CHADEMA inahitaji uongozi mpya sio uenyekiti pekee.

CHADEMA inahitaji uongozi mpya sio uenyekiti pekee.

econonist

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
20,189
Reaction score
29,663
Kwa maoni yangu naona CHADEMA inahitaji uongozi mpya kabisa. Naona watu wengi wanaangalia cheo Cha Mwenyekiti na kuacha kuangalia vyeo vingine. CHADEMA inahitaji Mwenyekiti mpya mwenye msimamo sio Leo anasema hivi kesho anabadilika. CHADEMA inahitaji mwenyekiti atakaye kuwa nembo ya chama ambayo kila mmoja ataitazamia.

Pia CHADEMA inahitaji Makamu Mwenyekiti mpya bara na visiwani. Makamu Mwenyekiti ambaye ni Kijana mwenye ushawishi na msimamo. Makamu Mwenyekiti anatakiwa kuwa mwenye maono sawa sawa na Mwenyekiti na mwenye itikadi sawa sawa na Mwenyekiti. Tumeona kwenye uongozi wa Sasa hivi, Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti Wana itikadi tofauti. Mwenyekiti ni vugu vugu Kwa CCM anashadadia maridhiano na CCM wakati Makamu Mwenyekiti yeye ni mpinga maridhiano na Hana urafiki na CCM . Hivyo ni muhimu Makamu Mwenyekiti ajaye awe na itikadi sawa na Mwenyekiti wake ili chama kisonge mbele.

Pamoja na hayo, CHADEMA inahitaji kuwa na Katibu Mkuu ambaye ni msomi wa Hali ya juu na mwenye ushawishi. CHADEMA inahitaji katibu Mkuu mpya mwenye exposure ya mambo ya utawala na fedha. Ambaye atakuja na mkakati wa kuijenga CHADEMA kiuchumi. Kutafuta wafadhili ndani na nje ya nchi watakao isaidia CHADEMA kwenye harakati zake. Katibu Mkuu asiwe mwanasiasa Sana, siasa awaachie Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti. Yeye aje na mbinu za kuleta fedha CHADEMA. CHADEMA ikikuwa kiuchumi ndipo mwanzo wa kushika Dola utaanza. Kwa Sasa chama hakina pesa hata za kuweka mawakala wa uchaguzi kwenye vituo vyote nchini, so Katibu Mkuu ajaye afanikishe hilo. Kwakweli tunahitaji Katibu Mkuu Mpya ambaye ni msomi aliyebobea kwenye utawala.

Pia, Kuna nafasi ya muhimu Sana ambayo CHADEMA inahitaji mtu mpya. CHADEMA inahitaji Mkurugenzi mpya wa Sera, Bunge na Mawasiliano. Huyu anatakiwa awe Kijana mwenye ushawishi kwa vijana na mwenye uwezo wa kuhamasisha vijana waje kujiunga CHADEMA. Kijana mbunifu na mwenye uwezo wa kuelezea matamko ya chama yakaeleweka. Mwenye uwezo wa kuingia sokoni na vijiweni kuongea na wananchi. Mkurugenzi wa Sasa wa Sera, Bunge na Mawasiliano Ndugu Mrema, amejitahidi kwa nafasi yake ila nadhani ni muda akiapisha damu changa. Maana CHADEMA inahitaji kuchukua base ya vijana ambao ndio wengi na ili kufanya hivyo inahitaji msemaji Kijana na mbunifu kwenye uhamasishaji.

Kama CHADEMA tunataka mabadiliko na kuhamasisha watu wajiunge kwenye chama, tufanye mabadiliko ya uongozi na kuleta watu watakao tupeleka mbele.
 
Kabisa mkuu , hasa maeneo ya ndani ndani kuna vijana wengi mno ni wafuasi wa upinzani ila hawana hamasa Kabisa, chadema wakifanikisha hilo watapata wanachama lukuki.
 
Kwa maoni yangu naona CHADEMA inahitaji uongozi mpya kabisa. Naona watu wengi wanaangalia cheo Cha Mwenyekiti na kuacha kuangalia vyeo vingine. CHADEMA inahitaji Mwenyekiti mpya mwenye msimamo sio Leo anasema hivi kesho anabadilika. CHADEMA inahitaji mwenyekiti atakaye kuwa nembo ya chama ambayo kila mmoja ataitazamia.

Pia CHADEMA inahitaji Makamu Mwenyekiti mpya bara na visiwani. Makamu Mwenyekiti ambaye ni Kijana mwenye ushawishi na msimamo. Makamu Mwenyekiti anatakiwa kuwa mwenye maono sawa sawa na Mwenyekiti na mwenye itikadi sawa sawa na Mwenyekiti. Tumeona kwenye uongozi wa Sasa hivi, Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti Wana itikadi tofauti. Mwenyekiti ni vugu vugu Kwa CCM anashadadia maridhiano na CCM wakati Makamu Mwenyekiti yeye ni mpinga maridhiano na Hana urafiki na CCM . Hivyo ni muhimu Makamu Mwenyekiti ajaye awe na itikadi sawa na Mwenyekiti wake ili chama kisonge mbele.

