Pre GE2025 CCM wamepita mitaani kuandikisha wapiga kura, je ni haki yao kikatiba?

Pre GE2025 CCM wamepita mitaani kuandikisha wapiga kura, je ni haki yao kikatiba?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Wasaam,

Leo nilikua mitaa ya Vingunguti nilienda salamia jamaa zangu nikashangazwa na viongozi wa CCM kupita nyumba hadi nyumba kuandiksha wapiga kura kwa kuwapa ahadi za kuja kuwagawia pesa na mikopo mbalimbali wakati uchaguzi ukiwadia.

Kiukweli hii ni rushwa ya kisiasa kama sio kampeni kabla ya kuruhusiwa kampeni, au tuseme labda ni haki yao kikatiba?

Naamini ingekuwa ni CHAMA chengine cha siasa basi police wangeshawazingira na msajili wa vyama vya siasa angeitisha press haraka na kulaani.
Watu wa 2024 siyo wa 1947. Wanahangaika sana Kwa kuwa hawaaminiki tena!
 
Wasaam,

Leo nilikua mitaa ya Vingunguti nilienda salamia jamaa zangu nikashangazwa na viongozi wa CCM kupita nyumba hadi nyumba kuandiksha wapiga kura kwa kuwapa ahadi za kuja kuwagawia pesa na mikopo mbalimbali wakati uchaguzi ukiwadia.

Kiukweli hii ni rushwa ya kisiasa kama sio kampeni kabla ya kuruhusiwa kampeni, au tuseme labda ni haki yao kikatiba?

Naamini ingekuwa ni CHAMA chengine cha siasa basi police wangeshawazingira na msajili wa vyama vya siasa angeitisha press haraka na kulaani.
Ulitaka nani apite
 
Guys, aisee mna lalamikia kitu ambacho binafsi naona ni nyie kutumia akili zenu ndogo tuu, kama unaona hutaki kadi ya chama chao si unakataa tuu au mnalazimishwa?

Mnaosema hy n rushwa em nambien n rushwa kvp wakati hawatoi pesa na wanaoandikishwa wanakubali wao wnyw?
Mbona kwenye mikutano ya chadema wanachama walikuwa wanaoandikishwa lkn cjawah kuona malalamiko yenu?
 
Uchaguzi wa 2025, CCM watatumia fedha nyingi sana ili kuhonga. Waarabu watamsaidia Samia ili abaki kuwa rais na wao waendelee kukomba nchi. Upinzani wanatakiwa kuanzisha kampeni ya ''kula kwa CCM, kura kwa upinzani''. Tukatei huyu kibaraka wa waarabu!
Wapinzani gani mzee? Waliopo wote ni wachumba tu mbele ya CCM.

Mwaka 2015 CCM alikuwa hatoboi ule uchaguzi ingawa walimuweka jembe magufuli ili wachane mkeka ila raia walikomaa kiume ndio maana namba ya wapinzani ikaongezeka pale bungeni.

Ila yule boya na tamaa zake za hela, akauza chama kwa lowassa hadi leo ile dhambi ya kusaliti raia wapigania haki na uzalendo inamchoma moyoni. Mzee snitch sana yule sio wa kumpa inchi. Yaani ni mara mbili tundulisu.
 
Kama haya uliyo eleza hapa yana ukweli wowote, hata theluthi moja tu ya ukweli (na sina sababu ya kukuhoji juu yake); ule unaoitwa "UJINGA" wa waTanzania unaanzia hapa hapa kuruhusu haya yaendelee kuwepo.

Lakini, kama nilivyo wahi kueleza, huu siyo "ujinga" wa waTanzania; bali ni sehemu ya mwendelezo wa "UTEKAJI" wa waTanzania na genge hili ndani ya CCM.

Hii ndiyo hatua inayotakiwa kukataliwa kwa nguvu zote na wote wanaojiamini wao siyo wajinga wala mateka.

Kuruhusu upuuzi wa namna hii kuendelea kuwepo ni dhambi kubwa sana waTanzania wa leo wanayoitendea nchi yao.

