CDF mstaafu Mabeyo amelikoroga, Makamu wa Rais ndiye alitakiwa kuwa mtu wa kwanza kila hatua kujua afya ya Rais

Wabongo bwana ujuaji mwingi Sana

Hivi unadhania mpaka mtu anakuwa CDF ni Jambo simple simple Sana eh

So wewe unajua utaratibu kuliko mkuu wa majeshi?

Tuache kujifanya wajuaji sana
Ujuaji si kosa kama unachojua ni sahihi na umekipata kwa juhudi zako binafsi..cheo, hadhi au Mali havimfanyi mtu kujua lolote kama yeye mwenyewe hana bidii ya kutaka kujua!
 
Katiba ndio inasema hivyo?
 
Nadhani kwa kiasi kikubwa mtazamo wako upo sahihi. Umesahau tu kujumuisha nafasi ya Bunge na Mahakama.

Ninachoona hapa ni mgongano wa mitazamo inayoegemea nadharia vs mazingira halisi.

Tujiulize, nani aliwakataza hao tunaoamini kuwa walistahili kushika hatamu wasishike hatamu! kwa nini nao walibaki kuwa wananchi!

Mazingira halisi ni kuwa Mkuu wa Serikali na Mkuu wa nchi anapokuwa katika hatari kubwa au nchi inapokuwa katika hatari kuingia au kuingizwa katika failed state kuna watu wanashika usukanai kwa ridhaa ya Mkuu mwenyewe au bila ridhaa yake regardless ya mwongozo wa kikatiba. Na mara nyingine hiyo ndio inakuwa mwisho wa katiba na desturi zilizokuwepo.

Ukimsikiliza kwa makini na ukatafakari kwa utulivu utaona kuwa the three giant ndio walishika usukani katika kipindi mhusika alipopoteza uwezo wa kuongoza hadi siku mbili baada ya kuondoka. wengine walikuwa wasikilizaji na wafuata maagizo. Lakini kubwa zaidi kulikuwa na sintofahamu kadhaa ndio maana mambo hayakwenda pengine vile wengi wangetarajia. Hizo sintofahamu hajaziweka wazi na pengine hazitokuja kuwa wazi kamwe. watabaki watu wachache wanaojua ni kilitokea, chanzo kilikuwa nini na waanzilishi wamechukuliwa hatua gani?

Pengine hao ambao wewe unahisi walipaswa kushika usukanai wangepewa fursa, pengine mambo yasingekuwa hivi yalivyo.

Hao ndugu watatu waliotuvusha wanastahili pongezi za hali ya juu sana, walizishinda nafsi na kuweka maslahi ya Tz mbele. Wangekuwa na tamaa au wangetetereka sijui tz ingekuwa ya namna gani hadi sasa.

Nahisi hao Giants huwa ni muhimu sana wakati wa uchaguzi mkuu hususan inapofika saa moja jioni baada mchakato wa kupiga kura kukamilika hadi saa ya kutangaza matokeo. Katika kipindi hicho hao watatu wasipokuwa na wewe imekula kwako. Ndugu yetu Lungu na Yule aliyepo Nyasa wanajua role ya hao watatu katika nyakati hizo.
 
Hizi dharau zenu ndio zilimponza mwendazake
 
Huna unalolijua wewe, swala la afya ya Rais ni swala la ulinzi na usalama wa nchi na ndo maana utaona hakuna viongozi walokuwa wakiruhusiwa kumtembelea isipokuwa wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama.
 
Nimeshangaa pia:
  • Dar es Salaam walikuwepo watatu: CDF, IGP & DGIS
  • Makamu wa Rais alikuwa Tanga, Waziri Mkuu alikuwa mkoani (Dodoma or elsewhere)
  • Lakini Waziri Mkuu aliitwa na alipata taarifa mapema, kabla ya Makamu wa Rais
Something is fishy here.
Inasemwa VP alilazimishwa kufanya ziara Tanga ili kuwekwa mbali
 
Chain of command
PRESIDENT >>V. P>>P. M huyo CDF ni mbali Sana anaripoti kwa waziri wa Ulinzi, Inakuwaje top secret ifahamike na CDF halafu VP na PM wasijue?

Pengine mwendazake alihisi kuna wasaliti hivyo akaamua kuvunja chain of command??
 
Magufuli aliweza kuagiza Mapadri waende, lakini alishindwa kuagiza aitiwe Makamu wake, hata amuachie wosia juu ya Majukumu anayomuachia, naona bado kuna vumbi halijatuama, nasubiri story zaidi.
Hukusikia hotuba ya Mabeyo Chato? hukusikia akimweleza Rais kwamba Hayati alimdokeza kitu atamuona ofisini ampe ujumbe wake? weupe upstairs kabisa.
 
Magufuli aliweza kuagiza Mapadri waende, lakini alishindwa kuagiza aitiwe Makamu wake, hata amuachie wosia juu ya Majukumu anayomuachia, naona bado kuna vumbi halijatuama, nasubiri story zaidi.
Yaani kweli unaona sasa unakufa na una nafasi ya kutubu. Umuite Kiongozi umwachie wosia wa namna ya kuendelea na majukum na uache njia ya kutengeneza njia yako huko uendako? Inashangaza sana.
 
Siyo tu hivyo,hata ktk familia km mtoto wa kiume ni mkubwa au wa kwanza kuzaliwa na tayari walau ana umri wa miaka 20+ na amefunzwa vyema,amekuwa karibu na baba yake,baba akisafiri anakabidhiwa mkuki,upinde na mishale yake halafu mama yake anakuwa kiongozi kivuli ijapo huwa hawajui kuwa wao ni viongozi vivuli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…