Countrywide
JF-Expert Member
- Mar 2, 2015
- 20,694
- 32,527
Habari wadau wa JF, leo nipo kuwakumbusha wanachadema wenzetu juu ya mwenendo wa chama kipindi hiki cha kampeni.
Mwanzo kabisa nilikuwa napinga kabisa watu kukichangia chama kwa maana hatujui hizo pesa zitatumikaje na pengine zinaweza kuishia mikononi mwa wajanja wachache kama ilivyo kwa miaka mingine.
Ila mimi ni binadamu na nina moyo wa huruma sana, siwezi kuweka msimamo kwa jambo ambalo najua linaenda au linamuumiza binadamu mwenzangu. Naweka angalizo, wanaotakiwa kuchangiwa ni wale ambao hawakuwahi kuwa wabunge na wala sio viongozi wakubwa chamani. Hali ya kifedha kwa CHADEMA kwa sasa ni mbaya mno, haijawahi kutokea.
Chama kinatakiwa kufanya kampeni za kwenda mbali zaidi ili kuwafikia wananchi wengi, lakini hadi sasa imeshindikana kutokana na uhaba wa pesa unaokikumba chama chetu. Hivi navyoongea kuna majimbo mengi sana (74) wagombea wa ubunge hawajaanza kampeni, hawa hawahusiani na wale waliokata rufaa ya kutoteuliwa.
Na tatizo la kutoanza kampeni ni uhaba wa pesa kwa maana hawana vitendea kazi kama magari na watu wa kuzunguka kuwasaidia kufanya hizo kampeni. Ninajua watu wanataka mabadiliko, lakini pia wanahitaji kuwanua hao wanaotaka kuwaletea mabadiliko na ndio maana nzima ya kampeni inapokuja.
Hivyo ni lazima kwa mgombea wa upinzani kufanya kampeni, ila kwa hali iliyopo ninaona dalili nyingi sana za majimbo mengi ya chama chetu chadema kwenda chama tawala. Tusije baadae kuanza kulalamika tumeibiwa kura wakati hadi sasa sehemu kubwa ya wagombea wetu hadi leo hawajaanza kampeni.
Hivyo kwa dhati ya moyo wangu, ninawaomba tuwachangie hawa watu ambao hawana kabisa rasilimali pesa.
Tuache kusema ruzuku imetumikaje kwa kwa kuwa wengi tunajua kilichotokea na pesa ilivyoliwa kijanja na baadhi ya viongozi wetu.
Chini ni picha ya mgombea wetu lissu alipokuwa zanzibar kwenye kampeni. Uchache huu wa watu pia ni sababu ya kukosekana pesa ambazo zingeweza kutumika kwa ajili ya matangazo ya kampeni na kufanya watu kuja wengi kwenye kampeni.
Hivyo tusaidie ili mambo yasiwe magumu zaidi ya yalivyo sasa. Leo hii lissu alibidi awe kwenye kampeni mkoa fulani, lakini yupo kwake Tegeta amelala
Mwanzo kabisa nilikuwa napinga kabisa watu kukichangia chama kwa maana hatujui hizo pesa zitatumikaje na pengine zinaweza kuishia mikononi mwa wajanja wachache kama ilivyo kwa miaka mingine.
Ila mimi ni binadamu na nina moyo wa huruma sana, siwezi kuweka msimamo kwa jambo ambalo najua linaenda au linamuumiza binadamu mwenzangu. Naweka angalizo, wanaotakiwa kuchangiwa ni wale ambao hawakuwahi kuwa wabunge na wala sio viongozi wakubwa chamani. Hali ya kifedha kwa CHADEMA kwa sasa ni mbaya mno, haijawahi kutokea.
Chama kinatakiwa kufanya kampeni za kwenda mbali zaidi ili kuwafikia wananchi wengi, lakini hadi sasa imeshindikana kutokana na uhaba wa pesa unaokikumba chama chetu. Hivi navyoongea kuna majimbo mengi sana (74) wagombea wa ubunge hawajaanza kampeni, hawa hawahusiani na wale waliokata rufaa ya kutoteuliwa.
Na tatizo la kutoanza kampeni ni uhaba wa pesa kwa maana hawana vitendea kazi kama magari na watu wa kuzunguka kuwasaidia kufanya hizo kampeni. Ninajua watu wanataka mabadiliko, lakini pia wanahitaji kuwanua hao wanaotaka kuwaletea mabadiliko na ndio maana nzima ya kampeni inapokuja.
Hivyo ni lazima kwa mgombea wa upinzani kufanya kampeni, ila kwa hali iliyopo ninaona dalili nyingi sana za majimbo mengi ya chama chetu chadema kwenda chama tawala. Tusije baadae kuanza kulalamika tumeibiwa kura wakati hadi sasa sehemu kubwa ya wagombea wetu hadi leo hawajaanza kampeni.
Hivyo kwa dhati ya moyo wangu, ninawaomba tuwachangie hawa watu ambao hawana kabisa rasilimali pesa.
Tuache kusema ruzuku imetumikaje kwa kwa kuwa wengi tunajua kilichotokea na pesa ilivyoliwa kijanja na baadhi ya viongozi wetu.
Chini ni picha ya mgombea wetu lissu alipokuwa zanzibar kwenye kampeni. Uchache huu wa watu pia ni sababu ya kukosekana pesa ambazo zingeweza kutumika kwa ajili ya matangazo ya kampeni na kufanya watu kuja wengi kwenye kampeni.
Hivyo tusaidie ili mambo yasiwe magumu zaidi ya yalivyo sasa. Leo hii lissu alibidi awe kwenye kampeni mkoa fulani, lakini yupo kwake Tegeta amelala