CHADEMA flip flopping at its best! Jisomee mwenyewe uone


Bulyankulu kama sikosei alileta Mrema. Mimi sibishi nini Lissu kafanya dada Asha, mimi shida yangu ilikuwa records, nashukuru umeelezea records zake kuhusu madini.

Inaonyesha unapempenda Lissu sababu unampenda. I will try to find his documentary and see what inside. But at this particular moment we just agree that Lissu is another attorney, who specialized on contracts. Also we just agreed that Lissu is an intern in politics, and he will get better if he will start listen before he respond.

Again, i dont under estimate the guy, i salute him on several things concern Mikataba. However he shows lack of experience in political forum, and this is normal for any intern in politics. He will need adviser who will tell him what to talk, and when to talk and what to say. It take a while to be a good experiancial politician, it take nothing to stand on the podiums and say your opinions.
 

Mrema alidakia hoja ya Bulyankulu toka kwa kina Lissu kama mwanasiasa kwa kuwa wao walikuwa wanaharakati hawakuweza kuifanya iwe kisiasa. Na ndio maana wakawa naye. Ushahidi wa mrema ulitoka kwao. Lissu is a radical lawyer, activist cum politician. Aligombea ubunge kwao Singida sikumbuki ni jimbo gani akiwa na miaka kati ya 18 au 19 tu.

Ukweli ni kwamba katika hili yuko kama yule aliyesema dunia ni duara wakati dunia nzima iliamini dunia ni kama meza. Alinyongwa! Lakini leo dunia inaimba alichokisema. Sikubaliani na approach ya Chacha Wangwe, lakini miezi mitatu ijayo mtakuja kusema Tundu Lissu alikuwa sahihi. Fedha za walipa kodi zimetumika bure katika hii kitchen party commitee( I am told this is the sentence he used at mjadala na the so called wasomi).

Yes, i love the guy. I don't love you because you have no record in this country yet you blast my beloved one whose love is to the country and to the people rather than mafisadi.

I will always love him

Asha
 
Yes, i love the guy. I don't love you because you have no record in this country yet you blast my beloved one whose love is to the country and to the people rather than mafisadi.

I will always love him


Asha

Like I said somewhere in this forum not long ago: at end of the day, women will always be women!
 
VRS

N men u ll always b! Huyo ni wewe kwenye picha? No wonder una wivu

Asha
 

I actual search his records, again the guy is just a lawyer and activist. He have a good record in mining sector, and that what i was asking for, "just his records"

On the other side, he is imatured in politics, he have his own hatred politics movement. Honest i listen him two or three times, and from my point of view he seems to stuck in 1960's rebellion politics, which doesn't have chance in 21 century. Sasa kutoitambua kamati ya madini kutawasaidia nini wachimbaji wadogo wadogo? He seems to adopt Al Sharpton tacticts, which will not move him even single step forwad.

So, what does he want? JK to adopt his policy about what need to be done? I guess he is in deep sleep if he think CCM will ever do anything that upinzani suggest. He need to shishi and let the kamati do the job.
 

Demokrasia gani CCM waliweka,si walilazimika kutokana na changamoto za mabeberu.Kuprove hilo leo hii CCM wanajaribu kwa kila namna kuua upinzani.Wangekua wanaupenda upinzani leo hii wasingejaribu kuua jambo amabalo hawatafanikiwa.Wanatumia watu wasio na uchungu na taifa hili kupondea hoja zitakalolisogeza taifa letu mbele.Leo hii magazeti mengi yanatumika na CCM kufanya spinning,mfano mmojawapo ni hapa kijiweni.watu kama wewe mnakuja hapa kuchafua hoja za msingi kama ulivyoleta hiyo mada kiudaku udaku hapo juu ili kupoteza mwelekeo wa hiki kijiwe.

Yaani unakua tayari kufanywa kituko hapa kijiweni kumwaga upupu wako hapa.Huko CCM tunajua huu uhuru au fursa ya wewe kutoa mawazo hawakupi ndio maana leo hii unapwewa uhuru huo hapa JF unautumia desperately unaongeaga upuuzi hata kwenye hoja serious.

