Cha kujifunza kutoka kwa wachangiaji wa Tanzania

Cha kujifunza kutoka kwa wachangiaji wa Tanzania

MwendaOmo

JF-Expert Member
Joined
Dec 16, 2013
Posts
774
Reaction score
723
Naomba kwamba wale wanaopenda kuharibu nyuzi kwa kuleta mapishano ya TZ vs KE watulie kidogo.

Kuna jambo moja ambalo nimegundua kuhusu baadhi ya wachangiaji wa TZ kwenye JF (Haswa kwa majukwaa mengine kama vile la siasa) Utapata kwamba mara nyingi, hawa ndugu zetu huwa na uwezo wa kuandika na kusoma mambo mengi kutushinda sisi. Sisemi eti anayeandika mambo mengi ana hoja kali, lakini nimekuja kuona kuwa nyuzi zetu nyingi iwe hapa, au Wazua, Nipate, au hata JamiiForums.com huwa ni fupifupi na hazina depth. Ni kana kwamba tumekuwa na attention span ndogo sana na tumezoea jumbe za WhatsApp na chochote kile kirefu sie husema "too long hebu summarize".

Sijui kama ni uvivu wa kusoma au nini. Au ni tatizo la elimu inayotokana na kutumia lugha ya kimombo kama medium of instruction. Ndio, kuna Wakenya ambao huleta mada kama haya, lakini mara nyingi utapata ni zile fupi-fupi tu; au, itakuwa ni article ya gazeti ambayo ameleta kuripoti. Ni nadra sana upate Mkenya ameleta mada ya zaidi ya maneno 500 ambayo ni analysis. Lakini kule jukwa la siasa, utapata mtu amechukua muda wake kuleta mada ndefu ambayo ni analysis tupu, na hata hana haya kuweka jina lake hapo. Naamini hili ni jambo la kujifunza kweli.
 
Watanzania Ni wazuri kwenye maneno kuliko vitendo, ndio sababu unapata hata kwenye kuandika wanaeleza mambo mobb.
 
Ungeenda kwenye intelligence forum ndio ungejua watanzania ni nani search mada za nyuma kidogo kipindi hicho watu tunashusha nondo mpaka CIA wanaweka mikono kichwani.

In short sehemu muhimu kwangu hapa JF from day one ni jukwaa la business na intelligence forum japo kuna baadhi ya vichwa kama vipo likizo this time.
 
Watanzania wengi hasa wa JF wako vizuri sana.
Hakuna kitu kinachohusu maisha yao kitajadiliwa kwa juujuu.
 
MwendaOmo,
Shukrani kwa kuona jambo zuri ndani ya chombo hiki cha kubadilishana maoni Afrika Mashariki.

Eneza habari hii nzuri kwa waKenya watembelee majukwaa yote ya Jamiiforums na kufaidika kwa uchambuzi wa taarifa, habari na chuguzi za kina siyo tu za Afrika Mashariki bali hata North America, Asia, Africa, Latin America, Mythology (Greek, Scandinavian, Middle East, far east, local) politics, philosophy, history, astronomy, astrology , diplomacy, war & peace, medicine, intelligence & security, international trade, entertainment, sports ... .
 
  • Thanks
Reactions: Oii
MwendaOmo, mimi ninakupongeza kwa kuliona hilo katika upande wa wachangiaji katika mijadala hapa jamii forum na kwengineko, mimi nimeliona hilo katika eneo la viongozi na serikali ya Kenya kwa ujumla, kwa miaka mingi sasa nimekua nikifuatilia maamuzi mbalimbali yanayotolewa na serikali au viongozi wa Kenya, yawe ni kuhusu miradi ya maendeleo, mahusiano ya kidiplomasia, usalama, biashara au hata ulinzi wa nchi, mengi ukiangalia unakuta ama hayakufanyiwa utafiti wa kutosha, ama busara haikutumika, au yamefanywa kiushabiki tu bila hata kuangalia maslahi mapana ya wakenya.

