Uchaguzi 2020 CHADEMA inahitaji political strategists kuishinda CCM

Uchaguzi 2020 CHADEMA inahitaji political strategists kuishinda CCM

Yaani hizi hoja zako zimenifanya nicheke ile mbaya, eti upinzani ukitaka kuitoa ccm imuunge mkono Magufuli, halafu 2025 ndio ichukue nchi. Umesema upinzani lakini umeitaja cdm tu. Sasa ngoja tuone kwenye uhalisia wa hizi hoja zako.

  1. UDP na TLP wamemuunga mkono Magufuli, hivyo tutarajie kuwa 2025 watachukua nchi kwa hii nadharia yako? Kwa taarifa yako Magufuli angeachiwa safari hii apite bila kupingwa angejiongezea muda wa kukaa madarakani. Wapinzani kushiriki uchaguzi huu, tena wakiwa wamefanyiwa kila aina ya ukatili, na kuendelea kupata watu wengi kwenye mikutano yao, ni wazi kuwa hakuna uwezekano tena wa nchi hii kuendelea kuongozwa tu na ccm kwa kura halali.
  2. Kwa taarifa yako ujenzi wa miundombinu ni tabia binafsi ya Magufuli na sio ccm. Hivyo hata akitangazwa mshindi sio akishinda bado ataendelea na hiyo miundombinu. Mpaka sasa tayari Magufuli ana miradi miwili mikubwa ya 15t+, na yote analazimisha amalize ndani ya muda wake halali wa kisheria, iwapo hatachezea katiba. Mpaka sasa hakuna mradi hata mmoja uliofikia robo ya kukamilika na tayari wananchi wameshaumia sana. Hivyo kama ni kutua hela hajatoa hata nusu ya pesa yaani 7t. Hivyo anatakiwa ndani ya hii miaka mitano lazima apate 8-10t, ni wapi atapata hizo hela, achia mbali mahitaji mengine? Kwa vyovyote kufika hiyo 2025 bado ccm itazidi kuwa kwenye wakati mgumu maana kupata hizi hela za kumalizia hiyo miradi ni kiama.
  3. Hoja ya cdm kuchukua nchi ikiwa imejaa miundombinu ya kila namna, na kuwa rahisi kuendesha nchi kwa kujali maslahi ya mtu mmoja mmoja. Hoja hii ni kiini macho, tazama deni la taifa mpaka sasa ni kiasi gani toka awamu hii iingie madarakani. Ni wazi serikali sasa inakopa sana, huku terms za mikopo ikiwa inafahamika na mtu mmoja na genge lake. Katika mazingira hayo, una uhakika gani wa kuendesha nchi kirahisi ukiwa na madeni mazito hivyo? Kuhusu hoja ya Corona hapa ndio nimeona hujui unaoongea nini, kwani Corona Ni ugonjwa wa kudumu mpaka useme wazungu watalazimisha nchi iwekwe lockdown? Halafu acha upotoshaji wa kijinga, ni nani anataka kuchukua nchi ili apewe maelekezo na wazungu? Hii ni dhahiri uko na hoja za kuokoteza.
  4. Kwamba sasa hivi cdm imeshiriki uchaguzi huu na haitashinda hata kidogo. Kwani kushiriki ni lazima ushinde? Ingekuwa kushiriki kwenye ushindani wowote lazima ushinde, basi ligi kuu ya nchi yetu ingekuwa na simba na yanga tu maana ndio wenye uwezo wa dhahiri kushinda ligi. Halafu uchaguzi mkuu sio urais tu, bali kuna wabunge na madiwani, na kura za urais hutoa wabunge wa viti maalum. Kama miaka hii mitano tuliaminishwa kuwa ccm imeua upinzani, na kinachoonekana ni tofauti, ni kipi kitafanya sasa na hiyo 2025 isiwe rahisi kuitoa ccm? Kwa taarifa yako cdm ingeingia mkenge wa huu ushauri wako fake, kufika 2025 katiba ingekuwa imeshabadilishwa na ingehalalishwa kuwa upinzani umekufa.
 
