Elections 2015 CHADEMA ikipewa Nchi, Oktoba 2015, Hakuna Hatari Kugeuka Utawala wa Kidikteta? Nauliza Tuu!

Elections 2015 CHADEMA ikipewa Nchi, Oktoba 2015, Hakuna Hatari Kugeuka Utawala wa Kidikteta? Nauliza Tuu!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,

Preamble: Chadema ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo jina tuu, ila uendeshaji wake ni wa kidikteta wa hali ya juu!. Katiba yake inavipengele vya kidikteta vinavyokwenda kinyume cha katiba ya nchi!, hii thread ni ya swali tuu, Hivi Chadema ilivyo, bado haijakabidhiwa nchi, inatoa maamuzi ya kiimla na udikiteta wa ajabu!, Jee Chadema ikikabidhiwa nchi hapo October 2015!, hakuna hatari ya uwezekano wa kuigeuza nchi yetu kuwa ni nchi ya utawala wa kidikteta wa ajabu?!. Hili ni swali tuu nauliza mimi Paskali

Tanzania ni nchi ya kidemokrasia inayofuatia misingi ya sheria, taratibu na kanuni kwa mujibu wa katiba ya JMT ya mwaka 1977.

Katiba ndio sheria mama, kila kitu kuhusiana na shughuli yoyote ndani ya JMT ni kwa mujibu wa Katiba!. Sheria yoyote, kanuni yoyote na taratibu yoyote, inayokwenda kinyume cha katiba ni batili!.

Katiba yetu imeweka utaratibu wa kutafuta haki ndani ya JMT ni kupitia mhimili wa mahakama. Vyama vyote vya siasa nchini, viko kwa mujibu wa sheria ya vyama vya siasa!.

Kwenye sheria ya vyama hivyo, vyama kabla ya kusajiliwa, vinapaswa kuwasilisha katiba ya chama hicho na kupitiwa na wanasheria, ikukutwa iko sawa kwa mujibu wa katiba ya nchi, ndipo chama hicho hupewa usajili wa muda, kisha usajili wa kudumu!.

Hivyo ndivyo Chadema ilivyofanya ule mwaka 1992. Uliwasilisha katiba safi ya kidemokrasia yenye ukomo wa vipindi vya uongozi, kuwa ni vipindi viwili tuu, na wanachama wa Chadema walikuwa wako huru kufuata sheria za nchi!.

Mwaka 2006, Chadema ilifanya mabadiliko ya katiba, katika mabadiliko hayo, kile kipengele cha ukomo wa madaraka, kilinyofolewa kinyemela bila kujadiliwa popote!, hivyo marekebisho yaliwasilishwa kwa msajili wa vyama, hayakuwa tena na kipengele hicho cha ukomo, na kiliyeyuka bila muhtaasari wa kikao chochote kilichokijadili kipengele hicho!, hivyo marekebisho yaliyowasilishwa kwa msajili, kipengele hicho hakikuwepo, as if kimejadiliwa na kufikia uamuzi kiondolewe!, wakati kiukweli, hakikujadiliwa popote na yeyote bali kilinyofolewa tuu kinyemela, na katiba iliyowasilishwa mwaka 2006 hakikuwepo tena!.

Lengo la watungaji wa katiba mama ya Chadema, lilikuwa zuri, kwa uongozi wa Chadema kuwa na ukomo wa vipindi viwili vya miaka mitano mitano ili kupokezana vijiti ili kuzuia uongozi wa kisultani!. Mwaka huo wa 2006, wakaingia wajanja fulani!, wakakinyofoa kipengele kile, sasa uongozi wa Chadema hauna ukomo!. Yaani ni uongozi wa maisha mpaka kiongozi atakapoamua mwenyewe kuwa sasa amechoka!.

Mabadiliko hayo ya katiba ya Chadema ya mwaka 2006, pia yalipenyeza kipengele kinachomzuia mwanachama wa Chadema, kupeleka kesi yoyote mahakamani kukishitaki chama!. Hi ni kipengele cha kidikteta kuminya haki, na kiko kinyume cha katiba ya JMT, ambayo inasisitiza chombo pekee cha kutoa haki ndani ya JMT ni mahakama!. Kwa kipengele hiki, Chadema imejijengea himaya yake ya kidikteta ndani ya JMT ambayo haiutambui mhimili wa mahakama when it comes kwenye haki za wanachama wake, lakini when ni kuhusu haki za chama, ni mbio mahakamani!.