Mmedumazana akili mno ndio maana bado mnachagua kiongozi kwa kupiga kura za ndio au hapanautaratibu wa kikomunisti.kijana ndio maaana hapo juu ulikua unaniuliza namaanisha Demokrasia ipi,kwako naona demkrasia ni msamiati hata kama unaijua labda unaijua kwa sababu ulisikia ikisemwa na watu au waalimu wako wa uraia jambo ambalo hukulifanyia kazi ukaliacha kinadharia (theoretically)hivyo hivyo.Ndiyo maana huwezi kuhoji jambo lolte kwa wakuu wako hadi leo hii ndio maana unajifunza kuongea hapa jamvini.Ndio maana hii nchi imefikia huku ilikofikia.

Pole sana,jiunge na vyama vya upinzani katika mazingira haya haya ya kisiasa yaliyopo nchini leo hii ukatoe hoja zako za msingi na kuikosoa serikali hii kandamizii li na wewe nikuite shujaa kama utathubutu.
 
Hebu jaribu nilikobold ndani ya quots,nilikosea kufanya quotations
 
Kijana hata mimi naona umejitahidi kweli maanake si kawaida yako.

Mzee ES inaelekea ulimpa kijana shule.Naona anaanza taratibu A,B,C,D ,E.....

Kwi kwi kwi kwi!
 


Huyu ni Tundu Lissu wakati huoooooooo. Halafu unasema hajafanya kitu, soma kwa makini-kumbe Bomani naye alihusika kwenye masuala ya madini huko nyuma...

 
Baadaye Cheyo alikuja kupewa hisani akaachana na hoja yake. Alipoulizwa akawa anajibu, sisi tumefanya uchunguzi, wengine waendelee
 
Zitto sasa kama 'upupu' CHADEMA

Habari Zinazoshabihiana
• Hiza, Akwilombe watumika kummaliza Zitto 27.09.2007 [Soma]
• Polisi yachunguza kauli za Mbowe, Kabwe 07.09.2007 [Soma]
• CHADEMA wafadhaishwa na sakata la Kabwe, Amina 11.05.2007 [Soma]

*Kamati Kuu yatabiriwa 'kutofua nazi' Jumamosi
*Akigawa chama katika makundi na aitwa 'fisadi'


Na Mwandishi Wetu

KAMATI Kuu ya CHADEMA ambayo inatarajiwa kukutana Jumamosi ijayo kujadili pamoja na mambo mengine ushiriki wa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Bw. Zitto Kabwe, katika Kamati ya Kuangalia Upya Mikataba ya Madini nchini, inaweza isibadili msimamo wa Mbunge huyo, imebainika.

Hatua hiyo inatokana na mbunge huyo kusimamia upande wa kutetea maslahi ya Taifa na si yake binafsi, hali ambayo imesababisha mtafaruku ndani ya chama chake na kuzaa kambi mbili, moja ikitetea msimamo wake na nyingine ikiupinga.

Habari zilizopatikana ndani ya chama hicho jana, zilisema wakati muasisi wa chama hicho, Bw. Edwin Mtei, akimtetea Bw. Zitto kuendelea kushiriki ndani ya Kamati hiyo, Mbunge wa Tarime, Bw. Chacha Wangwe, anaonekana kukereka.

"Kibaya zaidi hata kama mlivyoona jana kwenye magazeti sasa Wangwe anahisi kuwa Bw. Zitto amepewa 'kitu kidogo' na CCM ili akubali kuwa ndani ya Kamati hiyo...kosa ni nini kama ndicho tulikuwa tukikipigia kelele hata bungeni?," alihoji Bw. Mathayo Lazaro aliyejitambulisha kuwa mwanachama wa CHADEMA.

Alisema yatakuwa ni maajabu kwa Bw. Zitto kujitoa katika Kamati hiyo wakati ndiye aliyewasilisha hoja binafsi kuhusiana na mikataba ya madini na kuibua suala la Buzwagi.

Ndani ya CHADEMA tayari kuna hisia kuwa CCM ina mpango wa kukisambaratisha chama hicho na ndiyo sababu Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete, akamwingiza Bw. Zitto katika Kamati hiyo na yeye kukubali na kumpongeza Rais.

Hatua hiyo ilisababisha hasira miongoni mwa viongozi na wanachama wa CHADEMA ambao walieleza kushangazwa kwao na Bw. Zitto kumsifia na kumpongeza kiongozi wa chama tawala.

