Uchaguzi 2020 CHADEMA isishiriki Uchaguzi mkuu Oktoba 2020 sababu ya Corona

Uchaguzi 2020 CHADEMA isishiriki Uchaguzi mkuu Oktoba 2020 sababu ya Corona

Dalili za kutaka kutia mpira kwapani, pia wakumbuke susa ya Maalim Seif imesaidia nn???..
 
Cdm kama chama ni juu yao kushiriki au kuacha, ila sisi wapiga kura tunaojitambua hatuko tayari kupoteza muda wetu kushiriki uchaguzi wa kihuni. Bila tume huru ya uchaguzi, sisi tunaojitambua na kwa kutumia ushawishi wetu tutahakikisha watu hawashiriki huo uhuni uitwao uchaguzi. Sio lazima kiongozi kupatikana kwa njia ya kura, iwapo njia hiyo haiheshimiwi ni vyema kutafuta viongozi kwa njia nyingine. Ifahamike hata ccm wengi wao hawako kwenye nafasi zao kutokana na njia ya kura halali, wingi wa kura/viti vya ccm ni nje ya ushindani halali.
Duh kwahiyo hutapiga kura?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Achana na mambo ya kupindua. Hayo yalienda na akina Mobutu. Uchaguzi ni uchaguzi tu. Wewe ukisusia shauri yako. Wenyeviti wa mitaa mlisusia, hawapo wanachapa kazi? Na huu susiaeni muone. Wengine watahombea. Kura zitapigwa na serikali itaapishwa na itachapa kazi. Nanhi mtabaki mtandaoni mnaloloma!

Yalienda ina kina Mobutu wakati miaka miwili nyuma Nkurunziza aliponea chupuchupu? Saina tatizo na nyie kuingia madarakani wala kujitangaza, ila sina muda wa kwenda kupoteza wangu kupanga mstari kisha ninayemchagua asitangazwe. Ni bora muende wachache mnaoikubali ccm mkabariki hiyo hujuma, kuliko kwenda vituoni kuwajazia watu kisha mbadilishe matokeo kwa kujifanya mnakubalika. Watu wakiwa wachache vituoni mtajua kabisa mko madarakani, ila sio kwa ridhaa ya walio wengi. Watendaji wa mitaa ndio hao waliingia bila ridhaa ya umma, saa hii hata wakiitisha mkutano wanajikuta na wanaccm wachache tena wazee, hii imesababisha kudharauliwa kwa viongozi hao. Ni nani atajisikia vizuri kuaandaa sherehe kisha watu wakatokea wachache mpaka vyakula kubakia? Kama unakubalika kisha unapata wapiga kura wachache, hata kama unakaa madarakani nayo haina ladha.
 
Comrade niunge mkono kuwasaka wale wote walioshiriki kumlisha sumu JPM wakati akiwa waziri,waliomlisha mzee Mangula sumu,walioshiriki mauaji ya kibiti,walio mpiga risasi Mh.Lissu.
Unakazi nzito nenda na ya Wangwi,kolimbi,sokoini rudi ya filikunjombi nenda kwa kombi zurura kooote kumrudia ulimboki,mtafute saanani mambo nimengi Ila usichoke nakuunga mikono na miguu... wako wanaoteseka tusiwataje wapendwa wao hovyo
 
Hakuna mkubwa anaelewa utoto.
sema wewe huelewagi habari za wakubwa, watu wazima waliopita huku wamenielewa ila wenye akili zilizofungiwa kwenye maboksi hawajaambulia kitu
 
sema wewe huelewagi habari za wakubwa, watu wazima waliopita huku wamenielewa ila wenye akili zilizofungiwa kwenye maboksi hawajaambulia kitu

Rudi shule ukajifunze kanuni za uandishi hasa kuweka koma, nukta na matumizi ya herufi kubwa kila unapoanza sentensi. Uzuri sasa hivi elimu ni bure. Ukiweza hilo ndio uje uongee na wanaume sasa hapa jukwaani.
 
