Uchaguzi 2020 CHADEMA inahitaji political strategists kuishinda CCM

Uchaguzi 2020 CHADEMA inahitaji political strategists kuishinda CCM

Yaani hizi hoja zako zimenifanya nicheke ile mbaya, eti upinzani ukitaka kuitoa ccm imuunge mkono Magufuli, halafu 2025 ndio ichukue nchi. Umesema upinzani lakini umeitaja cdm tu. Sasa ngoja tuone kwenye uhalisia wa hizi hoja zako.

  1. UDP na TLP wamemuunga mkono Magufuli, hivyo tutarajie kuwa 2025 watachukua nchi kwa hii nadharia yako? Kwa taarifa yako Magufuli angeachiwa safari hii apite bila kupingwa angejiongezea muda wa kukaa madarakani. Wapinzani kushiriki uchaguzi huu, tena wakiwa wamefanyiwa kila aina ya ukatili, na kuendelea kupata watu wengi kwenye mikutano yao, ni wazi kuwa hakuna uwezekano tena wa nchi hii kuendelea kuongozwa tu na ccm kwa kura halali.
  2. Kwa taarifa yako ujenzi wa miundombinu ni tabia binafsi ya Magufuli na sio ccm. Hivyo hata akitangazwa mshindi sio akishinda bado ataendelea na hiyo miundombinu. Mpaka sasa tayari Magufuli ana miradi miwili mikubwa ya 15t+, na yote analazimisha amalize ndani ya muda wake halali wa kisheria, iwapo hatachezea katiba. Mpaka sasa hakuna mradi hata mmoja uliofikia robo ya kukamilika na tayari wananchi wameshaumia sana. Hivyo kama ni kutua hela hajatoa hata nusu ya pesa yaani 7t. Hivyo anatakiwa ndani ya hii miaka mitano lazima apate 8-10t, ni wapi atapata hizo hela, achia mbali mahitaji mengine? Kwa vyovyote kufika hiyo 2025 bado ccm itazidi kuwa kwenye wakati mgumu maana kupata hizi hela za kumalizia hiyo miradi ni kiama.
  3. Hoja ya cdm kuchukua nchi ikiwa imejaa miundombinu ya kila namna, na kuwa rahisi kuendesha nchi kwa kujali maslahi ya mtu mmoja mmoja. Hoja hii ni kiini macho, tazama deni la taifa mpaka sasa ni kiasi gani toka awamu hii iingie madarakani. Ni wazi serikali sasa inakopa sana, huku terms za mikopo ikiwa inafahamika na mtu mmoja na genge lake. Katika mazingira hayo, una uhakika gani wa kuendesha nchi kirahisi ukiwa na madeni mazito hivyo? Kuhusu hoja ya Corona hapa ndio nimeona hujui unaoongea nini, kwani Corona Ni ugonjwa wa kudumu mpaka useme wazungu watalazimisha nchi iwekwe lockdown? Halafu acha upotoshaji wa kijinga, ni nani anataka kuchukua nchi ili apewe maelekezo na wazungu? Hii ni dhahiri uko na hoja za kuokoteza.
  4. Kwamba sasa hivi cdm imeshiriki uchaguzi huu na haitashinda hata kidogo. Kwani kushiriki ni lazima ushinde? Ingekuwa kushiriki kwenye ushindani wowote lazima ushinde, basi ligi kuu ya nchi yetu ingekuwa na simba na yanga tu maana ndio wenye uwezo wa dhahiri kushinda ligi. Halafu uchaguzi mkuu sio urais tu, bali kuna wabunge na madiwani, na kura za urais hutoa wabunge wa viti maalum. Kama miaka hii mitano tuliaminishwa kuwa ccm imeua upinzani, na kinachoonekana ni tofauti, ni kipi kitafanya sasa na hiyo 2025 isiwe rahisi kuitoa ccm? Kwa taarifa yako cdm ingeingia mkenge wa huu ushauri wako fake, kufika 2025 katiba ingekuwa imeshabadilishwa na ingehalalishwa kuwa upinzani umekufa.