Akisisitiza msimamo wake wa kutaka kuona Bw. Zitto akiendelea kubaki ndani ya Kamati hiyo, Bw. Mtei alikaririwa akisema hiyo ni fursa nzuri kwa chama chake kufikisha maoni na msimamo wake serikalini.

Watu wa karibu na Bw. Zitto wanaofahamu msimamo wake, walisema Kamati Kuu ya CHADEMA katika kikao chake cha Jumamosi isipokuwa makini itakuwa imemegua jiwe moja muhimu katika msingi wake.

"Inaonekana Zitto hawamwelewi vizuri ni mtu mwenye msimamo na mbishi constructively (enye manufaa), hawezi kusimamia katika ubishi wa kijinufaisha binafsi, ingawa anaweza kutumiwa na wengine kujinufaisha,wasipomwelewa kama anavyoamini yeye watamkosa," alisema mwana CHADEMA mwandamizi ambaye hakutaka atajwe gazetini.

"Tayari tunaona hivi sasa anahusishwa na ufisadi, huyu ni yule ambaye baada ya kusimamishwa kazi bungeni, alipitishwa mikoani kama Mwenge wa Uhuru...leo anapewa nafasi nzuri ya kulitetea Taifa, anaanza kusakamwa eti kanunuliwa, mbona hatutaeleweka wana CHADEMA?," alihoji mwanachama huyo.

Baadhi ya wachunguzi wa masuala ya kisiasa wanasema ingekuwa bora kama CHADEMA ingelichukulia suala hili kwa umakini mzuri kwani kumbadilisha Bw. Zitto kunaweza kusababisha mgawanyiko mkubwa na hata chama hicho kumeguka.

"Mambo ya siasa huanza hivi hivi, huwezi kujua, mbunge huyu machachari wa CHADEMA anaangalia wapi na ana hisia zipi ndani ya chama chake, alikuwapo Dkt. Walid Kabourou, akiwa na wafuasi wengi tena Kigoma, yuko wapi sasa? Na huyu ni wa huko huko!

"Tumesikia, wazee wa Kigoma wao wanataka aendelee kubaki ndani ya Kamati, sasa hicho kikao cha Jumamosi kitasaidia nini? Kama si cha kubadili msimamo wa Bw. Zitto, sawa kifanyike, lakini kama ni kinyume chake, hatudhani kama Zitto atakubali kuwa kinyonga kwa hili," alisema Bw. Elibariki Ulotu, aliyejitambulisha kuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Wakati huo huo, Reuben Kagaruki, anaripoti kwamba
Mwenyekiti wa TLP, Bw. Augustino Mrema, amesema hatua ya Rais Kikwete kumteua Bw. Zitto kwenye Kamati huyo kunalenga kuwagombanisha katika umoja wao.

"Kamati aliyounda Rais Kikwete ni ya 'magrini' itatufanya tugombane na kutugawa bure."

Bw. Mrema alitoa kauli hiyo jana alipozungumza na gazeti hili kwa simu alipoombwa atoe maoni yake kuhusiana na hatua ya Rais Kikwete kumteua mbunge huyo kuwa katika Kamati hiyo.

Bw. Mrema alisema hawezi kumzungumzia, lakini anajua wazi kuwa Kamati hiyo haiwezi kufanya chochote.

Alisema yeye aliwahi kuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Ndani hivyo anafahamu mambo mengi.

"Tulipopata misukosuko tulikuwa tunatafuta mbinu za kuzima moto kwa lengo la kuwapoza wananchi, ili jambo lisogezwe mbele," alidai Bw. Mrema.

Alisema mbinu hiyo ndiyo anayotumia Rais Kikwete kumteua Bw.Zitto katika katika Kamati hiyo. Alitolea mfano Tume nyingi zilizoundwa baada ya Serikali kupata misukosuso lakini baada ya mambo kupoa, hakuna hatua zilizochukuliwa.

Alitaja baadhi ya tume hizo kuwa ni pamoja na ya Jaji Nyalali,ya Jaji Warioba na ya Jaji Kisanga. Alisema mbali na tume hizo, zipo tano zilizoundwa kwa ajili ya kushughulia mambo ya madini, lakini hadi sasa hakuna hatua zilizochukuliwa.