CHADEMA ni watu wa matukio, kesho wakiona Lissu amejaza stendi thread zitajaa humu za kudai Lissu aapishwe, ooh watu wameichoka CCM na bla bla kibao, kivumbi cha Kigoma Leo kimewanock out kidogo. Kuna vitu tu wananchi wanatamani Rais avisikie na wanamtumia Lissu kufikisha huo ujumbe, ila inshort wanazengo hawamwamini na sad enough wengi wao sio wapiga kura.

CHADEMA ipo poor organized, viongozi wapo scattered, sio Mbowe, sio Nyalandu wote wanafight for survival, Lissu anajaribu kupambana na somehow amerestore some spirit, but alone without strategic, it is impossible to outshine full organized CCM. Ni kichekesho kuona CCM inakabidhi nchi Kwa genge ambalo halieleweki kama CHADEMA, Broadcast zote, jaji mkuu, NEC, wanatangaza CHADEMA imeshinda, what a fu-ck ....

Kwa Safari hii CCM haihitajiki hata kutumia another alternative japo wamejipanga, kura tu zinatosha, wasiyumbishwe na makelele ya chura wao kama tembo waendelee Tu kuyanywa maji.

Membe alinena Jambo la msingi sana japo walimbeza, kuitoa CCM ni zaidi ya ushabiki wa kwenye majukwaa ambalo hawalijui hata hao mabeberu wapo upande wa CCM.

Ahaaaa ahaaaa huwa nacheka sana nikisikia ccm wanasema cdm ni watu wa matukio. Niliwahi kuwauliza viazi wenzako wa ccm, mbona hoja zinazochangiwa sana ni hizi wanazoita za matukio. Unakuta hoja inayoitwa ni ya matukio ina page zaidi ya 50, na kwenye social media nyingine ni hivyo hivyo. Kisha wanaoponda wameganda kwenye hoja hizo hizo kuzuia mashambulizi, halafu ikija hoja ya msingi haina wachangiaji hata ccm wanaojifanya sio watu wa matukio!

Nikataka wanaccm wenzako wanionyeshe ni jukwaa au mtandao upi wasipojadili matukio niwaone, hawana jipya. Kabla ya awamu hii kuingia madarakani tulizoea kuona midahalo, na mijadala huru kwenye vyombo vya habari. Kwa sasa vitu hivyo havipo, ila kuna mijadala ya kimsujudia Magufuli kuwa kafanya maajabu, na kuua upinzani. Saa hii ndio hiyo ili kupata watu amegeuza mikutano yake fiesta, kuongea kisukuma na kutishia wapiga kura eti hataleta maendeleo. Ni maendeleo gani kaleta ambayo atayaleta kwa hao watu miaka hii mitano? Ccm imejipanga, lakini mbeleko ya dola na tume ya uchaguzi bado ndio ngao yao kuu! Vichekesho hivi viko Tanzania tu.
 
Kila ikifika jioni, huwa nasikiliza kampeni za vyama kikiwemo CHADEMA nikitegemea kwamba labda watakuwa na sera mpya za kistaarabu, kwa bahati mbaya sijaona kitu cha namna hiyo.

Kwanza kabisa, sijasikia sera mahsusi za kuweza kuwashawishi Watanzania hasa wenye akili timamu. Zaidi sana nasikia tu sera za kuwavutia vijana wa rika fulani ambao kwa kweli hawajakomaa kiakili, wapo kwenye kipindi cha Bendera fuata upepo na waliojaa mihemko tu.

Kwa hiyo, mpaka leo hii Magufuli amemwacha Lissu mbali saaaaaana. Mimi huwa napita pita mitaani na vijiweni kufanya utafiti kidogo. Asilimia kubwa ya watu hata wa CHADEMA wanamkubali sana Magufuli, na wengi wanasema kwa upande wa Rais watampa kura Magufuli.