Nitatoa mifano michache tu, na kama kuna mtu mwenye mawazo tofauti na haya, nitaomba msaada anieleweshe kwa sababu hadi leo sioni kama maamuzi haya ni kwa faida pana ya wakenya, 1) Mradi wa laptop kwa wanafunzi wa Shule za msingi Kenya, 2) EPA, 3) Kubeba mafuta ghafi kwa barabara, 4) Budget ya Jeshi kuwa kubwa zaidi ya Uganda, Ethiopia, Tanzania, Rwanda, Burundi(Ethiopia ipo vitani Somalia na Eritrea) 5) Kuendelea na mass tourism vs Quality tourism ambayo inalipa mara tatu zaidi na inahifadhi mazingira, 6)Ujenzi wa bandari ya Lamu kwa sasa badala ya kuanza na Golan irrigation project ili kuwa na food security. Ninaomba kurekebishwa hilo jina Golan, sina uhakika kama ni jina sahihi.

Ninaomba kuwasilisha wanajamii wenzangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watanzania hata kwenye kuongea huwa na maneno mengi nafikiri ni hulka yao. Kuna polisi Mkenya alikua anasema akimkamata Mtanzania Itabidi asimpe fursa ya kuongea maana ataongea kama mashini.

Japo pia kuna wale huwa napenda analysis zao kule kwa hayo majukwa mengine, tatizo Watanzania wengi wana uzembe wa kusoma, utakuta mtu ameandika taarifa ndefu yenye analysis muhimu lakini jamaa wanachangia kwa maneno machache yaliyojaa kejeli.

Waandishi wengi walitamaushwa na ni wachache waliosalia wanaoandika vizuri hivyo. Ipo wakat JF ilikua ya great thinkers, siku hizi imevamiwa na madogo wavaa milegezo wasiokua na heshima.
 
MwendaOmo mimi ninakupongeza kwa kuliona hilo katika upande wa wachangiaji katika mijadala hapa jamii forum na kwengineko, mimi nimeliona hilo katika eneo la viongozi na serikali ya Kenya kwa ujumla, kwa miaka mingi sasa nimekua nikifuatilia maamuzi mbalimbali yanayotolewa na serikali au viongozi wa Kenya, yawe ni kuhusu miradi ya maendeleo, mahusiano ya kidiplomasia, usalama, biashara au hata ulinzi wa nchi, mengi ukiangalia unakuta ama hayakufanyiwa utafiti wa kutosha, ama busara haikutumika, au yamefanywa kiushabiki tu bila hata kuangalia maslahi mapana ya wakenya.

Nitatoa mifano michache tu, na kama kuna mtu mwenye mawazo tofauti na haya, nitaomba msaada anieleweshe kwa sababu hadi leo sioni kama maamuzi haya ni kwa faida pana ya wakenya, 1) Mradi wa laptop kwa wanafunzi wa Shule za msingi Kenya, 2)EPA, 3)Kubeba mafuta ghafi kwa barabara, 4) Budget ya Jeshi kuwa kubwa zaidi ya Uganda, Ethiopia, Tanzania, Rwanda, Burundi(Ethiopia ipo vitani Somalia na Eritria), 5)Kuendelea na mass tourism vs Quality tourism ambayo inalipa mara tatu zaidi na inahifadhi mazingira, 6)Ujenzi wa bandari ya Lamu kwa sasa badala ya kuanza na Golan irrigation project ili kuwa na food security. Ninaomba kurekebishwa hilo jina Golan, sina uhakika kama ni jina sahihi

