Tetesi: CCM wanaoutamani urais 2025 Wakinyimwa kugombea kutimkia upinzani na kujaza fomu za kugombea Urais

Tuwe wakweli kwa katiba hii hakuna mwana CCM YOYOTE atatanguliza pua lake kuchukua form dhidi ya Mama Samia.
Sisi tunaodai katiba mpya tushaona hii mambo mapema mno, kama unanibisha muulize Mzee Membe na yule Kijana wa Nazaleti watakukupa mkanda wote.
 
Usikariri mkuu, kwenye kila situation kuna options. Desperate times call for desperate measures. Usidhani watanzania wote ni makondoo yaliyojiinamia tu kusubiri kuchinjwa huku watu wachache wanaojiona wanamiliki nchii hii wakifanya wanavyotaka. Narudia tena, kuna namna.
 
Hujui lolote wewe kaa chini. nyie ndiyo ambao unabwabwaja hapa afu mkiambiwa mjitokeze kudai haki zenu mnakimbilia uvunguni na wake zenu.

Nimekwambia hivi hakuna mwana CCM YOYOTE serious atachukua form kushindana na Mama Samia 2025
 
Ilopelekwa original, ilipofika bungeni mazombie wakaanza kuchomoa ya muhimu na kuchomekwa mapuuza.
Mbali na zerikali tatu, kitu gani cha kuvutia kwenye ile original?

Niliisoma, sehemu kubwa ilikuwa kunakili yaliyo kwenye katiba iliyopo.
 
Mbali na zerikali tatu, kitu gani cha kuvutia kwenye ile original?

Niliisoma, sehemu kubwa ilikuwa kunakili yaliyo kwenye katiba iliyopo.
Rasimu ya Warioba ilisheheni matakwa ya wananchi Si ya wanasiasa pekee.

Nenda rudia kuisoma jukwaa la Katiba IPO.

Yule Mzee hatopumzika Hadi alichoandika kitimie. Ameeeen.
 
Rasimu ya Warioba ilisheheni matakwa ya wananchi Si ya wanasiasa pekee.
Nimeisoma zaidi ya mara mbili. Kama yale ndio matakwa ya wananchi, hao wananchi watakuwa na matatizo ya akili.

Ni mwananchi gani mwenye akili timamu, kwa mfano, atakayetaka mkoa wa Dar es salaam na mkoa wa kusini Pemba iwe na uwakilishi sawa bungeni?
 
K
Hujui lolote wewe kaa chini. nyie ndiyo ambao unabwabwaja hapa afu mkiambiwa mjitokeze kudai haki zenu mnakimbilia uvunguni na wake zenu.

Nimekwambia hivi hakuna mwana CCM YOYOTE serious atachukua form kushindana na Mama Samia 2025
Hongera sana kwa kunijua na kujua kua sijui kitu. Muda si mchache tutaona mimi na wewe nani wa kukaa chini. Wewe unakomalia mwana ccm mwana ccm. Mimi nakwambia ipo namna.
 
Umeusoma vzr muundo wa Serikali TATU au unasoma Ule uchakachuzi wa kina chenge!!
 
K

Hongera sana kwa kunijua na kujua kua sijui kitu. Muda si mchache tutaona mimi na wewe nani wa kukaa chini. Wewe unakomalia mwana ccm mwana ccm. Mimi nakwambia ipo namna.
ningekuelewa kama maneno haya angesema mwananchi ambaye si mwana CCM, wewe naona CCM huijui vizuri. Hiyo namna mbona ilikwamba kufanyika baada ya kifo cha mwendazake? hujui mambo mengi ya nchi hii... nchi hii iache kama ilivyo.

Kwa kukusaidia tu kakae na wana CCM wakongwe Mzee Membe na Ndugai wakupe shule fupi.
 
Umeusoma vzr muundo wa Serikali TATU au unasoma Ule uchakachuzi wa kina chenge!!
Warioba na timu yake walichoandika ni rasimu ya katiba ya muungano.

Katiba zingine za nchi washirika wa muungano zingeandikwa na nchi husika, japo wapuuzi walishindwa hata kuitaja Tanganyika kwa jina kwenye rasimu yao wakaita Tanzania bara.

Nakuuliza tena, kuna mwananchi mwenye akili timamu atatamani uwakilishi sawa kwa mikoa ya Dar na Pemba kusini kwenye bunge la muungano kama ilivyopendekezwa na hiyo rasimu ya Warioba?

Kama huna jibu pita kimya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…