Ndg yangu nataka nichangie kwenye pointing ya 4 tu. Mtoa mada hakusema vyama vya upinzani visishiriki uchaguzi huu. Alisema wasingeweka mgombea kwenye nafasi ya rais tu. Maanake nafasi nyingine za ubunge na udiwani waweke. Kuhusu kuangalia kura za rais kutoa wabunge wa viti maalum, huku ndo kuangalia maslahi ya muda mfupi na kuacha kupanga mipango ya muda mrefu. Katika siasa wakati mwingine lazima kukubali kupoteza maslahi fulani ya muda mfupi kwa ajili ya vitu vikubwa zaidi. Mtoa mada nimemkubali pointi zake. Na wewe hongera kwa kuchangia lakini kwenye ukweli ni muhimu tukubali. Mimi sijawahi kupigia kura ccm lkn safari hii namchagua magufuli tu kwenye Urais. Kwa wabunge na madiwani bado napima.
 
Ndg yangu nataka nichangie kwenye pointing ya 4 tu. Mtoa mada hakusema vyama vya upinzani visishiriki uchaguzi huu. Alisema wasingeweka mgombea kwenye nafasi ya rais tu. Maanake nafasi nyingine za ubunge na udiwani waweke. Kuhusu kuangalia kura za rais kutoa wabunge wa viti maalum, huku ndo kuangalia maslahi ya muda mfupi na kuacha kupanga mipango ya muda mrefu. Katika siasa wakati mwingine lazima kukubali kupoteza maslahi fulani ya muda mfupi kwa ajili ya vitu vikubwa zaidi. Mtoa mada nimemkubali pointi zake. Na wewe hongera kwa kuchangia lakini kwenye ukweli ni muhimu tukubali. Mimi sijawahi kupigia kura ccm lkn safari hii namchagua magufuli tu kwenye Urais. Kwa wabunge na madiwani bado napima.

Niambie kutokuweka mgombea wa urais kuna athiri vipi malengo ya muda mrefu.
 
CHADEMA inahitaji wataalamu wa stratejia ya siasa (Political Strategists) kuweza kuitoa CCM madarakani kwa urahisi. Vyama vikongwe na vyenye dola kama CCM vinahitaji kufanyiwa mkakati maalumu ambao hauhitaji nguvu. Kama ningepewa fursa ya kutoa ushauri wa kimkakati wa kuitoa CCM ningeshauri ifutavyo:-

1. Kwa wakati huu 2020 - 2025 Chama kijikite katika kuunga mkono mikakati muhimu ya kitaifa inayofanywa kuinua uchumi wa Taifa inayofanywa na CCM. Hii ingefanya CHADEMA kuonekana ni Chama kinachojali maslahi mapana na maendeleo ya Taifa. Masuala ya kupinga kila kitu hata ambayo yalikuwa sera zake toka mwanzo yanakiondolea Chama taswira ya dhamira ya kweli ya kuleta maendeleo kwa Taifa. Wasingeweka hata mgombea kwa nafasi ya Rais kwa kipindi hiki ili waonekane na kuaminiwa na wananchi kwamba hawana uroho wa madaraka, wanathamini maendeleo ya taifa, kwani maendeleo hayana vyama. Hii ingewafanya wananchi wakiamini chama zaidi. Misuguano na serikali kwa mambo ya msingi ya kitaifa ambayo kila mtu mwenye akili ya kawaida tu anaona, haina tija kwao. Mwenyekiti Mbowe aliwahi kumpongeza hadharani Rais Magufuli akiwa Hai kwa kazi ya maendeleo anayoifanya, na akasema, "MNYONGE MNYONGENI LAKINI HAKI YAKE MPENI". Kama Mwenyekiti alipongeza, ina maana Chama kinatambua na kuthamini kazi nzuri inayofanywa. Haiwezekani kugeuka tena na kuanza kuona kilichofanyika ni upuuzi. Ukigeugeu huo unafanya wananchi waone CHADEMA haina dhamira ya maendeleo ya kweli. Wanachokisema leo, kesho watakipinga.

