CCM wazushi Sana. Hapa kinachowashangaza ni nini?

Hapa siyo habari ya CCM, CHADEMA au chama kingine.

Ni kuhusu taifa na maendeleo yake.
Wachache kutumia kodi na rasilimali za nchi kuishi kama wapo peponi wakati watoto wanafundishwa katika hali hiyo, siyo sawa na haikubaliki popote kwenye watu wenye akili.

Vyama ni majukwaa tu ya kutafutia uongozi wa serikali na baada ya hapo viongozi ni wa wote.
Bajeti ya magari ya kifahari na matumizi mengine yasiyo na tija ikielekezwa kwenye elimu kwa 40% tu haya yatakuwa historia.

Lazima wananchi wakasirike wakiona hali hii badala kubishana kivyama kama mazuzu.
 
Iyo mitego ya kuuza mustakabali wako wa miaka mitano kwa sahani ya ubwabwa ndio ujinga wenyewe ninaouongelea. Point yangu ninkwamba hata CCM wakiamua uchaguzi uwe huru na wa haki, kutokana na ujinga na ushabiki wa wananchi bado CCM wanaweza kushinda haitakua rahisi kama wapinzani wanavyofikiri
 
Naona inakuwa vigumu kwetu kuelewana katika jambo rahisi hivi:
Hawa "wajinga" waondolee hivyo vishawishi hivyo vya pembezoni ili wawe huru kuutumia "ujinga" wao wanavyotaka wao.
Hilo ndilo ninalo omba CCM wasijihusishe nalo.
Hili la kusema tu, hawa ni "wajinga"; halafu hapo hapo unakwenda kwao kuwashawishi halikidhi wao kuwa wajinga.

Mkuu, 'Natafuta' waambie tu CCM kwamba hawa watu tayari ni wajinga, waache watumie ujinga wao katika chaguzi hizi; kwani kwa kuwa tayari ni wajinga, CCM wataendelea tu kupata ushindi!
 
Kwamba unamchagulia adui silaha vitani? Kama ujinga wa watu unawapelekea kuuza mustakabali wao kwa sahani ya ubwabwa, chumvi, kofia, kanga ,ahadi za uongo n.k basi huo ni uzembe wa wananchi wenyewe sio CCM.
 
CCM NI JANGA LA TAIFA HILI
 
Karumanzila hao
 
Kwamba unamchagulia adui silaha vitani? Kama ujinga wa watu unawapelekea kuuza mustakabali wao kwa sahani ya ubwabwa, chumvi, kofia, kanga ,ahadi za uongo n.k basi huo ni uzembe wa wananchi wenyewe sio CCM.
SAWA.
Kwa hiyo CCM wanafanya wanachopashwa kufanya.
Hili tumelimaliza.
 
SAWA.
Kwa hiyo CCM wanafanya wanachopashwa kufanya.
Hili tumelimaliza.
Unajua nini mkuu? Mimi pia sikubaliani na uongozi na CCM miaka 60+ ya uhuru na bado changamoto zile zile tunashindwa kuondokana nazo ni ishara kwamba wameshindwa kutuvusha lakini iyo haiondoi ukweli kwamba kuna kundi kubwa la wajinga linatuangusha wachache waelevu. Demokrosia ni hatari sana ikitumika kwenye jamii ambayo ina population kubwa zaidi ya wajinga.
 
Shikamoo Tanzania, watoto wao wanaposoma na hao ni mbingu na Ardhi. Hivi hawana aibu au huruma tu, wakawajengea madarasa hawa Malaika wa watu!!!

Mimi mtu asiyewahurumia watoto, namchukulia kama muuaji. Hata wanyama wana huruma na watoto wao.

Hapo wazazi wao wanakamuliwa kodi. Watoto wao wanaandikia kwenye mchanga na kukaa chini! Njoo Serikalini sasa, uone wanavyoishi kianasa, utasema ni nchi mbili tofauti!!!
 
Kila mara ninapokutana na hili la waTanzania kuitwa "WAJINGA", ninajikuta nakataa katakata kukubali ujinga wa waTanzania.
Kutoshiriki kwenye vurugu siyo ujinga. Lakini nakuhakikishia, pakitokea kiongozi/viongozi au chama wanachokielewa vyema, waTanzania hawa hawa utawaona wakiwa mstari wa mbele kuyaleta mabadiliko yanayo simamiwa na viongozi au vyama vya upinzani.

Ndiyo sababu tuna wahimiza sana na kuwasihi CHADEMA waende kwa wananchi hawa, kuanzia huko mitaani kwao kujijengea uaminifu kwao. Hili likifanyika, CCM hii ya 'Chura Kiziwi' hata watoe ubwabwa kiasi gani, hawatafua dafu.

WaTanzania kwa ujumla wetu, siyo wajinga hata kidogo. Kushindwa kwetu kuwashawishi waunge juhudi isiwe sababu ya kuwalaani hawa watu.
 
Mkamateni kiroboto Lucas Mwashambwa aje hapa amsifu mama kwa kutoa fedha za kununua majivu ili wanafunzi wasome.
 
Mkamateni kiroboto Lucas Mwashambwa aje hapa amsifu mama kwa kutoa fedha za kununua majivu ili wanafunzi wasome.
Hawashindwi hao chawa... Luka ni msomi wa kiwango cha shahada kama mwenzake Mwijaku...

Kama hao wana akili za namna hiyo, fikiria wale wenzangu na mie chawa mateja wa uswahilini wapo kwenye hali gani?
 
CCM NI MAπŸ’©πŸ’©πŸ’© Sasa mnapo chagua kuongozwa na vinyesi tutegemee nini ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…