Chadema acheni ubaguzi, Lissu anachangisha hela apate gari hamhamasishani, dogo kafungwa kule Mbeya familia ya Mbowe inachangisha

Mbowe ni dikteta wa Chadema ila yuko sahihi kumpambania kijana, tuendelee kupambana
 
kwenye mchango wa gari la Lisu huyo kijana si alichangia milioni 5 pia, au umesahau?🐒
 
Hata mimi wangenipa Namba ya simu ya kuchangia ningechangia chapchap, huyo kijana ameonesha uthubutu wa hali ya juu sana.
MAFISADI na MAJIZI mengine hayapelekwi mahakamani. Yanalindwa na mfumo, halafu kijana huyu amepelekwa mahakamani na kesi imekwenda kwa speed ya ajabu.
 
Jitahidi kulinda heshima yako kama mtu mzima kuna watoto humu ukihadaa umma hapa inakusaidia nini?una uhakika gani waliochangia ni kabila la Mbowe?Piga kura hapa uone ni watu wangapi watamuunga mkono huyo dogo unaemuita fala Mbwiga wewe
 
Usituambukize ujinga wako na habari zako za lissu ,tumeshafanya mengi Sana kwa ajili ya lissu ,huu ni wakati kuku wa kijivu ! Mchango wa gari ni mchango wa anasa ! Kwa sababu kama shida ilikuwa ni kumpa gari hata milion 30 inatosha kumnunulia gari zuri tu ! Tatizo lissu anataka anasa ndio maana milion 70 anaona Bado haitoshi ,watanzania hatuwezi kufanya vitu kwa mhemko
 
Ila nyie mnataka ya kuteka watu na kuwapeleka Osterbay polisi kuwatesa kisha kuwapeleka Katavi porini muwaue maiti ziliwe na fisi. Lakini Mungu akikataa na kumrudishia "mfu" uhai mnamdanganya "mama" yenu achangie badala ya kuwakamata kisha mumsifu kwa mchango wa kodi zetu sio?
Mna laana nyie!
 

Attachments

  • 20240704_075036.jpg
    150.3 KB · Views: 1
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…