Uchaguzi 2020 CHADEMA imeomba vyombo husika vifuatilie tetesi za kuwepo mipango ya kuvuruga mchakato wa kuelekea katika hatua za kurudisha fomu

Uchaguzi 2020 CHADEMA imeomba vyombo husika vifuatilie tetesi za kuwepo mipango ya kuvuruga mchakato wa kuelekea katika hatua za kurudisha fomu

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869
22 August 2020
Tunduma, Songwe
Tanzania



CHADEMA imeomba vyombo husika vifuatilie tetesi za kuwepo mipango ya kuvuruga mchakato wa kuelekea katika hatua za kurudisha fomu za wagombea. Hivyo wameomba uchunguzi na hatua za haraka za kiuchunguzi zifanyike ili kama kweli mipango hiyo ipo basi vyombo husika vilivyoahidi kusimamia uchaguzi huru na haki vizuie njama hizo ovu.

Tayari wagombea kadhaa wa udiwani wa CHADEMA waliohudumu muda mrefu kabla mabaraza ya madiwani hayajavunjwa kufuatia kumalizika kwa kazi zao 2015 -2020 wameitwa kuhojiwa uraia wao.

CHADEMA inashangaa vipi viongozi hao waliohudumu katika Baraza la Madiwani la Halmashauri waanze kuhojiwa kipindi hiki kuelekea mchakato wa kurudisha fomu unaotarajiwa kuhitimishwa tarehe 25 Agosti 2020 ili waweze kuomba kuchaguliwa na wananchi wa Tunduma.

Madiwani teule waliopendekezwa na CHADEMA, mbele ya waandishi wa habari waongea kuhusu kupokea simu zilizopigwa na watu waliojitambulisha ni maofisa wa Idara ya Uhamiaji kuitwa kwenda kuhojiwa uraia wao. Diwani wa kata ya Sogea Tunduma alihojiwa kwa masaa kadhaa ktk ofisi za Uhamiaji Tunduma na kutakiwa kupeleka viambatisho vya vyeti vya kuzaliwa kesho kutwa Jumatatu tarehe 24 Agosti huku madiwani wengine wa CHADEMA walioshindwa kufika ofisi za Uhamiaji wakiendelea kuombwa kufika ofisi za Uhamiaji.

Viongozi wa CHADEMA Tunduma wanasema hizo ni njama za kutengeneza mazingira madiwani wa CCM wapite bila kupingwa katika uchaguzi wa Oktoba 2020. Kwani mmoja wa wagombea wa udiwani wa CHADEMA aliyeitwa Uhamiaji ana kaka yake ambaye ni mgombea wa udiwani wa CCM lakini huyu wa CCM hajaitwa kuhojiwa uraia.
Source : DSS Tunduma
 
Naamini pamoja na kutoa angalizo, ni vyema chama pia kikaweka ulinzi binafsi ikiwa ni pamoja na kurekodi kila tukio! Tunduma hamshindwi kununua secret cameras kama pen, saa, miwani, kofia etc ili kuweka records sawa.

Huu sio wakati wa kutegemea sana kufanyiwa kila jambo Na watu walewale tunaowatuhumu! Kutegemea eti Polisi wawatendee haki saa hizi ni kujidanganya.

Chukueni extra mile baada ya hii ya kutoa report na hili liwe angalizo kwa Wagombea wote nchi nzima. Kwa mfano, sitegemei ule ujinga uliotokea Korogwe wa kupokea form Dada yangu Aminata Saguti tena kwenye ofisi za serikali utokee tena....
 
Uraia Waweza hojiwa muda wowote kabla 2015 Magufuli hakuwa madarakani rushwa na ufisadi ulikuwa nje nje kaingia kuhoji ruksa Kama mtu raia Hana Cha kuogopa
 
Kiukweli hata kama kuna nia njema, uhamiaji wamekosea sana aproach yao. Tume ya taifa waongee na vyombo vya dola, tabia ya kutisha wagombea wa upinzani kuelekea uchaguzi mkuu inaondoa uchaguzi kuwa huru na haki.chadema makao makuu msikae kimya, nendeni uhamiaji makao makuu ya jeshi La polis waambieni.msikae kimya.
 
Kiukweli hata kama kuna nia njema, uhamiaji wamekosea sana aproach yao. Tume ya taifa waongee na vyombo vya dola, tabia ya kutisha wagombea wa upinzani kuelekea uchaguzi mkuu inaondoa uchaguzi kuwa huru na haki.chadema makao makuu msikae kimya, nendeni uhamiaji makao makuu ya jeshi La polis waambieni.msikae kimya.
Uraia Ni suala mtambuka wewe
Anatory Amani wa ccm alishawahi kupokwa uraia wake katika mazingirq Kama haya ya uchaguzi,Kama uraia wako hauna utata ya nini kujipa presha?
 
Uraia Waweza hojiwa muda wowote kabla 2015 Magufuli hakuwa madarakani rushwa na ufisadi ulikuwa nje nje kaingia kuhoji ruksa Kama mtu raia Hana Cha kuogopa

Kwani Magufuli ndio kadhibiti rushwa na ufisadi, au kadhibiti matangazo ya rushwa na ufisadi? Wagombea wa ccm si karibia wote wameshinda kwa kutoa rushwa? Au unadhani tunasubiri propaganda zenu bila kuona wenyewe uhalisia? Kama kashindwa kudhibiti rushwa kwenye chama chake, rushwa ipi anapambana nayo?
 
CDM acheni utoto, yaani aliyetengeneza tatizo ndio mnataka huyo huyo alitatue?..

CDM hii tabia ya kulia lia bila kutatua tatizo nyie wenyewe kwa kupanga na kujipanga na watu wenu mtalia lia mpaka mwisho dunia...Haki haiji kifala fala hivi..
 
CCM wawania viti ikiwemo kata ya Mwakakati ya Tunduma mjini

 
CDM acheni utoto, yaani aliyetengeneza tatizo ndio mnataka huyo huyo alitatue?..

CDM hii tabia ya kulia lia bila kutatua tatizo nyie wenyewe kwa kupanga na kujipanga na watu wenu mtalia lia mpaka mwisho dunia...Haki haiji kifala fala hivi..
Vyombo vya dola vichague kutumikia ccm au nchi yetu basi, uhamiaji walikuwa wapi Siku zote? Huu sio uzalendo kwa taifa letu Bali ni usaliti kwa taifa letu
 
Uraia Ni suala mtambuka wewe
Anatory Amani wa ccm alishawahi kupokwa uraia wake katika mazingirq Kama haya ya uchaguzi,Kama uraia wako hauna utata ya nini kujipa presha?
Swala mtambuka linaanza Leo? Watu wamekuwa madiwani toka nyuma muwachunguze Leo? Kinachofanywa na uhamiaji ni kuchochea chuki kwa jamii, kwa maoni yangu ni usaliti kwa taifa
 
Vyombo vya dola vichague kutumikia ccm au nchi yetu basi, uhamiaji walikuwa wapi Siku zote? Huu sio uzalendo kwa taifa letu Bali ni usaliti kwa taifa letu

Aisee acheni kulia lia basi haitowasaidia..Chukueni hatua kama hamuwezi kaeni kimya maisha yaendelee...CDM miaka yote nyie mnalalamika tu mnaonewa kwenye hili lile kila siku, miaka yote..CHUKUENI HATUA KAMA MNA UHAKIKA MKO UPANDE WA HAKI...
 
Kiukweli hata kama kuna nia njema, uhamiaji wamekosea sana aproach yao. Tume ya taifa waongee na vyombo vya dola, tabia ya kutisha wagombea wa upinzani kuelekea uchaguzi mkuu inaondoa uchaguzi kuwa huru na haki.chadema makao makuu msikae kimya, nendeni uhamiaji makao makuu ya jeshi La polis waambieni.msikae kimya.
Kwan wanahojiwa upinzani tu?? Mbona mnapenda kulia kijinga nyie chadem

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Hivi kama wewe ni raia wa Tanzania kuna shida gani ya kutoa vitambulisho vyako halali au vidhibitisho vya uraia?

Kama kuwa kiongozi kwa miaka 5 iliyopita ni kidhibitisho cha uraia, basi waambie uhamiaji hivyo.

Hakuna nchi duniani inayoruhusu raia wa nchi nyingine awe kiongozi.
 
Back
Top Bottom