Zanzibar 2020 CCM Zanzibar yakaribisha wanaccm kuchukua fomu za Urais, yasema uteuzi utafanyika Dodoma siyo Unguja

Zanzibar 2020 CCM Zanzibar yakaribisha wanaccm kuchukua fomu za Urais, yasema uteuzi utafanyika Dodoma siyo Unguja

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
CCM Zanzibar imesema ni ruksa kwa wanaccm wanaotamani urais wa Zanzibar kwenda kuchukua fomu.

Naibu Katibu mkuu wa CCM Zanzibar amesema uteuzi wa jina la Mgombea utafanyika jijini Dodoma na siyo Zanzibar na kisha litapelekwa Tume ya uchaguzi.

Chanzo: ITV habari

Maendeleo hayana vyama!
 
June 13, 2020
Unguja, Zanzibar
Tanzania
CCM ZANZIBAR YATOA RATIBA YA UCHUKUAJI WA FOMU ZA URAIS KWA AJILI YA UCHAGUZI MKUU 2020

Naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar Dkt. Abdullah Juma Mabodi akizungumza na waandishi wa habari mjini Zanzibar.
  • Kufuatia Kamati Kuu ya CCM kuketi mjini Dodoma na kutoa ratiba na taratibu za kugombea nafasi za uongozi
  • tarehe kuchukua fomu ni kuanzia kuanzia 15 Juni -30 Juni 2020
  • Kutafuta wadhamini wa urais wa Zanzibar wasiopungua 250 na watoke ktk mikoa mitatu ya Zanzibar. Sharti mikoa iwe 2 Unguja na mmoja Pemba. Wajumbe wa Halmashauri Kuu hawaruhusiwi kumdhamini mgombea.
  • Fomu za urais Zanzibar lazima zithibitishwe na katibu wa wilaya wa CCM
  • Mgombea urais CCM lazima ayakubali Maadili ya Chama Cha Mapinduzi kuanzi mtu binafsi, huko nyuma historia yake n.k
  • Uchaguzi ndani ya chama si ushindani bali ni kutafuta aliye bora iwe ngazi ya urais na ngazi zingine zote
  • Mtia nia hatakiwi kuja kwa shangwe, dufu, ngoma, matarumbeta, vipeperushi , nderemo haziruhusiwi ila mtia nia anaweza kuja na watu kadhaa kumsindikiza.
  • Taratibu hizo ni kuzuia kuonesha makundi au mtia nia kuwatisha wengine kwa kuwa na wapambe wengi wakati anatafutwa aliye bora na si ushindani
Source : KTV TZ ONLINE
 
Na hili linadhihirisha kuwa huwa wanachaguliwa Rais wao
CCM Zanzibar imesema ni ruksa kwa wanaccm wanaotamani urais wa Zanzibar kwenda kuchukua fomu.

Naibu Katibu mkuu wa CCM Zanzibar amesema uteuzi wa jina la mgombea utafanyika jijini Dodoma na siyo Zanzibar na kisha litapelekwa Tume ya uchaguzi.

Chanzo: ITV habari

Maendeleo hayana vyama!
 
CCM Zanzibar imesema ni ruksa kwa wanaccm wanaotamani urais wa Zanzibar kwenda kuchukua fomu.

Naibu Katibu mkuu wa CCM Zanzibar amesema uteuzi wa jina la mgombea utafanyika jijini Dodoma na siyo Zanzibar na kisha litapelekwa Tume ya uchaguzi.

Chanzo: ITV habari

Maendeleo hayana vyama!
Rais wa nchi ya Zanzibar anachaguliwa Tanganyika? Hicho ni kimkoa cha majini! Ni Gavana wa Mkoa wa majini! as Hong Kong is!
 
Nimeelewa kuwa mwana CCM anayehusudu hoja za upinzani au aliyetayari kufanya kazi na upinzani hawezi kupitishwa kuwa mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM kuongoza serikali ya nchi ya Zanzibar.
 
Ngoja tuanze kuangalia wale wanaoweza labda kutia nia Zanzibar kwa tiketi ya CCM nafasi ya urais SMZ

February 17, 2020

FULL HISTORIA YA MAMA SAMIA

Mama Samia anakubali hoja nzito za wapinzani, nilikataa pendekezo la kuwa Makamu wa Rais

Makamu wa Rais wa serikali ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Hassan Suluhu asema kilichomsukuma kuingia katika siasa ni maoni na hoja za mashiko za wapinzani Bungeni / Baraza la Wawakilishi ambazo hazijibiwi vyema kwa hoja na mawaziri wa serikali.

Hilo la kukerwa na majibu ya serikali yasiyokidhi hoja za wapinzani, Mama Samia akajiona ni kama Activist / Mwanaharakati ingawa ni CCM anayehusudu maswali magumu yajibiwe kwa hoja thabiti.

Mama Samia anaongeza kabla ya kuingia siasa alikuwa anaona nondo za wapinzani huku upande wa serikali ambayo ni ya CCM bara na Visiwani pia, mawaziri huja na majibu hafifu yasiyo ridhisha kwake na wanaofuatilia shughuli za Bunge.



Pamoja na kukunwa na hoja zilizoenda shule za wapinzani, Mama Samia aliwaeleza wasikilizaji ametokea ktk familia ya kawaida ambapo baba yake alikuwa mwalimu wa shule na mama yake mama wa nyumbani aliyetumia nafasi kuwafundisha na kuwasaidia kazi za masomo wakitoka shule.

Hiyo ilimsukuma kujiendeleza kimasomo kila wakati na kufanya kazi katika serikali ya SMZ na muda mrefu katika NGO's mbalimbali za kimataifa kabla ya kujiunga na siasa kupitia viti maalum CCM.

