Elections 2010 CHADEMA iwaachilie walioshinda kura za maoni wagombee

Elections 2010 CHADEMA iwaachilie walioshinda kura za maoni wagombee

Status
Not open for further replies.
hapa ni patamu kweli

lakini kama kwenye mchujo wanachama walikuwa wachache kwanini uchaguzi usirudiwe kuliko kupanga matokeo ofcn?
hawa wanasiasa wanachukulia siasa very lightly kama wakikaa na wake zao majumbani, siwaelewi kabisa, and they are really letting Dr. Slaa chances down

BTW, hivi hamjajiuliza when it comes to women chadema wanachemsha sana kwenye chaguzi na teuzi?? what wrong?
 
KUrudia wimbo ule ule, kwa watu wale wale ukitegemea watacheza ni kujisumbua. NImeshatolea jibu hilo.
Hakuna cha kujisumbua hapa wewe ni ndumilakuwili una double standard huku unasema hivi kule unasema vile ukitarajia utawachanganya wananchi am sorry to say this it is a shame.

Haitoshi kusema umeshatolea jibu you have to admit the mistake. Mtu unataka kupandikiza mbegu chafu ya jinsia halafu tunyamaze we have to say stop this kama tulivyomwambia Malaria Sugu aache udini.
 
Kitu cha msingi kabisa kuzingatia katika mjadala huu ni kwamba, kwa CHADEMA, inayofanya uteuzi wa wagombea wa nafasi za ubunge na hata urais ni Kamati Kuu. Kura za maoni na Maoni ya Kamati ya Utendaji ni nyenzo tu za kuisaidia Kamati Kuu kufanya maamuzi na kutoa mapendekezo yake kwa vyombo vya juu zaidi kimaamuzi. Ndio maana hata Dk Slaa aliombwa kugombea na Kamati Kuu baada ya utafiti wa takribani mwaka mmoja, na wala sio kwamba yeye alijitokeza. Hii ni kwa sababu swala la uongozi kwa CHADEMA, hasa kwa kazi kubwa kama ubunge na urais ni swala zito la chama na nchi, badala ya kuwa swala la mtu binafsi. Kwa wenzetu, kama walivyowahi kusema wao wenyewe, ni swala la mtu binafsi na familia zao. To us the party and the country stand taller than the individual. We are prepared to hurt an individual if that hurting will heal the party and the nation. Tatizo ninaloliona katika mjadala huu ni kwamba watu wanajadili with a CCM system in mind. Ours is a different system altogether. If there is something wrong with the system, then let the debate deal with it.

Hii ni Philosophy Ngumu sana kueleweka kwa sisi tulio nje ya chama! Chama ni wanachama kama kuna nyakati inabidi kuumiza wanachama kwa manufaa ya chama na taifa! Tunarudi kwenye mambo ya kiimla ya CCM
 
Acid samahani kwa kukukwaza............i was just pondering yaliyosemwa na Luteni kuwa labda wagombea walipigiwa kura na watu 12 na wa kwanza kushinda kwa kura sita, kwa hiyo kutengua maamuzi ya hao watu 12 kwa mgombea bora zaidi si tatizo.

nilikuwa najiuliza hivi aliyoyasema Luteni yawezekana kweli au ni ya kusadidika kama mfumo dume wa chadema uliotajwa na mwanakijiji.

juu ya hivyo nashukuru kwa jibu lako ............inaonyesha Luteni yuko karibu na jibu zaidi ya nilivyodhani....
Gaijin hao watu 12 nilikuwa natolea mfano tu matokeo halisi ya Segerea yalikuwa hivi

Rachel Mashishanga alipata kura 48 akifuatiwa na F. Mpendazoe aliyepata kura 28 sikumbuki zilizoharibika.
 
Hakuna cha kujisumbua hapa wewe ni ndumilakuwili una double standard huku unasema hivi kule unasema vile ukitarajia utawachanganya wananchi am sorry to say this it is a shame.