Kwa nini Magufuli? Pamoja na sababu zingine, lakini jinsi alivyoshughulikia Issue Corona, watu wanamkubali sana Magufuli. Huyu mwingine shida inayompunguzia sifa ni kukosa staha, adabu, ustahimilivu nk. katika kuongea. Ikumbukwe kuwa, Watanzania hawajazoea na hawapendi shari.

Nakupa big up mkuu. CHADEMA hili hawalielewi, wanadhani kura zipo kwa mabodaboda. Watu wenye akili timaru hawawezi kuchagua Lissu. Mbowe mwenyewe kiukweli hataki Lissu apite. Maana uenyekiti wake utakuwa mashakani. Lissu amepewa fursa ya kugombea kwa sababu zifuatazo:-

1. Kumpoza maumivu ya risasi, kuondoa lawama kwa Lissu na kuonesha kuwa Mbowe hakuhusika kwenye mpango wa kumpiga risasi.

2. Wamempa mtego. Akishinda watamchekea kiunafiki huku wakiumia. Sababu hawaamini akili za Lissu, hawajui kesho ataamka na lipi. Lissu akishinda atashinda kwa nguvu zake sio nguvu za Chama chake. Lakini baada ya kushinda watamtumia ipasavyo kufanikisha malengo yao ya kujitajirisha wakijifanya walimpa support kwenye ushindi wake.

3. Wamempa fursa ili ashindwe na uwe ndo mwisho wake kwa CHADEMA. Watasema wamempa nafasi ameshindwa. Aache na wengine wajaribu kete zao.

Baada ya Lissu kushindwa uchaguzi CHADEMA watamlaumu sana na kuona ameharibu Chama. Maana baada ya uchaguzi Chama kitapoteza credibility kabisa na kitakuwa kwenye misuguano mikali na serikali na kupigwa pini kila mahali. Lissu asishangae kufukuzwa uanachama.
 
Kitu pekee Chadema wanahitaji kwa sasa ni namna salama ya kulinda kura baada ya kutumbukizwa kwenye sanduku.Otherwise ushindi ni wàzi wazi
 
Umenena, watanzania wengi bado ni wakarimu na wanapenda watu wanyeyekevu. Lissu anasema sana kama mtu mwenye dharau na kuonyesha anajua kila kitu (muck know) na watanzania hawapendezwi na hilo.

Umesema ukweli usiopingika.
 
Kwa mtazamo wako uko sahihi. Kitendo cha kuichokonoa ccm wakati huu ni muhimu sana. Wajue tu kwamba kumbe miaka mitano waliyojitutumua is nothing. Kwamba watu wanataka mabadiliko bila kujali Magufuli kafanya nini.

Sasa cdm ikianza tena kuunga mkono juhudi sio mkakati bali kujimaliza. Ujue wazi na ccm wanao watu wa mikakati, tena wabobezi. Wananchi hawawezi elewa pale wakisikia cdm inaunga mkono mambo fulani.

Suala hapa ni kutikisana hadi huko walikoshikilia washindwe na wadondoke
 
Yaani hizi hoja zako zimenifanya nicheke ile mbaya, eti upinzani ukitaka kuitoa ccm imuunge mkono Magufuli, halafu 2025 ndio ichukue nchi. Umesema upinzani lakini umeitaja cdm tu. Sasa ngoja tuone kwenye uhalisia wa hizi hoja zako.

