tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 24,225
- 22,632
Naona mafisi bado wanazidi kugombea mfupa uliooza. Mungu anawaona.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna mambo kadhaa ambayo CCM wanataka kutuchanganya hapa. Lakini kama usemi unavyoenda - you can fool some people sometimes but not all the people all the time.
Je, Kinana na Makamba wameonana na Kamati ya Maadili ya CCM au wamekutana na Makamu Mwenyekiti na Katibu Mkuu wa CCM?
Tunaelewa kwamba Kamati ya Maadili ilikuwa Dodoma, ambako ndiko Membe alihojiwa. Je tuseme ilibidi wajumbe wa kamati ya maadili wakimbizwe kuja Dar Salaam kuwahoji Kinana na Makamba baada ya kuachwa solemba wakiwasubiri kule Dodoma?
Tuambieni ukweli kwamba:
Ikiwa hivyo ndivyo, nawapongeza sana Kinana na Makamba kwa busara walizotumia hadi sasa. Natumaini walimwambia Makamu Mwenyekiti na Katibu Mkuu wa CCM kwamba awamu ya tano waache tabia chafu ya kudukua maongezi binafsi ya viongozi waliostaafu na waliopo madarakani, kwa kuwa sio tu ni tabia ya kimbea bali pia inavunja sheria za nchi.
- Kinana na Makamba wamegoma kwenda Dodoma kuifuata Kamati ya Maadili
- Kinana na Makamba wameifichia CCM aibu kwa kuonyesha kwamba wameitikia wito kwa masharti kwamba hawatakwenda Dodoma bali watakuja Dar esSalaam kuonana na Makamu Mwenyekiti na Katibu Mkuu wa CCM
- Kinana na Makamba wamewapa masharti CCM kwamba lazima mapokezi yao yaonyeshe hakuna bifu kati yao na CCM kwa viongozi wakuu wa CCM kuwapokea kwa shangwe pale Lumumba kwa ajili ya kupigwa picha.
Sent using Jamii Forums mobile app