Haitoshi kusema umeshatolea jibu you have to admit the mistake. Mtu unataka kupandikiza mbegu chafu ya jinsia halafu tunyamaze we have to say stop this kama tulivyomwambia Malaria Sugu aache udini.

rekodi iko inasimama yenyewe. CCM na CHadema wote wawili hawakutakiwa kuingilia kubadilisha matokeo ya kura za maoni. Kura hizo zilitakiwa zisimame kuheshimiwa. No matter the cost. Thats what democracy is all about. Kama msimamo huo ni kosa naomba radhi.
 
Hii ni Philosophy Ngumu sana kueleweka kwa sisi tulio nje ya chama! Chama ni wanachama kama kuna nyakati inabidi kuumiza wanachama kwa manufaa ya chama na taifa! Tunarudi kwenye mambo ya kiimla ya CCM

I hope watu watanielewa.. nataka Chadema iwe juu na zaidi ya CCM. Kuanzia inavyoongozwa, sera zake, mfumo wake wa utawala na mtazamo wake. Bado kasumba ya CCM imeharibu karibu vyama vyote vya upinzani.
 
rekodi iko inasimama yenyewe. CCM na CHadema wote wawili hawakutakiwa kuingilia kubadilisha matokeo ya kura za maoni. Kura hizo zilitakiwa zisimame kuheshimiwa. No matter the cost. Thats what democracy is all about. Kama msimamo huo ni kosa naomba radhi.

Kweli kabisa na mimi huo ndio mtizamo wangu. Vinginevyo tutakuwa tunajidanganya tu kuwa tuna demokrasia kumbe wapi. Na kama mambo yenyewe ndio hivi basi nadhani hata maana ya demokrasia hatuijui au hawaijui.
 
I hope watu watanielewa.. nataka Chadema iwe juu na zaidi ya CCM. Kuanzia inavyoongozwa, sera zake, mfumo wake wa utawala na mtazamo wake. Bado kasumba ya CCM imeharibu karibu vyama vyote vya upinzani.

Kwa hili niko pamoja na wewe! Nadhani copying na kupaste kutoka kwenye chama mama (CCM) bila kufanyiwa editing inakost democrasia hata CHADEMA! Ninaandika kwa uchungu kuvunja moyo akina Regia na Rachel
 
Gaijin hao watu 12 nilikuwa natolea mfano tu matokeo halisi ya Segerea yalikuwa hivi

Rachel Mashishanga alipata kura 41 akifuatiwa na F. Mpendazoe aliyepata kura 28 sikumbuki zilizoharibika.

nimekuelewa mkuu..........kama segerea watu walikuwa chini ya 100 moja, huko kilombera walikuwa 50!

nadhani nilishalizungumzia hili kuwa chadema kimefanya kosa kwa kuwa na watu wachache mno wanaoshindania nafasi inayowaniwa na pia kuwa hao wagombewa wanapigiwa kura na watu wachache sana.

hata hivyo kwa mujibu wa demokrasia, hata mgombea akipata kura 2 kati ya 3 zilizopigwa ni kuwa ameshinda.

Labda chadema walijua awali kuwa hawana watu wa kutosha wa kupiga kwenye kura za maoni ndio maana uteuzi wa mwisho ukawa unafanywa na viongozi wa juu. ...................

:confused2:
 
Mojawapo ya vitu ambavyo sipendi kwenye CCM ni huu utaratibu wa kikomunisti ambapo watu fulani katika majoho yao wanatengua maamuzi ya kura kwa ajili ya maslahi ya "chama". Badala ya kuwachuja watu kabla ya kupiga kura CCM ikabuni mtindo mbovu kabisa wa kuwachuja watu baada ya kura.

Matokeo yake, mtu ambaye amefanya vizuri kwenye kura za maoni na kwa uhalali wote anaweza kujikuta anaenguliwa baadaye kwa sababu na kisingizio chochote kile. Hivyo, mfumo wa rushwa, kubebana na kuburuzana umeendelea kudumishwa.

Sasa, chama ambacho kinataka kuleta mabadiliko cha CHADEMA kinasikitisha kuwa nacho kimerithi na kukumbatia mfumo huo huo mbovu. Habari kwamba baadhi ya wagombea wake walioshinda katika kura za maoni baada ya kufanyia jasho kuenguliwa na vikao vya juu vya "chama" ni habari za kusikitisha na zinaonesha kuwa mfumo ule ule mbovu wa demokrasia ya 'chama' umerithishwa ndani ya Chadema na utaleta matatizo yale yale (kama bado haujaleta).

