CCM pawaka moto Dodoma

Inv, usimuunder estimate jamaa, kule nyuma amezungumzia recorders za kwenye peni, frame za miwani mpaka zile za kwenye sole za viatu.

Mimi namuaminia, jamaa karekodi kila kitu toka jana, shughuli yake ni kuupload hiyo 4GB!.
Pokea simu basi...

I wanna assist him/her doing something bigger than than within a fraction of a minute
 
Mzee kama umepewa green light ya mambo we weka tu hapa uwanjani labda uwape kazi hawa mods katika kuiedit na kuifanyi ukarabati manake naamini kuna maneno mengine humo ukimuona mtu huwezi kumheshimu tena hata akiwa baba ako kwa utumbo wanaoufanya huko. Hivi wanalipwa per diem hawa? Kama ngapi hivi? Manake unaweza wakina Rostam wamefadhili kikao sasa wataadhibiwa kweli?
 
Mkuu,

Kwa hili naomba nitofautiane na wewe.

Sioni busara ya kuweka Audio tape haa jamvini ya kikao halali cha chama.

Ningeshauri utaratibu wa mmoja wetu kusoma na kutupatia briefing kama ambavyo FM ES huwa anafanya.

YY

Mimi natofautiana na wewe kidogo mzee wangu. Mi nafikiri ili kusaidia jamii na kujua ni watu wa aina gani wanaendesha serikali yao ni vizuri hii iwe upload yote.

watu wajue nini kinaendelea behind closed door, na that will be motivation for change in leadeship.. Miaka mingi watanzania tunakuwa tunadanganywa na hawa watu na sidhani ni vyema kuendelea kuwabeba kwa kuamini kwamba si busara kutoa yale ambayo yatawasaidia jamii nzima kwasababu ya kuishimu chama cha watu wachache.
 
Ila Invisible una uhakika na usalama wa jamvi letu? Manake kuikosa JF its unbearable zile siku mbili au moja zilikuwa ni kama mwaka kila dk nilikuwa nachek kama imerudi
 
soon kutakuwa na uchaguzi CHADEMA.....tutaomba tena kwa msisitizo AUDIO-UPLOADING ya the whole saga.....!
 
Uchaguzi wa CHADEMA ambao uliahoirishwa kutokana na SKENDO YA RUSHWA CHADEMA.....!
Tutajua ni jinsi gani MBOWE IS AGAINST ZITTO & HIS ALLIES
 
soon kutakuwa na uchaguzi CHADEMA.....tutaomba tena kwa msisitizo AUDIO-UPLOADING ya the whole saga.....!
Pole mkuu;

Nothing personal here... Akija mtu na madai kuwa ana audio ya kikao tutamkomalia atoe japo vijidakika vitatu hivi, kuonyesha uhakika wa anachoandika!
 
Pole mkuu;

Nothing personal here... Akija mtu na madai kuwa ana audio ya kikao tutamkomalia atoe japo vijidakika vitatu hivi, kuonyesha uhakika wa anachoandika!

Ni kweli wakati wanapokuja ifanyike hivyo,hapo litakuwa jambo la msingi mkuu ili JF isiweze kuendeshwa kwa habari za upotoshaji,yani tutaweza kuepuka half baked stories and innuendos.
 
Jamani mbona tunadanganyika kirahisi namna hii hao jamaa wawili wa 16 na kilewo inawezekana kweli walikuwa kwenye kikao lakini wako kikazi zaidi ya kuihabarisha JF inawezekana wanataka kujua ni vipi tunapa sources za mambo humu nachotaka kuwaambia wengine humu ni ma psychologist wana uwezo wa kumsoma mtu nini anataka hata kwa maandishi yake believe me or not sisi tusubiri yatakayojiri hata kama yatatolewa na Chiligati tutayajadili hayo hayo na kuyapima ukweli wake.
 
Mkuu,

I salute you! Hatukatai kila hoja anayoleta mtu, tunapenda mtu aje na walau uthibitisho wa kauli yake. Sasa kama kilewo na mwenzake walikuja kuyapima maji kina basi huenda yameishia kwenye magoti tu...

Naamini watarejea na walau dakika 3 tulizoomba na wakaahidi kuleta hahahaha!
 