Pamoja na hayo, CHADEMA inahitaji kuwa na Katibu Mkuu ambaye ni msomi wa Hali ya juu na mwenye ushawishi. CHADEMA inahitaji katibu Mkuu mpya mwenye exposure ya mambo ya utawala na fedha. Ambaye atakuja na mkakati wa kuijenga CHADEMA kiuchumi. Kutafuta wafadhili ndani na nje ya nchi watakao isaidia CHADEMA kwenye harakati zake. Katibu Mkuu asiwe mwanasiasa Sana, siasa awaachie Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti. Yeye aje na mbinu za kuleta fedha CHADEMA. CHADEMA ikikuwa kiuchumi ndipo mwanzo wa kushika Dola utaanza. Kwa Sasa chama hakina pesa hata za kuweka mawakala wa uchaguzi kwenye vituo vyote nchini, so Katibu Mkuu ajaye afanikishe hilo. Kwakweli tunahitaji Katibu Mkuu Mpya ambaye ni msomi aliyebobea kwenye utawala.

Pia, Kuna nafasi ya muhimu Sana ambayo CHADEMA inahitaji mtu mpya. CHADEMA inahitaji Mkurugenzi mpya wa Sera, Bunge na Mawasiliano. Huyu anatakiwa awe Kijana mwenye ushawishi kwa vijana na mwenye uwezo wa kuhamasisha vijana waje kujiunga CHADEMA. Kijana mbunifu na mwenye uwezo wa kuelezea matamko ya chama yakaeleweka. Mwenye uwezo wa kuingia sokoni na vijiweni kuongea na wananchi. Mkurugenzi wa Sasa wa Sera, Bunge na Mawasiliano Ndugu Mrema, amejitahidi kwa nafasi yake ila nadhani ni muda akiapisha damu changa. Maana CHADEMA inahitaji kuchukua base ya vijana ambao ndio wengi na ili kufanya hivyo inahitaji msemaji Kijana na mbunifu kwenye uhamasishaji.

Kama CHADEMA tunataka mabadiliko na kuhamasisha watu wajiunge kwenye chama, tufanye mabadiliko ya uongozi na kuleta watu watakao tupeleka mbele.
Shida ya ya Tanzania , vyama sio vya wanachama, ni vyama vya viongozi by "bagonza" hawana utaratibu wa kuandaa viongozi , utakuta ni wale wale, hii ni shida sana, utasikia Lema, Mbowe, myika,pambalu, heche,wenje, sugu, sio boni yai, miaka nenda rudi, tatizo kubwa Tanzania upinzani tunasafari ndefu mno
 
Kabisa mkuu , hasa maeneo ya ndani ndani kuna vijana wengi mno ni wafuasi wa upinzani ila hawana hamasa Kabisa, chadema wakifanikisha hilo watapata wanachama lukuki.

Kweli kabisa mkuu. CHADEMA Ina wafuasi wengi sana mkuu sema ndio hivyo hamasa hakuna.
 
Shida ya ya Tanzania , vyama sio vya wanachama, ni vyama vya viongozi by "bagonza" hawana utaratibu wa kuandaa viongozi , utakuta ni wale wale, hii ni shida sana, utasikia Lema, Mbowe, myika,pambalu, heche,wenje, sugu, sio boni yai, miaka nenda rudi, tatizo kubwa Tanzania upinzani tunasafari ndefu mno

Kweli mkuu hi ni changamoto kubwa sana kwenye vyama vya upinzani.
 
Mimi niseme waziwazi bila kupepesa macho, kwa uzwazwa wa Watanganyika, plus njaa, kujikomba, kupenda heshima nk, hakuna mtu wala chama kitakacholeta maendeleo taraji yenye tija kwa wananchi wake. Hakuna kiongozi yeyote atakaekuwa kauzu kiasi cha kuwaondoa hawa watawala wa sasa.

Watu wanasema wanataka viongozi wapya wa CHADEMA wenye misimamo, misimamo ipi, mbona kila wakihitisha maandamano mnajificha chini ya uvungu. Hapo mnataka watoe tamko gani ili muone misimamo yao. Mnasema hawana misimamo sababu leo wanasema hili kesho wanabadilika. Niseme tu kuwa wanabafilika kutokana na asili ya hadhira (nature of the audience), mazingira/hali ya wakati huo (the prevailing context), nk.

Hakuna mtu mwenye akili timamu anaweza kuwapigania watu wasio na akili timamu, wasiojielewa wasiojitambua wala kuthamini maana ya uwepo wao hapa duniani ("ashakumu si matusi). Tukumbuke hawa viongozi tunaosema hawana misimamo nao ni wanadamu wana roho, na wana familia zinazowategemea, ndo maan kila wakichungilia ndani ya mioyo ya Watanganyika nakuona ouga, kutokujali, kutokujithamini, kutu ya wivu dhidi yao, usaliti, uchawa, uoga, nk, huamua kubadilika.

Watanganyika wengi wamejikomboa kitamaduni tu lakini ni maskini na fukara wa kutupwa wa fikra. Na ndo maana hata elimu iliyopo ni ya mkono uende kinywani siyo kwa future development.

Hata jambo dogo tu la ku-assess muungano uliopo limeshindikana, limebaki la wanasiasa kwa kigezo cha kuwa wengine haliwahusu maana haliwatei ugali mezani, mtaweza kukiondoa chama kilichojichimbia mizizi nusu Karne!! Ebu fikiria suala la katiba mpya, ni raia gani kwa sasa analizungumzia, hapo mnataka nani awasemee km nyie wenyewe hamjisemei, badala yake wanasiasa ndo wanahodhi michakato yote. Na wakifanya hivyo wanajitokeza wasomi MTAMBUKA na kusema kwa nini wanasiasa wanahodhi michakato. Hivi hao utaweka kundi gani. Acha tu Mboe et al, wafanye watakavyo maan hawana backups yenye akili timamu.

Nimemaliza: BANDOKITITA.
 
Back
Top Bottom