Mwanachama ukipeleka jambo lolote mahakamani, ukishindwa, hapo ndipo mwisho wa uanachama wako wa Chadema!.

Sasa nawauliza wanasheria na watetezi wa haki za binaadamu, hivi mwana Chama wa Chadema akikosa haki ndani ya chama chake akaitafute wapi?!.

Kama Chadema hivi tuu ni chama na bado hakijapewa dola, kimepenyeza vifungu vya kidikteta na kinyume cha katiba kwa kutoutambua mhimili wa mahakama, jee kikipewa nchi hiyo October, si ni kina uwezekano kabisa wa kuisimamisha kabisa katiba yenyewe na kutangaza utawala wa kiimla na kidikiteta jumla?!.

Hili la Katiba ya Chadema, nimewahi kulizungua hapa na nilishutumiwa sana na kunyooshewa vidole kuwa mimi ni CCM!.

Leo nimelikumbuka na kulizungumzia hapa, kufuatia mwanachama fulani wa Chadema, kupoteza uanachama wake, simply kwa kosa la kutafuta haki yake kwenye vyombo halali vya kutoa haki!.

Kwa udikiteta huu, na unaokwenda kinyume cha katiba ya nchi, enyi members wa jf wenye uelewa na sheria na katiba, ndio mnataka kutueleza nini kuhusiana na Chadema katika kufuata sheria taratibu na kanuni?!.

Nalirudia swali la msingi, Katiba ya Chadema ni "Unconstitutional" Jee ni Batili?. Na Chadema Ikipewa Nchi, Hakuna Hatari Kugeuka Dikteta?!.

Paskali

NB. Paskali ni mwanachama wa chama cha siasa!, ila pia ni an independent political commentator, asiyeegemea upande wowote, ambaye anazungumzia jambo lolote, kuhusu chama chochote. Sio mfuasi, mshabiki, wa kambi yoyote, au kiongozi yoyote, bali kama Mtanzania mwingine yoyote, kuna watu anaowakubali kijamii, kiuchumi na kisiasa, na siku ya kupiga kura, atapiga kura kuchagua kiongozi anayekupenda and not necessarily ni mgombea wa chama chake!.

Update 1.

Paskali

Unaidadisi Katiba ya CHADEMA? Basi, ilete tuijadili. Fanya scanning, tuoneshe Katiba ya awali na hiyo ya sasa ambayo unadai kwamba vipengele vimenyofolewa.

Wawakilishi wa wanachama waliokuwapo kwenye Mkutano Mkuu ndio walioipitisha. Unataka kutuambia kwamba wao ni watawala wa kiimla?

UMETUMWA?

Tunawajua watu wa aina yako. Baadae ukishindwa kujibu hoja unakaa kimya.

Haya, changamoto kwako. Tuletee hizo katiba unazodai zimechakachuliwa, tuuone ukweli. Wala usituletee soft copy. SCAN THE BLOODY THING. Weka hapa. Tutasoma wenyewe!

La sivyo, KAA KIMYA!
Mkuu MwanaHaki, kwanza asante kwa post hii, uzi huu unaelekea post 100, hii ndio posti ya kwanza kuijibu kwa sababu ndio post pekee iliyojikita kwenye subject matter!, na kufuatia post hii, nimeipeleka kule juu ili wenye kuhitaji kuujua ukweli, waujue ukweli, tuwaache hawa wajinga wajinga waendelee kupiga porojo!.

Hii sio mara ya kwanza kulizungumzia hili la Katiba ya Chadema kunyofolewa kipengele hicho cha ukomo wa madaraka!. Nilipouliza mwanzo nilijibiwa hivi.