Ninaomba kuwakilisha wanajamii wenzangu

Sent using Jamii Forums mobile app

Kwa hili la serikali nakuelewa. Hapa kenya, kuna maamuzi ya aina mbili: maamuzi yanayofanywa na wanasiasa na maamuzi yanayofanywa na civil servants. Kwa yale uliyoyataja, Mradi wa laptop haswa ndio ule wa kisiasa zaidi. Hata ule wa kusafirisha mafuta na barrels, pia huo ni upuuzi wa kisiasa tu. EPA ni pragmatic decision ambayo inatokano na pale tulipo kiuchumi. Ili tuweze kuwa na nguvu za kiuchumi zaidi, ni lazima tuwe na philosophy ya self-reliance, na hapa ndipo tumekosa kabisa. Tunafikiri jinsi ya kuexport vitu ulaya, badala ya kufikiri jinsi ya kutengeneza vile vitu ambavyo tunaagiza kutoka nje. Hili si tatitzo la pupa au shallowness, bali ni la mindset.

Barabara ya Lapsset yaweza kufanywa pamoja na GALA irrigation. Ikumbukwe ya kwamba hizi barabara zinatokana na mipango ya miaka ya sabini. Tumechelewa muno.

Kitu ambacho nimegundua na serikali ya Kenyatta ni kuwa mengi hutegema waziri husika. Waziri akiwa proactive, basi mambo yake yatafanywa. Natumai Uhuru akishinda awamu ya pili atawachagua mawaziri walio na nguvu za kufanya kazi. Utapata kuwa mpango wa KDF ni wa KDF na wao wako na mipango yao. Waziri wa ardhi naye kalala hana shughuli yoyote fedha zarudi kwenye treasury tu.
 
Watanzania hata kwenye kuongea huwa na maneno mengi nafikiri ni hulka yao. Kuna polisi Mkenya alikua anasema akimkamata Mtanzania Itabidi asimpe fursa ya kuongea maana ataongea kama mashini.

Japo pia kuna wale huwa napenda analysis zao kule kwa hayo majukwa mengine, tatizo Watanzania wengi wana uzembe wa kusoma, utakuta mtu ameandika taarifa ndefu yenye analysis muhimu lakini jamaa wanachangia kwa maneno machache yaliyojaa kejeli.

Waandishi wengi walitamaushwa na ni wachache waliosalia wanaoandika vizuri hivyo. Ipo wakat JF ilikua ya great thinkers, siku hizi imevamiwa na madogo wavaa milegezo wasiokua na heshima.

Haha. Eti wavaa milegezo. Nimekuwa nikijiuliza; ni kwanini JF ilikuja ikawa forum kubwa hivi? Naamini hawa wachangiaji na wachanganuzi ndio walisaidia sana
 
Hongera sana MwendaOmo kwa kupata fursa ya kutembelea majukwaa mengine!

Ni ukweli kuwa hapa JF kuna watu wamejaliwa uandishi hadi unafurahi! Lakini pia kuna watu huwa ni wavivu wa kusoma. Nahisi forum hii imechangia kubadili wengi! Kuna msemo ulikuwa maarufu sana hapa tz unasema ukitaka kumficha mtz kitu basi kiweke kwenye maandishi!

Hii ilikuwa inaashiria kuwa kuna baadhi kama sio watu wengi ni wavivu wa kusoma makala, au vitabu n.k.
 
Kwa hili la serikali nakuelewa. Hapa kenya, kuna maamuzi ya aina mbili: maamuzi yanayofanywa na wanasiasa na maamuzi yanayofanywa na civil servants. Kwa yale uliyoyataja, Mradi wa laptop haswa ndio ule wa kisiasa zaidi. Hata ule wa kusafirisha mafuta na barrels, pia huo ni upuuzi wa kisiasa tu. EPA ni pragmatic decision ambayo inatokano na pale tulipo kiuchumi. Ili tuweze kuwa na nguvu za kiuchumi zaidi, ni lazima tuwe na philosophy ya self-reliance, na hapa ndipo tumekosa kabisa. Tunafikiri jinsi ya kuexport vitu ulaya, badala ya kufikiri jinsi ya kutengeneza vile vitu ambavyo tunaagiza kutoka nje. Hili si tatitzo la pupa au shallowness, bali ni la mindset.

