Uchaguzi 2020 CCM wanahitaji ushindi wa 85%, lakini mbinu wanayofikiria kuitumia ni kupitia mawakala, wakifanikiwa hilo watajipa ushindi wa 92%

Uchaguzi 2020 CCM wanahitaji ushindi wa 85%, lakini mbinu wanayofikiria kuitumia ni kupitia mawakala, wakifanikiwa hilo watajipa ushindi wa 92%

Kadoda nguku

JF-Expert Member
Joined
Apr 22, 2019
Posts
332
Reaction score
475
CCM wamekuwa wakijinasibu kwamba watashinda kwa kishindo,lakini mbinu pekee wanayofikiria kuitumia ni hii ya mawakala.

Zipo namna mbili za kutumia, mosi ni kuwatimua mawakala wote na vituoni wabaki mawakala wa ccm tu kwa kila kituo, hii mbinu ikifanikiwa matokeo yake hayatakuwa tofauti na yale ya serikali za mitaa, na kwa kuwa CCM hawana chembe ya aibu wataitangazia dunia kwamba wameshinda uchaguzi mkuu kwa kishindo na baada ya hapo maisha yanaendelea kama kawaida ijapokuwa kutakuwa na matukio mengi ya visasi kama mnavyojua Jiwe ni mtu anayependa hayo.

Njia ya pili ni kutoruhusu mawakala kutopata nakala ya matokeo. Ili wapinzani washindwe kwenda hata mahakamani kwa kukosa uthibitisho.

Wapinzani wakifanikiwa kudhibiti hayo maeneo 2 CCM hawatafikisha hata 45% nimefanya utafiti kwa makundi mbalimbali ya wafanyakazi, machinga, wafanyabiashara na wakulima wameendelea kusisitiza kwamba hawajasahau Yale yaliyofanyika miaka 5 ,na wanasema kura nu siri, na maamuzi yako mioyoni mwao.

Kwa sababu kila kona ya nchi hii watu wameagizwa kuhakikisha chama kinashinda kwa kishindo kwa zaidi ya 81% kila eneo na kuna baadhi wameahidiwa na hyo mbinu ya mawakala ndio itakayotumika ni vema upinzani kuhakikisha inakuja na mbinu mbadala ya kukabiliana na hiyo mbinu haramu.

Wapinzani wakifanikiwa hayo ni dhahiri kwa Mara ya kwanza kizazi hiki kinaingia katika historia ya kushuhudia chama kilicholeta uhuru kinaondoka madarakani, na hii historian ya kudumu

Suluhu nzuri ni Chadema kuweka mawakala wengi. Mfano, kila eneo mawakala wa ACT, Chauma wanakuwa ni watu toka chadema ili wakiwazuia wachadema bado anabaki yule wa chauma na ACT, Wakimtoa wa chadema na ACT, anabaki wa chauma. Na kama kuna sehemu vyama vingine vinashangaa shangaa unampa barua mtu wa chadema unagonga mhuri wa katibu wa nccr wilaya anaenda kuwa wakala wa NCCR anachoma ndani anakwenda kufanya kazi ya kumtetea mgombea wa Chademà.
 
Ccm haiwezi kuiba kura, Rais Magufuli anapendwa sana na Watanzania

Pia usije ukamfananisha lowasa na huyo msaliti wa Nchi
Tukumbushane , mwaka 2015 walishindwa nni kuwatumia hao mawakala hadi wakaishia kupata kura 58% ?
 
Karata waliyona ccm nikuiba kura mwaka huu mtaumbuka
 
Lowasa alikuwa pandikizi Lisu Ni mpinzani kiasili
Yeah,upo sahihi. Na hicho ndicho kinachomtesa ccm. Safari hii upinzani umepata mpinzani asilia. Walitegemea sana tumsimamishe yule Nyalandu ili wapate cha kusema kwamba aliiba twiga ,fisadi sasa hoja kama hizo hazipo tena
 
Ccm haiwezi kuiba kura, Rais Magufuli anapendwa sana na Watanzania

Pia usije ukamfananisha lowasa na huyo msaliti wa Nchi
Utaje na makundi yanayompenda ni wafanyakazi,wakulima wa korosho,wamachinga au wachaga,au wamakonde wa mtwara, au wahaya wa kagera waliopo mzomea
 
Rate ya ushindi wa rangi ya kijani inapungua kwa Asilimia ishirini kila baada ya miaka mitano , Chukua 58% -20% = 38%.
Sasa ukichukua 100% -38%= 62%.

Moja kwa moja hapo upinzani unakuwa na Asilimia 62% za ushindi,
Professa na vyama vingine wanagawana Asilimia 1, waziri wa mambo ya nje mstaafu na chama chake wanamuunga mkono mpakwa mafuta.

Mpakwa mafuta anaweza jipatia 61%.
 
Rate ya ushindi wa rangi ya kijani inapungua kwa Asilimia ishirini kila baada ya miaka mitano , Chukua 58% -20% = 38%.
Sasa ukichukua 100% -38%= 62%.

Moja kwa moja hapo upinzani unakuwa na Asilimia 62% za ushindi,
Professa na vyama vingine wanagawana Asilimia 1, waziri wa mambo ya nje mstaafu na chama chake wanamuunga mkono mpakwa mafuta.

Mpakwa mafuta anaweza jipatia 61%.
Walahi huku mitaani wakifikisha hata 35% washukuru Mungu.CCM imekataliwa kila kona mwaka huu na haijawahi tokea
 
Walahi huku mitaani wakifikisha hata 35% washukuru Mungu.CCM imekataliwa kila kona mwaka huu na haijawahi tokea
Yeah hiyo 38% itaendelea kushuka Mana wanafki wengi, wao hawaongei wazi Wanaenda kummaliza mtu kwenye sanduku tu .
 
Yeah,upo sahihi. Na hicho ndicho kinachomtesa ccm. Safari hii upinzani umepata mpinzani asilia. Walitegemea sana tumsimamishe yule Nyalandu ili wapate cha kusema kwamba aliiba twiga ,fisadi sasa hoja kama hizo hazipo tena
Lisu ni clean Hana kashfa yeyeto Ni mtetezi wa wanyonge na sio mnyongaji wa wanyonge
 
Hii ni moja ya hofu au mashaka niliyonayo mimi kama mimi hasa iwapo watafanikiwa kuapishwa wote hii ikiwa ni Plan B baada ya hii ya inayoendelea sasa kufeli.

Je, tumejipangaje kwa hili?

Ushauri:Tuwalinde mawakala kama tunavyotaka kulinda kura.
 
Back
Top Bottom