WanaJF,

Pamoja na kuwa sitaki kuingilia mjadala katika hatua hii, naomba kuthibitisha kuwa:
I) Katibu Mkuu wa Chadema, kwa mujibu wa Katiba na Kanuni ya Chadema, ndiyo mhimili mkuu na mwenye jukumu la kutunza na kuhakikisha Katiba ya Chama inatunzwa.

2) Nataka kuwahakikishia wanachadema wote, kuwa nilikuwepo nimekuwa ndani ya Chadema kuanzia 1998 ambapo nilikuwa Makamu Mwenyekiti Bara, na baadaye 2003 Kaimu Katibu Mkuu, na hatimaye Katibu Mkuu. Hivyo nimeshiriki kikamilifu kuandaa Katiba ya 2004 na pia Katiba ya 2006 baada ya Rebranding ya Chama. Nataka niwahakikishie wanachadema, hakuna toleo lolote la Katiba ndani ya Chadema imeweka " muda wa Uongozi kuwa vipindi viwili tu", kuanzia Katiba aliyoiasisi Mzee Mtei na kupitishwa na Mkutano Mkuu, wala si ya 2004 au ya 2006. Kama kuna mtu anasema ilikuwepo na imeondolewa kinyemela, basi aonyeshe kifungu hicho kwenye Katiba yeyote ile, au miniti za kikao chochote kile.
Soma kwa makini hapo kwenye bold!, kisha tazama hapa kama ulivyoshauri, tena ni scanned copy na sio soft copy!
Suala hili lilifafanuliwa vyema na JJ Mnyika kama hivi.
Pasco nimesoma mjadala ulioanzisha na majibu ya Dr Slaa. Nimekubaliana na katibu mkuu kuna marekebisho kwenye majibu yake ya awali, katiba ya mwaka 2004 iliondolewe katika orodha ya katiba alizozitaja. Suala la kwamba kuna kipengele kiliondolewa kinyemela halina ukweli, na kilichofanyika 2006 ni kuandika katiba upya kama ambavyo nimeeleza kwenye majibu hayo.. Mjadala mwema. JJ
Pasco, Pamoja na marekebisho niliyoeleza kuhusu majibu ya Dr Slaa kwamba katiba ya 2004 iondolewe kwenye orodha kama nilivyochangia hapo awali. Katiba ya mwaka 2004 haiwezi kuwa ushahidi wa hayo madai yasiyokuwa ya kweli. Katiba ya mwaka 2004 mimi ninayo hapa nilipo, kwenye kifungu cha 6.3.2 kina kipengele cha 'muda usiozidi vipindi viwili katika cheo kimoja kwa ngazi moja'. Hata hivyo, huu sio ushahidi wa kwamba kipengele hiki kimeondolewa 'kinyemela'. Hii ni kwa sababu tatu; Mosi, 2006 hatukuwa tunafanya marekebisho ya katiba kwa maana ya kuondoa au kuacha kifungu cha katiba ya mwaka 2004. Tuliandika katiba upya, ndio maana tarehe 13 Agosti 2006 pale PTA tukafanya uzinduzi wa katiba mpya ya CHADEMA. Kwenye mchakato wa kukusanya maoni ya katiba mpya na hatimaye maandalizi ya rasimu ya katiba mpya, hili suala halikuingia kabisa. Halikupitishwa kwenye mapendekezo ya sekretariati, kamati kuu, baraza kuu na hata mkutano mkuu kwa kadiri ya kumbukumbu zangu. Hivyo huwezi kuzungumzia 'kuondoa kinyemela' kipengele ambacho hakikuingia.. JJ
Majibu ya Mnyika anasema 2006 walitunga katiba mpya!, taarifa iliyopo ofisi ya Msajili sio katiba mpya bali ni marekebisho ya Katiba!.
Ukomo wa Uongozi -Katiba ya Chadema 2004 .png
Ukomo wa Uongozi Ulionyofolewa Kinyemela 2006.png

Yaani Chadema imewasilisha marekebisho ya katiba yenye kifungu ambacho kimenyofolewa kinyemela, hakikujadiliwa popote, yaani katiba ya 2004 imeweka ukomo wa vipindi viwili vya uongozi, katiba ya 2006 ikavinyofoa kinyemela na sasa uongozi wa Chadema ni for life!. Excuse ya kuhalalisha uharamia huu, ni kuiita katiba ya 2006 ni katiba mpya!. Katika constitutional making process zote za kutunga katiba mpya, katiba ya zamani hujadiliwa kipengele kwa kipengele, na ndipo katiba mpya hutungwa. Hakuna mahali popote kipengele hiki cha ukomo wa kipindi cha uongozi, kilijadiliwa!, kwa lugha rahisi, kipengele hiki kili 'just vanish into thin air!.

