Pre GE2025 CHADEMA hoja yenu iwe ni kuzuia wizi wa kura na siyo kuzuia uchaguzi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Atakaye chagua CHADEMA ndio atakaye ipeleka nchi hii kuangamia kabisa. Chagua kwa umakini 2025
 
Yaani na yeyote yule ambae amepinga ,anapinga sera za Hayati J.P. Magufuli. Asichaguliwe. CHADEMA na Mamluki wenzao wote. Hawachaguliki.
 
Mifumo ya uchaguzi ndiyo inspalilia wizi wa kura.
Tutazuia uchaguzi hadi pale kura za watz zitakapoheshimiwa
 
Kina Mbowe, Dr. Slaa, Lowasa walishafanya sana hayo, Kujaribu kucheza na timu ambayo kuanzia refa mpaka Linesmen ni wa Tajiri, Guess what! Mpaka leo CCM inatamba!
njia pekee ni kuzuia mechi isiwepo kabisa ili kuzua ushindi batili, they must be bloodshed for that to happen though.
 
Huu ujinga wako ulio uandika hapa ni kwasababu upo nyuma ya keyboards..... waulize waliopo field wakupe uhalisia

Just imagine 60% ya wagombea wanaenguliwa..... wewe umekaa unasubiri kulinda kura?
60% ya wapiga kura wako hawajioni kwenye daftati siku ya kupiga kura
80% ya mawakala wako wanaenguliwa kinyemela wanabaki mawakala wa ccm tu
Hata mpinzani akipata kura 10,000 na ccm kura 3,000 na msimamizi akitangaza Ccm kapata 10,000 na mpinzani 3,000 unadhani utafanya nini
Ukienda mahakamani mahakama ni za kwao
Hata wakala wako akigoma kusini haizuii chochote

Mnajiropokea ujinga tu hapa
 
Kwa jinsi ninavyoiona hoja ya CHADEMA ya no reform no election haija kaa vizuri inalenga kukiua chama moja kwa moja
Umeanza mada yako na mstari mbovu kabisa; na mengine yaliyo fuata pamoja na kuwa yanajadilika lakini uzito wake umepunguzwa na hitimisho lako bovu hilo!

Kama kudai HAKI ya kupiga kura bila mizengwe ni "kukiua chama", utategemea vipi kusimamia kura zinazo pigwa katika mazingira ya hovyo kabisa, halafu utoke jasho na damu kuzipigania? Hivi kweli unaelewa unachotaka kijadiliwe kwenye mada yako hii?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…