Inabidi nieleze uhusiano wa zoezi hili na "utekwaji" wanaofanyiwa waTanzania bila wao kujitambua.
Waziri wa Mambo ya Ndani (Msabuni, ndiyo najua jina lake); hivi karibuni amenukuliwa akihimiza wajumbe wa nyumba kumi kuwafikia wananchi kwa zoezi hilo; na kajitapa kwamba yeye ndiye mkuu wa "mapolisi".
Sasa kinacho shangaza, vyama vya upinzani, hususani CHADEMA ni kama hawaelewi kinachozungumzwa na mtu kilaza kama huyo.

CCM tayari wamo kazini kuvuruga uchaguzi wa serikali za mitaa, kwa maandalizi ya kuvuruga uchaguzi mkuu!

Halafu kila mtu anajifanya kama hajui chochote kinacho endelea!
Ni kama unaona CHADEMA ndio tatizo kubwa kwa yanayoendelea nchini.

Unatarajia CHADEMA wafanye nini hasa?
 
Ni kama unaona CHADEMA ndio tatizo kubwa kwa yanayoendelea nchini.

Unatarajia CHADEMA wafanye nini hasa?
Tatizo ni CCM, tusijaribu kuvuruga mwelekeo tunao ujua sote.

Ndiyo, matumaini makubwa kwa sassa hivi ni CHADEMA zaidi ya chama kingine chochote cha siasa, na hili halihitaji maelezo, hasa kwa mtu kama wewe.

"Matarajio kwa CHADEMA"? Kuna asiyejuwa yanayofanywa na CCM kuvuruga chaguzi? Huu ni uhalifu. Uvunjifu wa sheria.
Mahakama iliyo wazi ni ya wananchi wenyewe, wapiga kura, ambao kura zao tayari mipango inafanyika kuziharibu.
Bado unaniuliza nataka CHADEMA wafanye nini? Waende mahakamani na mahakama itaamua yenyewe ifanye nini.

Mkuu 'Drifter', kila tunapokutana unakuwa 'defensive' sana kuhusu wajibu wa CHADEMA kwa wananchi wa nchi hii.

Masauni kuanza kuwatumia wajumbe wa nyumba kumi kumi huko mitaani; CHADEMA kweli hawana jibu juu ya upumbavu wa aina hiyo? Sasa watafanya kazi gani CHADEMA na wawe na mategemeo gani kwenye chaguzi hizi kama njia zilezile zinazofahamika miaka yote zinaendelea kutumika kuvuruga chaguzi.
Hebu wewe nieleze matumaini ya CHADEMA hasa yapo wapi?
 
Ujinga wa Mwananchi ni Utajiri wa Chama pendwa!
 

Attachments

  • FB_IMG_1478834455434.jpg
    FB_IMG_1478834455434.jpg
    55.6 KB · Views: 1
Tatizo ni CCM, tusijaribu kuvuruga mwelekeo tunao ujua sote.

Ndiyo, matumaini makubwa kwa sassa hivi ni CHADEMA zaidi ya chama kingine chochote cha siasa, na hili halihitaji maelezo, hasa kwa mtu kama wewe.

"Matarajio kwa CHADEMA"? Kuna asiyejuwa yanayofanywa na CCM kuvuruga chaguzi? Huu ni uhalifu. Uvunjifu wa sheria.
Mahakama iliyo wazi ni ya wananchi wenyewe, wapiga kura, ambao kura zao tayari mipango inafanyika kuziharibu.
Bado unaniuliza nataka CHADEMA wafanye nini? Waende mahakamani na mahakama itaamua yenyewe ifanye nini.

Mkuu 'Drifter', kila tunapokutana unakuwa 'defensive' sana kuhusu wajibu wa CHADEMA kwa wananchi wa nchi hii.

Masauni kuanza kuwatumia wajumbe wa nyumba kumi kumi huko mitaani; CHADEMA kweli hawana jibu juu ya upumbavu wa aina hiyo? Sasa watafanya kazi gani CHADEMA na wawe na mategemeo gani kwenye chaguzi hizi kama njia zilezile zinazofahamika miaka yote zinaendelea kutumika kuvuruga chaguzi.
Hebu wewe nieleze matumaini ya CHADEMA hasa yapo wapi?
Relax. Nimesoma maandishi yako kadhaa. Kuhusu CCM kuwa tatizo hiyo ni fact na reality yetu. Hakuna asiyejua na haina mjadala.

Kuhusu suluhisho, nimekusoma ukilalamika kuwa Watanzania wako tayari kubadilisha hali lakini CHADEMA ni kama vile hawajielewi. Yaani “hawachukui nafasi yao” kama chama kikuu cha upinzani. You can still correct my understanding of your main concern.