2. Kutosimamisha mgombea kwenye uchaguzi wa mwaka huu, kungefanya CCM watambe sana na kuendelea na makosa wanayoyafanya wakidhani wananchi wanafurahia. CCM wangeendelea kujitegea mabomu wao wenyewe hadi 2025. Wangeendelea na mambo ya miundombinu bila kushughulikia uchumi wa mwananchi mmoja mmoja. Kufika 2025 kila mwananchi angekuwa ameichoka CCM. CHADEMA wangeendelea kukusanya takwimu za makosa ya CCM hadi 2025. Ingekuwa rahisi sana kwa CHADEMA kuitoa madarakani CCM sababu wananchi wote wangekuwa tayari wamejaa chuki kwa CCM. Kwa hulka ya Magufuli angeendelea kushughulika miradi mikubwa ya kimkakati bila kuangalia maslahi ya watu wa kawaida. Sasa hivi CHADEMA imefanya CCM iwe makini zaidi na wakishinda uchaguzi watarekebisha mambo mengi aliyoyapigia kelele Lissu. Ni wazi kwamba Magufuli atashinda tena.

3. Kumwacha Magufuli kuendelea hadi 2025, kungewasaidia CHADEMA kuchukua nchi ikiwa imejaa miundo mbinu ya kila namna, na hivyo kuongoza nchi kwa urahisi. Wangekuwa na kazi moja tu ya kushughulikia maslahi ya mtu mmoja mmoja. Sasa hivi hata Lissu akishinda (kitu ambacho hakiwezekani) atapata shida sana katika kuweka mambo sawa. Wananchi wanatarajia akishinda matatizo yao yataisha ndani ya mwaka mmoja. Ukweli ni kwamba matatizo ya wananchi hayawezi kuisha ndani ya mwaka mmoja. Mwaka ukipita bila kumaliza kero zao, malalamiko yataanza, na yataigharimu sana CHADEMA katika uchaguzi wa 2025. Kitu cha kwanza kitakachogharimu CHADEMA ikishinda ni corona. Washirika wao wa nje watawataka waiweke nchi kwenye Lockdown. Hilo ni lazima. Ni Magufuli tu mwenye jeuri ya kuendelea kuwakatalia wazungu. Lissu hawezi kuwakatalia. Na akikubaliana nao ajue atakosana na kila mwananchi. Kusubiri hadi 2025, kungesaidia CHADEMA kuingia madarakani kukiwa hakuna mambo ya Corona duniani. Hivyo, mashinikizo ya kimataifa juu ya corona hayatakuwepo tena.

4. Sasa hivi CHADEMA imeshiriki uchaguzi huu, lakini kushinda sio rahisi hata kidogo. Na wakishindwa hawatarudi tena 2025. CCM itatumia sera zake na zao pia kuondoa kero kwa wananchi. CHADEMA haitakuwa na hoja tena 2025. Kwa hiyo kutovumilia miaka 5 ijayo kutawakosesha ndoto ya kushika dola hivi karibuni. Miaka 5 haikuwa mingi kuvumilia ikiwa ni mkakati wa kuitoa CCM madarakani kwa urahisi.

Kwa mawazo yako CDM haina strategists? Kama hiyo ndiyo update mpya ya kina katawi - ujue makopo na kuyarokota tayari kuna wahusu.

Kumwachia jiwe hadi 2025 siyo option. Huyu kama CCM ina strategist yeyote wa maana alipashwa kushauri hilo. Jiwe kwa kushindwa kutenda na hata kushindwa kusimama na haki anachukiwa kuliko maelezo.

Jiwe hafai. Hana unyonge wowote ati kuna haki yoyote apewe Kwa lipi la maana alilofanya?
 
Mtoa mada ameeleza vizuri athari za kuweka mgombea kwenye uchaguzi huu. Labda urudie kuisoma uielewe.

Mamba anashauri watu kuvuka mto salama. Hayo kama siyo maajabu ya Firauni basi hakuna mengine.
 
