Wakuu,
Siko mbali sana kutoka kwenye jiko la Chama Cha Mapinduzi (CCM) ofisi ndogo a hata makao makuu kwenyewe. Hii nimeipata muda huu kuwa mikakati iliyokuwa imepangwa kupata ushindi wa kishindo wa asilimia 89% imekwama na sasa inasukwa namna ya kupata ushindi wa 83%.
Hatua hiyo inatokana na kutishwa na ujio wa Dk. Slaa katika kinyang'anyiro, amewatisha.
Mbinu zitakazofanyika kupata ushindi huo zinapangwa sasa na jamaa wakiongoziwa na wazee wa riging; ambao wanajua kazi zao.
Ntawajulisha muda
ungesema imeshinda kwa asilimia 38 ningekuelewa
ungesema imeshinda kwa asilimia 38 ningekuelewa
Nadhani ana maana ktk ule uchaguzi wao ambao chama pekee cha upinzani kilichoshiriki kilikuwa ni TAKUKURU,ambacho kiliambulia viti vichache sana kimojawapo kikiwa ni cha Iringa Mjini!!!!
nakumbuka ile ligi ya uengereza, timu hubmizwa magoli 7.
nikiangalia naona hamna tofauti na siasa za tz, Jk anavyoshambulia kwa kichwa, miguu na hata kupiga tiktaka , hupiga chenga atakavyo, hupiga mashiti ya mbali na hata mashuti ya karibunaona kipa wa chadema na mabeki wamechoka na hujiangusha ovyo na wengine hupiga viatu na tayari baadhi ya wachezaji wake kuanza kupewa kadi manjano na wengine nyekundu huku zikiwa zimebaki dakika za nyongeza jk 7 dk slaa 1
Kama uhuru wa kuongea ndiyo hivi basi JF na Mods hawajui maana yake.nakumbuka ile ligi ya uengereza, timu hubmizwa magoli 7.
nikiangalia naona hamna tofauti na siasa za tz, Jk anavyoshambulia kwa kichwa, miguu na hata kupiga tiktaka , hupiga chenga atakavyo, hupiga mashiti ya mbali na hata mashuti ya karibunaona kipa wa chadema na mabeki wamechoka na hujiangusha ovyo na wengine hupiga viatu na tayari baadhi ya wachezaji wake kuanza kupewa kadi manjano na wengine nyekundu huku zikiwa zimebaki dakika za nyongeza jk 7 dk slaa 1
Kama uhuru wa kuongea ndiyo hivi basi JF na Mods hawajui maana yake.
Wewe unafikiri viongozi wa CCM wanatofauti gani na watu kama hawa, viongozi wanajua madudu wanayoyafanya kwa makusudi kwa kiwango chao huko waliko na hawa waliotumwa humu wanafuata maelekezo ya viongozi hao hao huku wakijua wanafanya kwa makusudi. Kwa hiyo hakuna tofauti wanachozidiana ni viwango na sehemu za kazi tu. Kinana na Makamba wanatumia jukwaa kusema Kikwete alianguka kwa saumu hawa wanatumia umember wa JF kusema kitu kile kile.Mkuu kama watendaji wa CCM akili zao ni kama hizi za hawa sniffers walioletwa hapa, nchi inahitaji mapinduzi ya kweli. Wakiamka akina Mpambalyoto watashangaa sana wao walipambana na risasi za Mjerumani sisi tunashindwa ha kupambana na ujinga wa wanasiasa
Ni kweli CCM wameshashinda kabla ya kupiga kura. Issue ni by how much? Kwa nini wameshashinda? Kwanza Tume ya Uchaguzi ni taasisi ya CCM kiaina kama ilivyo UWT. Uongozi wote wa NEC ni makada wa CCM. Wanaubiri maji mchana usiku wanakunywa mvivyo (wine). Mwandishi Tegambwage ameadika makala akisema yale maadili ya NEC waliosaini vyama vyote ni kulinda maslahi ya chama tawala. Kampeni hazipaswi kuikosoa CCM ila kusema wewe utafanya nini kwa watanzania. What a mockery!
Wote tunamuona Msajili wa nyama Judge Tendwa alivyo shabiki mkubwa wa CCM na hili halina ubishi.
Kilichotokea kwa wagombea wa vyama vya upinzani kuenguliwa mapema ni sawa na kupiga kipenga kwenye mbio za riadha mchezo ukatishwe huku ukiruhusu wengine waendelee na mbio. Hata kama NEC itabadilisha matokeo na kuruhusu wagombea waigie kwenye kinyanganyiro tayari kuna ushindi wa Kisaikolojia kwa CCM. Binafsi naona kheri uchaguzi wa 2005. Safari ni upuuzi mtupu!