Barabara ya Lapsset yaweza kufanywa pamoja na GALA irrigation. Ikumbukwe ya kwamba hizi barabara zinatokana na mipango ya miaka ya sabini. Tumechelewa muno.

Kitu ambacho nimegundua na serikali ya Kenyatta ni kuwa mengi hutegema waziri husika. Waziri akiwa proactive, basi mambo yake yatafanywa. Natumai Uhuru akishinda awamu ya pili atawachagua mawaziri walio na nguvu za kufanya kazi. Utapata kuwa mpango wa KDF ni wa KDF na wao wako na mipango yao. Waziri wa ardhi naye kalala hana shughuli yoyote fedha zarudi kwenye treasury tu.
Ninashukuru kwa maelezo haya, sasa tujikite katika maeneo matatu ambayo umeyatolea ufafanuzi, tuanze na hili la Bandari ya Lamu vs Galana irrigation project, hivi kulikua na uharaka gani wa kujenga hii bandari kwa haraka kiasi hiki, tena kwa kutumia pesa ya ndani, kwanini wasingeanza na Galana kwanza kuwa na uhakika wa chakula na uhakika wa maji kwa wananchi, kwa sasa Kenya inapitia kipindi kigumu sana cha upatikanaji wa chakula na maji ya kutumia kwa Kenya nzima, hadi jiji la Nairobi linaupungufu mkubwa wa maji, na hali itaendelea kuwa mbaya mwaka huu kwa sababu kulingana na utabiri wa hali ya hewa, hata mwaka 2018 kutakuwa na upungufu wa mvua, kwa nini wasingechelewesha ujenzi wa bandari ya Lamu hadi wamalize miradi hii muhimu zaidi kwa maisha ya wananchi, kumbuka Bandari ya Mombasa bado inauwezo wa kukidhi mahitaji ya Kenya kwa miaka mingine kumi ijayo, ukizingatia upanuzi unaofanyika bandarini hapo, na ujio wa SGR maana yake mizigo haitokaa muda mrefu bandarini, hivyo kutoa nafasi ya kupokea na kuhifadhi mizigo mingi zaidi.

Kuhusu LAPSET, baada ya Uganda kupitisha mafuta yake Tanzania, na kuna kila dalili kwamba TOTAL ataunganisha visima vya Kenya na Hoima kule Uganda, economic viability ya LAPSET ipo mashakani sana, sasa kwa nini serikali ya Kenya isisubiri kwanza ili kuona kama hiyo bandari ya Lamu bado itakuwa na faida kwa sasa?.

kuhusu bajeti ya jeshi, hili nalo ni eneo ambalo serikali ya Kenya inazika na kupoteza pesa nyingi pasipo na ulazima wowote, nguvu za jeshi la Kenya ni mara 20 zaidi ya zile za Alshabab, kuzidi kununua vifaa vya kijeshi kila siku kwa kisingizio cha kupambana na Alshaabab ni kupoteza pesa ambazo zingetumika katika maeneo ya msingi zaidi, kama utafuatilia, KDF walipata mafanikio zaidi siku za mwanzo walipoingia Somalia kuliko miaka hii ya karibuni ambayo imepewa bajeti kubwa na ununuzi wa vifaa vingi vya jeshi umefanyika.

Ninawakilisha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watanzania hata kwenye kuongea huwa na maneno mengi nafikiri ni hulka yao. Kuna polisi Mkenya alikua anasema akimkamata Mtanzania Itabidi asimpe fursa ya kuongea maana ataongea kama mashini.

Japo pia kuna wale huwa napenda analysis zao kule kwa hayo majukwa mengine, tatizo Watanzania wengi wana uzembe wa kusoma, utakuta mtu ameandika taarifa ndefu yenye analysis muhimu lakini jamaa wanachangia kwa maneno machache yaliyojaa kejeli.