Ndio maana nakuuliza wewe binafsi unatarajia CHADEMA wafanye nini ili kufanikisha huo “utayari” wa Watanzania kuondoa tatizo CCM?
 
Nimeiona hii pia Babati -Vijijini juzi.Mfanyakazi mwenzangu alikuwa analalamika kwamba amepigiwa simu na mkewe kuwa nyumbani amefika Balozi wa CCM na watu kadhaa wamemuomba vitambulisho vya kupigia kura chake na hata cha mme wake kama amekiacha,ili waviandikishe.Jamaa alipandwa jaziba sana akamwambia --Wapatie tu na uondoke nao kabisa--.Sijui nini kiliendelea huko,ameenda likizo kwake leo ngoja akirudi nitamuuliza kilikuwa ni nini na kipi kimejiri.JF haijawahi kutindikiwa nyeti za kila nyanja.
 
Relax. Nimesoma maandishi yako kadhaa. Kuhusu CCM kuwa tatizo hiyo ni fact na reality yetu. Hakuna asiyejua na haina mjadala.

Kuhusu suluhisho, nimekusoma ukilalamika kuwa Watanzania wako tayari kubadilisha hali lakini CHADEMA ni kama vile hawajielewi. Yaani “hawachukui nafasi yao” kama chama kikuu cha upinzani. You can still correct my understanding of your main concern.

Ndio maana nakuuliza wewe binafsi unatarajia CHADEMA wafanye nini ili kufanikisha huo “utayari” wa Watanzania kuondoa tatizo CCM?
Duh!
Mkuu 'Drifter', hivi labda sijielezi vizuri ili nieleweke, maana unaendelea kuniuliza swali ambalo nilidhani mara nyingi sana huwa ninalijibu, na hata hapo juu nimejibu.
Hakuna la ziada wanalotakiwa CHADEMA kulifanya zaidi ya kufanya kazi na wananchi wenyewe.
CHADEMA hawana uwezo wa kuwaondoa CCM bila ya wananchi kuifanya kazi hiyo
Jambo hili hili nimeliimba miaka kadhaa sasa, na bado naulizwa maswali juu yake?

Huyo Waziri wa Mambo ya ndani (Masabuni), anajuwa wapi pa kwenda kuwalaghai wananchi; huko mitaani kwao, nyumba kwa nyumba. Itakuwaje CHADEMA wasijue pa kwenda ili kukomesha ujinga wa kiongozi kama huyo!

Kazi ya CHADEMA safari hii ni nyepesi zaidi kuliko nyakati zingine zozote ilizo wahi kupambana na CCM. Historia nayo inaonyesha wazi kwamba chama hicho kinapojipanga na kukataa hujuma za CCM hupata mafanikio makubwa. Rejea mwaka ambao CHADEMA ilifanikiwa kuwa na wabunge wengi zaidi Bungeni. Wengi wa wabunge hao walipatikana kwa kukataa hujuma za CCM.

Sasa utanilaumu, kwa kukumbushia kazi nzuri iliyowahi kufanyika huko siku za nyuma, lakini ikawa kama historia hiyo haipo tena!
 
Kuandikisha wapiga kura ni "JUKUMU la TUME YA UCHAGUZI" SIYO LA CHAMA CHOCHOTE CHA SIASA.
 
Wasaam,

Leo nilikua mitaa ya Vingunguti nilienda salamia jamaa zangu nikashangazwa na viongozi wa CCM kupita nyumba hadi nyumba kuandiksha wapiga kura kwa kuwapa ahadi za kuja kuwagawia pesa na mikopo mbalimbali wakati uchaguzi ukiwadia.

Kiukweli hii ni rushwa ya kisiasa kama sio kampeni kabla ya kuruhusiwa kampeni, au tuseme labda ni haki yao kikatiba?

Naamini ingekuwa ni CHAMA chengine cha siasa basi police wangeshawazingira na msajili wa vyama vya siasa angeitisha press haraka na kulaani.
Ccm watafanya vyovyote wanavyotaka,ila unabii ni lazima utumie. Ccm jiandaeni kisaikolojia Maana mbingu ilishaamua tunasubiri wakati tu.
 
Ccm ina mbinu nyingi za ushindi hadi za ziada kutegemea tu mazingira ya eneo husika la uchaguzi.
 