Alisema kamati hiyo haiwezi kubadili chochote kwenye mikataba ya madini kwani mingi iliyosainiwa ni ya muda mrefu. "Mikataba ambayo Serikali imesaini ni ya miaka mingi hatuwezi kuibadili kwa sasa, labda Yesu arudi," alisema Bw. Mrema.

Alisema endapo Rais Kikwete atachukua hatua ya kuvunja mikataba iliyosainiwa, wahusika wanaweza kushitaki kwenye Mahakama ya Kimataifa na kuifanya Tanzania ikumbwe na yale yanayotokea Zimbabwe.

Bw. Mrema alisema kama Rais Kikwete anataka kutunga sheria ya mikataba ya madini hilo ni jambo rahisi. "Ni kiasi cha kuweka sheria kuwa mwekezaji akija atapata asilimia 49 na sisi (Watanzania) tutapata 51 ya mapato hakuna haja ya kuunda kamati," alisema Bw. Mrema na kuongeza kuwa kuunda kamati za aina hiyo, ni sawa na kuwachezea Watanzania.
 
Bw. Mrema alisema kama Rais Kikwete anataka kutunga sheria ya mikataba ya madini hilo ni jambo rahisi. "Ni kiasi cha kuweka sheria kuwa mwekezaji akija atapata asilimia 49 na sisi (Watanzania) tutapata 51 ya mapato hakuna haja ya kuunda kamati,"

Sasa naona hata wanasiasa wakongwe wanaanza kuongea Upupu mtupu!..Naanza kuamini kuwa kuna jicho baya la watu ktk uteuzi wa Zitto kwani hakuna anayetoa sababu za maana kuhusiana na uteuzi huo.
Eti - rais anaweza kusema toka leo mwekeshaji atapata asilimia 49, bila kuwepo na umuhimu wa kamati - Damn!
Hii nchi imekuwa ya Kisultan ama? maanake hawa ndio viongozi wetu hawa.
 
TAARIFA KWA UMMA

Maoni yangu Binafsi kuhusu Kamati ya Madini
iliyoteuliwa na Rais Kikwete

• Napinga Muundo, Mfumo na Mamlaka ya Kamati; nahoji
dhamira ya Rais Kikwete
• Sijawahi kupinga, sipingi na sitapinga Zitto Kabwe
kuteuliwa kwenye Kamati
• Zitto aingie kwenye Kamati kuendelea kuhoji na
kutuwakilisha
• Kupinga Kamati si maslahi binafsi, ni maslahi ya
Taifa- kupinga kwa nia ya kitaifa ni uzalendo.
• Gazeti la Mtanzania na Rai nipeni haki ya
kunisikiliza; chukueni maoni yangu toka kwangu
mwenyewe kuondoa kupotosha na kunichafulia jina.


Toka Rais Kikwete aunde Kamati ya Madini Novemba 13 na
kumteua Zitto Kabwe kama mmoja wa wajumbe, sijawahi
kujitokeza hadharani kutoa maoni yangu kuhusu suala
hilo hata nilipotakiwa kufanya hivyo na vyombo kadhaa
vya habari. Nilikwepa kutoa maoni yangu kutokana na
sababu mbili: Mosi, tayari nilishatoa maoni yangu
kuhusu kamati hii ya Rais toka Novemba 4 mara baada ya
Kauli ya Rais katika mkutano mkuu wa CCM. Pili; Mara
baada ya Novemba 14 Viongozi mbalimbali wa CHADEMA
walikuwa wametoa maoni yao kuhusu suala hili na kwa
kiasi wengine maoni yalitofautiana na baadhi ya vyombo
vya habari vikatafsiri kuwa ni mgogoro- hivyo sikutaka
kuongeza jina langu katika orodha ya watoa maoni
kuepusha kuendeleza hisia za kwamba
tunamgogoro-nilinyamaza kimya na kuyawasilisha maoni
yangu katika vikao vya chama chetu. Hata Novemba 17
ambapo Kurugenzi ya Vijana tuliandaa Kongamano la
Wasomi ambapo suala la Kamati hii pia lilijadiliwa,
sikutoa maoni yangu yoyote kuhusu hii kamati kwa
sababu ambazo nimezieleza.