Kwamba wagombea kama Regia Mtema (kilombero) na Rachel Mashishanga (Segerea) wameombwa kuachia nafasi zao kuwapisha watu wengine (wote wanaume) ni jambo la kufanya watu kutikisa vichwa vyao. Chadema haiwezi kuendelea kusubiria viti vya vijana au wanawake ili kuwapa nafasi za kugombea.

Moyo wa ujasiri uliooneshwa na kina dada hao hata wakaamua kugombea kwenye majimbo na kuonekana kuwa wako tayari kuhukumiwa na wapiga kura wote ni jambo ambalo Chadema inapaswa na ilipaswa kulitetea na kuwapigania hadi dakika ya mwisho. Kina dada hawa wameonesha ujasiri na utayari ambao haupaswi kubomolewa kwa sababu Makao Makuu wanataka watu fulani.

Mpendazoe na huyo wakili wa Kilombero wote walikuwa na nafasi ya kugombea toka mwanzo kama wangetaka. Lakini haya ya kuonekana kubebwa na chama kwa sababu yoyote hayaoneshe "demokrasia" bali ukiritimba wa mfumo dume ambao utawasumbua Chadema baadaye. Ni kweli kuwa katika nafasi karibu zote za juu za Chadema zinashikiliwa na wanaume lakini sitaki kuamini kuwa hilo pekee linaweza kuwafanya wasione umuhimu wa kuwalinda wagombea wake waliojitokeza.

Ninachosema ni kuwa Chadema inataka demokrasia basi iwe tayari kulipa gharama yake. Isiwe kama CCM ambayo kwake demokrasia ni anasa. Ukiondoa tuhuma za vitendo vya rushwa au ukiukwaji wa maadili Chadema iwaachilie wagombea wake walioshinda kura za maoni wasimame kama wagombea wa chama. Hao wengine kama kweli wanataka nafasi hizo wasubiri 2015.

Watanzania wanataka kitu "tofauti" na CCM; wanata kuona mfumo tofauti wa kisiasa na chama tofauti na wa CCM. Wanajua kuwa baadhi ya matatizo yaliyopo leo hii ni matokeo ya mfumo mbovu wa utawala wa kisiasa wa CCM. Lakini kama Chadema hawako tayari kubadilisha mfumo wao ili uwe wa kidemokrasia zaidi (la kushangaza ni kuwa ni chama cha "demokrasia" angalau CCM ni cha "mapinduzi.. kupinduana"). Tuwape Watanzania sababu ya kutumaini kilicho bora. Lakini kwenye madogo haya inakuwa kazi kwa makubwa itakuwaje? Natumaini cool heads will prevail.
Go Regia
Go Rachel

Kina R n R wasikate tamaa kwani hata kama wataenguliwa ukweli unabakia umeandikwa kuwa walishinda kura za maoni na walienguliwa na chama si kwa sababu ya rushwa au tuhuma za kukiuka maadili bali kwa sababu walikuwa ni aidha ni wanawake au hawakuwa tayari kupiganiwa na chama hadi ushindi.

Tafadhali toa "scenerio" nzima ili tutoe maoni sahihi. Kwa mfano walioanguiwa ni kina nani kwa sababu gani?
 
rekodi iko inasimama yenyewe. CCM na CHadema wote wawili hawakutakiwa kuingilia kubadilisha matokeo ya kura za maoni. Kura hizo zilitakiwa zisimame kuheshimiwa. No matter the cost. Thats what democracy is all about. Kama msimamo huo ni kosa naomba radhi.
Sasa nimeanza kukuelewa, kwa vile unasema kura ziheshimiwe then ile Makala yako ya trh 4 August Tanzania Daima tunaweza kusema kiutu uzima uliteleza kidogo kuiambia NEC CCM isiheshimu maamuzi ya kura za maoni.

Baada ya hapo ndipo tuongelee maamuzi ya Chadema kama yana busara ama la.
 