Tatizo ni Vyombo vya kutoa Haki kama Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Vyombo vya ulinzi na Usalama ambavyo kwa kila mbinu vinaisaidia CCM kubaki madarakani.HAPA NDIPO PENYE TATIZO!
Kwa hiyo hata kama ingekuwa mwaka 2025,2035,2045,nk uwezekano wa Chama cha Upinzani kuitoa CCM madarakani kwa mazingira haya haupo!
Hili litamalizwa mwaka ambao Wananchi watakapofikia ukomo wa Uvumilivu kisha waingie mabarabarani kuleta Mapinduzi yasiyotarajiwa.
 
Tatizo ccm ina watu wenye kukipenda chama kama chama pamoja na mapungufu yake ila upinzani kuna watu wenye kuchukia huu utawala wa ccm.

Huwa nafikiri kuwa kama kweli ccm imechokwa na watu na kuchukiwa na ipo madarakani kwa nguvu ya dola tu,basi sidhani kama ingewezekana hata kuwasomba watu kwenye malori(watu waliyoichoka ccm na huichukia) na kuwapeleka kwenye kampeni za ccm au kwamba hao watu wejipeleke wenyewe kwenye mikutano ya ccm kuangalia wasanii,hao watu watakuwa hawako serious.
 
CHADEMA inahitaji wataalamu wa stratejia ya siasa (Political Strategists) kuweza kuitoa CCM madarakani kwa urahisi. Vyama vikongwe na vyenye dola kama CCM vinahitaji kufanyiwa mkakati maalumu ambao hauhitaji nguvu. Kama ningepewa fursa ya kutoa ushauri wa kimkakati wa kuitoa CCM ningeshauri ifutavyo:-

1. Kwa wakati huu 2020 - 2025 Chama kijikite katika kuunga mkono mikakati muhimu ya kitaifa inayofanywa kuinua uchumi wa Taifa inayofanywa na CCM. Hii ingefanya CHADEMA kuonekana ni Chama kinachojali maslahi mapana na maendeleo ya Taifa. Masuala ya kupinga kila kitu hata ambayo yalikuwa sera zake toka mwanzo yanakiondolea Chama taswira ya dhamira ya kweli ya kuleta maendeleo kwa Taifa. Wasingeweka hata mgombea kwa nafasi ya Rais kwa kipindi hiki ili waonekane na kuaminiwa na wananchi kwamba hawana uroho wa madaraka, wanathamini maendeleo ya taifa, kwani maendeleo hayana vyama. Hii ingewafanya wananchi wakiamini chama zaidi. Misuguano na serikali kwa mambo ya msingi ya kitaifa ambayo kila mtu mwenye akili ya kawaida tu anaona, haina tija kwao. Mwenyekiti Mbowe aliwahi kumpongeza hadharani Rais Magufuli akiwa Hai kwa kazi ya maendeleo anayoifanya, na akasema, "MNYONGE MNYONGENI LAKINI HAKI YAKE MPENI". Kama Mwenyekiti alipongeza, ina maana Chama kinatambua na kuthamini kazi nzuri inayofanywa. Haiwezekani kugeuka tena na kuanza kuona kilichofanyika ni upuuzi. Ukigeugeu huo unafanya wananchi waone CHADEMA haina dhamira ya maendeleo ya kweli. Wanachokisema leo, kesho watakipinga.

2. Kutosimamisha mgombea kwenye uchaguzi wa mwaka huu, kungefanya CCM watambe sana na kuendelea na makosa wanayoyafanya wakidhani wananchi wanafurahia. CCM wangeendelea kujitegea mabomu wao wenyewe hadi 2025. Wangeendelea na mambo ya miundombinu bila kushughulikia uchumi wa mwananchi mmoja mmoja. Kufika 2025 kila mwananchi angekuwa ameichoka CCM. CHADEMA wangeendelea kukusanya takwimu za makosa ya CCM hadi 2025. Ingekuwa rahisi sana kwa CHADEMA kuitoa madarakani CCM sababu wananchi wote wangekuwa tayari wamejaa chuki kwa CCM. Kwa hulka ya Magufuli angeendelea kushughulika miradi mikubwa ya kimkakati bila kuangalia maslahi ya watu wa kawaida. Sasa hivi CHADEMA imefanya CCM iwe makini zaidi na wakishinda uchaguzi watarekebisha mambo mengi aliyoyapigia kelele Lissu. Ni wazi kwamba Magufuli atashinda tena.