Hata hivyo, nalazimika kwa shingo upande kuyatoa maoni
yangu kwa umma. Sababu mbili zimenisukuma nitoe kauli
yangu leo. Mosi, habari za gazeti la Mtanzania ambalo
katika matoleo kadhaa ya wiki hii limekuwa likinitaja
na mara moja ukurasa wa mbele kwamba napinga Zitto
Kabwe kuwepo kwenye Kamati(gazeti limewasilisha kwa
niaba yangu kitu ambacho sijakisema) na Gazeti la Rai
toleo la Jana(22/11/2007) ambalo si tu limerudia maoni
ya gazeti lake dada kwa niaba yangu- bali pia
limenihukumu natunguliza mbele maslahi yangu binafsi
badala ya maslahi ya Taifa. Katika hali hii ya
kutolewa maoni kwa wiki nzima, nikinyamaza wasomaji na
watanzania wenzangu wanaweza kudhani kwamba hayo ndiyo
maoni yangu. Nimeamua nitoe taarifa hii kutoa wazi
maoni yangu. Pili; kikao cha Kamati kuu ya CHADEMA
kinakaa kesho Jumamosi 24/11/2007- kwa vyovyote vile,
katika kikao hicho chama kitatoka na msimamo mmoja wa
chama baada ya kupokea maoni mbalimbali, hivyo baada
ya kikao hicho mimi kama kiongozi zitaweza tena kuwa
na fursa ya kuwasilisha maoni yangu binafsi kuhusu
suala hili. Nitawasilisha msimamo wa chama kama sehemu
ya uwajibikaji wa pamoja hivyo sitapata wasaa tena wa
kukanusha na kutoa maoni yangu binafsi tofauti na yale
yaliyoandikwa na magazeti ya Mtanzania na Rai. Napaswa
kusema sasa, ama ninyamaze milele.


Novemba 4, 2007 nilitoa msimamo wangu pale tu Rais
alipotangaza kuunda kamati hii- kwa ujumla katika
msimamo huo nilihoji dhamira ya Rais kuunda kamati
mpya wakati ya Masha aliyoiunda pindi alipoingia
madarakani na ikatangazwa kuwa imempatia ripoti yake
Septemba 2006 hatujaelezwa ilibaini nini na imeshindwa
kubaini nini ili iwe sababu ya kuundwa kwa kamati
nyingine. Pia nilisema wazi kwamba wapinzani hawapaswi
kunyamaza kwa kuwa tu watahusishwa kwenye kamati,
wapinzani wanapaswa kuendelea kutetea maslahi ya taifa
popote walipo na umma wa watanzania unapaswa kuendelea
na mjadala kuhusu madini na rasilimali zingine za
taifa. Na kwa ujumla nilieleza kwamba katika mazingira
hayo suala sio kuundwa kwa kamati, suala ni kutekeleza
matokeo ya kamati, na suala hili linahitaji kitu
kimoja tu- Dhamira ya kisiasa ya kuchukua hatua. Huu
ni msimamo wangu ambao sikuhitaji tena kuutolea maoni
baada ya Rais kuunda kamati mpya Novemba 13, 2007.

Mara baada ya Rais kuunda Kamati ya Madini na kumteua
Zitto Kabwe Novemba 13, (narudia tena)- sijawahi kutoa
msimamo wangu kwa chombo chochote cha habari.Kwa
waraka huu; nawasilisha rasmi maoni yangu kwa umma
kuhusu Rais kuunda Kamati ya madini:

Napinga Muundo, Mfumo na Mamlaka ya Kamati na nahoji
dhamira ya Rais Kikwete katika kuunda kamati yenye
muundo, mfumo na mamlaka kama kamati hii chini ya
Mwenyekiti Jaji Msaafu Mark Bomani. Baadhi ya masuala
ya kujiuliza yaliyopelekea niwe na maoni haya
nimeyadokeza kwenye ujumbe wangu niliowapatia baadhi
ya wahariri Novemba 19 mwaka 2007. Sijawahi kupinga,
sipingi na sitapinga Zitto Kabwe kuteuliwa kwenye
Kamati. Zitto aingie kwenye Kamati kuendelea kuhoji na
kutuwakilisha. Kupinga Kamati si maslahi binafsi, ni
maslahi ya Taifa- kupinga kwa nia ya kitaifa ni
uzalendo. Gazeti la Mtanzania na Rai nipeni haki ya
kunisikiliza; chukueni maoni yangu toka kwangu kuondoa
kupotosha na kunichafulia jina.