Sasa nimeanza kukuelewa, kwa vile unasema kura ziheshimiwe then ile Makala yako ya trh 4 August Tanzania Daima tunaweza kusema kiutu uzima uliteleza kidogo kuiambia NEC CCM isiheshimu maamuzi ya kura za maoni.

tatizo unatafuta explanation ambayo haitokuwepo; maelezo yangu juu ya makala ya jumatano nimeshayatoa na sikuteleza mahali popote. Aliyeteleza ni mhariri.

Baada ya hapo ndipo tuongelee maamuzi ya Chadema kama yana busara ama la.

maamuzi ya Chadema hayahusiani na makala yangu na hata kama makala yangu ingekuwa imedai vinginevyo suala la Chadema ni la Chadema vile vile na linaongoleka pasipo kujali maoni yangu.
 
rekodi iko inasimama yenyewe. CCM na CHadema wote wawili hawakutakiwa kuingilia kubadilisha matokeo ya kura za maoni. Kura hizo zilitakiwa zisimame kuheshimiwa. No matter the cost. Thats what democracy is all about. Kama msimamo huo ni kosa naomba radhi.

Hapa nakuunga na miguu.
 
Kitu cha msingi kabisa kuzingatia katika mjadala huu ni kwamba, kwa CHADEMA, inayofanya uteuzi wa wagombea wa nafasi za ubunge na hata urais ni Kamati Kuu. Kura za maoni na Maoni ya Kamati ya Utendaji ni nyenzo tu za kuisaidia Kamati Kuu kufanya maamuzi na kutoa mapendekezo yake kwa vyombo vya juu zaidi kimaamuzi. Ndio maana hata Dk Slaa aliombwa kugombea na Kamati Kuu baada ya utafiti wa takribani mwaka mmoja, na wala sio kwamba yeye alijitokeza. Hii ni kwa sababu swala la uongozi kwa CHADEMA, hasa kwa kazi kubwa kama ubunge na urais ni swala zito la chama na nchi, badala ya kuwa swala la mtu binafsi. Kwa wenzetu, kama walivyowahi kusema wao wenyewe, ni swala la mtu binafsi na familia zao. To us the party and the country stand taller than the individual. We are prepared to hurt an individual if that hurting will heal the party and the nation. Tatizo ninaloliona katika mjadala huu ni kwamba watu wanajadili with a CCM system in mind. Ours is a different system altogether. If there is something wrong with the system, then let the debate deal with it.

Huu mfumo ni mbovu kabisa, inawezekana unasaidia wakati chama kinakuwa ila si mfumo wa Kidemokrasia. Ni mfumo ambao utauwa Chama. Mfumo wenye harufu mbaya, ya upendeleo, malalamiko na usio na uwazi. Mfumo ambao hauleti kipimo cha kukubalika kwa wapiga kura bali kwa viongozi. Mfumo wa primary na mchakato kuendeshwa majimboni unafaa zaidi kwani huko ndiko wapiga kura walipo. Ni lazima mgombea akubalike kwa wapiga kura si viongozi.

Ingefaa hizo kamati zenu zipitishe na kuchuja majina ya wagombea kabla ya kura za maoni. Kura iwe ni maamuzi ya mwisho yasiyopingwa, pale kura zinapokuwa zimefuata taratibu bila kuvunja sheria za uchaguzi za chama.
 
Huu mfumo ni mbovu kabisa, inawezekana unasaidia wakati chama kinakuwa ila si mfumo wa Kidemokrasia. Ni mfumo ambao utauwa Chama. Mfumo wenye harufu mbaya, ya upendeleo, malalamiko na usio na uwazi. Mfumo ambao hauleti kipimo cha kukubalika kwa wapiga kura bali kwa viongozi. Mfumo wa primary na mchakato kuendeshwa majimboni unafaa zaidi kwani huko ndiko wapiga kura walipo. Ni lazima mgombea akubalike kwa wapiga kura si viongozi.