Wasaam,

Leo nilikua mitaa ya Vingunguti nilienda salamia jamaa zangu nikashangazwa na viongozi wa CCM kupita nyumba hadi nyumba kuandiksha wapiga kura kwa kuwapa ahadi za kuja kuwagawia pesa na mikopo mbalimbali wakati uchaguzi ukiwadia.

Kiukweli hii ni rushwa ya kisiasa kama sio kampeni kabla ya kuruhusiwa kampeni, au tuseme labda ni haki yao kikatiba?

Naamini ingekuwa ni CHAMA chengine cha siasa basi police wangeshawazingira na msajili wa vyama vya siasa angeitisha press haraka na kulaani.
Kama una ushahidi wa usemayo, ama nenda wewe mwenyewe kuripoti Tume ya Uchaguzi; au wasilisha tuhuma zako kwenye Chama chako upendekeze wafanye hivyo badala yako.

Aidha, kama uyasemayo ni kweli, hapo kuna makosa mawili; kwanza kufanya kampeni hivi sasa hairuhusiwi kwa kuwa haijatangazwa kampeni zianze. Pili, hata kama tayari kampeni zingekuwa zimeidhinishwa, hakuna chama binafsi kinachoruhusiwa kuandikisha wapiga kura.

Ni Tume ya Uchaguzi pekee inayofanya kazi hiyo. Hivyo, kushinda kwa suala lako likifika mahali panapohusika ni asilimia 100. Labda tu ushindwe kuthibitisha kwamba unayoyatuhumu kweli yalitokea.
 
Wapinzani gani mzee? Waliopo wote ni wachumba tu mbele ya CCM.

pa inchi. Yaani ni mara mbili tundulisu.
Acha unazi wa kihayawani wewe ...Matokeo yalipinduliwa tu,CCM na Magufuli walichakazwa na Hayati Lowasa.Ni mtu wa kariba yako tu mwenye kuamini eti Magufuli alimshinda Lowasa.Huyo Mmasai alichakaza mpaka kanda ya ziwa ambako Magufuli anakotoka,tena Mkoani Geita ndiyo kabisaaaa,mpaka Chato na Magufuli ameenda akiwa analijua hili.Fuatilia kama Magufuli aliwahi kurudi kufanya mkutano Mjini Geita katika mihula yake ya utawala nje ya kipindi cha kampeni.Ajenda kuu mpaka sasa ni CCM wango'ke kwanza....Fursa ya mbinu yoyote yenye kuweza kufanikisha hili kwa amani ni lazima itumike.CCM wanatumia mbinu kubaki madarakani,na wataondolewa kwa mbinu pia.
 
Wasaam,

Leo nilikua mitaa ya Vingunguti nilienda salamia jamaa zangu nikashangazwa na viongozi wa CCM kupita nyumba hadi nyumba kuandiksha wapiga kura kwa kuwapa ahadi za kuja kuwagawia pesa na mikopo mbalimbali wakati uchaguzi ukiwadia.

Kiukweli hii ni rushwa ya kisiasa kama sio kampeni kabla ya kuruhusiwa kampeni, au tuseme labda ni haki yao kikatiba?

Naamini ingekuwa ni CHAMA chengine cha siasa basi police wangeshawazingira na msajili wa vyama vya siasa angeitisha press haraka na kulaani.
elections is a process, elections is very expensive ni vizuri ikaeleweka vizuri hii 🐒

hata hivyo,
unadhani ushindi wa kishindo hua ni tukio la ghafla? CCM ni familia,
na kama ndugu wa familia moja mchakato wa kukumbushana wajibu muhimu wa kila mwanachama huanzia nyumbani....

kama sio hivyo,
unadhani dhumuni la balozi wa nyumba kumi wa CCM ni nini basi? na kwanini anasimamia nyumba kumi tu, na sio ishirini n.k, japo ikimpendeza hata 30 anaweza kuzisimamia na kuzitembelea ilimradi anafahamika eneo hilo....?

kuhitimisha,
hiyo ndio mikakati ya ushindi wa kishindo uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu wa mwaka ujao. Ni muhimu kurilax kabisa...

CCM hukutana nyumbani na mikutanoni majukwaani. na kwenye chaguzi, hainaga haya wala mzaha hata kidogo 🐒
 
Back
Top Bottom