CECAFA KAGAME CUP 2011 Finals in Tanzania

CECAFA KAGAME CUP 2011 Finals in Tanzania

kuna mtangazaji mmoja wa star tv anawaponda sana wachezaji wa kibongo alimponda sana mrope kwamba pasi zake za mwisho hazina tija anafanya kazi kuubwa lkn pasi ya mwisho inakuwa fyongo hahaaa akamponda sana mwape hana control tehe tehe awe makini atapata kichapoooo

Huyo ni John Kanakamfumu......Ni kocha huyu..

Yeye kila kitu anasema 'tatizo la wachezaji wa Tanzania'............Ni mmojawapo wa makocha wabovu wa Bongo...
 
Kungekuwa kuna tatizo katika usajili sidhani kama TFF na CECAFA wangempa kibali/kadi ya kushiriki Kagame cup....Tatizo ni mawasiliano miongoni mwa viongozi wa Ruvu shooting stars........Na inasemekana kuna viongozi wa Ruvu wanataka kulipwa cash ilhali Yanga wanataka kuwalipa kwa hundi......Kama kungekuwa na tatizo nadhani hata Yanga nao wangesita kumchezesha leo......
Etieee!! Kama kweli ndivyo ilivyo basi Yanga watanusulika, lkn kuna aja ya Viongozi kujitokeza kwenye media ili kukanusha shutuma zilizotolewa na viongozi wa Ruvu Shooting kupitia media pia kwani zilikuwa nzito.
 
Matokeo ya Morogoro:

Ulinzi Stars 9:1 Port (Full Time)

St.George 1:1 APR (Mechi inaendelea)
 
Etieee!! Kama kweli ndivyo ilivyo basi Yanga watanusulika, lkn kuna aja ya Viongozi kujitokeza kwenye media ili kukanusha shutuma zilizotolewa na viongozi wa Ruvu Shooting kupitia media pia kwani zilikuwa nzito.

Jana Makamu mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Yanga Seif Ahmed ameeleza vizuri tu na kusema kwamba hakuna tatizo lolote na tayari wamemalizana na Ruvu shooting
 
Nurdin Bakari ni kifaa aisee.........


Muunganiko wake na Rashid Gumbo pale kwenye kiungo unatia raha..............
Siku niliposikia Nurdin Bakari kaenda yanga nilichukia sana sijui simba walimwacha kwa kosa gani...Nurdin ni kifaa hasa na anauwezo wa kucheza namba nyingi tu yaani 2,3,6,8,11 tofauti na wachezaji wengi wa kitanzania..
 
Kwa mchezo huu wa kutolewa jasho na Eiman, Yanga wasitegemee kufika mbali.
 
Jana Makamu mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Yanga Seif Ahmed ameeleza vizuri tu na kusema kwamba hakuna tatizo lolote na tayari wamemalizana na Ruvu shooting
Madai ya Ruvu ni kama yaliyo jitokeza kwa Africa Lyon zidi ya simba wakidai Samatta ni mchezaji wa kwao badala ya kudai pesa yao...Kimsingi Ruvu wana dai pesa zao na pesa siyo tatizo kwa maelezo ya kiongozi wa yanga kuwa Ruvu wanataka cash wakati yanga wanataka kuwalipa kwa hundi..
 
Kwa mchezo huu wa kutolewa jasho na Eiman, Yanga wasitegemee kufika mbali.

Yanga hawajabanwa bana.......Tatizo ni kwenye umaliziaji,hakuna mawasiliano mazuri kati ya Davies Mwape,Keneth Asamoah,Julius Mrope na Kigi Makassy...............Wanakosa mabao ya wazi na wakitulia watafunga magoli mengi tu.......Ndio kwanza dakika ya 55
 
Yanga inabidi wafanye shooting za mbali na si mpaka waingie golini............Kipa wa Elman ni bomu kweli,mbovu
 
Back
Top Bottom