Ingefaa hizo kamati zenu zipitishe na kuchuja majina ya wagombea kabla ya kura za maoni. Kura iwe ni maamuzi ya mwisho yasiyopingwa, pale kura zinapokuwa zimefuata taratibu bila kuvunja sheria za uchaguzi za chama.

pole pole nadhani utaanza kuambiwa na wewe huitakii mema Chadema!!
 
tatizo unatafuta explanation ambayo haitokuwepo; maelezo yangu juu ya makala ya jumatano nimeshayatoa na sikuteleza mahali popote. Aliyeteleza ni mhariri.
Basi wahariri wetu ni bogus kabisa wanakosea toka
Heading: Wabunge waliogongana Richmond warudishwe
Hadi conclusion:Ni kwa sababu hiyo ninaamini wabunge wafuatao warudishwe bungeni

Ngoja na mimi ni conclude, huwa napenda sana kufuatilia vitu na huwa si mvivu wa kutafuta facts popote zilipo ni utamaduni wangu niliojijengea labda kwa vile ni field yangu. Nilikuwa nataka nione stance yako juu ya kura za maoni ni vizuri umesema ziheshimiwe lakini nilipoangalia Makala yako ilikuwa contrary, kwa vile umesema kosa ni la mhariri nitaenda na hilo, na kwa kujiridhisha nimetoa hint hapo juu kwamba inawezekana mhariri alikosea vyote viwili heading na conclusion kitu ambcho ni nadra sana kutokea ili mbeleni nisije kujikuta mjinga kwa kukubali kitu nisichokuwa na uhakika nacho.
 
Basi wahariri wetu ni bogus kabisa wanakosea toka
Heading: Wabunge waliogongana Richmond warudishwe
Hadi conclusion:Ni kwa sababu hiyo ninaamini wabunge wafuatao warudishwe bungeni

Ngoja na mimi ni conclude, huwa napenda sana kufuatilia vitu na huwa si mvivu wa kutafuta facts popote zilipo ni utamaduni wangu niliojijengea labda kwa vile ni field yangu. Nilikuwa nataka nione stance yako juu ya kura za maoni ni vizuri umesema ziheshimiwe lakini nilipoangalia Makala yako ilikuwa contrary, kwa vile umesema kosa ni la mhariri nitaenda na hilo, na kwa kujiridhisha nimetoa hint hapo juu kwamba inawezekana mhariri alikosea vyote viwili heading na conclusion kitu ambcho ni nadra sana kutokea ili mbeleni nisije kujikuta mjinga kwa kukubali kitu nisichokuwa na uhakika nacho.

Hapana hakukosea Heading; heading ni yangu. Kuna maneno ambayo si yangu: Makala ya awali niliyotuma kwa mhariri ni hii hapa:


WABUNGE WALIOGONGANA SUALA LA RICHMOND WARUDISHWE BUNGENI


Na. M. M. Mwanakijiji


Leo Chama cha Mapinduzi nchini kinapiga kura ili kuweza kuanza mchakato wa kujua ni kina nani watakuwa wagombea wa chama hicho kwenye nafasi za udiwani, uwakilishi na Ubunge kwa kipindi kijacho cha miaka mitano. Mamia ya wana CCM watajitokeza kupiga kura ili kutoa mapendekezo yao katika utaratibu wa kura za maoni ambapo wanachama mbalimbali wamejitokeza kugombea wengine ikiwa ni marudio na wengine ikiwa ni mara ya kwanza.


Tukiondoa taarifa ambazo tumezisikia hasa wiki hii iliyopita hasa mazingaombwe ya TAKUKURU na wale wanaodaiwa kuhusika na vitendo vya rushwa masikio ya wachunguzi wengi wa kisiasa nchini yanabakia katika kundi la watu wachache ndani ya CCM ambao kwa takribani miaka miwili sasa limekuwa katika mgongano mkubwa. Leo kumbe ndiyo ile “leo ni leo” ya kwenye methali kwa kundi hili. Hili ni ku kundi ambalo lilijikuta linakipasua Chama cha Mapinduzi kufuatia sakatala la kashfa ya Richmond na masuala mengine ya ufisadi.


