CCM oneni aibu kung'ang'ania viwanja nchini visivyotunzwa

Viwanjanni vya SERIKALI na si CCM, wao wamevipora tu na kuandika hati.
siku ipo na saa inakuja ambapo mali zote za nchi zitarudi.
CCM KIRUMBA, NANGWANDA SIJAONA, SHEIKH KARUME ARUSHA , SAMORA IRINGA NI MALI ZA WATANZANIA WOTE, ILA CCM WAMEJIMILIKISHA,
 
Endelea kuota mkuu
Hata Kipindi Nyerere Anadai Uhuru Kuna Watu Kama Wewe Walikua Wanamkatisha Tamaa Mwalimu Kwa Maneno Kama Yako. Lakini Baada ya Uhuru Kupatikana Hao Hao Walio Kuwa Wanambeza Wakawa Watu Wa Kwanza Kuingia Barabarani Kushangilia.

"Watu Kama Nyinyi Hamkosekani Kwenye Jambo Lolote".
 
Neno zito sana mkuu, ukombozi wa Tanganyika unakuja
 
Narudia tena endelea kuota mkuu
 
Kwani Hivi Viwanya Vyote Vimejengwa Na Ccm?.
Viwanja vilijengwa kabla ya mfumo wa vyama vingi,vilitakiwa wapewe halmashauri katika eneo husika, nashangaa wamejimilikisha wao na pia wanasheria wamelala kuhusu hii issue!!!
 
Well said, ndo maana ligi yetu haitoi mshi
Endelea kuota mkuu
Rais wetu ni msomi na katibu wake mkuu ni waelewa kwelikweli, hata wao kama viongozi wasoni kuwahi kutokea CCM sidhani kama wataruhusu CCM itafute pesa za kukarabati viwanja vya mpira.

Sidhani kama itawawia vigumu kuikabidhi wazara ya habari na michezo viwanja hivyo.
 
Kwanini wizara isitengeneze viwanja vyake badala ya kukaa nakusubiri huruma ya ccm au kwanini team zisiwe na.uwanja kama azam badala ya kukomalia viwanja vya ccm ?
 
Hoja gani wakati ushahidi hakuna hapa
Unachosema wewe ni Sawa na kusema magereza yote, barabara zote, shule zote na kila kitu kilichofanywa kabla ya vyama vingi nchini ni mali ya CCM. Huna hoja.
 
Unachosema wewe ni Sawa na kusema magereza yote, barabara zote, shule zote na kila kitu kilichofanywa kabla ya vyama vingi nchini ni mali ya CCM. Huna hoja.
Unalazimisha au.umeamua kujiaminisha ujinga , hilo ni tatizo lako watu wanazungumzia viwanja wewe unaleta magereza , CCM ina mali zake na.serikali ina mali zake , tena zinafahamika
 
Unalazimisha au.umeamua kujiaminisha ujinga , hilo ni tatizo lako watu wanazungumzia viwanja wewe unaleta magereza , CCM ina mali zake na.serikali ina mali zake , tena zinafahamika
CCM ilikuwa na timu zipi za mpira wa miguu hadi ijenge viwanja, ni timu zipi zilikuwa zinalipa hela ngapi kwenda kwenye mfuko wa CCM wakati wa siasa za chama kimoja? Sio kwamba unajisemea Tu wewe?
 
CCM ilikuwa na timu zipi za mpira wa miguu hadi ijenge viwanja, ni timu zipi zilikuwa zinalipa hela ngapi kwenda kwenye mfuko wa CCM wakati wa siasa za chama kimoja? Sio kwamba unajisemea Tu wewe?
Ahahahahahaha kumbe ujui kitu kijana , ebu kajifunze tena ndio urudi hapa
 
Ndani ya miaka kumi hayo maviwanja yatakuwa magofu, so far vimeshachoka maana havitunzwi......watu wanakusanya kodi za viduka vinayozunguka uwanja tu.
 
Hivyo viwanjwa vingereshwa chini ya Halmashauri vingetunzwa vizuri zaidi na vingekuwa bora kuliko ilivyo sasa.

Vv
 
Ni kusubiri wakati tuu ufike nao tuwanyanganye kama wao walivyopora viwanja hivyo vya wananchi. Wanang'ang'ania wakati kuvitunza hawawezi na hela wanachukua.
 
Nmeandika threads nyingi sn humu kuhusu CCM kutelekeza hv viwanja. Hawa jamaa sjui wanaona raha gani wanapoona kwenye tv wachezaji wetu wakihangaika kumiliki mpira na wengine wakiishia kuumia. CCM hawana aibu,wivu wala soni wanapoona viwanja vya nchi zingine . Wao ni siasa mwanzo mwisho 24/7.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…