Kwa maoni yangu: Muundo wa Kamati unazua mjadala- Rais
aliahidi kwenye mkutano Mkuu wa CCM kwamba angeunda
kamati itakayoshirikisha jamii kwa upana zaidi ikiwemo
asasi za kiraia-lakini kamati iliyoundwa imejaa
watendaji wa serikali na makada wa chama tawala huku
asasi za kiraia zikiwa hazina mwakilishi hata mmoja
tofauti na ahadi ya Rais. Katika hotuba yake Rais
alizungumzia uwakilishi-lakini katika uteuzi wake Rais
amefanya uteuzi wa watu binafsi ingawa wanatoka katika
taasisi mbalimbali ikiwemo vyama vya upinzani. Katika
Lakini hili ni suala dogo. Kubwa zaidi katika muundo
wenyewe ni Rais kuwahusisha baadhi ya wajumbe wenye
tuhuma za ufisadi ambazo Rais alikuwa anazifahamu
kabisa toka wakati akiwa Waziri katika serikali na
wengine wanamgongano wa kimaslahi ambao uko bayana.
Kama aliwahujua watu hawa, nini dhamira ya kuwateua?
Je, hakuna watanzania wengine ikiwemo toka katika
chama chao ambao uadilifu wao hautiliwi mashaka ya
kiasi hicho?

Mfumo wa Kamati unazua mjadala-Hadidu rejea za kamati
zimetogezwa lakini katika hadidu rejea zilizotajwa
masuala ya haki za binadamu katika maeneo ya migodi na
ya uchafuzi wa mazingira hayajaguswa. Nini cha pekee
ambacho kamati hii itafanya ambacho Kamati ya Masha
iliyokamilisha kazi yake mwaka jana haijafanya? Imani
yangu ni kuwa suala hili litatazwa vyema- ripoti ya
Kamati ya Masha itawekwa wazi kwa umma, Kamati ya
Bomani itafanya kazi yake kwa uwazi na kuwa na vikao
vya masikilizano na umma(public hearings) na ripoti
yote itawekwa wazi kwa umma.

Mamlaka ya Kamati yanaibua mjadala- Uamuzi wa Rais
Kikwete kuunda Kamati badala ya Tume unanifanya nihoji
dhamira yake. Rais Kikwete anafahamu kabisa kuwa
Kamati haina mamlaka ya kutosha ya kuita mashahidi na
kuwataka kutoa ushahidi wa kiapo kama ambavyo Tume ya
Rais inavyo. Uamuzi wa kuunda Kamati unafanya dhamira
ihojiwe, je masuala ya madini ikiwemo sheria na
mikataba hayana masuala nyeti yanayohitaji mamlaka ya
Tume kuweza kuyafuatilia? Kwa vyovyote vile- kamati ya
Jaji Bomani pamoja na kuundwa na Rais kwa mujibu wa
sheria za nchi yetu haiwezi kuwa na mamlaka
makubwa(executive authority). Kama Rais Kikwete
aliweza kuunda tume kadhaa haraka katika kipindi
kifupi cha utawala wake, ni vipi suala hili ameacha
kuliundia tume na badala yake ameunda kamati? Suala la
Mamlaka ni nyeti kwa kuwa ikumbukwe kuwa suala
alilolitaka Zitto Kabwe bungeni ni kuundwa kwa Kamati
Teule ya Bunge ambayo ni wazi ingekuwa na mamlaka
yanayoshabihiana na yale ya Tume ya Rais.