Yalienda ina kina Mobutu wakati miaka miwili nyuma Nkurunziza aliponea chupuchupu? Saina tatizo na nyie kuingia madarakani wala kujitangaza, ila sina muda wa kwenda kupoteza wangu kupanga mstari kisha ninayemchagua asitangazwe. Ni bora muende wachache mnaoikubali ccm mkabariki hiyo hujuma, kuliko kwenda vituoni kuwajazia watu kisha mbadilishe matokeo kwa kujifanya mnakubalika. Watu wakiwa wachache vituoni mtajua kabisa mko madarakani, ila sio kwa ridhaa ya walio wengi. Watendaji wa mitaa ndio hao waliingia bila ridhaa ya umma, saa hii hata wakiitisha mkutano wanajikuta na wanaccm wachache tena wazee, hii imesababisha kudharauliwa kwa viongozi hao. Ni nani atajisikia vizuri kuaandaa sherehe kisha watu wakatokea wachache mpaka vyakula kubakia? Kama unakubalika kisha unapata wapiga kura wachache, hata kama unakaa madarakani nayo haina ladha.
Tulioko "site" tunayoyaona ni tofauyi a uyasemayo na hilo hilo ndio tatizo lenu. Mnakaa nyuma ya keyboards zenu na kuanza ku invent mambo. Mtaani hali ni shwari sana. Tunasubiria kupiga kura kwa hari ya juu. Na watakaojitokeza kupiga kura safari hii tutavunja rekodi. Ninachokushauri, mjiandae na hoja nyingine. Hiyo haitakiki!!!
 
Rudi shule ukajifunze kanuni za uandishi hasa kuweka koma, nukta na matumizi ya herufi kubwa kila unapoanza sentensi. Uzuri sasa hivi elimu ni bure. Ukiweza hilo ndio uje uongee na wanaume sasa hapa jukwaani.
Nashukuru angalau umetambua uwepo wa elimu bure

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chadema sanyingine wanamaamuzi ya kijinga... Waligomea serikali za mitaa kijinga na uchaguzi huu bila tume huru hali itakuwa mbaya. Inafaa wajifunze siasa za demokrasia ya kistaarabu na kimaendeleo.
-Kilakitu wanapinga na elimu zao ndooogo kabisa.

- hawafanyi cha maana (hata mafuriko majimboni mwao hawaendi kusaidia) kisa eti hawakusanyi kodi wao nikula na familia zao.
- wanahitajika lkn hawajielewi,hawajengi maelewano na maridhiano no mipasuko na madharau.

- wanachafua/kutusi watu bila ushahidi kisa wapande kisiasa,walimfanyia hivyo lowassa badae wakala matapishi na hata kinana mpaka kumwomba radhi sasa sijui wanamtaka chamani.

- hawasimamii jambo wakafanikisha mf. katiba,tume ya uchaguzi nk.
Chama kitaanguka vibaya hiki inabidi kijivue gamba kibadilike lasivyo kitapotea kama CUF!!
Huu mwandiko wa msomi au msomaji?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tulioko "site" tunayoyaona ni tofauyi a uyasemayo na hilo hilo ndio tatizo lenu. Mnakaa nyuma ya keyboards zenu na kuanza ku invent mambo. Mtaani hali ni shwari sana. Tunasubiria kupiga kura kwa hari ya juu. Na watakaojitokeza kupiga kura safari hii tutavunja rekodi. Ninachokushauri, mjiandae na hoja nyingine. Hiyo haitakiki!!!