Na kipengele kinachokiuka katiba ya JMT ni hiki.

x. CHADEMA itashughulikia matatizo ya viongozi nawanachama kwa kufuata taratibu zilizowekwa kwa mujibu wa Katiba ya Chama, wala hata siku moja haitashughulikia mambo kama hayo Mahakamani. Mwanachama atakayeshindwa kufuata taratibu na ngazi za Chama hatavumiliwa na atafukuzwa uanachama.

Paskali
 
Tunahitaji maamuzi sahihi kwa wakati huu huu sio mwaka kesho! Hata hivyo ile mvua ya mabomu imefikia wapi! Na hayo ndo maamuzi sahihi!!???
 

Wanabodi!.

Kama Chadema hivi tuu ni chama na bado hakijapewa dola, kimepenyeza vifungu vya kidikteta na kinyume cha katiba kwa kutoutambua mhimili wa mahakama, jee kikipewa nchi hiyo October, si ni kina uwezekano kabisa wa kuisimamisha kabisa katiba yenyewe na kutangaza utawala wa kiimla na kidikiteta jumla?!.

Hili la Katiba ya Chadema, nimewahi kulizungua hapa na nilishutumiwa sana na kunyooshewa vidole kuwa mimi ni CCM!.

Leo nimelikumbuka na kulizungumzia hapa, kufuatia mwanachama fulani wa Chadema, kupoteza uanachama wake, simply kwa kosa la kutafuta haki yake kwenye vyombo halali vya kutoa haki!.

Kwa udikiteta huu, na unaokwenda kinyume cha katiba ya nchi, enyi members wa jf wenye uelewa na sheria na katiba, ndio mnataka kutueleza ni i kuhusiana na Chadema katika kufuata sheria taratibu na kanuni?!.

Nalirudia swali la msingi,
Katiba ya Chadema ni "Unconstitutional" Jee ni Batili?. Na Chadema Ikipewa Nchi, Hakuna Hatari Kugeuka Dikteta?!.

Pasco.


NB. Kwa msisitizo: Pasco wa jf, sio mwanachama wa chama chochote cha siasa!, hajawahi kujiunga na chama chochote cha siasa, wala hana mpango wowote wa kujiunga na chama chochote, kwa lengo la lolote, bali ni political commentator, ambaye anazungumzia jambo lolote, kuhusu chama chochote. Sio mfuasi, mshabiki, wa kambi yoyote, au kiongozi yoyote, bali kama Mtanzania mwingine yoyote, kuna watu anaowakubali kijamii, kiuchumi na kisiasa, na siku ya kupiga kura, atapiga kura kuchagua kiongozi.


Kila mwanachama lazima asome katiba vizuri aielewe kabla hajafanya lolote. soma hapo kwenye nyekundu

8.0. HATUA ZA KINIDHAMU KWA WABUNGE, MADIWANI,WENYEVITI WA VIJIJI/MITAA NA VITONGOJI
UTANGULIZI:

Wabunge, Madiwani, Wenyeviti na Vijiji/Mitaa na Vitongoji katikaChama, ni sauti za Chama Serikalini na ni nyenzo za kuweza kutafsiriSera na Ilani ya Chama kwa vitendo Serikalini. Ni makada wakuonyesha misimamo ya Chama katika mambo mbalimbali yahusuyonchi yetu kwa kutumia majukwaa yao kwa mujibu wa nafasi zao.Ni watu ambao umma umewapa dhamana kubwa kwa heshima yaona heshima ya Chama chetu. Kwa hiyo ni wajibu wa Chamakuwaheshimu, kuwalinda na kuwasaidia kutimiza majukumu nawajibu wao kwa Chama na kwa umma kwa uhuru na kujiamini kwakufuata taratibu zilizopo kwa mujibu wa Katiba ya Chama.