  1. UDP na TLP wamemuunga mkono Magufuli, hivyo tutarajie kuwa 2025 watachukua nchi kwa hii nadharia yako? Kwa taarifa yako Magufuli angeachiwa safari hii apite bila kupingwa angejiongezea muda wa kukaa madarakani. Wapinzani kushiriki uchaguzi huu, tena wakiwa wamefanyiwa kila aina ya ukatili, na kuendelea kupata watu wengi kwenye mikutano yao, ni wazi kuwa hakuna uwezekano tena wa nchi hii kuendelea kuongozwa tu na ccm kwa kura halali.
  2. Kwa taarifa yako ujenzi wa miundombinu ni tabia binafsi ya Magufuli na sio ccm. Hivyo hata akitangazwa mshindi sio akishinda bado ataendelea na hiyo miundombinu. Mpaka sasa tayari Magufuli ana miradi miwili mikubwa ya 15t+, na yote analazimisha amalize ndani ya muda wake halali wa kisheria, iwapo hatachezea katiba. Mpaka sasa hakuna mradi hata mmoja uliofikia robo ya kukamilika na tayari wananchi wameshaumia sana. Hivyo kama ni kutua hela hajatoa hata nusu ya pesa yaani 7t. Hivyo anatakiwa ndani ya hii miaka mitano lazima apate 8-10t, ni wapi atapata hizo hela, achia mbali mahitaji mengine? Kwa vyovyote kufika hiyo 2025 bado ccm itazidi kuwa kwenye wakati mgumu maana kupata hizi hela za kumalizia hiyo miradi ni kiama.
  3. Hoja ya cdm kuchukua nchi ikiwa imejaa miundombinu ya kila namna, na kuwa rahisi kuendesha nchi kwa kujali maslahi ya mtu mmoja mmoja. Hoja hii ni kiini macho, tazama deni la taifa mpaka sasa ni kiasi gani toka awamu hii iingie madarakani. Ni wazi serikali sasa inakopa sana, huku terms za mikopo ikiwa inafahamika na mtu mmoja na genge lake. Katika mazingira hayo, una uhakika gani wa kuendesha nchi kirahisi ukiwa na madeni mazito hivyo? Kuhusu hoja ya Corona hapa ndio nimeona hujui unaoongea nini, kwani Corona Ni ugonjwa wa kudumu mpaka useme wazungu watalazimisha nchi iwekwe lockdown? Halafu acha upotoshaji wa kijinga, ni nani anataka kuchukua nchi ili apewe maelekezo na wazungu? Hii ni dhahiri uko na hoja za kuokoteza.
  4. Kwamba sasa hivi cdm imeshiriki uchaguzi huu na haitashinda hata kidogo. Kwani kushiriki ni lazima ushinde? Ingekuwa kushiriki kwenye ushindani wowote lazima ushinde, basi ligi kuu ya nchi yetu ingekuwa na simba na yanga tu maana ndio wenye uwezo wa dhahiri kushinda ligi. Halafu uchaguzi mkuu sio urais tu, bali kuna wabunge na madiwani, na kura za urais hutoa wabunge wa viti maalum. Kama miaka hii mitano tuliaminishwa kuwa ccm imeua upinzani, na kinachoonekana ni tofauti, ni kipi kitafanya sasa na hiyo 2025 isiwe rahisi kuitoa ccm? Kwa taarifa yako cdm ingeingia mkenge wa huu ushauri wako fake, kufika 2025 katiba ingekuwa imeshabadilishwa na ingehalalishwa kuwa upinzani umekufa.

Watu wenye shari utawaona tu. Matusi, kejeli, nk. Mungu akusaidie.
 
Watu wenye shari utawaona tu. Matusi, kejeli, nk. Mungu akusaidie.

Nimekupa ukweli wako kwenye huu uhuni ulioandika hapa, hivyo unatafuta maneno ya utetezi dhaifu. Kaa kimya, au huu ushauri wako anzisha chama utumie mbinu hizo za kichovu kuchukua nchi.
 
5. Pia CCM 2025 mgombea anabadirika, hivyo atakuja na sera zake including hizo za upinzani. Kama utakumbuka sera ya ufisadi Magufuli ameitekeleza ambapo wapinzani hawana huo wimbo tena.
 
Nimekupa ukweli wako kwenye huu uhuni ulioandika hapa, hivyo unatafuta maneno ya utetezi dhaifu. Kaa kimya, au huu ushauri wako anzisha chama utumie mbinu hizo za kichovu kuchukua nchi.