Mama Samia alipofanikiwa kuteuliwa Mwakilishi wa Viti Maalum alipata faraja kubwa akitegemea kutasaidia kukijenga chama cha CCM kuwa na watendaji wajibu-hoja-wazuri, kutokana na kuona mawaziri wa serikali na wabunge wa CCM kukosa hoja motomoto au majibu yakuridhisha kwa maswali na hoja nzuri za wapinzani na kuzidiwa wakiwa bungeni au baraza la wakilishi wakionekana / kusikika 'live' .

Ghafla bin vu, Mama Samia alipoingia Baraza la Wakilishi akateuliwa kuwa Waziri wa Sera Ajira Maendeleo ya akina Mama na Vijana ktk Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Na miaka 5 baadaye akawa waziri wa Biashara na Utalii katika SMZ. Baadaye akagombea kiti Makunduchi Zanzibar na kufanikiwa kuwa mbunge wa Zanzibar katika Bunge la Jamhuri ya Muungano na kuteuliwa kuwa Waziri wa Mazingira na hatimaye mgombea Mwenza wa Urais na kuwa Makamu wa Rais wa Tanzania.

Hakutegemea kupewa nafasi hizo ghafla hivyo na pia akikumbuka nondo za wapinzani bungeni kupitia maswali, akaona amewekwa mstari wa mbele kukabiliana na hoja zinazowagusa wananchi ambazo hazipatiwi majibu ya kuwaridhisha wananchi.

Source: Millard Ayo
 

June 17, 2020
Kisiwandui Afisi Kuu ya CCM
Unguja, Zanzibar

Dr. Hussein Ali Mwinyi achukua fomu ya kutia nia Urais SMZ


Hussein Ali Mwinyi (born 23 December 1966) is a Tanzanian CCM politician and Member of Parliament for Kwahani constituency since 2005. He is the current Minister of Defence and National Service.


EDUCATION
SCHOOL NAME/LOCATIONCOURSE/DEGREE/AWARD
START DATE
END DATE
LEVEL
HAMMERSMITH HOSPITAL, LONDON, UK
PHD​
1994​
1997​
PHD​
HAMMERSMITH HOSPITAL, LONDON, UK
MASTERS (MEDICINE)​
1991​
1997​
MASTERS DEGREE​
MARMARA UNIVERSITY MEDICAL SCHOOL, ISTANBUL TURKEY
DOCTOR OF MEDICINE​
1985​
1991​
CERTIFICATE​
TAMBAZA HIGH SCHOOL
A-LEVEL EDUCATION​
1984​
1985​
HIGH SCHOOL​
AZANIA SECONDARY SCHOOL
O-LEVEL EDUCATION​
1982​
1984​
SECONDARY​
MANOR HOUSE JUNIOR SCHOOL, CAIRO, EGYPT
PRIMARY EDUCATION​
1977​
1981​
PRIMARY​
OYSTERBAY PRIMARY SCHOOL
PRIMARY EDUCATION​
1972​
1976​
PRIMARY​
EMPLOYMENT HISTORY
Company Name
Position
From
To
Ministry of Defence and National ServiceMinister
2014-01-20​
2015​
Ministry Of HealthMinister
2012​
2014-01-20​
Vice-President's Office - Union AffairsMinister
2006​
2/8/2008​
Ministry of HealthDeputy Minister
2000​
2005​
Ministry of Defence and National ServiceMinister
2/13/2008​
To Date​
Hubert Kairuki Memorial UniversityLecturer
1998​
2000​
Hubert Kairuki Memorial UniversitySpecialist Doctor
1998​
1999​
Ministry of Health - Muhimbili HospitalRegistrar
1994​
1995​
Ministry of Health - Muhimbili HospitalDoctor
1993​
1993​
Marmara UniversityIntern
1991​
1992​

POLITICAL EXPERIENCE
Ministry/Political Party/Location
Position​
From​
To​
Chama Cha Mapinduzi, CCMMember - National General Council
2005​
Todate​
The Parliament of TanzaniaMember - Kwahani Constituency
2005​
2015​
Chama Cha Mapinduzi, CCMMember - Kwahani /Mkuranga Political Committee
2000​
To Date​
The Parliament of TanzaniaMember - Mkuranga Constituen
 
June 15, 2020
Unguja, Zanzibar

Balozi Ali Abeid Amani Karume achukua fomu

Mara baada ya kuchukua Fomu Balozi Ali Abeid Karume amesema kwamba iwapo chama cha Mapinduzi CCM kitampa ridhaa ya kuwa mgombea wa nafasi hiyo na kuwa Rais wa Zanzibar, anatarajia kuendelea dhamira ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuyalinda, kulinda Muungano wa Tanganiyika na Zanzibar na kuendeleza Sera za CCM.

Pia Balozi Karume amesema, "nitapenda ugawaji wa Ardhi uendelee hasa kwa wananchi ambao wanaihitaji kwa masuala ya Kilimo, Ujenzi pia tutajenga makazi bora".
Source: Millard Ayo

Toka maktaba :

26 Apr 2019

Balozi Ali Karume


WAZIRI wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo (SMZ),Balozi Ali Karume, amesema upo uwezekano mkubwa wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Zanzibar kwa mara ya Pili ifikapo mwaka 2025. Balozi Karume, amesema hayo alipokuwa akihojiwa katika kipindi cha “Twende pamoja na Munir Zakaria” (April 25,2019),kuhusu miaka 55 ya Muungano kupitia Kituo cha Bomba FM Radio, (87.5 Zanzibar)
Source : Bomba TV
 
Back
Top Bottom