(a) WABUNGE & WENYEVITI WA HALMASHAURI:
Ili hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi ya Mbunge auMwenyekiti wa Halmashauri zifuatazo zitakiwa zifuatwe:-

i. Malalamiko juu ya utovu wa nidhamu au jambo lolotelinalolalamikiwa yafikishwe kwenye kikao cha Kamati Kuukwa maandishi kupitia ofisi ya Katibu Mkuu.

ii. Kamati Kuu bila kulazimika kuita pande zinazohusika,itajadiri mantiki ya lalamiko na kuona kama kuna hoja yamsingi katika lalamiko husika.

iii. Kamati Kuu ikiridhika kuwa kuna hoja ya msingi itaundaKamati ya watu kati ya 5 na 7 ili kuchunguza suala linalolalamikiwa kwa kuwapa hadidu za rejea.

iv. Kamati katika uchunguzi wake italazimika kuwaitawalalamikaji na mlalamikiwa na kuwahoji juu ya sualahusika na kupata ushahidi wa pande zote.

v. Kamati hiyo haitakuwa na uamuzi wowote juu ya suala hilobali itaandika taarifa ya uchunguzi na kutoa mapendekezokwa Kamati Kuu.
vi. Kamati Kuu baada ya kupokea mapendekezo hayoinawezi kuchukua hatua za dharura kama itaona inafaa juuya suala hilo ili kunusuru Chama kama kuna hali yakutishia hatima na uhai wa Chama, na kupendekeza hatuaza mwisho kwenye Baraza Kuu.

vii. Baraza Kuu litatoa uamuzi juu ya suala hilo bila kulazimikakuita pande zinazohusika na kuruhusu hatua ya rufaakwenye Mkutano Mkuu.

viii. Kama upande wowote katika kesi hiyo haukubaliani nauamuzi wa Baraza Kuu utakata rufaa kwenye MkutanoMkuu, lakini kwa wakati wote kabla ya rufaa yakekusikilizwa upande huo ukubali na utii maamuzi ya BarazaKuu. Kushindwa kufanya hivyo litakuwa ni kosa lakinidhamu ambalo adhabu yake ni kubatilisha (kutupwa)kwa rufaa yake.

ix. Mkutano Mkuu utakuwa na maamuziya mwisho kwajambo lolote na pande zinazo husika ni lazima zitiimaamuzi ya Mkutano Mkuu. Mtu yeyote atakayeshindwakutii uamuzi wa Mkutano Mkuu atakuwa anatofautiana naChama na kuanzia saa hiyo uanachama wake utakuwaumekoma.

x. CHADEMA itashughulikia matatizo ya viongozi nawanachama kwa kufuata taratibu zilizowekwa kwa mujibu wa Katiba ya Chama, wala hata siku moja haitashughulikia mambo kama hayo Mahakamani. Mwanachama atakayeshindwa kufuata taratibu na ngazi za Chama hatavumiliwa na atafukuzwa uanachama.

xi. Upande wowote unaohusika na mgogoro unawezakuomba kuitwa na kikao chochote kinachoshughurikiasuala hilo ili kuota ufafanuzi zaidi.
 
8.0. HATUA ZA KINIDHAMU KWA WABUNGE, MADIWANI,WENYEVITI WA VIJIJI/MITAA NA VITONGOJI
UTANGULIZI:

Wabunge, Madiwani, Wenyeviti na Vijiji/Mitaa na Vitongoji katikaChama, ni sauti za Chama Serikalini na ni nyenzo za kuweza kutafsiriSera na Ilani ya Chama kwa vitendo Serikalini. Ni makada wakuonyesha misimamo ya Chama katika mambo mbalimbali yahusuyonchi yetu kwa kutumia majukwaa yao kwa mujibu wa nafasi zao.Ni watu ambao umma umewapa dhamana kubwa kwa heshima yaona heshima ya Chama chetu. Kwa hiyo ni wajibu wa Chamakuwaheshimu, kuwalinda na kuwasaidia kutimiza majukumu nawajibu wao kwa Chama na kwa umma kwa uhuru na kujiamini kwakufuata taratibu zilizopo kwa mujibu wa Katiba ya Chama.

