CHADEMA haina katibu mwenezi?

Malaria 2

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2023
Posts
6,846
Reaction score
10,288
Hivi mheshimiwa Lissu chama anakiendesha vipi? Katibu mwenezi mwenyewe? Mbona mambo yanaaza kuharibika mapema mno?

Kama ndani ya chama yupo mwaka 20 kama kiongozi wa juu, inafika mwezi anashindwa kuchagua uongozi uliotimia au haamini watu ndani ya CHADEMA?

Mbowe hayupo tena kwa kumbebesha lawama, tunataka kuona Chama kinaendeshwa kwa uwazi
 
Team Mbowe au Team Gombe? Punguza jazba....budget chama lazima iangaliwe....wanajipanga tuliza mshonoo
 
Mimi na pend3keza Malaria awe mwenezi wetu.
 
Mpeni muda Lissu atengeneze team yake! Mtiti ulikuwa mzito msiharakishe mambo. Rome was not built in a day!
 
Wewe ni CHADEMA? Ile meeting ya juzi hukuiona au hukuifuatilia? Kile NI chama na ule ni uongozi mpya wa chama kitaifa sio uongozi wa kikao cha harusi
 
..sijawahi kusikia Chadema ina Katibu Mwenezi.
 
Lissu Hana papara anakisuka chama taratibu ili oktoba amrudishe mtu unguja kulea wajukuu
 
Nanukuu "Baada ya Mkutano huu Mkuu, tutahitaji kujifungia ili kujipanga, ili kuja na kauli Moja ya Chama, sio kauli ya Mwenyekiti, ni kauli ya Chama..."

Tusubiri wamalize internal arrangements
 
Tunasafisha Nyumba na tunakusii uwe na subira mdogomdogo.
Hakuna linaloharibika CHADEMA. Tushamuondoa Mh.Mbowe na tunamalizia na huku chini.

Subira mkulu
 
Nanukuu "Baada ya Mkutano huu Mkuu, tutahitaji kujifungia ili kujipanga, ili kuja na kauli Moja ya Chama, sio kauli ya Mwenyekiti, ni kauli ya Chama..."

Tusubiri wamalize internal arrangements
Asanti sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…