3. Kumwacha Magufuli kuendelea hadi 2025, kungewasaidia CHADEMA kuchukua nchi ikiwa imejaa miundo mbinu ya kila namna, na hivyo kuongoza nchi kwa urahisi. Wangekuwa na kazi moja tu ya kushughulikia maslahi ya mtu mmoja mmoja. Sasa hivi hata Lissu akishinda (kitu ambacho hakiwezekani) atapata shida sana katika kuweka mambo sawa. Wananchi wanatarajia akishinda matatizo yao yataisha ndani ya mwaka mmoja. Ukweli ni kwamba matatizo ya wananchi hayawezi kuisha ndani ya mwaka mmoja. Mwaka ukipita bila kumaliza kero zao, malalamiko yataanza, na yataigharimu sana CHADEMA katika uchaguzi wa 2025. Kitu cha kwanza kitakachogharimu CHADEMA ikishinda ni corona. Washirika wao wa nje watawataka waiweke nchi kwenye Lockdown. Hilo ni lazima. Ni Magufuli tu mwenye jeuri ya kuendelea kuwakatalia wazungu. Lissu hawezi kuwakatalia. Na akikubaliana nao ajue atakosana na kila mwananchi. Kusubiri hadi 2025, kungesaidia CHADEMA kuingia madarakani kukiwa hakuna mambo ya Corona duniani. Hivyo, mashinikizo ya kimataifa juu ya corona hayatakuwepo tena.

4. Sasa hivi CHADEMA imeshiriki uchaguzi huu, lakini kushinda sio rahisi hata kidogo. Na wakishindwa hawatarudi tena 2025. CCM itatumia sera zake na zao pia kuondoa kero kwa wananchi. CHADEMA haitakuwa na hoja tena 2025. Kwa hiyo kutovumilia miaka 5 ijayo kutawakosesha ndoto ya kushika dola hivi karibuni. Miaka 5 haikuwa mingi kuvumilia ikiwa ni mkakati wa kuitoa CCM madarakani kwa urahisi.
Muda wa kuandika ujinga unaupata wapi?
 
Dola (Majeshi) yakae pembeni uone kama CCM itasalia madarakani kupitia boksi la kura

Hujui mambo ya National Security and Politics ndo maana unasema Majeshi likae pembeni. Anayedhani Majeshi yakae pembeni kwenye politics anajidanganya. Haipo popote duniani. Majeshi ni sehemu ya politics za nchi husika. Tofauti ni kwamba hawagombei nafasi za kisiasa tu basi.
 
Chadema kikwazo cha kutoshinda ni tumeccm hii tumefake kamwe haiwezekani kuwatangaza Chadema kama washindi. Ccm imechokwa Nchi nzima.

CCM ikishindwa Ni bora kuongozwa na CUF sio CDM. CDM ni vibaraka wakubwa, wezi na watakuwa wasaliti wa nchi hii. Huwezi kukabidhi nchi kwa watu wanoonekana dhahiri watapoteza maslahi ya taifa. Watu wanaopanga kuweka rehani madini ili kupata pesa za kuendesha nchi, akili zao zimefilisika. Watauza nchi kwa Wachina mara moja halafu wachukue chao waende Ughaibuni. Hakuna sera ya maana waliyoitangaza hadi sasa. Sera yao ni matusi, kejeli, vurugu. Hawana haja na maendeleo ya nchi, tungewaona kwenye maendeleo ya Chama chao kwa matumizi mazuri ya ruzuku.
 