Waandishi wengi walitamaushwa na ni wachache waliosalia wanaoandika vizuri hivyo. Ipo wakat JF ilikua ya great thinkers, siku hizi imevamiwa na madogo wavaa milegezo wasiokua na heshima.
Mkuu kuhusu watu kuchangia kwa maneno machache yenye kejeli ni kwa sababu ya tofauti kama sio za kisiasa basi itakuwa juu ya hoja husika! Kifupi hapa JF ikitokea ukaandika kitu hata uwe umeandika kwa uchambuzi namna gani, kama kuna watu wana mtazamo tofauti na ulichokiandika utaona wanakitolea mapovu tu!

Japokuwa kule jukwaa la great thinkers hata kama mtu anatofautiana na wewe kimtazamo, mtajadili kistaarabu kwa hoja.
 
Kweli kabisa. Watz huwa wanaandika maneno mengi. Wengine utadhani insha, mimi hio ilinishinda. Ufupi tu bora point ipite vzr.
 
Mkuu kuhusu watu kuchangia kwa maneno machache yenye kejeli ni kwa sababu ya tofauti kama sio za kisiasa basi itakuwa juu ya hoja husika! Kifupi hapa jf ikitokea ukaandika kitu hata uwe umeandika kwa uchambuzi namna gani, kama kuna watu wana mtazamo tofauti na ulichokiandika utaona wanakitolea mapovu tu!

Japokuwa kule jukwaa la great thinkers hata kama mtu anatofautiana na wewe kimtazamo, mtajadili kistaarabu kwa hoja.
Sijawahi fika huko kwa great thinker. Wacha nitapita huko
 
Kweli kabisa. Watz huwa wanaandika maneno mengi. Wengine utadhani insha. Mimi hio ilinishinda. Ufupi tu bora point ipite vzr...

Jay456watt,
Mkuu kutokana na ''insha'' ndefu za kiuchunguzi, zenye rejea kibao (references) na hoja-shawishi (having a constructive argument) ndani ya JamiiForums, mtandao huu unaibuka kuwa super brand ya kipekee Afrika Mashariki katika kujadili kwa kina masuala mazito na ndiyo maana bunge / serikali/ vyuo vikuu/ taasisi / watu binafsi n.k kutupia jicho kila mara kuangalia nini kinajadiliwa.

Hapo ndipo tunapo tofautisha TWAR warriors (TWAR = twitter war) na Great Thinkers wa JamiiForums tunapojaribu kuongeza ufahamu au kujadili mambo muhimu lazima makala iwe ndefu kama insha.
 
Jay456watt,

Mkuu kutokana na ''insha'' ndefu za kiuchunguzi, zenye rejea kibao (references) na hoja-shawishi (having a constructive argument) ndani ya JamiiForums, mtandao huu unaibuka kuwa super brand ya kipekee Afrika Mashariki katika kujadili kwa kina masuala mazito na ndiyo maana bunge / serikali/ vyuo vikuu/ taasisi / watu binafsi n.k kutupia jicho kila mara kuangalia nini kinajadiliwa.

Hapo ndipo tunapo tofautisha TWAR warriors (TWAR = twitter war) na Great Thinkers wa JamiiForums tunapojaribu kuongeza ufahamu au kujadili mambo muhimu lazima makala iwe ndefu kama insha.
very true
 
Nadhani swala hapa ni kutokana na Watanzania wakipata mada wanayoipenda wana hamasika na hawajali muda wanao utumia katika kuchangia fikra zao. Sioni tatizo hapo kwasababu hata wanao wajibu na wao wako passionate na majibu yao ilimradi pande mbili zinaelewana, Tunafahamu wenzetu Kenya mna utamaduni wa kuchunga muda na ndio maaana mnajali kufupisha mada au hata shuguli za kijamii. Na naamini huo ulikuwa ni utamauni Wakenya mliuchukuwa kutoka kwa Waingereza, maana na wao wako hivyo hivyo.
 
Back
Top Bottom