbaya zaidi kwasababu aliyepewa kumiliki hajui thamani yake, mwenye mali yake kanyang'anywa! Ubaya/uzuri ligi ina kuwa broadcasted live mpaka n'jee wanaona uchafu wetu. Itahitaji siku mwenyeketi wa chama awe anaona aibu kama sisi wapenda mpira tunayoiona kuja na solution ya hii kitu. Matumaini yangu yapo kwa Kassim Majaliwa kwenye hili. Magu kwa jinsi anavyo komaliaga vitu hili lilikuwa swala dogo ila naona ameangalia kwingine.
 
Mmiliki ni ccm , aliejenga sio habari kubwa
Kwa Akili Yako Ndio Unaona Sio Habari Kubwa Kwa sababu Kwa Sasa Ccm Ndio Mtawala. Ila Kuna Tarehe, Siku
Au Mwaka Hivyo Viwanja Vitarudi Serikalini Kama Zilivyo Rudi Shule Na Hospital.

Muda Ndio Mwalimu Mkuu.
 
Kwa Akili Yako Ndio Unaona Sio Habari Kubwa Kwa sababu Kwa Sasa Ccm Ndio Mtawala. Ila Kuna Tarehe, Siku
Au Mwaka Hivyo Viwanja Vitarudi Serikalini Kama Zilivyo Rudi Shule Na Hospital.

Muda Ndio Mwalimu Mkuu.
Viwanja vikirudi serikalini unitag mkuu
 
Vitunzeni basi hivyo viwanja! Daah baba zetu bila kujali itikadi zao walichangia ujenzi wa hivyo viwanja! l?Leo hii vimekuwa mali ya ccm? Kumbe hiki chama wizi kilianza zamani eeeh!
Endelea kuota mkuu
 
Vitunzeni basi hivyo viwanja! Daah baba zetu bila kujali itikadi zao walichangia ujenzi wa hivyo viwanja! l?Leo hii vimekuwa mali ya ccm? Kumbe hiki chama wizi kilianza zamani eeeh!
Mtu dhaifu lawama ni tabia yake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…