Source TBC.

Taarifa toka Dodoma, ni kuwa wajumbe karibu wengi kwenye mkutano wa NEC ya CCM wanapendekeza kamati ya Mzee Mwinyi iongezwe muda ili kuweza kuendelea kumalizia tofauti zilizopo baina ya wana CCM.

Katibu mwenezi wa CCM, kutoa taarifa rasmi mara tu baada ya mkutano kumalizika hata iwe saa nane ucku, atakuwa na press confrence muda huwo!!!!!!!
 
Hivi hizi kamati zinatoa wapi pesa ? Isije ikawa wanatengeza 'ajira milioni moja' kwa fedha za taxpayers.
 
Usanii Mtupu! Hawatafanya lolote lile jipya la kukibadilisha chama hiki kilichoamua kuwa chama cha mafisadi badala ya chama cha mapinduzi.
 
Uzuri ni kwamba JF haitishiwi nyau. Kama walidhani tutawapapatikia kuomba tukutane nao falagha ili watupe hizo audio basi wamenoa. JF inavyanzo vyake vya taarifa muhimu na kazi hizo huwa zinafanywa kwa moyo na ustadi wa hali ya juu.

Nawapa pole wale wanaokuja na mawazo ya kifisadi na kuweka mitego eti..."ninayo audio lakini nimejiunga juzi nisiwaharibie jf...." hawa wana mawazo kwamba tutawapapatikia na kusema hebu invisible awasiliane nao na hapo tuangamize wanachama wetu. Hapo wamenoa ....narudia tena.
 

Kamati ya mapendekezo imebadilika na kuwa "Kamati ya mapendekezo ya kumaliza tofauti" Ha ha ha! Usanii on the make,i mean at its best! Je hiyo kamati ni ya usuluhishi?

Wanachotakiwa ni kutoa mapendekezo kama ilivyosemwa hapo awali,halafu si lazima mapendekezo hayo yaondoe tofauti kwasababu sidhani kama kamati hiyo inahusiana kwa namna yoyte ile na "Usuluhishi"

Kamati imeongezewa muda lakini muda huo ni wa kufanya mambo ya tofauti na msingi wa uundwaji wa kamati hiyo,yani sasa ni yale mambo ya "Cheusi ,chekundu" Did you see it or not?was it black or red? Yani ni "Now you see it,and now you don't" Kaazi!
 

Wakituletea sawa , mimi nilianza kuwa na wasi wasi mapema tu walipoulizwa wanawezaje kuripoti toka ndani ya kikao wakasema eti hawakukaguliwa hadi kwenye soli za viatu na kalamu zao pia nikajiuliza hawa majasusi wameenda na vifaa hivyo kwa ajili ya kuhabarisha JF tu au? wanawezaje kuji expose namna hii kwa dangerous job bila kulipwa chochote, tukawauliza wawe wanatutajia majina hawakujibu, kama wao ni CIA wengine humu ni Ex FBI
 
Tutasubiri taarifa ya katibu mwenezi si ndo huwa anakuwa responsible manake naona jamaa alipopewa nafasi ya kuupload kaingia mitini kabisa wa 16 na mwenzio kilewo hasa wa 16 ulikuwa unatoa updates hapa mpaka sasa nawaona ni wababishaji au na mko huko na hapa mmetumwa tu la kama ukiniprove wrong naahidi kuwaomba radhi lakini as things stand now with no proof no names habari yenu haijawa valid na haina heshima ya kuajadiliwa kiasi hiki hapa na ndo maana tulipokuwa tuanomba majina ya wanaochangia hizo mada mkawa mnababaisha mbona 6 mlimtaja?

JF IS MORE CLEVER THAN U THINK
 
hata kwa kuongezewa muda -hakuna lolote,lakini CCM kuna ufa tena mkubwa,mwenyekiti ajaribu kuziba nyufa hizo,jmba lisije dondoka mikononi mwake-tutamkaumu,sana kwani CCM tunaipenda sana,lakini sasa tunafikia ukingoni.
 
..Naona terms of reference zimebadilika tena....badala ya kutafuta matatizo ya misuguano ndani ya chama, sasa kamati imekuwa ya usuluhishi......Huu ni usanii..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…