Kufuatia sakata hilo la Richmond na baadaye suala la Rais Mstaafu Mkapa na mgodi wa Kiwira wana CCM walijikuta wakigawanywa na kuwa na makundi makubwa mawili. Wale ambao wanaamini aliyekuwa Waziri Mkuu ambaye alijiuzulu kufuatia kuhusishwa na kashfa ya Richmond kuwa alionewa na wale ambao wanaamini kabisa kuwa Kamati Teule ilimwonea Waziri huyo Mkuu kwa kutompa nafasi ya “kujitetea”. Mpasuko huo ukatiwa nguvu na mpasuko wa kundi la wabunge ambao waliamini kuwa aliyekuwa Rais wa Tanzania Bw. Ben Mkapa alitumia madaraka vibaya pale alipodaiwa kujipatia mgodi wa Kiwira yeye, familia yake na watu wake wengine wa karibu. Suala hilo la kujipatia mgodi kinyemela liliwafanya baadhi ya wabunge wadai kuwa Rais huyo mstaafu avuliwe kinga ili hatimaye aweze kulazimishwa kujibu katika mahakama ya Sheria.


Kati ya masuala hayo mawili yakaibuka masuala mengine yatokanayo na hayo hasa pale ambapo vyombo mbalimbali vya habari vilipojikuta vinalazimishwa kuchukua upande aidha kwa sababu za kiitikadi au vikiwa vinasukumwa na wamiliki wake au na watu wenye maslahi ya kifedha na vyombo hivyo kiasi kwamba mgongano wa kisiasa ulivuka mipaka na kuwa mgongano wa binafsi katika ya makundi mbalimbali ya waandishi wa habari, wanasiasa, wafanyabiashara na kulazimisha jamii vile vile kuwa na pande mbili kuhusiana na masuala hayo.


Kinyume na ambavyo ilitarajiwa kwamba hatimaye mpasuko huo wa kimaslahi ndani ya CCM ungesababisha kundi moja kujitoa hali halisi ni kuwa siku ya leo imefika huku makundi yote mawili yakiwa na mashabiki na wapambe wake yakiwa yameshikana mapembe kama ng’ombe wagombanao na hakuna aliye tayari kumuachia mwingine. Ukiondoa kujiondoa kwa mmoja wa kundi hilo Bw. Fred Mpendazoe ambaye alijiunga na CCJ na baadaye Chadema, makundi yote mawili yameonekana kujitokeza kugombea tena nafasi za ubunge.
Katika kipindi hiki kilichopita kundi moja lile linalojulikana kuwa la “wapiganaji CCM” limekuwa likilalamika kuwa kundi jingine la “mafisadi” limekuwa likijaribu likitumia mbinu mbalimbali ili kufanya wanachama hao wa kundi la kwanza kushindwa katika chaguzi za ndani za CCM na kuwa wasipate nafasi ya kuweza kushiriki katika uchaguzi mkuu.


Hapo awali kauli hizo zimekuwa zikipuuzwa na vyombo vya dola na hakuna hata mtu mmoja ambaye ameweza kuonesha ushahidi wowote kuwa kumekuwa na mchezo mchagu kwenye majimbo mbalimbali zaidi ya tuhuma tu. Hata pale ambapo baadhi ya watu wametuhumiwa kuwa wametumwa na mafisadi kugombea ukweli unabakia kuwa hakuna ushahidi wowote aidha wa maandishi, picha, sauti, au vielelezo vingine ambao umeweza kutolewa kushawishi jamii kuwa kumekuwa na mchezo mchafu.


Japo hakuna ushahidi wa hilo haina maana jambo hilo halikuwepo. Tukichukulia taarifa za watu mbalimbali kukamatwa katika matukio mbalimbali yanayotajwa kuwa na mazingira ya rushwa wiki iliyopita ni wazi kuwa aidha kuna mtu anachezea akili za taifa zima au tuna vyombo vibovu kabisa vya kusimamia sheria. Inashangaza kuwa baada ya taarifa ya “kamata kamata” ya wiki iliyopita hadi leo siku ya uchaguzi hakuna mtu HATA MMOJA ambaye amefikishwa mahakamani kwa kosa lolote la kutoa au kupokea rushwa na wote wameachwa (hata wale tulioambiwa wamehojiwa usiku kucha) kushiriki uchaguzi.