(a) WABUNGE & WENYEVITI WA HALMASHAURI:
Ili hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi ya Mbunge auMwenyekiti wa Halmashauri zifuatazo zitakiwa zifuatwe:-

i. Malalamiko juu ya utovu wa nidhamu au jambo lolotelinalolalamikiwa yafikishwe kwenye kikao cha Kamati Kuukwa maandishi kupitia ofisi ya Katibu Mkuu.

ii. Kamati Kuu bila kulazimika kuita pande zinazohusika,itajadiri mantiki ya lalamiko na kuona kama kuna hoja yamsingi katika lalamiko husika.

iii. Kamati Kuu ikiridhika kuwa kuna hoja ya msingi itaundaKamati ya watu kati ya 5 na 7 ili kuchunguza suala linalolalamikiwa kwa kuwapa hadidu za rejea.

iv. Kamati katika uchunguzi wake italazimika kuwaitawalalamikaji na mlalamikiwa na kuwahoji juu ya sualahusika na kupata ushahidi wa pande zote.

v. Kamati hiyo haitakuwa na uamuzi wowote juu ya suala hilobali itaandika taarifa ya uchunguzi na kutoa mapendekezokwa Kamati Kuu.
vi. Kamati Kuu baada ya kupokea mapendekezo hayoinawezi kuchukua hatua za dharura kama itaona inafaa juuya suala hilo ili kunusuru Chama kama kuna hali yakutishia hatima na uhai wa Chama, na kupendekeza hatuaza mwisho kwenye Baraza Kuu.

vii. Baraza Kuu litatoa uamuzi juu ya suala hilo bila kulazimikakuita pande zinazohusika na kuruhusu hatua ya rufaakwenye Mkutano Mkuu.

viii. Kama upande wowote katika kesi hiyo haukubaliani nauamuzi wa Baraza Kuu utakata rufaa kwenye MkutanoMkuu, lakini kwa wakati wote kabla ya rufaa yakekusikilizwa upande huo ukubali na utii maamuzi ya BarazaKuu. Kushindwa kufanya hivyo litakuwa ni kosa lakinidhamu ambalo adhabu yake ni kubatilisha (kutupwa)kwa rufaa yake.

ix. Mkutano Mkuu utakuwa na maamuziya mwisho kwajambo lolote na pande zinazo husika ni lazima zitiimaamuzi ya Mkutano Mkuu. Mtu yeyote atakayeshindwakutii uamuzi wa Mkutano Mkuu atakuwa anatofautiana naChama na kuanzia saa hiyo uanachama wake utakuwaumekoma.

x. CHADEMA itashughulikia matatizo ya viongozi nawanachama kwa kufuata taratibu zilizowekwa kwa mujibu wa Katiba ya Chama, wala hata siku moja haitashughulikia mambo kama hayo Mahakamani. Mwanachama atakayeshindwa kufuata taratibu na ngazi za Chama hatavumiliwa na atafukuzwa uanachama.

xi. Upande wowote unaohusika na mgogoro unawezakuomba kuitwa na kikao chochote kinachoshughurikiasuala hilo ili kuota ufafanuzi zaidi
 
umeandika kwa kiwango cha chini sana. Ukiwa mwanachama wa TFF hupaswi kupeleka mashtaka mahakamani. Sababu ni rahisi sana, exhaust remedy zote zilizo ndani ya chama kama ukiwa bado aggrieved una haki ya kwenda mahakamani. Labda kama neno ouster clause ni kubwa sana kwako kulifahamu
 
Hatari gani unayoiongelea Pasco,Mbona tupo utawala wa kidikteta tayari? Ama u dikteta ni nini? Kama watu wanauwawa,vitisho na vyombo vya Usalama kutumikia amri za watu na waziri mkuu kuamuru watu wapigwe..Tupo katika udikteta tayari labda kama udikteta unaoongelea wewe una exception kwa baadhi ya watu kufanya.
 