Wewe mtoa mada hiyo mipango yako ni ya kipumbavu sana,unadhani unaweza mtoa mtu aliyeshika dola ambaye kuanzia tume ya uchaguzi,polisi,wakurugenzi wa uchaguzi unateua yeye???

The only way kuindoa CCM ni watu kuelezwa maovu ya chama kisha kupitia umma kwa damu pekee! Hamna njia nyingine acha kujidanganya.

Akili yako ni dhaifu sana. Hiyo njia nakuhakikisha haitawafanikisha kwa lolote.
 
Povu zitoooo lakini wakati huo huo huyo mwizi aliyekwapua 2.7 trillions kama ilivyoripotiwa kwenye ripoti za CAG Assad na CAG Kichere ndiye unamuona mzalendo!!! Wapuuzi kama wewe ni tatizo kubwa Nchini

CCM ikishindwa Ni bora kuongozwa na CUF sio CDM. CDM ni vibaraka wakubwa, wezi na watakuwa wasaliti wa nchi hii. Huwezi kukabidhi nchi kwa watu wanoonekana dhahiri watapoteza maslahi ya taifa. Watu wanaopanga kuweka rehani madini ili kupata pesa za kuendesha nchi, akili zao zimefilisika. Watauza nchi kwa Wachina mara moja halafu wachukue chao waende Ughaibuni. Hakuna sera ya maana waliyoitangaza hadi sasa. Sera yao ni matusi, kejeli, vurugu. Hawana haja na maendeleo ya nchi, tungewaona kwenye maendeleo ya Chama chao kwa matumizi mazuri ya ruzuku.
 
speaking of strategies, Chadema or even ACT are miles ahead of CCM.

CCM kinachowabeba ni nguvu ya dola full stop. na counter pekee ya nguvu ya dola ni "nguvu ya umma" ambayo Chadema (bara) & ACT (Zanzibar) kwenye uchaguzi huu ndiyo wanaonekana kui mobilise with a radical push for total revolt. kauli zinazotolewa na wagombea wa upinzani this time haijawahi kutolewa kwenye uchaguzi mwingine wowote huko nyuma.

and am worried kuwa kunaweza kuwa na international intervention at some point. kikubwa CCM watumie zaidi busara na kuachia matokeo ya uchaguzi yaamuliwe kupitia ballot box, basi.
Umemaliza mkuu, you nailed it. Hakuna cha strategy wala bibi yake strategy wakati mwenzio tegemeo lake kuu ni kuiba ushindi through NEC, polisi and other organs... Just imagine mkakati wa kuengua wagombea was full of figisu halafu useme Kuna strategies??
 
Kila ikifika jioni, huwa nasikiliza kampeni za vyama kikiwemo CHADEMA nikitegemea kwamba labda watakuwa na sera mpya za kistaarabu, kwa bahati mbaya sijaona kitu cha namna hiyo.

Kwanza kabisa, sijasikia sera mahsusi za kuweza kuwashawishi Watanzania hasa wenye akili timamu. Zaidi sana nasikia tu sera za kuwavutia vijana wa rika fulani ambao kwa kweli hawajakomaa kiakili, wapo kwenye kipindi cha Bendera fuata upepo na waliojaa mihemko tu.

Kwa hiyo, mpaka leo hii Magufuli amemwacha Lissu mbali saaaaaana. Mimi huwa napita pita mitaani na vijiweni kufanya utafiti kidogo. Asilimia kubwa ya watu hata wa CHADEMA wanamkubali sana Magufuli, na wengi wanasema kwa upande wa Rais watampa kura Magufuli.

Kwa nini Magufuli? Pamoja na sababu zingine, lakini jinsi alivyoshughulikia Issue Corona, watu wanamkubali sana Magufuli. Huyu mwingine shida inayompunguzia sifa ni kukosa staha, adabu, ustahimilivu nk. katika kuongea. Ikumbukwe kuwa, Watanzania hawajazoea na hawapendi shari.
Ilani nzima ipo humu mitandaoni in pdf umeshaipakua na kuisoma kwa utulivu au unapanua domo kama mamba??
 
Back
Top Bottom