Hivyo basi, kama TAKUKURU, Polisi na wale wenye kuwaamuru wameona kuwa makosa yote ambayo yamefanyika hayakuwa na ushahidi mzito wa kumpeleka mtu yeyote mahakamani na hivyo kuwaacha wagombea wagombee na kupigiwa kura basi ni budi niseme kwamba jaribio lolote la kuleta mashtaka baada ya kura za maoni ni upotoshaji mkubwa wa demokrasia na ni kuchezea utawala wa sheria. Ninachosema ni kuwa TAKUKURU na Polisi wasiwachezee Watanzania kwa kujaribu kuvuruga mchakato wa kuwapata wagombea ndani ya CCM hasa kwa kutoa taarifa kwa kamati mbalimbali za CCM kuwa fulani na fulani alifanya hivi na vile wakati wa kura za maoni.


Hilo likishaeleweka hatuna kukubali jambo jingine ambalo ni muhimu kuwa wale wabunge wote ambao waligongana Bungeni kwenye masuala ya Richmond, Mkapa na Kiwira wana CCM wataona ni bora wawarudishe tena Bungeni. Ninaamini kabisa kuwa itakuwa ni makosa makubwa kwa wana CCM kutowarudisha wabunge hao wote kwani kwa kufanya hivyo kutawapa ushindi kundi moja nje ya Bunge.


Binafsi sipendi ushindi wa mezani. Kwa vile CCM imeshindwa kutafuta suluhu ya makundi haya licha ya kuundwa kwa kamati ya Mzee Mwinyi basi kujaribu kutafuta suluhu nje ya Bunge litakuwa ni kosa kubwa zaidi. Fikiria kwamba Bunge lijalo linakuja halafu Mwakyembe na Selelii wametupwa nje huku Rostam na Lowassa wakiwa wameingia tena (kama inavyotarajiwa) je hawatotumia nafasi zao Bungeni kuhakikisha “wabaya wao” wanashughulikiwa na hata kutumia mtindo wa Kamati Teule kuweza kujisafisha zaidi? Japo hilo ni jambo zuri kwa upande mmoja mimi ninaamini tusiwaachie haya makundi mawili yakwepane.


Wana CCM wanajukumu la kuwarudisha wabunge wote waliohusika na masuala haya Bungeni ili wakamalizane Bungeni kwani hakuna atakayepewa ushindi wa chee. Sitaki tufike mahali Rostam na Lowassa wapoteze Ubunge halafu kina Mwakyembe na Selelii wakirudi Bungeni waamue kuwamaliza kabisa bila ya wao kupata nafasi ya kujitetea.


Kwa vile suala hili lilianzia Bungeni ni lazima liishie Bungeni na hakuna ujanja wa njia za mkato. Ninaamini wale wagombea wengine waliojitokeza katika majimbo ya wabunge hawa watakuwa ni wasindikizaji wazuri na wametoa changamoto nzuri lakini wana CCM watatambua kuwa kinachogombaniwa ni zaidi ya majimbo ya kisiasa. Wananchi katika majimbo yote yenye wabunge hawa wapambani na wale wenye kulaumiwa watatambua kuwa suala ambalo limelikabili taifa kwa miaka hii miwili ni kubwa mno kiasi kwamba kama ingekuwa ni mechi ya soka basi ningeweza kusema kilichopita ni kipindi cha kwanza tu. Katika kipindi hicho timu moja imefungwa magoli mawili.


Wana CCM kwenye kura za maoni watafanya makosa makubwa endapo wataamua kuondoa wachezeaji uwanjani badala ya kuja na kumaliza kipindi cha pili ati kwa vile wameonewa na kufungwa mabao mawili. Timu yenye akili ni ile inayokuja kwenye kipindi cha pili kwa nguvu zaidi na mbinu mpya ili kujibu mashambulizi huku ile timu nyingine nayo ikijipanga vizuri zaidi kulinda magoli yao na ikibidi kuongeza mengine.


Ni kwa sababu hiyo ninaamini wabunge wafuatao warudishwe Bungeni ili wakamalizie mechi yao kwani katika Tanzania ya leo, hakuna ushindi wa chee au wa kubebwa.