Nadhani unafikiri sisi tuliopo huku mitandaoni tuko kwenye nchi nyingine, hivyo hatuyajui ya huku mtaani. Kwa taarifa yako tunapost kutokea humu humu mitaani, na tunachoongea ni hicho hicho kilicho mitaani. Tofauti ya huku mitaani ni matandaoni ni uhuru wa kufunguka. Huko mitaani ukifunguka kama huku mitandaoni, lile kundi lenu la watu wasiojulikana linakunyakua. Ila huku mitandaoni tunafunguka waziwazi. Ushahidi upo kwenye idadi ndogo ya watu kujitokeza kujiandikisha kupiga kura. Ni kweli wachache hao watakaojitokeza kupiga kura wataitachugua ccm, hatimaye ccm itapata ushindi wa asilimia 100, lakini kundi kubwa halitajitokeza kupiga kura. Huu ndio uhalisia na wala sio porojo, hivyo jiandaeni kushinda kama mlivyofanya uchaguzi wa SM ili kuficha aibu ya idadi ndogo ya wapiga kura.

Kitakachofanyika ni kupika idadi ya wapiga kura kwani serikali hii ni mabingwa wa kupika data, na wananchi wamedhirisha hilo kupitia ugonjwa huu wa corona. Mpaka sasa tume ya uchaguzi imeongopa waliojiandikisha ni 30m jambo ambalo si kweli. Naendelea kusisitiza kuwa ccm sio chama cha kizazi hiki, ndio maana inatumia mabavu, na njia nyingine za aibu kulazimisha kukaa madarakani bila ridhaa ya umma.
 
Nadhani unafikiri sisi tuliopo huku mitandaoni tuko kwenye nchi nyingine, hivyo hatuyajui ya huku mtaani. Kwa taarifa yako tunapost kutokea humu humu mitaani, na tunachoongea ni hicho hicho kilicho mitaani. Tofauti ya huku mitaani ni matandaoni ni uhuru wa kufunguka. Huko mitaani ukifunguka kama huku mitandaoni, lile kundi lenu la watu wasiojulikana linakunyakua. Ila huku mitandaoni tunafunguka waziwazi. Ushahidi upo kwenye idadi ndogo ya watu kujitokeza kujiandikisha kupiga kura. Ni kweli wachache hao watakaojitokeza kupiga kura wataitachugua ccm, hatimaye ccm itapata ushindi wa asilimia 100, lakini kundi kubwa halitajitokeza kupiga kura. Huu ndio uhalisia na wala sio porojo, hivyo jiandaeni kushinda kama mlivyofanya uchaguzi wa SM ili kuficha aibu ya idadi ndogo ya wapiga kura.

Kitakachofanyika ni kupika idadi ya wapiga kura kwani serikali hii ni mabingwa wa kupika data, na wananchi wamedhirisha hilo kupitia ugonjwa huu wa corona. Mpaka sasa tume ya uchaguzi imeongopa waliojiandikisha ni 30m jambo ambalo si kweli. Naendelea kusisitiza kuwa ccm sio chama cha kizazi hiki, ndio maana inatumia mabavu, na njia nyingine za aibu kulazimisha kukaa madarakani bila ridhaa ya umma.
Ahahahahahah! Mmeishakata tamaa hata kura bado kwasababu mnajua ushindi wa CCM ni wa uhakika. Tena safari hii hadi ulimwengu utakubali!
 
Ahahahahahah! Mmeishakata tamaa hata kura bado kwasababu mnajua ushindi wa CCM ni wa uhakika. Tena safari hii hadi ulimwengu utakubali!

Unajua maana ya kukata tamaa na kupuuza uchaguzi? Narudia tena hakuna mtu mwenye akili timamu anaweza kwenda kusimama kwenye mstari wa kupiga kura, huku maelekezo yakiwa ni kumtangaza mgombea wa ccm. Kwa taarifa yako hatushiriki uchaguzi ili tushinde sisi tu, bali tunashiriki ili mgombea anayekubalika na wengi atangazwe, na sio huu upuuzi uliokuja kwenye chaguzi zetu chini ya awamu hii ya tano.
 
Back
Top Bottom