maamuzi sahihi hutoka kwa muda sahihi
mahakama imetoa uamuzi, cdm kupitia MWANASHERIA WAKE imeeleza nini maana ya uamuzi wa mahakama kwa zzk na cdm

ccm inapokosea ni kuchelewa kutoa uamuzi
hivi kwa akili ya kawaida Sospita muongo, Tibeijuke walitakiwa kuchukuwa wiki kadhaa kuondoshwa uwaziri?
unaonaje kama rais angewatimua hao walitajwa hapo juu just siku ya pili baada ya taarifa ya escrow bungeni asingejiongezea kuaminika na kuogopwa??
ccm walishindwa kuwavua magamba lowassa, rostam na chenge kwa ujinga huu wa kuchelewa kutoa uamuzi
uamuzi wa haraka ni muhimu, hujenge nidhamu na huwafanya wenye nia mbaya kukiogopa chama/taasisi
 
Hapo ndo unafiki wa pasco unapoaanza mtu akisimamia katiba mnasema dikitetor akishidwa kusimamia mnaanza ooh hakuna uwajibikaji.
je mnataka wafanye nini?
PASCO NI MFUASI WA LOWASSA
ZITTO NI MFUASI WA LOWASSA
ZITTO kaachwa na CCM aadhibike kwa kuwa ni mfuasi wa lowassa
 
Acheni propaganda za kuwatishia watu. Nani alikuambia nchi inaongozwa kwa katiba za vyama vya siasa? Tunayo katiba ya nchi na ndiyo maana hatutaki kufnya makosa ya kuburuzwa na katiba ya chenge. Tunahitaji katiba safi itakayoutongoza kwenye utanzania wetu na si katiba za vyama.

Sasa mnataka CHADEMA kiwage kinachekelea chekelea hata pale mtu anapokuwa ameharibu? Hafukuzwi utanzania, bali anafukuzwa kwenye chama ili ajipange upya na akijiweka sawa awe mwanachama bora. Mtanzania akikosea atahukumiwa kwa mujibu wa katiba ya nchi na si katiba ya chama.

AU KWA VILE KIKWETE ANAONGOZA NCHI KWA KUTMIA KATIBA YA CCM, BASI MNAHOFU KWAMBA TANZANNIA ITAMILIKIWA NA CHADEMA SASA? TZ NI YA WATANZANIA TU NA SISI WATANZANIA TUNA UHURU WA KUAHMA VYAMA VYA SIASA NAMNA TUNAYOPENDA, LAKINI TUNABAKI KUJIVUNIA UTANZANIA WETU!.


ILA AWAMU YA TANO UKAWAAAAAAAAAAAAAAAAA!. CCM MMETUUMIZA VYA KUTOSHA TENA HATUPENDI KUWASIKIA WALA KUWAONA ONA MNAJUA!!!!!!!!!!!!!!!! Ohhhhhhhhhhhhhhhooooooooooo, shauri yenu, endeleeni kujishaua shaua mtandani wakati kuna watu wana vipaji tofauti!.
 
pasco
mnafiki mwenzako zitto ndo huyo chadema ilishamdampo mchukueni kama mnampenda mmpe kiendo ndani ya ccm
 
ITAUWA WATU WENGI SANA.
just imagine uwe na waziri kama sugu halafu ujifanye kumchimbachimba,kama hajatuma watu wakakunyonga ama kukupiga shaba.
lema awe waziri umletee vyoko,utaokotwa mtaloni minus your head.
 
...Nalirudia swali la msingi, Katiba ya Chadema ni "Unconstitutional" Jee ni Batili?. Na Chadema Ikipewa Nchi, Hakuna Hatari Kugeuka Dikteta?!.

Pasco.