Ukitafakari masuala hayo kiundani utaoana suala la
kujadiliwa si kuwepo au kutokuwepo kwa Zitto Kabwe
kwenye kamati- Hoja ni Kamati yenyewe na dhamira ya
Rais Kikwete katika kuiunda Kamati hiyo. Katika
muktadha huo basi; maoni yangu ni kuwa kama serikali
haitarekebisha kasoro hizo zilizopo kuhusiana na hiyo
kamati, Zitto Kabwe kama mmoja wa wajumbe bado
anapaswa kuendelea kushiriki ili kuwasilisha na
kuwakilisha fikra mbadala katika kamati hiyo. Zitto
akawe hamira ya kuumusha na kuchachusha hoja na
mchakato wa kamati ya Bomani. Na kuendelea kumjadili
Zitto Kabwe badala ya kuendelea kujadili masuala hayo
ni kukwepesha mjadala wa msingi.

Kwa maoni yangu, CHADEMA kama chama cha demokrasia na
maendeleo kimefanya uamuzi wa busara mpaka sasa
kuruhusu mjadala huu. Maoni tofauti baina ya baadhi ya
wanaCHADEMA yamewasaidi kuimulika kamati na kufahamu
undani wake- utamaduni huu wa kuhoji na kutoa fikra
mbadala ni muhimu kwa mustakabali wa taifa letu na
unapaswa kuendeleza. Imenisikitisha kwamba Gazeti la
Mtanzania na Rai wamemua wazi kusambaza ujumbe kwamba
kwa kuwa na maoni hayo mimi(na wamenitaja kwa jina)
kwamba natanguliza maslahi binafsi badala ya maslahi
ya Taifa. Na wamehusisha maoni yangu na kuchunguzana
nani atagombea urais 2010 kupitia CHADEMA mintaarafu
umaarufu wa Mbowe na Zitto. Kwa maoni yangu, huu ni
mkakati mwingine wa wakagawe uwatawale (divide and
rule); haya mambo ya Urais yanatoka wapi tena wakati
Zitto hata miaka 40 ya kugombea Urais atakuwa
hajafikisha wakati huo? Bahati njema, naamini viongozi
wa CHADEMA hawawezi kuchonganishwa na habari za
magazetini.

Kwa maoni yangu mimi, hoja zote zinatetea maslahi ya
taifa na ni za kizalendo. Wanaotaka kamati iwe na
muundo, mfumo mzuri na mamlaka zaidi wanatetea maslahi
ya taifa na ni wazelendo kama ambavyo wenye mtizamo
tofauti nao ni wazalendo. Ni kupitia fikra hizi
mbadala ndipo tunapata kilichobora zaidi na kukiendea
kama taifa. Hivyo, kama ambavyo itikadi ya CHADEMA
inaamini katika siasa zilizojuu ya vyama zinazosimamia
ziadi maslahi ya taifa. Hivyo hivyo, wanaopinga
muundo, mfumo na mamlaka ya kamati, hawafanyi hivyo
kwa manufaa ya kisiasa ya CHADEMA, wanataka CHADEMA
itumike kama chombo tu cha kutumika kusimamia fikra
hizi mbadala na matokeo yoyote mazuri ya fikra hizi
yatasimamia rasilimali za taifa na matokeo yale
yatanufaisha watanzania wote bila kujali itikadi.
Wazalendo hawakai kimya wanapoona jambo lolote katika
taifa lao linakwenda tofauti na hoja zao ama za
makundi ya kijamii ambayo wanayawakilisha. Maoni ya
pande zote ni mazuri kufanya watchdog function kwa
kamati; kwa mfano mijadala kama hii inaweza kupelekea
kamati kuacha kufanya kazi kwa kificho; kamati kufanya
kazi kwa undani zaidi na pengine hata kufanya matokeo
ya Kamati hii kutekelezwa kwa sababu ya ufuatuliaji wa
karibu wa wa vyombo vya habari na umma. Mambo haya ni
muhimu yakajadiliwa wakati kamati inaendelea kufanya
kazi kwa sababu kazi ya kamati miezi mitatu
inagharamiwa na walipa kodi watanzania; fedha hizi
zingeweza kutumika kujenga madarasa- hivyo kama kamati
haitafanya kazi kwa kadiri ya matakwa ya umma matokeo
yake ni hasara kwa taifa kwa ujumla bila kujali
itikadi. Ifahamike mjadala kuhusu ufisadi na hatma ya
rasilimali za Tanzania ni suala pana kuliko Kamati ya
Bomani. Nikumbushe kauli niliyoitoa mwaka 2005 wakati
wa uchaguzi- “Tanzania ni yetu sote; SIASA SIO UADUI”.

Naamini Kamati kuu ya kesho baada ya kupokea maoni
mbalimbali italipokea na kulitolea msimamo wa chama
suala hili na PAMOJA TUTAFIKA.

Nautoa waraka huu leo Ijumaa 23 Novemba mwaka 2007:


John Mnyika
Mkurugenzi wa Vijana Taifa(CHADEMA)
0754694553
mnyika@yahoo.com

PS: Natarajia Gazeti la Mtanzania la 24/11/2007 na
Gazeti la Rai la Wiki ijayo mtachapa maoni yangu kama
sehemu ya maadili ya vyombo vya habari ya kutoa fursa
kwa mhusika kutoa maoni yake kabla ya kuandika habari
inayomhusu. Naamini mtachapa ufafanuzi wangu kuhusu
suala hili.


Kwa maelezo zaidi na rejea(tazama viambatanisho):

Sehemu ndogo ya maoni yangu ya 4 Novemba 2007 Kama
yalivyonukuliwa Na Tanzania Daima 5 Novemba,
2007(maoni baada ya Mkutano Mkuu wa CCM)

Ujumbe kwa baadhi ya Wahariri nilioutoa 19 Novemba,
2007
 
Ndugu Mnyika,
Keep it up mkuu,at least umewakumbusha kile walichotakiwa kufanya.Haya magazeti ya propaganda siku hizi nayachukulia kama udaku.Rai na gazeti la mtanzania yameboa sana.Lakini huu ulikua ni mkakati katika vita haramu
 
Please read this before you proceed. You've been warned!

Admin nashukuru kwa prompt intervention yako.Inasikitisha sana mtu anajenga hoja yake halafu anaibuka mwingine anam-harass/discourage kwa grounds ambazo purely ni gender. Please admin. hawa watu wachukuliwe hatua haraka, hatuwezi kuvumilia zaidi kuona hawa dada zetu wanadhalilishwa kwenye forum inayoheshimika kama hii ya JF.
 
Haya malumbano tuliyategemea. Ndiyo tatizo la vyama vyetu vya upinzani, ndiyo maana havitaweza kukamata rungu. Zitto kuwepo kwenye kamati sioni kama ni tatizo, kwani alitafuta nafasi ya kuweka mambo bayana bungeni akabaniwa. Sasa huu ni wakati wake wa kufanya kweli halafu mnaanza kugawanyika. Kwa hiyo mlitaka aendelee kupiga porojo majukwaani bila kuwepo action?

Kama tulimwamini mpaka tukamtembeza mikoani kuelezea matatizo ya mikataba yetu, iweje leo hatumwamini kuwepo kwenye kamati? Mi nadhani tumpe nafasi afanye kazi, Zitto anajua nini cha kufanya tumpe sapoti tu. Kama kutatokea tatizo ndani ya kamati sidhani kama atakaa kimya bila kuweka bayana.

Tuache ushabiki wa kipuuzi ambao hauna maslahi kwa taifa letu.
 
Muoneni sasa kada alipo, yaani waaaay back before the firm, nilikuwa nao hawa jamaa, i was among the first online kada's uniting with the so called wapinzani, we used to get together discuss issues na wazee yaani way back, NIKAONA KUNA KILA HAJA YA KUWA MPINZANI, kama unabisha you do the history*reference jina:KadaMpinzani, baada ya kukosa utendaji wa haki, kuzidisha siasa kupita kiasi angalau nilijua ni POLITICAL LUGGAGE, now am watching wapinzani kuongea vyovyote wanavyoweza to get their day by,thats the reason why i like to celebrate being a CCM Kada so i can visualize the collages and images of my life nilipokuwa na wapinzani JF with no regrets of hate, NOW ITS HARD FOR THEM TO BREATHE kama wapo kwenye high altitude, no wonder everything i touch turns into CCM haooo yaani hate kupita kiasi wakati nilishasema sana tuweni pamoja, tuwafichue jamaa bila ya kujali vyama,WAKAKATAA NA KUSEMA SI UENDE MWENYEWE* now i rather walk on the sideways talking than kuwa na hawa jamaa.

Anyway weekend njema !
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…