Ukweli unauma ndo maana unatoka povu. Ukweli utabaki kuwa ukweli. Kama umechukia meza wembe. CDM mwaka huu sahau ushindi na mwaka 2025 sahau ushindi. Kwa sababu ya udhaifu wenu katika kupanga mikakati, itawagharimu kweli. Mtabaki kutukana tu. Hiyo ndo itabaki kuwa sera yenu kuu. Wenzenu wataendelea kujijenga kwa kurekebisha makosa. Nyie mtaendelea kusindikiza na jeuri ya matusi. Acha uje uone kivumbi tarehe 28 Oct. Hata mkinyang'anywa ushindi, hakuna mtu atakayeandamana kutetea wahuni. Watanzania sio wajinga.
 
Ukweli unauma ndo maana unatoka povu. Ukweli utabaki kuwa ukweli. Kama umechukia meza wembe. CDM mwaka huu sahau ushindi na mwaka 2025 sahau ushindi. Kwa sababu ya udhaifu wenu katika kupanga mikakati, itawagharimu kweli. Mtabaki kutukana tu. Hiyo ndo itabaki kuwa sera yenu kuu. Wenzenu wataendelea kujijenga kwa kurekebisha makosa. Nyie mtaendelea kusindikiza na jeuri ya matusi. Acha uje uone kivumbi tarehe 28 Oct. Hata mkinyang'anywa ushindi, hakuna mtu atakayeandamana kutetea wahuni. Watanzania sio wajinga.

Nichukie nini, mimi nimekupa kitu na box. Hiyo tarehe 28 unayotambia hakuna uchaguzi, bali ni kilele cha maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura. Sio hata tukinyang' anywa ushindi, maana ni lazima ushindi uporwe, kwani ccm imekata moto kwenye ushindani. Hilo suala la kuandamana kaa ukiomba ukondoo uendelee, kinyume na hapo jiandae kutapika hirizi. Muhuni mkubwa ww.
 
Mkuu hoja yako ni ya hovyo Sana, mkakati wowote lazima uweze kuchukua nafasi ya Sasa na sio kusubiri five years.

Pili mkakati wowote mzuri unaangalia mapungufu ya Sasa na kucease opportunity ili kuharibu Sana na kuweka mikakati ya wakati ujao na sio kuacha vacuum.

Sasa jiukize CCM kukiwa na tume huru itatoboa? Hata polepole alishakiri.

Pili angalia nguvu ya Dola iliyopo nyuma ya CCM, Kama upinzani usianza counter attack Sasa hiyo 2025 itakuaje?

Upinzani umenyimwa media, umebanwa kulipia mabango kabla kuyabandika, umenyimwa pesa, je unafikiri 2025 watafanya nini Kama Mwaka huu wasipopambana?

Angalia uchaguzi wa serikali za mitaa walivyofanya, hiyo Hali ukitaka kukomaa kwenye uchaguzi huu.
 
Yaani nzi wa kijani ndo uwashauri Chadema????😂😂😂

Kweli Ccm mna hali mbaya mwaka huu!! Watanzania tunaenda kuandika historia kuu mwaka huu. Subirini, Tundu Lissu ndo Raisi wa Tanzania 2020 - 2025
 
Nichukie nini, mimi nimekupa kitu na box. Hiyo tarehe 28 unayotambia hakuna uchaguzi, bali ni kilele cha maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura. Sio hata tukinyang' anywa ushindi, maana ni lazima ushindi uporwe, kwani ccm imekata moto kwenye ushindani. Hilo suala la kuandamana kaa ukiomba ukondoo uendelee, kinyume na hapo jiandae kutapika hirizi. Muhuni mkubwa ww.
Macho ya wenye dunia yote yako Tanzania hiyo October 28 ndugu. Subiri uone CCM anavyoshikishwa adabu
 
Strategic ya chadema iko strong sana ikisaidiana na vipenyo walioko ndani ya NEC
 
Back
Top Bottom