NB. Kwa msisitizo: Pasco wa jf, sio mwanachama wa chama chochote cha siasa!, hajawahi kujiunga na chama chochote cha siasa, wala hana mpango wowote wa kujiunga na chama chochote, kwa lengo la lolote, bali ni political commentator, ambaye anazungumzia jambo lolote, kuhusu chama chochote. Sio mfuasi, mshabiki, wa kambi yoyote, au kiongozi yoyote, bali kama Mtanzania mwingine yoyote, kuna watu anaowakubali kijamii, kiuchumi na kisiasa, na siku ya kupiga kura, atapiga kura kuchagua kiongozi.

Kwani Udikteta una tatizo gani? Kwangu mimi poa tu kama udikteta ndiyo utakao tutoa hapa tulipo kwenye dimbwi la Umaskini, ujinga, Unyonge n.k basi na iwe hivyo!

Jamii zote Duniani zina lengo moja la kuboresha na kutatua matatizo ya Wananchi wake ila njia za kufika huko ndio hutofautiana, hivyo kama CHADEMA wakiwa Madikteta kwanza mimi kwangu hata kama wakifuta Chaguzi nchini powa tu cha muhimu nchi iende na iondoke hapa tulipo, cha muhimu hawa watawala wa sasa hivi Kikwete, Pinda &Co. wauwaji wa maalbino na Mungu awalaani waondoke hilo ndiyo muhimu!
 
Nalirudia swali la msingi, Katiba ya Chadema ni "Unconstitutional" Jee ni Batili?. Na Chadema Ikipewa Nchi, Hakuna Hatari Kugeuka Dikteta?!.

Pasco.

Kaka msomi wa kitivo cha sheria cha Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam, natumai hapo chuoni ulisoma pia mambo ya mantiki.

Kwa mtaji huo, je, hilo swali lako lina mantiki kweli?

"Katiba ya Chadema ni "Unconstitutional" Jee ni Batili?"


Duuh!
 
Pasco ndio maana kuna vyama vingi.. Unachotakiwa kufanya ni kusoma katiba ya chama na kuona kama kuna kipengele kinakukwaza basi unaenda kwenye chama kingine..



NB. Kwa msisitizo: Pasco wa jf, sio mwanachama wa chama chochote cha siasa!, hajawahi kujiunga na chama chochote cha siasa, wala hana mpango wowote wa kujiunga na chama chochote, kwa lengo la lolote, bali ni political commentator, ambaye anazungumzia jambo lolote, kuhusu chama chochote. Sio mfuasi, mshabiki, wa kambi yoyote, au kiongozi yoyote, bali kama Mtanzania mwingine yoyote, kuna watu anaowakubali kijamii, kiuchumi na kisiasa, na siku ya kupiga kura, atapiga kura kuchagua kiongozi.

Hii kauli yako ni sawa na mlevi wa pombe ya pingu anaedai hajajisaidia haja kubwa wakati anafuatwa na manzi nyuma..
 
Last edited by a moderator:
Pasco Pascoooooooooooooooo

Hahahahahahahahahahahahahahahahahahahahahahahahahahahahahahahhahhaha

Pascooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooo

Unajua brother tumelelewa katika mfumo ambao unashindwa kuchukua maamuzi kutokana na sheria na katiba

Sasa tunapoona watu wanachukua hatua kutokana na sheria na katiba tunaogopa saaaaana

Nilidhani katika hili pasco utakuwa muelewa sana

Nashangaa kwa kweli...You are better than this.
 
Last edited by a moderator:
We Pasco sometimes unaniacha hoi.
1.Unajifanya neutral? Kwa hiyo leo unamkana rasmi EL?
2.Haki gani unayoiongelea kutotolewa na mahakama? Nijuavyo huyo unayeficha jina lake,Mwite Mhusika Mkuu(MM) angeshafukuzwa pamoja na akina Mwigamba na Kitila kwa makosa yanayoendana.Yeye kaamua kwenda kutafuta haki mahakamani.Asijadiliwe.Na mahakama imefanya kazi yake,imeona MM hana haki ya kuzuia chama chake kisimjadili.Haki ya kumjadili na kumwadhibu wanayo chama chake.Hapa mahakama haijafanya kazi yake? Imezuiliwa wapi na CHADEMA?
3.Tukiwa wakweli tutakubali kuwa MM amepata alichostahili,tena siku nyingi.
 
Back
Top Bottom