CHADEMA ina mtaji mkubwa kisiasa kuliko CCM na ACT wazalendo, ruzuku na madaraka visiwaondoe kwenye reli

CHADEMA ina mtaji mkubwa kisiasa kuliko CCM na ACT wazalendo, ruzuku na madaraka visiwaondoe kwenye reli

CDM kaza boti! mna mtaji mkubwa sana wa wanachama wenu!
Mkizidiwa wekeni bakuli mezani watu wanapiga donation maisha yanaendelea!
ILA mkataeni shetani na mambo yake yote na gilba zake zote ipo siku haki itatamalaki.
 
Chama cha maana kikichobakia Tanzania kinachotetea maslahi ya nchi ni CDM tu!!
 
Hii ndiyo gharama ya kuwa nyumbu, una mbunge mmoja tu lakini bado una ushawishi sana!!
Ndiyo shida ya kuwa nguruwe wa CCM
Screenshot_20200628-103658.jpg
 
Mimi pia najiuliza, hivi watanzania tungekua na tume huru ya uchaguzi na jeshi la polisi lisilopelekeshwa na akina pole pole, CCM ingekua madarakani kweli?

Sent from my TECNO W4 using JamiiForums mobile app
Hilo siwezi kujua kwa sababu pamoja na kwamba ccm inafanya figisufigisu kwenye chaguzi ila bado hadi leo ina wapiga kura wengi tu hasa akina mama na wazee,hivyo hata mimi natamani kuwe na uchaguzi uliyo huru kabisa halafu hali itakuwa vp maana sasa kumekuwa na imani ya kwamba kila chaguzi upinzani ndio unashinda ila ccm inatumia dola kujitangaza yeye kuwa ndio mshindi.
 
Siasa Ni mkakati, siasa ni kujua mapungufu ya mpinzani wako, siasa safi nikuweka wananchi mbele nakuzika matamanio binafsi kwa mgongo wa itikadi.

Tangu chadema watoe tamko lakuwafukuza viongozi na wanachama 19 mashambulizi toka ACT na CCM yamekuwa mengi sana.

Hakuna linalofanywa bila kuitaja chadema, adui wa ACT amekuwa ni Chadema na wananchi kwa ujumla na si CCM Tena.

Kauli mbiu iliyopo Sasa Ni umoja wa Taifa na Mambo ya Tanzania kujadiliwa Tanzania, ila hakuna anayesema wanajadili Kati ya Nani na Nani na hayo majadiliano yanafanywa wapi na wahusika ni wakina nani.

Ifike mahali tutambue wananchi Wana nguvu kuliko viongozi isipokuwa tu viongozi Wana nguvu ya dola. Chadema ina Mbunge mmoja tu bungeni lakini ina wabunge zaidi ya milioni 30 uraiani. Tunapokosa uhalali wakuongoza haimaanishi lazima tusiwe na wakuwaongoza ila lazima tusijiamini na wale tunaowaongoza.

Naamini msimamo wa chadema unafaida kubwa kisiasa kuliko msimamo wa ACT na CCM.....Wana watu nyuma yao wengine wana familia zao nyuma yao.
Acc ya chama imesoma ruzuku ya mwezi nov halafu kimya,ndio mkakati gani huo 🤣
 
Siasa ni mwanaharamu sana,yani juzi tu hapa A.C.T ilikuwa ndo kipenzi cha Chadema leo wamekuwa chui na paka!!
haya ngoja tuone nini kitafata.
 
Huwa najiuliza hivi Tanzania tungekuwa hatutumia Facebook na JF hivi hii chadema tungekuwa tunaiona kama tunavyoichukulia humu mitandaoni? Kwa maana huko mitaani chadema ingekuwa inazungumzwa kama ilivyo huku mitandaoni?
Kwani waliopo mtaani hawapo JF na Facebook ama mtaani wanaishi watu wasio ma smartphone!!

Hvi Lissu alipoenda porini Itilima huko na kukuta maelfu ya watu je huko nako walikuwa FB?

Kipindi cha Dr Slaa na Zitto bungeni kulikuwa na mitandao ya jamii? Je ilikuwaje CHADEMA ikapaa kiushawishi nchi nzima hadi kuwa chama kikuu.

Nasubiri majibu
 
Pole sana. Asiyekubali kushindwa sio mshindani. Sisi sio CCM Lakini nakwambia JPM ameshinda na angeshinda. Nyie kazi mnazozijua Ni kubisha mpaka humu akisema mtu hoja tofauti Nanyi , hata kama kasema we Dume mtapinga jinsia zenu na kumsingizi JPM kazibadili
Hata mimi nakubali JPM angeshinda of course sababu ya wajinga bado wapo wengi Tz hasa huko maporini. Ila kinachopingwa ni 80%+ haiingii akilini kabisa. Yaani majimbo na kata zote nchini zinaipenda CCM!!

JPM kma angeshinda basi ni 50-60% basi.... Kma tu US licha ya kelele kwa trump lakini Biden hajashinda kwa kishindo. So hiko ndio tume huru ingesaidia.... Hopefully na wabunge ingekua hivyo hivyo gap ya 60-40 ila sio majimbo yote.