Edward Lowassa (Monduli)
Rostam Aziz (Igunga)
Peter Serukamba (Kigoma Mjini)
Anne Kilango Malecela (Same Mashariki)
Dr. Harrison Mwakyembe (Kyela)
Lucas Selelii (Nzega)
Aloyce Kimaro (Vunjo)
Said Juma Nkumba (Sikonge)


Wana CCM wafanyie taifa hisani kwa kurudisha kundi hili zima Bungeni ili wakamalizie mechi waliyoianzisha. Jaribio lolote la taratibu za kichama kumwengue yeyote hapo ni kujaribu kuipatia timu moja ushindi wa mezani. Tuwaache wote hawa warudi wakagongane tena huko Bungeni au wakapatane. Ushindi wa chee hakuna.


Niandikie: Mwanakijiji@jamiiforums.com
 
Kama kutakuwa na objectivity katika kulijadili suala hili basi huenda lawama dhidi ya Chadema zingeweza kuwa tofauti.Chama hiki kinakabiliwa na dilemma ya demokrasia,na sio kosa lao.Nitoe mfano japo sio wa kisiasa.Hivi timu inapopanda daraja na kufanikiwa kucehza ligi kuu,je ikitaka kutwaa ubingwa (na sio kushiriki tu kwenye ligi hiyo) haitopaswa kuunda timu ya ushindi?Of course,itakuwa sio haki kuwatosa wachezaji walioipandisha timu daraja lakini what if viwango vya wachezaji hao haviwezi kustahimili mikikimikiki ya ligi kuu?Na what if kama kuna wachezaji mahiri wenye potential ya kuleta kombe kwenye timu hiyo wapo willing kujiunga nao?

Tukija kwa Chadema,tunafahamu kuwa kura zao za maoni licha ya kujumuisha wanachama wachache (kutokana na idadi ndogo ya active members) pia sio sample mwafaka sana ya potential voters kwenye uchaguzi mkuu.Hilo sio kosa hasa ikizingatiwa kuwa hata CCM imekuwa ikipata kura nyingi zaidi ya idadi ya wanachama wake milioni 5 or so.Tutambue kuwa siasa za Tanzania,na sehemu nyingi Afrika bado zinaelemea zaidi kwa mgombea kuliko chama.Huo ni mfumo ambao utachukua miaka mingi kubadilika.

Ni kwa kutambua hivyo basi Chadema wanalazimika kufanya maamuzi magumu ya kupata wagombea wenye potential ya kutoa upinzani kwa CCM na pengine kukiwezesha chama hicho kupata idadi kubwa ya wabunge.Sasa je mnaoitakia mema Chadema mngependa "waridhishe demokrasia kwa kupitisha wagombea wenye uwezo haba wa kushinda" au waje na wagombea wanaoweza kuipatia ushindi?Tukumbuke huu ni mwaka wa uchaguzi na la muhimu zaidi ni ushindi HALALI.Mnaolinganisha udikteta wa CCM na "huu wa Chadema" mnasahau kuwa wakati "udikteta huu wa Chadema" unalenga kupata wagombea wenye potential ya ushindi (na process hii haisukumwi na rushwa au ufisadi) CCM hufanya mchezo huo kwa vile tu flani ana fedha za kutosha,anaweza kuhonga wapiga kura wengi na pengine anakidai chama hicho fadhila flani.

Pengine ni muhimu kwetu kutafakari kwa mapana zaidi dhima ya demokrasia hasa kwenye mwaka wa uchaguzi a kujiuliza,kwa mfano je linapokuja suala la kuteua wagombea kipi kiwe muhimu zaidi: wagombea walioteuliwa kwa njia za demokrasia au nafasi ya wagombea hao kushinda kwenye uchaguzi husika alimradi uteuzi wao haufanywi kwa njia zisizo halali?Au,kipi kiwe kipaumbele kwa chama katika mwaka wa uchaguzi kati ya kuenzi demokrasia na nafasi ya chama kufanya vizuri alimradi processes hizo zinafanywa kihalali na transparent?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom