Mr Why
JF-Expert Member
- Nov 27, 2019
- 2,235
- 4,252
Chama cha Chadema hakina heshima kwa viongozi wake, kinataka kumwondoa Mh Mbowe kihuni bila kujali mchango wake mkubwa ndani ya Chama hiki, Mbowe alitakiwa kustaafishwa kwa heshima kubwa
Mh Mbowe amejenga Chama kwa gharama kubwa ya fedha na Wanachama kwa zaidi ya miaka 30 historia hii ni kubwa sana
Mbowe wakati akianza uenyekiti Chama kilikua na hali mbaya sana hasa idadi ndogo ya wanachama pamoja na fedha za kujikimu
Hivyo basi Mh Mbowe alitakiwa kustaafishwa kwa heshima kubwa sana katika mchango wake huu mkubwa na sio kihuni kama vile kinavyofanya kwa sasa
Tatizo hili limeanzishwa na Tundu Lissu mwanasiasa mwenye mdomo mrefu sana kuliko wanasiasa wengine ndiyo maana akaingizwa kwenye jaribio la risasi miaka iliyopita, hii redio yenye sauti kubwa sana inashutumu uongozi wa Mh Mbowe mara kadhaa hii inaleta picha kuwa Lissu ni mtu asiye na heshima wala adabu kwa Mwenyekiti wa Chama
Angekuwa na heshima angemshauri Mh Mbowe katika vikao vyao vya Chama ili wakija hadharani watuoneshe matukio mawili tu ya Mbowe kustaafu na Lissu kupewa Uenyekiti badala yake hili jambo linafanyika kihuni mwisho Mh Mbowe aonekane hana mchango wowote na kuvunjiwa heshima yake moja kwa moja
Mh Mbowe atambue kuwa kitendo hiki kwake ni cha kumshushia heshima na kuharibu mchango wake wote ndani ya Chadema hivyo basi maumivu yake yatalaani Chama hiki na hakitafanikiwa tena huu ndio utakuwa mwanzo wa Chadema kufa
Mh Mbowe amejenga Chama kwa gharama kubwa ya fedha na Wanachama kwa zaidi ya miaka 30 historia hii ni kubwa sana
Mbowe wakati akianza uenyekiti Chama kilikua na hali mbaya sana hasa idadi ndogo ya wanachama pamoja na fedha za kujikimu
Hivyo basi Mh Mbowe alitakiwa kustaafishwa kwa heshima kubwa sana katika mchango wake huu mkubwa na sio kihuni kama vile kinavyofanya kwa sasa
Tatizo hili limeanzishwa na Tundu Lissu mwanasiasa mwenye mdomo mrefu sana kuliko wanasiasa wengine ndiyo maana akaingizwa kwenye jaribio la risasi miaka iliyopita, hii redio yenye sauti kubwa sana inashutumu uongozi wa Mh Mbowe mara kadhaa hii inaleta picha kuwa Lissu ni mtu asiye na heshima wala adabu kwa Mwenyekiti wa Chama
Angekuwa na heshima angemshauri Mh Mbowe katika vikao vyao vya Chama ili wakija hadharani watuoneshe matukio mawili tu ya Mbowe kustaafu na Lissu kupewa Uenyekiti badala yake hili jambo linafanyika kihuni mwisho Mh Mbowe aonekane hana mchango wowote na kuvunjiwa heshima yake moja kwa moja
Mh Mbowe atambue kuwa kitendo hiki kwake ni cha kumshushia heshima na kuharibu mchango wake wote ndani ya Chadema hivyo basi maumivu yake yatalaani Chama hiki na hakitafanikiwa tena huu ndio utakuwa mwanzo wa Chadema kufa