Tuwe serious kidogo
 
Pole sana. Asiyekubali kushindwa sio mshindani. Sisi sio CCM Lakini nakwambia JPM ameshinda na angeshinda. Nyie kazi mnazozijua Ni kubisha mpaka humu akisema mtu hoja tofauti Nanyi , hata kama kasema we Dume mtapinga jinsia zenu na kumsingizi JPM kazibadili
Mimi ni mtu mmoja, sio taasisi. Usitumie neno "nyie" kuniongelea mimi mtu mmoja!
 
Ilitakiwa ukimaliza kuandika hapo useme umeingiza sh ngapi kwenye account ya chadema kwa ajili ya mafuta ya magari na kulipa watumishi
Ahahahahahahahajahah! Eti Chadema ina wabunge milioni 30 mtaani. Ahahahahahah! Wabunge walioshindwa kupiga kura, wakashindwa kulinda kura zao na wakashindwa kuingia mtaani kudai "ushindi" wao hadi Mgombea Lissu Ubelgiji akahama nchi kwa aibu! Ahahahahahah! Hongera sana kwenu WABUNGE MILIONI 30!!!!!
 
Kwani waliopo mtaani hawapo JF na Facebook ama mtaani wanaishi watu wasio ma smartphone!!

Hvi Lissu alipoenda porini Itilima huko na kukuta maelfu ya watu je huko nako walikuwa FB?

Kipindi cha Dr Slaa na Zitto bungeni kulikuwa na mitandao ya jamii? Je ilikuwaje CHADEMA ikapaa kiushawishi nchi nzima hadi kuwa chama kikuu.

Nasubiri majibu
Mie nimeuliza tu swali mkuu,maana kilichopo mitandaoni si sawa na huko mitaani ndio maana hata yale maandamano ya Lissu kwa kuangalia hali ilivyokuwa mitandaoni ilishangaza kuona siku ya tukio watu mitaani wanaendelea na shughuli zao kama kawaida kama hakuna kilichotokea wakati mitandaoni hali ilikuwa tofauti.

Kwahiyo naona chadema ina nguvu kubwa sana mitandaoni kuliko huku mitaani,sisemi kuwa haina watu huku mitaani ila haipo kama ambavyo ilivyo mitandaoni.
 
Mie nimeuliza tu swali mkuu,maana kilichopo mitandaoni si sawa na huko mitaani ndio maana hata yale maandamano ya Lissu kwa kuangalia hali ilivyokuwa mitandaoni ilishangaza kuona siku ya tukio watu mitaani wanaendelea na shughuli zao kama kawaida kama hakuna kilichotokea wakati mitandaoni hali ilikuwa tofauti.

Kwahiyo naona chadema ina nguvu kubwa sana mitandaoni kuliko huku mitaani,sisemi kuwa haina watu huku mitaani ila haipo kama ambavyo ilivyo mitandaoni.
Mkuu hta Mobutu DRC alikataliwa ila mbona wapinzani walipoitisha maandamano yalifeli? Vp Museveni 2016 Besigye alipoitisha maandamano?

Mbona Lissu alipotua kutoka ubelgiji watu waliandamana bila polisi kuingilia? Kma wangeruhusu alafu watu wasijitokeze hapo ungekuwa na hoja.

But baada ya vitisho then mnakuja kujisifia kuwa tupo mitandaoni sidhani kma ni sahihi.

Kenyatta hakuzuia maandamano ya Odinga na wote tuliona nguvu yake mpka akajiapisha Urais. Nyie mngeachia tu then tungeona kma yangefeli ili ssa tufanye analysis fair.
 
Mkuu hta Mobutu DRC alikataliwa ila mbona wapinzani walipoitisha maandamano yalifeli? Vp Museveni 2016 Besigye alipoitisha maandamano?

Mbona Lissu alipotua kutoka ubelgiji watu waliandamana bila polisi kuingilia? Kma wangeruhusu alafu watu wasijitokeze hapo ungekuwa na hoja.

But baada ya vitisho then mnakuja kujisifia kuwa tupo mitandaoni sidhani kma ni sahihi.

Kenyatta hakuzuia maandamano ya Odinga na wote tuliona nguvu yake mpka akajiapisha Urais. Nyie mngeachia tu then tungeona kma yangefeli ili ssa tufanye analysis fair.
Tatizo mkuu sio tu watu hawajafanya hayo maandamano bali watu walikuwa bize na shughuli zao wala hakukuwa na dalili zozote kuonesha kuwa watu walikuwa teyari kwa maandamano ila polisi ndio kikwazo,na ukiangalia mitandaoni watu walikuwa wanaonesha kuwa wameshachoka hakuna tena wanalohofia liwalo na liwe. Hiyo ndio ilikuwa hali ya mitandaoni,sasa ajabu tena watu hao kuogopa mkwara wa polisi.

Huo ni mfano mmoja tu lakini kiujumla chadema ya mitandaoni ni tofauti na huku mtaani.
 
Back
Top Bottom